Sikirimimimasikini
JF-Expert Member
- Dec 27, 2019
- 2,926
- 15,634
Wanaintelijensia wa Marekani wamesema kuwa Russia inatumia silaha za ajabu nchini Ukraine.
Wanainteligensia hao wamebaini kuwa makombora ya balistiki (Iskandar-M short range ballistic missiles) yanayovurumishwa na majeshi ya Russia nchini Ukraine yameongezewa vionjo au vikorombwezo fulani vipya, tofauti na hapo zamani yalivyozoeleka.
Vikorombwezo hivyo vigeni, hutolewa na makombora hayo pale yanapotambua yametagetiwa na mifumo ya ulinzi wa anga wa adui. Vikorombwezo hivyo huzivuruga rada za mifumo ya ulinzi wa anga ya jeshi la Ukraine (air defense systems), na pia huyachanganya makombora yanayotumwa (na Ukraine) kudungua silaha hizo.
Vikorombwezo hivyo vipya ndivyo vinavyopelekea mifumo ya ulinzi wa anga ya jeshi la Ukraine na silaha za kulinda anga hilo kushindwa kuyadungua makombora ya Russia.
======
Wanainteligensia hao wamebaini kuwa makombora ya balistiki (Iskandar-M short range ballistic missiles) yanayovurumishwa na majeshi ya Russia nchini Ukraine yameongezewa vionjo au vikorombwezo fulani vipya, tofauti na hapo zamani yalivyozoeleka.
Vikorombwezo hivyo vigeni, hutolewa na makombora hayo pale yanapotambua yametagetiwa na mifumo ya ulinzi wa anga wa adui. Vikorombwezo hivyo huzivuruga rada za mifumo ya ulinzi wa anga ya jeshi la Ukraine (air defense systems), na pia huyachanganya makombora yanayotumwa (na Ukraine) kudungua silaha hizo.
Vikorombwezo hivyo vipya ndivyo vinavyopelekea mifumo ya ulinzi wa anga ya jeshi la Ukraine na silaha za kulinda anga hilo kushindwa kuyadungua makombora ya Russia.
======