Maajabu 8 ya mkoa wa Mara

Ila ukeketaji ndio jambo linalotia doa mkoa huu, cha ajabu zaidi, huko mara mwanamke anaweza kumuoa mwanamke mwenzie, wanaita "Nyumba Ntobhu'.
Ila elewa hii sio ndoa ya ushoga, hii ni mira tu ya mwanamke kumchumbia na kumtolea mahari mwanamke mwenzie ili aweze kumliki na kumletea uzao( yani ukiolewa nyumba ntobhu huyo mwanamke alie kuoa atakuchagulia ama kukuruhusu kuwa na mahusiano na mwanaume flani ili uweze kupata ujauzito na watoto watakao zaliwa wataesabika niwa huyo mwanamke alie kuoa na sio wa mwanaume aliekupa ujauzito) hii ufanywa na wamama wasio weza kuzaa ama umri wa kuzaa umepita na wanaitaji mtoto wa kurithi mali zao na majina yao
 
Kuna Kijiji kinaitwa Rung'abure daah nilikaa pale Kuna wababe serikali imeshindwa kujenga hata kituo Cha polisi pale.​
Huwa hawachelewi kukatana mapanga pale. maduka mengi yamejaa mapanga wanauza sana​
 
Hayo makabila yoote uliyoorodhesha ni makabila mawili tuu ambayo ni ya kikurya yanayoongea mura na makabila ya kijita wa chasugu.
 
Hizo ni koo sio makabila.
 
Tohara bila ganzi. Kama ka ngozi kakibanwa na zipu tuu ni msala. Sasa unapata picha ngozi yote inakatwa bila ganzi,, pah ngozi hamna unatulia
 
Hayo makabila yoote uliyoorodhesha ni makabila mawili tuu ambayo ni ya kikurya yanayoongea mura na makabila ya kijita wa chasugu.
Nimeongelea kuhusu lahaja, rejea kusoma
 
Wajaruo,washashi mbona hujawataja kwenye makabira
 
Ila ukeketaji ndio jambo linalotia doa mkoa huu, cha ajabu zaidi, huko mara mwanamke anaweza kumuoa mwanamke mwenzie, wanaita "Nyumba Ntobhu'.
Idadi ya jamii zinazokeketa ni kubwa kuliko jamii zisizokeketa! Fanya utafiti utabaki mdomo wazi..
 
Wajaruo,washashi mbona hujawataja kwenye makabira
Neno Washashi ni maarufu sana kwa "Wasukuma", kuhusu Waluo nimewataja na hilo neno "Warujuo" halipo katika lugha ya Kiswahili ila ni namna ambavyo watu wamezoea kuwaita hiyo. Waluo watakuja kuelezea mengi zaidi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…