Maajabu 10 ya "Aje" ya Alikiba na miujiza yake

Maajabu 10 ya "Aje" ya Alikiba na miujiza yake

AdvocateFi

JF-Expert Member
Joined
Jan 15, 2012
Posts
11,492
Reaction score
5,047
Wasalaam!
Takribani ni miezi 4 kama si mitano kabisa tangu msanii wa label ya Sony music international "Alikiba" (KingKiba) kuachia official release ya wimbo wa "AJE" ambao kiukwel trend ya wimbo huu ilianza wiki chache kabla ya kuja kuvuja katika mitandao ya kijamii ikiwa kama demo hadi badae official release ya original version ambayo ilikuja kuachiwa kama exclusively song kwenye kituo cha kimataifa cha runinga "Mtvbase Africa, Soundcity na badae traceUrban tv ambapo ukiwa ndiyo wimbo wa kwanza kuachiwa na Alikiba akiwa chini ya mkataba mpya wa Sony international music.

Bila shaka wimbo huu wa "Aje" ni wimbo uliofanikiwa zaidi kuliko nyimbo zote kwa hapa East Africa tangu mwaka umeanza na huenda wimbo unaoweza kuja kufikia angalau robo ya ukubwa wa Aje pengine usiwe wimbo mwingine wowote zaidi ya "Ajeremix" itakayoenda kuachiwa kama bonus track kabla ya mwaka haujaisha.

Katika mada yetu leo hii nitajikita zaidi katika kuelezea maajabu 10 na miujiza ya wimbo huu "Aje" na factors zinazosadifu ukubwa wa wimbo huu East Africa na Africa nzima kwa ujumla, kama ifuatavyo.

1.Aje imekuwa no# 1 kwa kuuzwa katika mtandao wa ITunes upande wa Kenya katika list ta nyimbo 100, za mastaa wakubwa dunian ([HASHTAG]#Aje[/HASHTAG] No1 in Top 100 ITunes kenya).

2.Aje imekuwa no#2 Kununuliwa katika mtandao wa Itunes nchini Oman katika Top100 itunes oman

3.Aje imekuwa no# 1 kununuliwa piwa (Downloads) kwenye mtandao mkubwa wa kuuza nyimbo Africa wa "Diezer" ambapo tangu mwaka umeanza hakuna wimbo wowote kutoka east Africa uliweza kuweka rekodi hiyo.

4.Aje imekuwa no# 1 katika cha charts za East Africa top 10 za kituo cha kimataifa cha Nigeria "Soundcity" kwa week 2 mfululizo

5. [HASHTAG]#AJe[/HASHTAG] imekuwa no#1 kwenye mtandao wa Mkito.com kwa kupakuliwa (Downloads) katika nyimbo zilizodownload kuanzia mwezi may had sasa.

6.[HASHTAG]#Aje[/HASHTAG] imempa Alikiba tuzo za African oscar awards za Nigeria kama wimbo bora wa mwaka(Song of the year) na msanii bora wa mwaka (Artist of the year)

7. Aje imempa alikiba nominations ktk category zaidi ya 13 kutoka katika tuzo mbalimbali za kimataifa mpka sasa.

8.Aje Ilishika nafasi ya 2 kwenye African Top 10 za trace urban tv.

9. Aje imeshika no 5 katika charts za 30 urban hits za trace urban.

10.Aje imemuingizia Alikiba zaidi ya million 800 kwa muda wa miezi minne kupitia mauzo ya mitandaoni , ufunguzi wa endorsements na show kubwa alizoitwa ambapo vyote hivyo vimevutwa na mzimu wa Aje.

Lastly. Aje imeendelea kumfanya Alikiba kama miongoni mwa wasanii hot na threat kwa sasa Africa na bila shaka Aje ndiyo iliyompa Alikiba shavu la kwenda kuperfom Mtvamama awards na pia Aje ndiyo itakayompa Alikiba nominations ya tuzo hizo zitakakazofanyika October 22 mwaka huu.

Itaendelea....
 
Wanakuja wale wa kambi nyingine
 
Hiyo namba 10 Ina mana sasa Kiba Ni bilionea siyo? Na kama Ni hivyo basi awe anaishi kwake na sio kwenye nyumba ya kupanga, bilionea kupanga nyumba ya kodi ya laki 5 kwa mwezi Ni majangazi

Alikiba si mtu wa show off, kwa taarifa tu, December mwishon atakamilisha ujenzi wa ghorofa yake tabata,
 
Hiyo namba 10 Ina mana sasa Kiba Ni bilionea siyo? Na kama Ni hivyo basi awe anaishi kwake na sio kwenye nyumba ya kupanga, bilionea kupanga nyumba ya kodi ya laki 5 kwa mwezi Ni majangazi
Hii yako itakuwa ni namba 10(a)
 
Aje ni bonge la kopo.

Halafu yule Mnaija M.I aliyezinguliwa na demu wa kibongo mpaka anajifunza kusema "sawasawa mambo veepee?" huku anachukua digits na location za Google Map ameupendezesha sana ule wimbo mpaka nikatafuta album yake. Jamaa naye ni mzuri anajua kupangilia lyrics na ku flow.

 
Hebu ielezee vzr namba 10, manake usije ukawa unampaka mafuta kwa mgongo wa chupa mwenzio
 
Alikiba kenya alimuharibia mondi hadi leo mitandaoni mameneja wake wanaandika taarabu
 
Aje ni bonge la kopo.

Halafu yule Mnaija M.I aliyezinguliwa na demu wa kibongo mpaka anajifunza kusema "sawasawa mambo veepee?" huku anachukua digits na location za Google Map ameupendezesha sana ule wimbo mpaka nikatafuta album yake. Jamaa naye ni mzuri anajua kupangilia lyrics na ku flow.

Hiyo ni demo ya Aje remix ambayo ilivuja, tutaitoa tayar video tushafanya na directors wawili wakubwa Africa "mejialabi na justine Campos
 
Hopes zinajenga lakini, mimi ni fan wa kiba zaidi, though nasimama kama mtanzania, yoyote kwa wakatati wowote akipeperusha bendera atapata support yangu
 
Hopes zinajenga lakini, mimi ni fan wa kiba zaidi, though nasimama kama mtanzania, yoyote kwa wakatati wowote akipeperusha bendera atapata support yangu

Asante mkuu kwa hekima iliyotukuka
 
Back
Top Bottom