Siku nzima nilibaki ndani nikiki tafakari kile kibao (kinga). Kuna wazo likanijia, nikaona sehem pekee pakwenda kupatupa ni baharini.
Kwakaribu nikaona ni Kurasini.
Ilipo fika jioni nikatoka nje, mpaka Chihota, nikachuka boda boda mpaka kurasini beech, kwakua sikutaka jamaa (boda boda) anigande nikamuomba aniache relini nikampa chake akarudi.
Nikaenda mpaka beech, maeneo flani hivi kitambo walikua wanauza ganja, nikawaacha kama hatua flani hivi wale jamaa (wala bange) hapo nikavua viatu vyangu nakuingia kwenye maji.
Maji ya mafutini, nikageuka nyuma kucheki kama kuna mtu ananitazama, nikagundua kila mtu anahabari zake.
Nikaingia mfukoni nikakitoa kile kibao (kinga) na kukirusha kwenye maji.
Sikutaka kuchelewa, nikapanda juu (relini) nikachukua tonda nakurudi mtaani.
Siku hiyo sikutaka hata pombe nikawai kuingia chumbani mapemaa nakujilaza.
Katika safari zangu zote ninazo kujaga Tanzania, safari hii sikuifurahia kabisa.
Japo nilikuja na pesa lakini nilijikuta niko bize hata muda wakutulia na washkaji sikua nao.
Nilisha zoea nikija na Mkwanja, humchukuaga rafiki yangu Dsalu nakumuomba anitembeze jijini, lakini safari hii hata yeye mwenyewe alikua akinishangaa.
Nakumbuka hata lile dili la kununua kiwanja Mbande lilikufa, dakika ya mwisho familia iliamua kuni nunulia chamanzi na kujenga kipindi mimi mwenyewe nisha kimbia.
Usiku wa siku hiyo kwangu ulikua mkubwa sana, sababu nililala mapema na kichwa kulikua hakija beba alcohol, ivyo nili lala kidogo, linipoamka sikupata usingizi kwa haraka.
Mida kama ya saa tisa usiku, mara nikaanza kuona ule umweku mweku mule ndani, chumba kizima kina mwekua mwekua, nikanyanyuka kitandani, nikaisogelea switch ya taa na kubonyeza.
Taa ikawaka lakini ule umweku mweku bado upo tu, nikaona ngoja nilipue chiga kwanza, nikatoa sigara mfuko wa shati, kibiriti huwa napenda kukiweka mezani, nilipo ikalibia meza, niki cheki mezani nakiona kile kibao pale mezani, sigara yenyewe nikairusha niliko itoa.
Nilitulia pale nikiki angalia kile kibao, mara nikasikia ule mlio Pah (kama chupa ya bia iliyo pasuliwa)
Zilipita kama dakika kazaa ule umweku mweku ukapotea na usingizi ukanipitia.
Asubuhi nilipo amka nyumba ya jirani nasikia kilio watu wanalia, nikajua tayari kuna mtu kesha jipiga.
Jirani alikua maarufu kiasi msiba wake watu walijaa sana.
Mpaka mama yangu nae akaja, mimi mwenyewe nilihudhuria mazishi.
Pale msibani niligundua watu wengi walikua wananiangalia sana, hasa wazee.
Hata tulipo kua makabulini, niliwaona wazee flani kama wananioneshea kidole.
Maziko yaliisha nikarudi nyumbani.
Mama na yeye nilimkuta yuko nyumbani teyari kesha rudi msibani.
Siku hiyo mama ali lala hapo hapo nyumbani, ilipo fika usiku, mama aliniita tena chemba.
Tilipu hii mama aliniomba niondoke, nirudi nilipo toka, (mocambique) ama nitokomee popote tu.
Mama aliniambia niondoke nisije kuuawa, maana story zangu zina vuma mtaa mzima.
Watu (wazee wa mtaa) wamejua kua nina kitu kinacho wadhuru wachawi.
Sikutaka nimfiche mama, nili muhadithia story nzima jinsi nilivyo jaribu kukitupa kile kibao (Mala mbili) lakini bila mafanikio.
Basi mama akaniambia, nakupenda mwanangu sitaki uu wawe, ondoka, nenda popote tu.
Siku kama mbili nilizimaliza nikiwa chumbani peke yangu, nikitoka nae kibaa cha jirani, nachukua Konyagi zangu na kujimiminia.
Kwa kweli maisha siku ya furahia kabisa.
Nikaona sio poa wacha nisepe zangu, maana sasa mpaka dada na yeye alikua haishi kunihimiza niondoke.
Kabla ya kuondoka, nikaona ngoja nikamtembelee babu yangu (mzaa baba) yeye huwa nampenda sana.
Yeye ndio alie ni rithisha Jina, huwa siwezi kuja Tanzania bila kumtembelea.
Babu yangu yeye anaishi Hanga, njia ya kwenda nyamisati.
Nilifika kwa babu, na kweli nilimkuta.
BADO KIDOGO NIMALIZIE, JAMBO LINAINGILIANA.
TUSAMEHANE JAMANI NITARUDI KUIMALIZIA.