Uchaguzi 2020 Maajabu hayataisha Tanzania, pamoja na yote haya wananchi wataichagua CCM

Uchaguzi 2020 Maajabu hayataisha Tanzania, pamoja na yote haya wananchi wataichagua CCM

Mwamuzi wa Tanzania

JF-Expert Member
Joined
Apr 7, 2020
Posts
15,486
Reaction score
45,256
Habari wakuu!
Kwa umri wangu mdogo wa miaka takribani 30 nimejifunza mengi, sijabahatika kuvuka mipaka ya Tanzania lakini nimefika karibu mikoa 20 ya Tanzania bara.

Hulka na silka za Watanzania zinafanana.

Kwa uelewa wangu wa mambo ya kisiasa niliojifunza mitaani na mitandaoni nimehitimisha kuwa CCM inauwezo wa kushinda kwenye sanduku la kupigia kura kwa miaka 15 mbele. Yaani 2020, 2025 na 2030 watashinda kwa damu baada ya mtifuano utakaopelekea ccm kushinda kwa asilimia za single digit na hapo ndio utakuwa mwisho wa CCM kupata ushindi kwa miaka ya hivi karibuni. Kwa nini ninasema CCM watashinda ndani ya miaka 15 ijayo?

Wananchi wa Tanzania ndani ya hii miaka 15 bado wengi watakuwa hawajapata elimu ya msingi( namaanisha form 4), pili kizazi cha Nyerere (watu watii na wavumilivu) kitaendelea kuwepo kwa idadi kubwa ndani ya hii miaka 15.

Naamini ujinga na upumbavu unaowapelekea watanzania kusahau mambo haraka bado vinahitaji miaka si chini ya 15 kufutika.

Rushwa na takrima Tanzania bado changamoto, mtu anaweza kuuza kura yake kwa elfu 20 tu na kubadili uamuzi. Chama tawala ndicho chenye nguvu ya kifedha.

Ninaamini CCM October 2020 watapata kura nyingi za halali licha ya ;

- Watumishi wa umma kutopanda mshahara tangu 2015.
- Sarafu ya Tanzania kushuka kwa miaka hii 5.
-Bei za bidhaa mbalimbali kupanda.
-Uvunjaji holela wa katiba
-Ukosefu wa ajira kwa vijana, ikumbukwe ajira ni haki ya kijana pamoja na kwamba haijaandikwa kwenye katiba.
-Kupanda kwa gharama za matibabu(huduma za afya).

Asanteni.
 
Kweli mkuu, wengi wa watanzania ni waoga, lakini ni kwa sababu bado hali ngumu hatujaipata ya kutufanya tuwe na maamuzi magumu.

Ila ukitokea watu wakashindwa kupata mahitaji ya msingi itakuwa rahisi kuweza kuondoa uoga. maana unakuwa huna chuguo la sivyo ufe.
Sasa ni bora kufa unajipigania kuliko kufa kikondoo.
 
Hakuna km Ccm Tanzania na wala hakuna wakuitoa Ccm madarakani kwa miaka mingi ijayo

Ccm ni urithi wa Watanzania, hatuwezi kumvunjia heshima Nyerere
 
Hao CCM mnawapa sifa zisizo stahili.wenye ccm wenyewe wanajua ccm haijawahi kushinda uchaguzi wa rais na wabunge wengi kwa chaguzi kadhaa na ndiyo sababu hawawezi kukubaliana na wazo la tume huru ya uchaguzi wala katiba mpya.nikuunga mkono kwamba after 15 years wajinga watakuwa wameisha nchi hii na hivyo watanzania wataweza kuamua wenyewe juu ya tume huru na katiba mpya badala ya kusubiri mwenyekiti wa ccm ndiye awaamulie
 
Hakuna mtu anaichaguaga ccm mkuu....wameshatangaza vita ya kushinda kwa goli la mkono, kuwatisha wakurugenzi watakaotangaza wapinzani, na kutumia dola kubaki madarakani......
 
Tofautisha wananchi kuichagua ccm, na tume ya uchaguzi kutumika kuwatangaza wanaccm kuwa washindi wa uchaguzi.
Tume ya uchaguzi mpaka itangaze matokeo lazima mawakala wa vyama vilivyoweka wagombea laziman wasaini form za matokeo. Jimboni lazima mgombea nae asaini. Mpaka ngazi ya taifa. Sasa hilo la kusema tume inatangaza inavyotaka. Hao mawakala wanakuwa wapi? Kwa nini wanasaini?
 
Tume ya uchaguzi mpaka itangaze matokeo lazima mawakala wa vyama vilivyoweka wagombea laziman wasaini form za matokeo. Jimboni lazima mgombea nae asaini. Mpaka ngazi ya taifa. Sasa hilo la kusema tume inatangaza inavyotaka. Hao mawakala wanakuwa wapi? Kwa nini wanasaini?

Mawakala sasa hivi wanapigwa sana na green guard kwa uratibu wa jeshi la polisi. Ili wakala wa upinzani abaki salama ni lazima akubali kusaini matokeo ya kubumba. Hili silisemi kwa bahati mbaya, maana ni maagizo kabisa toka juu. Kama wamefikia mahali mbunge anahama chama, kisha anaitwa aendelee na bunge,ndio itakuwa hiyo tume?
 
Mawakala sasa hivi wanapigwa sana na green guard kwa uratibu wa jeshi la polisi. Ili wakala wa upinzani abaki salama ni lazima akubali kusaini matokeo ya kubumba. Hili silisemi kwa bahati mbaya, maana ni maagizo kabisa toka juu. Kama wamefikia mahali mbunge anahama chama, kisha anaitwa aendelee na bunge,ndio itakuwa hiyo tume?
Acha nicheke tu.
 
Back
Top Bottom