Cesar Saint
JF-Expert Member
- Nov 18, 2016
- 423
- 726
Leo nikiwa maeneo fulani nikiwa nafuatilia mchezo wa CHAN kati ya Tanzania na Sudan nikawa napata story fupi ya mpira yenye kusisimua kuhusu mchezaji wa zamani wa Yanga marehemu mzee SAID NASSOR MWAMBA KIZOTA .
Unaambiwa ilikuwa mwaka 1993 ndio mwaka ambao fundi huyu aliwapa burudani mashabiki wa Yanga na kumfanya kuwa kipenzi cha mashabiki wa timu hiyo.
Basi kipindi hicho Yanga ikiwa inajiandaa kuvaana na Sport Club Villa ya Uganda katika fainali ya klabu bingwa afrika mashariki na kati mjini Kampala Uganda.
Timu ilikuwa imeshaondoka na kutangulia nchini Uganda jamaa alikuwa anaendelea na mishe zake akiwa na tuhuma za kupiga ulabu alipokuwa kambini basi akawa amepoa kwa dada yake maeneo ya mwembe yanga aitwaje White Mama (jina maarufu)
Basi watu wa Yanga baada ya kujishauri muda mrefu wakamfuata na kumchukua mahali hapo na kumpeleka nchini Uganda kuamkia siku ya fainali.
Siku ilipofika jamaa bila kufanya mazoezi ya pamoja na timu akaingia mzigoni akaweka kamba mbili wavuni huku goli la tatu la Yanga likifungwa na Lunyamila hivyo kuifanya Yanga kutawazwa ubingwa mbele ya SC Villa nchini Uganda Kizota akarudi na ufungaji bora wa michuano hii na katika mwaka huo huo akabeba kiatu cha ufungaji bora ligi kuu ya Tanzania bara kipindi ikidhaminiwa na TBL.
Mechi kubwa iliyoacha historia kipindi hicho ni ilipowakutanisha watani wa jadi Kizota alipiga goli mbili huku moja ya goli maridhawa akimchambua na kumfanya atakavyo goli kipa mahili wa wakati huo Mohamed Mwameja .
Wakati mwengine fundi huyu alitupiwa virago na wana Jangwani kwa tuhuma za kuhujumu timu walipopokea kipigo cha 4-1 kutoka kwa Simba na Kizota akadondokea Simba
Kizota Vs Mmachinga
Mwaka 1995 ;Wakali hawa wa kufumania nyavu na kuchezea mpira walikutana katika Mbungi ya kkoo moto ulikuwa mkali pale ambapo Mmachinga alipopachika goli la kuwapa Yanga uongozi kipindi cha kwanza,wakati Yanga wakijua turubai limehamia kwa jirani Kizota anapiga goli maridadi la kusawazisha na kuwachanganya Yanga ambao kutahamaki wanapigwa kamba ya pili na Mchunga Bakari ‘Mandela’ kukamilisha hesabu ya 2-1 na mchezo kuishia hivyo.
YANGA WAMPIGIA MAGOTI
Yanga walitambua makosa yao na kumsotea Fundi huyu wa mpira na kwa vile alikuwa akiishi maeneo hayo ya mitaa ya Jangwani haikuwa kazi sana kumpata na kumvisha tena uzi wa watoto wa Jangwani kwa mara nyingine.
AKUTANA TENA NA SIMBA
Kizota anakutana tena na Simba mwaka 1996 na kushiriki katika matokeo ya sare ya maajabu jijini Arusha 4-4
Hahah kuna hili la kizota na waarabu jamaa alienda uarabuni na kupiga mpira wakina maradona jamaa wakamtaka hadi abadilishe uraia usifanye masihara moto anaouwasha mtu mpaka waarabu waelewe somo (hii ni stori nyingine)
Kizota pia amechezea timu ya taifa na kupata mafanikio ikiwemo challenge cup
Fundi huyu wa mpira alifariki dunia tar 11/02/2007 kwa ajali ya gari maeneo ya Veterinary akitokea kushuhudia mchezo wa marudiano, Kombe la Shirikisho la Soka Afrika, Raundi ya Awali kati ya wenyeji Simba dhidi ya Textil de Pungue ya Msumbiji ulioisha kwa Simba kutolewa kwa njia ya matuta 3-1 baada ya sare pacha ya 1-1 .
View attachment 1213794
Mungu ailaze mahala pema peponi roho ya fundi huyu wa mpira na wengine wengi waliotangulia mbele ya haki.
Timu alizopitia Kizota ni pamoja na Shirika la posta Tabora (wakiti huo ikijulikana kama Posta na Simu) ,Yanga,Simba,Al Nasar ya Oman na Al Jazeera ya uarabuni Abu Dhabi.
Hebu tupia hapa kisa chochote unachofahamu au kusikia kuhusiana na wachezaji wa zamani wa Tanzania kama Sunday Manara ‘Computer’ ,Zamoyoni Mogella ‘Golden Boy’ ,Maulid Dilunga ‘Mexico’Juma Pondamali ‘Mensa’ ,Omar Hussein ‘Keegan’, Mohamed Hussein ‘Mmachinga’ ,Ezekiel Greyson ‘Jujuman’ ,Ally Yusufu ‘Tigana’ ,Athuman China na wengine wengi
Unaambiwa ilikuwa mwaka 1993 ndio mwaka ambao fundi huyu aliwapa burudani mashabiki wa Yanga na kumfanya kuwa kipenzi cha mashabiki wa timu hiyo.
Basi kipindi hicho Yanga ikiwa inajiandaa kuvaana na Sport Club Villa ya Uganda katika fainali ya klabu bingwa afrika mashariki na kati mjini Kampala Uganda.
Timu ilikuwa imeshaondoka na kutangulia nchini Uganda jamaa alikuwa anaendelea na mishe zake akiwa na tuhuma za kupiga ulabu alipokuwa kambini basi akawa amepoa kwa dada yake maeneo ya mwembe yanga aitwaje White Mama (jina maarufu)
Basi watu wa Yanga baada ya kujishauri muda mrefu wakamfuata na kumchukua mahali hapo na kumpeleka nchini Uganda kuamkia siku ya fainali.
Siku ilipofika jamaa bila kufanya mazoezi ya pamoja na timu akaingia mzigoni akaweka kamba mbili wavuni huku goli la tatu la Yanga likifungwa na Lunyamila hivyo kuifanya Yanga kutawazwa ubingwa mbele ya SC Villa nchini Uganda Kizota akarudi na ufungaji bora wa michuano hii na katika mwaka huo huo akabeba kiatu cha ufungaji bora ligi kuu ya Tanzania bara kipindi ikidhaminiwa na TBL.
Mechi kubwa iliyoacha historia kipindi hicho ni ilipowakutanisha watani wa jadi Kizota alipiga goli mbili huku moja ya goli maridhawa akimchambua na kumfanya atakavyo goli kipa mahili wa wakati huo Mohamed Mwameja .
Wakati mwengine fundi huyu alitupiwa virago na wana Jangwani kwa tuhuma za kuhujumu timu walipopokea kipigo cha 4-1 kutoka kwa Simba na Kizota akadondokea Simba
Kizota Vs Mmachinga
Mwaka 1995 ;Wakali hawa wa kufumania nyavu na kuchezea mpira walikutana katika Mbungi ya kkoo moto ulikuwa mkali pale ambapo Mmachinga alipopachika goli la kuwapa Yanga uongozi kipindi cha kwanza,wakati Yanga wakijua turubai limehamia kwa jirani Kizota anapiga goli maridadi la kusawazisha na kuwachanganya Yanga ambao kutahamaki wanapigwa kamba ya pili na Mchunga Bakari ‘Mandela’ kukamilisha hesabu ya 2-1 na mchezo kuishia hivyo.
YANGA WAMPIGIA MAGOTI
Yanga walitambua makosa yao na kumsotea Fundi huyu wa mpira na kwa vile alikuwa akiishi maeneo hayo ya mitaa ya Jangwani haikuwa kazi sana kumpata na kumvisha tena uzi wa watoto wa Jangwani kwa mara nyingine.
AKUTANA TENA NA SIMBA
Kizota anakutana tena na Simba mwaka 1996 na kushiriki katika matokeo ya sare ya maajabu jijini Arusha 4-4
Hahah kuna hili la kizota na waarabu jamaa alienda uarabuni na kupiga mpira wakina maradona jamaa wakamtaka hadi abadilishe uraia usifanye masihara moto anaouwasha mtu mpaka waarabu waelewe somo (hii ni stori nyingine)
Kizota pia amechezea timu ya taifa na kupata mafanikio ikiwemo challenge cup
Fundi huyu wa mpira alifariki dunia tar 11/02/2007 kwa ajali ya gari maeneo ya Veterinary akitokea kushuhudia mchezo wa marudiano, Kombe la Shirikisho la Soka Afrika, Raundi ya Awali kati ya wenyeji Simba dhidi ya Textil de Pungue ya Msumbiji ulioisha kwa Simba kutolewa kwa njia ya matuta 3-1 baada ya sare pacha ya 1-1 .
View attachment 1213794
Mungu ailaze mahala pema peponi roho ya fundi huyu wa mpira na wengine wengi waliotangulia mbele ya haki.
Timu alizopitia Kizota ni pamoja na Shirika la posta Tabora (wakiti huo ikijulikana kama Posta na Simu) ,Yanga,Simba,Al Nasar ya Oman na Al Jazeera ya uarabuni Abu Dhabi.
Hebu tupia hapa kisa chochote unachofahamu au kusikia kuhusiana na wachezaji wa zamani wa Tanzania kama Sunday Manara ‘Computer’ ,Zamoyoni Mogella ‘Golden Boy’ ,Maulid Dilunga ‘Mexico’Juma Pondamali ‘Mensa’ ,Omar Hussein ‘Keegan’, Mohamed Hussein ‘Mmachinga’ ,Ezekiel Greyson ‘Jujuman’ ,Ally Yusufu ‘Tigana’ ,Athuman China na wengine wengi