Maafa Kariakoo: Usichangishe fedha tumia akaunti ya Serikali

Maafa Kariakoo: Usichangishe fedha tumia akaunti ya Serikali

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Serikali kupitia Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu, Dkt Jim James Yonazi ametoa akaunti maalum ya Serikali ambayo Watanzania wataitumia ili kutuma fedha kwa ajili ya kuwachangia waliopata maafa Kariakoo.

Jina la Akaunti
National Relief Fund

Namba ya Akaunti
9921159801

Pia, Soma: Live Updates Kuporomoka kwa Ghorofa Kariakoo Nov 16: Watu 7 wengine waokolewa


Misaada kwa ajili ya waathirika wa kuporomoka kwa jengo Kariakoo itolewe kwenye akaunti moja- Dkt. Yonazi

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge na Uratibu Dkt. Jim Yonazi amesema msaada wa kifedha kwa ajili ya kusaidia walioathirika na kuporomoka kwa jengo la ghorofa Kariakoo Jijini Dar es Salaam unatolewa kwa akaunti maalum ya maafa ya 9921159801 ambayo ipo Benki Kuu ya Tanzania na kushughulikiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu.

Dkt. Yonazi ameyasema hayo leo Novemba 18, 2024 wakati akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusu hali inayoendelea katika zoezi la uokoaji.

Amesema akaunti hiyo ni pekee nchini ambayo inakusanya misaada ya kifedha kwa ajili ya maafa.

"Kuna watu wana nia njema kabisa ya kuwasaidia Watanzania, lakini naomba tujizuie kabisa kukusanya michango ya kifedha kutoka kwa mtu yeyote bila kupitia akaunti hii". Amesema Dkt. Yonazi.

Aidha amesema akaunti hiyo ni maalumu imethibitishwa na serikali ili kuweza kuhakikisha misaada inawafikia walengwa na inatimiza malengo ya kutoa misaada hiyo.

Amesema kwa sasa operesheni inaendelea mpaka pale watakapokamilisha zoezi la kuokoa baadhi ya watu ambao bado hawajaokolewa.
IMG-20241118-WA0009.jpg
IMG-20241118-WA0008.jpg
IMG-20241118-WA0007.jpg
IMG-20241118-WA0005.jpg
 
Serikali kupitia Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge na Uratibu, Dkt Jim James Yonazi ametoa akaunti maalum ya Serikali ambayo Watanzania wataitumia ili kutuma fedha kwa ajili ya kuwachangia waliopata maafa Kariakoo.

Jina la Akaunti
National Relief Fund

Namba ya Akaunti
9921159801

Pia, Soma: Live Updates Kuporomoka kwa Ghorofa Kariakoo Nov 16: Watu 7 wengine waokolewa

Walipa kodi, fedha zao zinapangwa bajeti kwa waziri mkuu kwenye mfuko wa maafa, hivyo watanzania wote wanaolipa kodi wameshiriki kwenye maokozi ya Kariakoo, huo mfuko kama hauna fedha bajeti ya dharura ya serikali ipitishwe,tupo tayari na tunaunga mkono!

#Kuchangisha nje ya hapo ni wizi, ufisadi na siasa ju ya damu za marehemu na manusura[hakuna mhanga na msiwaite wahanga, hawakukimbilia kutaka kufunikwa ila imewakuta, wahanga ni waislamu wapalestina wanaojilipua mabomu ili wafe na wengine]
 
Serikali kupitia Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge na Uratibu, Dkt Jim James Yonazi ametoa akaunti maalum ya Serikali ambayo Watanzania wataitumia ili kutuma fedha kwa ajili ya kuwachangia waliopata maafa Kariakoo.

Jina la Akaunti
National Relief Fund

Namba ya Akaunti
9921159801

Pia, Soma: Live Updates Kuporomoka kwa Ghorofa Kariakoo Nov 16: Watu 7 wengine waokolewa

Iliziende kwenye mfuko wa ccm kumbafu zao, mbona kuna pesa nyingi ccm wanazigawa tu mtaani pikipiki mpya zinamwagwa kila wilaya kwa maelfu sasa kwanini wasitoe pesa kuwasaidia hao watu
 
Serikali kupitia Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge na Uratibu, Dkt Jim James Yonazi ametoa akaunti maalum ya Serikali ambayo Watanzania wataitumia ili kutuma fedha kwa ajili ya kuwachangia waliopata maafa Kariakoo.

Jina la Akaunti
National Relief Fund

Namba ya Akaunti
9921159801

Pia, Soma: Live Updates Kuporomoka kwa Ghorofa Kariakoo Nov 16: Watu 7 wengine waokolewa

Huu ni wizi wa waziwazi kabisa, wanataka kulitumia janga hili katika kujiongezea vipato haramu vya ziada. Je, fedha za bajeti ya maafa zinafanya kazi gani? Kwa nini wasichote huko na kuzitumia katika janga hili?
Kama bajeti ya maafa haipo, Je, kwa nini wasipitishe bajeti ya dharula ili kupata fedha za kuhudumia kwenye janga hili!

Je, Serikali inataka kuligeuza janga hili kama chanzo cha mapato kama ilivyokuwa kwa janga la tetemeko la Ardhi kule Bukoba????
 
Serikali kupitia Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge na Uratibu, Dkt Jim James Yonazi ametoa akaunti maalum ya Serikali ambayo Watanzania wataitumia ili kutuma fedha kwa ajili ya kuwachangia waliopata maafa Kariakoo.

Jina la Akaunti
National Relief Fund

Namba ya Akaunti
9921159801

Pia, Soma: Live Updates Kuporomoka kwa Ghorofa Kariakoo Nov 16: Watu 7 wengine waokolewa

Aaah siwezi kuchangia fedha zangu huko..
Bora nichangie kwa wanaochangisha walau hata wakila nitaona walichopeleka
 
Pesa za kodi na mikopo mnazovimbishia matumbo yenu hazitoshi bado mnataka kufisadia kidogo kilichobakia mikononi mwa raia!! Kwendeni zenu hii serikali ina pesa za kusaidia waathirika bila kupitisha kapu kwa raia. Nyie si ndio mlitoa dola bilioni kwa Uturuki mwaka jana? Inakuwaje mnashindwa kutenga bilioni kwa waathirika ambao pia walipa kodi!!
 
Yaani Kuna watu wanajua kukamatia fursa. Huyu alikuwa Dodoma kufungua duka lake lakini naona kaacha karukia kuchangisha. Na watanzania kama makenge wanatoa TU..
Hivi si tunatoa Kodi na tuna mfuko wa maafa au kamati ya maafa ambayo obvious ina fungu la maafa?????? Michango ni sawa kama ni large scale maafa lakini kwa Ghorofa Moja!!?? Serikali Haina kama 1B ya kushighulikia hili.. yaani marehemu na majeruhi na wasaidiaji wa uokozi????

Wajanja Sasa wanatumia fursa kutunisha mifuko yao. Kumbav
 
Mtanzania yeyote yule usichange, kuna bajeti ya maafa. Huwa hawasemi ina kiasi gani, inatumika vipi. Leo watu wachangie nini tena? Hizo pesa wanazitaka kuzipeleka ccm, kwaajili ya kuzichezea kwenye uchaguzi. Raisi kasema kila kitu watagharamia, kwahiyo wanategemea pesa za Wananchi?

Wamechelewa sana, uzuri Kariakoo, kuna magroup ya kuchangiana na hiyo kazi imeshaanza. Hizo pesa zitafika kwa wahusika, maana ni kama familia. Unayetoa huko serikalini wape kwa mapenzi yako.
 
Sidhani kama alimaanisha serikali haina pesa,bali nimeona kuna watu binafsi wanahamasisha watu wachange na wameweka acc zao binafsi kwa umaarufu wao watu wengi wamechanga,Nadhani ili kuepusha sintofaham za watu kudhulumiwa ni bora hzo pesa zikusanywe na serikali kama kuna watu wataguswa.
 
Hata hili wanachangiana kmmk hiyo nchi inatumia kiasi gani kwenye maanasa ya ajabu? Nachukia hilo li nchi basi tu, hayo magharama anayotumia bikizee kule brazil yasingetosha, bongo ni upuuzi sana.
Wangefupisha tu safari na matumizi ya siku moja huo msafar....wangemjengea na jengo lililoporomoka
 
Za maafa zimepigwa zamani naona
Wameamua kuchangisha upya bila aibu
Sasa hawa wamekuwa kama wanaozunguka au kuomba za rambirambi
Mpaka serikali inaomba michango
 
Back
Top Bottom