Maajabu haya: Shaka asema Ajira zaidi ya milioni 35 zimezaliwa miezi sita ya Rais Samia

Ajira mnaitafsiri vipi?

Halmashauri nilipo imetoa mikopo ya pikipiki 20 kwa wanavikundi 20 ndani ya miezi hii minne.

Kifupi tayari serikali imetoa ajira kwa hao wanavikundi 20 kwa halmashauri moja.

Vikundi vingine pia vimepewa pesa kulingana shughuli zao kama mafundi seremala, mafundi kushona,wafyatua tofari n.k.

Hizi zote ni ajira. Lakini tatizo letu tuamini ajira ni nafasi za kuwa katika ofisi fulani tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Inategemeana na tafsiri yake, ila kama mpaka wapiga debe amewajumlisha humo basi hakuna shida.
Unaweza kuwa na mwili mkubwa kama tembo lakini ukawa na akili ndogo kama sisimizi.
 
Mil.3.5 na sio mil.35
 
Majaliwa alisema asilimia 24 ya watanzania wana ajira,huyu Shaka anaibuka na haya ya milioni 3.5 waliopata ajira ndani ya kipindi hiki cha Samia Suluhu. Siku ukianza kuona unawaamini CCM ujue siku zako za kuishi duniani zinakaribia.
 
Mil.3.5 na sio mil.35
"Katika kipindi kifupi cha mheshimiwa Rais Samia uwekezaji mkubwa Tanzania umefanyika wa dola bilioni 3.5 ambapo kwa haraka haraka ajira zaidi ya milioni 35 zimekwenda kuzaliwa, sasa hiyo ni miezi sita. Mheshimiwa Rais endelea kuupiga mwingi, kiwanja umekidhibiti vizuri una baraka zote za chama"

Shaka
 
Zitakwenda au zimekwenda kuzalishwa?

Dola bil.3.5 ni sawasawa na Tilioni 7 ambazo zinaweza kweli kuzalisha wastani wa ajira zaidi ya mil.3.5 sio mil.35..
 
Zile standard zilikuwa za juu mno. Ukizirukia vibaya unavunja kiuno!!!
 
Alafu tunajiuliza kwann Tz ni maskini daah[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Duuh[emoji1787][emoji1787]

Jokes aside... hivi viwanda viliishia wapi?
 
Usimuamini mtu wa jinsia ya tatu kamwe

Sent from my Nokia 5.1 Plus using JamiiForums mobile app
 
Wakti Bw. Lameck anasema watu 7 kati ya 100 ndo wenye ajira tena rasmi, mwache huyo nna mashaka nae, au unesahau ya bw. Haraka haraka enzi za mwendazake

Sent using Jamii Forums mobile app
 
ACHA KUPOTOSHA PITIA HII
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…