M - Gas biashara imewashinda. TBS futieni leseni hawa wapuuzi

Mkuu...je gas ya kg 15 waweza kutumia mwaka?
Au kuna uwezekano gas ikashindiliea ukatumia milele?

Basi M-gas gas yake ikiisha unanunua kam vocha hata kwa buku 2 unaendelea kutumia instant
 
mwenye kampuni si alikuwa na kesi , hivo hiyo kesi iliishia wapi?
 
Kumbe iko hivyo?
 
Kufanya biashara tz kazi watz ni wezi by nature. Jamaa yangu anayo anaitumua ananiambia wafanyakazi unaongea nao wanafunga mawasiliano ya kifaa so wanakupa gas kwa bei chee
 
Kwahio M gas wanakuletea mtungi wao wenye gas halafu ukinunua ndio unapata access ya kutumia gas?
Wabongo wagumu sana kujieleza, yaani mtu kitu anakitumia ila kukitolea maelezo mepesi anashindwa.
M-gas niliiona siku moja kwa jamaa yangu chuo, mtungi wa size ya kawaida kama mingine ila imefungwa electronic device juu na nadhani inasoma GPS kwenye mtandao wa kampuni.

Badala ya mtu kutoa hela ya pamoja ya kununua mtungi na jiko, anatoa hela kidogo anapewa hivyo vitu kama kukodishwa kisha analipia subscription kama Luku. Usipolipa gesi haitoki na ikizima unaweza lipia hata gesi ya hela ya chini kama elfu moja ukapika. Kuna kadi mteja anapewa.

Likitokea tatizo wanatengeneza wao, ukiisha mtungi wanajaza wao. Ila kuna mkataba ukilipia kwa miezi kadhaa mtungi unakuwa wako nadhani hapo wanadeactivate electronic device au wanaitoa. Nahisi wakitaka kuvunja mkataba wanaweza sababu unakuwa umekodishiwa haujanunua, mfano umechukua mtungi alafu ni bachelor unapika mara mbili kwa mwezi.

Haya maelezo niliyajua kwa siku moja na sijawahi utumia. Watumiaji wenyewe ndio hawa hawawezi kutuelekeza.
 
Kufanya biashara tz kazi watz ni wezi by nature. Jamaa yangu anayo anaitumua ananiambia wafanyakazi unaongea nao wanafunga mawasiliano ya kifaa so wanakuoa gas kwa bei chee
Wapo wafanyakazi wa Zuku, kila wakija kufunga WiFi kwa yeyote wanamwambia sehemu yake haina signal au wanadai signal zimejaa ila kuna namna nyingine "wanaweza kukusaidia".

Ikiwa signal zipo kweli wanakuunganisha ukifanya namna, ikiwa hazipo wanasitisha signals za mteja mwingine wanakuuzia wewe. Mteja akija kulalamika wanamzungusha.

Hii nchi upuuzi mwingi
 
Okay nimekuelewa.
 
Kazi ipo. Unafungua biashara kuajiri vijana wao wanakuibia kesho kampuni inakufa wanalia hakuna ajira.
 
Tz kuanzia watawala mpaka wananchi wote matapeli. Namna hii wawekezaji wataogopa kufungua biashara TZ kwa namna wafanyakazi wanahujumu kampuni.
 
Una talanta ya uticha vp hujawahi kufikiria kuwa mwalimu. straight and clear explanation
 
πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€
 
Aisee kuendesha biashara bongo ukiachana na TRA sisi wenyewe tunaharibiana. Yani mtz akiingia kazini ukiwa umempa ajira plan yake ni kutafuta namna akuibie. Hajali hasara unayopata. Unamwajiri mtu famasi, kumbe anakuja na dawa zake ndizo anauza wewe unashangaa hakuna mauzo. Kazi yako kumpa mshahara na kulipia fremu lakini kumbe yeye anauza dawa zake.
 
haha dah.

na wewe waliyekufungia siku wakipata mteja mpya wanasitisha signals wanampa mwingine.
tabia za watz zimelaaniwa
 
Ndicho nilichokuwa najaribu kueleza.
Thanka for clarification.
 
Uwezo wa Watz wengi kichwani upo vizuri wakibishana kuhusu Mpira na habari za Mbususu tu.
 
Sasa gharama ya hiyo MGAS na mtungi wa gas ya kawaida utofauti wake 7ko wapi, kama mimi napika kila siku. Yaani nina familia ??
 
Ni huduma nzuri mnoo ya kisasa, inaondoa kazi ya kubebana na mitungi na unanunua muda wowote hata usiku wa manane
Gesi kwenye mtungi ikiisha kama inavyoisha mitungi ya kawaida unafanyaje?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…