Maagizo ya machinga na Corona kupuuzwa nini chanzo? Ni kivuli cha Magufuli?

Maagizo ya machinga na Corona kupuuzwa nini chanzo? Ni kivuli cha Magufuli?

Elitwege

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2017
Posts
5,294
Reaction score
10,970
Tulishuhudia mkuu wa mkoa wa Dar Bw. Amos Makala alipoapishwa tu alitoka mbio mbio kwenda kutangaza oparation ya kuondoa machinga na ombaomba wote ili jiji lirudi kwenye hadhi yake ya usafi, lakini mpaka leo agizo hilo halijatekelezwa.

Makala alifanya mpaka kikao na wakuu wa wilaya, madiwani na wenyeviti wa mitaa kuwapa maagizo ili kuwezesha kuwatoa wamachinga, mpaka magari yalianza kupita mitaani yakitangaza wamachinga wote waondoke lakini mpaka leo kimya shughuli zinaendelea kama kawaida.

Haikupita muda kamati ya Corona iliyoundwa na rais Samia ikaja na mapendekezo ya kuwataka wanachi wote kuvaa barakoa na kufanya social distance, pia walimtaka waziri wa afya atangaze idadi ya wagonjwa wa corona wanaopatikana kila siku ,pia wiki mbili baadae chama cha madaktari Tanzania kikatoa tamko la kuwataka watanzania kuepuka mikusanyiko, kunawa mikono na kuvaa barakoa muda wote.

Freeman Mbowe na Chadema pia mapema kabisa alitangaza kuwa yeye amechanjwa na kuwataka watanzania kuvaa barakoa na kujiandaa kupokea chanjo, maagizo yote hayo yamepuuzwa na wananchi mpaka sasa.

Pita sabasaba, kwenye mwendokasi, Kariakoo wananchi wanaendelea na maisha yao kama kawaida kana kwamba kamati ya Corona na chama cha madaktari hawajatoa tamko lolote!

Chanzo cha maagizo haya kupuuzwa nini? Je, ni Kauli za Magufuli bado zinaendelea kuishi kwenye ubongo wa watu?

Baadhi ya wananchi wamehojiwa kuhusu maagizo hayo wamesema maagizo hayo hayana tija yoyote zaidi ya kutafuta namna ya kuwatia hofu watu.
 
Shujaa amelala lakini ametuachia mashujaa aliowanoa. Chuma JPM alinoa chuma SSH.

Mtu akimwangalia SSH kwa mtazamo kwamba ni mwanamke na kwamba ni dhaifu anajikosea na anajidanganya sana

Ni makosa kumlinganisha JPM na SSH lakini ukweli ni kwamba Tanzania bado iko kwenye mikono salama ya mama wa taifa.

Rais John Pombe Magufuli atabaki kuwa rais shujaa wa karne hii

 
Rais SSH amewajengea hofu viongozi wa mikoa na wilaya baada ya kuwatumbua DC na mkurugenzi wake pale Morogoro mjini. Mama anajipendekeza kwa machinga na bodaboda ili 2025 wampigie debe.

Na kuhusu korona mzimu wa Magufuli juu ya kuhimiza watu watumie njia za kishirikina za kujifukiza bado upo. Na kwa kuwa watanzania wengi ni wajinga na ni washirikina itakuwa ngumu kuchukua tahadhari.

Labda mama atumie mbinu ya Durtete, mtu asiyetaka kuvaa barakoa na chanjo jela.
 
Kuna haja serikali kutumia nguvu kidogo ili kufanya wananchi waelewe umuhimu wa kutii maagizo na kujikinga dhidi ya maambukizo ya Corona.

Hakuna kivuli cha Mwendazake wala nini; ni ujinga tu!
 
Kwa upande wa issue ya Corona late Magufuri alifanya maamuzi magumu sana.

Kuna watu hapa ni bendera fuata upepo, sababu kuna anayempinga fulani naye anafuata nyayo ukimuuliza kwa nini?.
Hana jibu la msingi.
 
Mkuu unaishi wapi?

Kariakoo machinga wote wamevunjiwa, wameekewa limit usawa wa kiuno bidhaa zao zisizidi hapo, wanaruhusiwa tu kuweka bidhaa kwa kuzitandaza.

Hii ni hekima iliotumika kuwaacha Hali ya kuwa hawazibi maduka.
 
"..Ni ujinga kuchanjwa chanjo isiyojulikana dhidi ya ugonjwa usiojulikana..." ni maneno ya mkazi wa jiji la Moscow nchini Urusi, nchi iliyotengeneza chanjo yake yenyewe ila wananchi hawana imani kabisa na chanjo hiyo, pamoja na uwepo wa chanjo ni 15% tu ya wakazi wa Moscow waliopewa chanjo!
Chanzo: France 24 tv
 
Mkuu unaishi wapi?

Kariakoo machinga wote wamevunjiwa, wameekewa limit usawa wa kiuno bidhaa zao zisizidi hapo, wanaruhusiwa tu kuweka bidhaa kwa kuzitandaza.

Hii ni hekima iliotumika kuwaacha Hali ya kuwa hawazibi maduka.
ndicho kinajadiliwa hapa,tamko lilikuwa waondoke.

kwani unadhani hoja ni wao kuziba biashara au kuuza bila kulipa kodi,na kunyima wateja wenye frem rasmi!!!!
 
Imani ipi?
Tanzania ni nchi tajiri!, Wazungu sio wajomba zetu hadi tupewe misaada bure, ukiona mpinzani wako anakupongeza ujue umeishaharibu tayari (kama kadema wanavyompongeza Bi Mkubwa)....
 
Kwa sasa mazgizo ya korona ni kuwarizisha mabeberu.....!
 
Aisee kuwatoa machinga inabd uwe na roho ngumu kinyama , hayupo mwenye roho hyo , Maghufuli angetamka chap kidog wanasepa jamaa alikuwa na roho nzito sana
 
Back
Top Bottom