Lulu (Elizabeth Michael) kuachiwa kwa dhamana

Lulu (Elizabeth Michael) kuachiwa kwa dhamana

Ninahisi huko mahabusu alikuwa salama zaidi kuliko atakavyokuwa uraiani...
Just thinking....
 
Anajidai analia huku kaharage hapo chini kanamtekenya kanamhitaji Mbako
 
Lulu hakuua ni udhaifu wa hayati manumba kutojua mbinu za upelelezi.
 
Ni vema kutumia kichwa kufikiri kuliko kukitumia kufugia nywele.. Quoted.. Fred Werema
 
Nadhani ni vigumu kusema anachukuliaje dhamana ya 'mkwewe' sanasana inamkumbusha uchungu wa kuondokewa na mwana. Vinginevyo mchakato wa kesi hii tangu utata wa umri hadi kwa DPP,vyombo vya habari vilikuwa vikiripoti. Kwa hiyo mama Steven kulichukulia inategemea na vitu kama hivyo.
 
kwenye ukweli uongo hujitenga tusubiri dakika tisini ya lulu itafika tu.
 
Eti alionekana viwanja vya mkuu wa kaya ndo wakagombana na kanumba kuwa alifuata nini kule. Kalikurupukia kuliwa wacha mapredeshee wazidi kagonga.
 
Ukute alikuwa na matatizo ya moyo au high cholesterol .bahati mbaya
 
734825_471892562874743_399692185_n.jpg


Habari zilizotufikia hivi punde zinadai kuwa Mahakama kuu ya Tanzania imemwachia kwa dhamana msanii wa filamu nchini Tanzania, Elizabeth Michael aka Lulu aliyekuwa mahabusu katika gereza la Segerea jijini Dar es Salaam.

Wiki iliyopita mawakili wa muigizaji huyo waliwasilisha maombi ya dhamana kwa mahakama hiyo kuu ya Tanzania.

Wanasheria hao Peter Kibatala, Kennedy Fungamtama na Fulgence Massawe waliomba dhamana hiyo itolewe haraka kwakuwa muombaji amekaa mahabusu kwa zaidi ya miezi saba na kwamba kosa lake linaweza kupewa dhamana.

Lulu anakabiliwa na kesi ya kumuua bila kukusudia Steven Kanumba April 7, 2012, huko Sinza Vatican, jijini Dar es Salaam.

Kanumba alidaiwa kuwa kwenye ugomvi na Lulu aliyekuwa mpenzi wake nyumbani kwake Sinza.

SOURCE: ITV



UPDATES:

- Sasa ndio wanakagua documents za wadhamini mahakamani...
- Kuna mambo hayajakamilika hivyo anarudi jela, hadi kesho...

FINAL UPDATE (03:00 PM, 28, Jan, 2013)
Lulu hajaachiwa, atarudishwa mahakamani kesho kwakuwa Msajili wa Mahakama Kuu hakuwepo na hii ilikuwa ni kesi ya 'Kuua bila kukusudia'.

Kesho wadhamini watawasilisha nyaraka zao mbele ya msajili ndipo anaweza kuachiwa...

Tutawafahamisha kitachojiri mahakamani kesho


LULU1.bmp
Mimi naona wagambo gambo wa magereza wanauza sura tu hapa!
 
Back
Top Bottom