Maajabu ya fundi wa mpira, Said Mwamba Kizota

Maajabu ya fundi wa mpira, Said Mwamba Kizota

Ukizungumzia lishe ni wazi kabisa picha ya marehemu Kizota zinaonyesha hakuwa na physical fitness kulinganisha na players wetu wa sasa .

Kwenye picha utaona mwili mkubwa ambao haujajengeka kabisa, no wonder inasemekana alikuwa anapiga sana pombe
Unaugua wewe, tena kichwani. Hicho chuma kimekulia kwenye moto, sio hawa wafuga makalio wanarukaruka wakigongwa mguuni wanatingisha vidole vya mkono.

Hivi unaweza kumlinganisha Kizota na Ajibu au Samata wewe? Kama ulikuwa mdogo, uliza uambiwe. Ule mfupa umejaa wewe...hatari!

Kwanza kwa taarifa yako, tangu hawa wabishi wastaafu soka, hakuna timu yeyote ya Tanzania iliyothubutu kukwea pipa na kombe. Ni huyu mume and company ndio waliandika historia ya kwenda kwenye ardhi ya watu wakakichafua na kumchukua mwali wakarudi naye katika ardhi ya Tanganyika. Na mambo haya yamefanywa na Yanga peke yake
 
Alifariki kwa kugongwa na gari katika eneo LA ndani ya kituo cha mafuta karibu na uwanja wa Taifa.
 
Unaugua wewe, tena kichwani. Hicho chuma kimekulia kwenye moto, sio hawa wafuga makalio wanarukaruka wakigongwa mguuni wanatingisha vidole vya mkono.

Hivi unaweza kumlinganisha Kizota na Ajibu au Samata wewe? Kama ulikuwa mdogo, uliza uambiwe. Ule mfupa umejaa wewe...hatari!

Kwanza kwa taarifa yako, tangu hawa wabishi wastaafu soka, hakuna timu yeyote ya Tanzania iliyothubutu kukwea pipa na kombe. Ni huyu mume and company ndio waliandika historia ya kwenda kwenye ardhi ya watu wakakichafua na kumchukua mwali wakarudi naye katika ardhi ya Tanganyika. Na mambo haya yamefanywa na Yanga peke yake

Una kichaa wewe.

Yaani unamlinganisha Samatta na huyo mlevi?

Samatta in terms of professionalism hana wa kushindana nae, ameutunza sana mwili wake, huwezimlinganisha na hao wanywa Chang’aa wenu wa zamani
 
Yaani mpira ulikuwa zamani huyu alikuwa anauwezo wa kuwa beki na kuwa mshambuliaji hatareee ,binafsi niliacha kushadadia,kubishana,na kuhudhuria uwanja wa taifa baada ya LUNYAMILA kustaafu mpira
Mchezaji aliyepunjwa sifa na HESHIMA .
 
Yaani mpira ulikuwa zamani huyu alikuwa anauwezo wa kuwa beki na kuwa mshambuliaji hatareee ,binafsi niliacha kushadadia,kubishana,na kuhudhuria uwanja wa taifa baada ya LUNYAMILA kustaafu mpira
wewe ni jau yaani mpira wa zamani wa kumpigia mtu magoti unauita mpira?
huyo hafiki ata robo ya uwezo wa Iddy nado.
 
Ukitazama maumbo ya Wachezaji wa zamani na wa Sasa hivi utagundua kuna Tatizo kubwa sana siku hizi
miili sio tatizo hata moringa mbona ana mwili mkubwa tu na anapigwa chenga na watoto wadogo kabisa
 
Sio tatizo mkuu , acheni kukariri.

Mifumo ya mpira imebadilika sana , sahizi mpira hauchezwi na Giants, mpira unachezwa na watu wenye maumbo madogo , haya Mapinduzi yalianza kufanyika Barcelona wakiifuata falsafa ya Cruyf..

Nenda England kaangalie Man city wanavyowasha Moto, angalia maumbo ya wachezaji kama Bernard Silva, sterling, Aguero, Gundogan n.k, wachezaji wadogo wadogo kiumbo ni ngumu kuwakaba na pili wana mbio balaa , hao MaGiant wenu wa zamani kwa mpira wa sahizi wangeweza kujiharishia uwanjani maana wangekimbizwa kwa kugongewa pasi kama 800 hivi fupi fupi mpaka wauone Moto.
mwili wa kizota ni wa wachezaji wa watford waliopigwa 8 juzi na city
 
Majina tu hayo uliyonitajia tu chini hapo mpaka mwili umenisisimka. Kipindi hicho tulikuwa kwenye dunia nyingine kuhusu soka. Kipindi hicho YANGA na simba zilikuwa zinajulikana Africa nzima. Zilikuwa na mashabiki kibao Uganda,Kenya na kwingineko Africa. MUNGU amrehemu SAID MWAMBA KIZOTA. Angalau nafarijika nikimuona LUNYAMILA
 
Una kichaa wewe.

Yaani unamlinganisha Samatta na huyo mlevi?

Samatta in terms of professionalism hana wa kushindana nae, ameutunza sana mwili wake, huwezimlinganisha na hao wanywa Chang’aa wenu wa zamani
Umri wako hauruhusu kujua misuli iliyokuwepo nchi hii. Hawa watoto laini wasingefanania kuwapeleka kushindana na watu kama kina George Semogerere. Mtafute mzee wako muulize jinsi ndimu ilivyopigwa zamani. Siku hizi ni promosheni tu zinawabeba watu, ni kama tu kwenye muziki.
 
Umri wako hauruhusu kujua misuli iliyokuwepo nchi hii. Hawa watoto laini wasingefanania kuwapeleka kushindana na watu kama kina George Semogerere. Mtafute mzee wako muulize jinsi ndimu ilivyopigwa zamani. Siku hizi ni promosheni tu zinawabeba watu, ni kama tu kwenye muziki.

Nimeangalia wengi wa vijana hawajui historia ya mpira wa Tanzania ila wanajua zakina Rud Gullit na Marco Van basten au hata wakina Paul Gascoigne Zico na wengine wengi.

Hii yote inatokana na ukosefu wa uwasilishaji wa historia hii unaona matukio kama Simba Day au wiki ya wananchi wako wanakimbizana na kuchangisha pesa na kutambulisha wachezaji wapya na kutozungumzia historia ya vilabu hivi na baadhi ya lulu zilizopita hapo.

Baadhi ya vijana wanafikiri kuweka kambi uturuki au South Africa ni jambo jipya kwa Simba na Yanga au National Team .

Mbaya zaidi hata vyombo vya habari na watangazaji wa habari za michezo unamsikia anakwambia huyu mchezaji kwa mfano Juma anacheza kama Zidane hivyo hadhira kuanza kumfuatilia zidane ili wamjue na kuwazima wakina Gagarino au Sekilojo chambua

Ni kweli zama zimebadilika na mpira umekuwa na kitabu kukubwa zaidi lakini hii haiondoi sifa au uwezo walikuwanao watu hawa kwenye soka na ni kuwakosea heshima unapopambanisha na vijana wa sasa kwani kila zama na watu wake .

Kizota si bora kuliko Samatta na Samatta si bora kuliko Kizota

Vijana wanasikia story za Juma Pondamali Mensa kutokana na kuendelea na shughuli za mpira mpaka hivi karibuni ikiwemo tukio lake la kumrudishia mpira fowadi wa timu pinzani Tanzania ikiongoza 1-0 tena ilikuwa na hawa hawa wasudani na kudaka tena mpira achilia mbali tukio lake la kudaka na kuficha mpira pale uwanja wa taifa lakini wakongwe watakuwekea mtu mwengine hatari hapo Idd Panzi Faza(walakini kwenye jina)

Au Jinsi Mohamed Hussein Mmachinga alivyokuwa anafanya matusi pale jangwani

Chibechibe chibindu hahah wana Yanga mpo!

Unamwona Nyoni wanasimba wanamkumbuka George Masatu au Victor costa Nyumba

Wapi Reli morogoro kiboko ya vigogo wakiwa na beki namba mbili hodari Peter Mkwela
 
Umri wako hauruhusu kujua misuli iliyokuwepo nchi hii. Hawa watoto laini wasingefanania kuwapeleka kushindana na watu kama kina George Semogerere. Mtafute mzee wako muulize jinsi ndimu ilivyopigwa zamani. Siku hizi ni promosheni tu zinawabeba watu, ni kama tu kwenye muziki.

Mzee

Picha za huyo Mlevi si ndio hizo hapo Juu?

Tunajua Old is Gold lakini muacheni kusifia hadi mkaanza kufanya kufuru.

Kama huyo mwenzako anayemlinganisha Samatta na huyo Kizota!
 
Nitajie timu kubwa ulaya iliyojaa Giants....

Ukinitajia kina VVD, nitakutajia kina firmino, keita,Mane, Salah , Xhaqiri na wengineo ambao sio Giants...

Every General rule has exceptions.
Wale wana miili mikubwa siyo kama wetu.Kuna jamaa alirushiwa jezi na Joe Hart aliivaa ikampwaya.jamaa anakaa kinondoni hapo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mzee

Picha za huyo Mlevi si ndio hizo hapo Juu?

Tunajua Old is Gold lakini muacheni kusifia hadi mkaanza kufanya kufuru.

Kama huyo mwenzako anayemlinganisha Samatta na huyo Kizota!
Huyo mlevi, huyo mlevi...una ugomvi naye au ulevi ndio namna pekee unayomtambua?

Sijui macho yako yamejawa na husda au upofu, maana unamzungumzia utadhani unamwongelea mtu mwenye kimo cha Mohamed Ibrahim wa 5imba, kumbe unamzungumzia Kizota, mtu na misuli yake.

Shida yako unajua upande mmoja wa shilingi na mdomo mwingi. Mimi Kizota nimemuona na hawa wanaocheza leo nimewaona. Kuna watu wasikie tu, sijaona body stamina yao katika kizazi hiki cha chips mayai.
 
Leo nikiwa maeneo fulani nikiwa nafuatilia mchezo wa CHAN kati ya Tanzania na Sudan nikawa napata story fupi ya mpira yenye kusisimua kuhusu mchezaji wa zamani wa Yanga marehemu mzee SAID NASSOR MWAMBA KIZOTA .

View attachment 1213754

View attachment 1213733

Unaambiwa ilikuwa mwaka 1993 ndio mwaka ambao fundi huyu aliwapa burudani mashabiki wa Yanga na kumfanya kuwa kipenzi cha mashabiki wa timu hiyo.

View attachment 1213755

Basi kipindi hicho Yanga ikiwa inajiandaa kuvaana na Sport Club Villa ya Uganda katika fainali ya klabu bingwa afrika mashariki na kati mjini Kampala Uganda.

View attachment 1213764

Timu ilikuwa imeshaondoka na kutangulia nchini Uganda jamaa alikuwa anaendelea na mishe zake akiwa na tuhuma za kupiga ulabu alipokuwa kambini basi akawa amepoa kwa dada yake maeneo ya mwembe yanga aitwaje White Mama (jina maarufu)

Basi watu wa Yanga baada ya kujishauri muda mrefu wakamfuata na kumchukua mahali hapo na kumpeleka nchini Uganda kuamkia siku ya fainali.

Siku ilipofika jamaa bila kufanya mazoezi ya pamoja na timu akaingia mzigoni akaweka kamba mbili wavuni huku goli la tatu la Yanga likifungwa na Lunyamila hivyo kuifanya Yanga kutawazwa ubingwa mbele ya SC Villa nchini Uganda Kizota akarudi na ufungaji bora wa michuano hii na katika mwaka huo huo akabeba kiatu cha ufungaji bora ligi kuu ya Tanzania bara kipindi ikidhaminiwa na TBL.

Mechi kubwa iliyoacha historia kipindi hicho ni ilipowakutanisha watani wa jadi Kizota alipiga goli mbili huku moja ya goli maridhawa akimchambua na kumfanya atakavyo goli kipa mahili wa wakati huo Mohamed Mwameja .

Wakati mwengine fundi huyu alitupiwa virago na wana Jangwani kwa tuhuma za kuhujumu timu walipopokea kipigo cha 4-1 kutoka kwa Simba na Kizota akadondokea Simba

View attachment 1213765

Kizota Vs Mmachinga

Mwaka 1995 ;Wakali hawa wa kufumania nyavu na kuchezea mpira walikutana katika Mbungi ya kkoo moto ulikuwa mkali pale ambapo Mmachinga alipopachika goli la kuwapa Yanga uongozi kipindi cha kwanza,wakati Yanga wakijua turubai limehamia kwa jirani Kizota anapiga goli maridadi la kusawazisha na kuwachanganya Yanga ambao kutahamaki wanapigwa kamba ya pili na Mchunga Bakari ‘Mandela’ kukamilisha hesabu ya 2-1 na mchezo kuishia hivyo.

View attachment 1213753

YANGA WAMPIGIA MAGOTI
Yanga walitambua makosa yao na kumsotea Fundi huyu wa mpira na kwa vile alikuwa akiishi maeneo hayo ya mitaa ya Jangwani haikuwa kazi sana kumpata na kumvisha tena uzi wa watoto wa Jangwani kwa mara nyingine.

View attachment 1213751

AKUTANA TENA NA SIMBA
Kizota anakutana tena na Simba mwaka 1996 na kushiriki katika matokeo ya sare ya maajabu jijini Arusha 4-4

View attachment 1213749

Hahah kuna hili la kizota na waarabu jamaa alienda uarabuni na kupiga mpira wakina maradona jamaa wakamtaka hadi abadilishe uraia usifanye masihara moto anaouwasha mtu mpaka waarabu waelewe somo (hii ni stori nyingine)

Kizota pia amechezea timu ya taifa na kupata mafanikio ikiwemo challenge cup

Fundi huyu wa mpira alifariki dunia tar 11/02/2007 kwa ajali ya gari maeneo ya Veterinary akitokea kushuhudia mchezo wa marudiano, Kombe la Shirikisho la Soka Afrika, Raundi ya Awali kati ya wenyeji Simba dhidi ya Textil de Pungue ya Msumbiji ulioisha kwa Simba kutolewa kwa njia ya matuta 3-1 baada ya sare pacha ya 1-1 .

View attachment 1213748
View attachment 1213766
View attachment 1213794

Mungu ailaze mahala pema peponi roho ya fundi huyu wa mpira na wengine wengi waliotangulia mbele ya haki.

Timu alizopitia Kizota ni pamoja na Shirika la posta Tabora (wakiti huo ikijulikana kama Posta na Simu) ,Yanga,Simba,Al Nasar ya Oman na Al Jazeera ya uarabuni Abu Dhabi.

Hebu tupia hapa kisa chochote unachofahamu au kusikia kuhusiana na wachezaji wa zamani wa Tanzania kama Sunday Manara ‘Computer’ ,Zamoyoni Mogella ‘Golden Boy’ ,Maulid Dilunga ‘Mexico’Juma Pondamali ‘Mensa’ ,Omar Hussein ‘Keegan’, Mohamed Hussein ‘Mmachinga’ ,Ezekiel Greyson ‘Jujuman’ ,Ally Yusufu ‘Tigana’ ,Athuman China na wengine wengi
Asante kwa historia nzuri
 
Huyo mlevi, huyo mlevi...una ugomvi naye au ulevi ndio namna pekee unayomtambua?

Sijui macho yako yamejawa na husda au upofu, maana unamzungumzia utadhani unamwongelea mtu mwenye kimo cha Mohamed Ibrahim wa 5imba, kumbe unamzungumzia Kizota, mtu na misuli yake.

Shida yako unajua upande mmoja wa shilingi na mdomo mwingi. Mimi Kizota nimemuona na hawa wanaocheza leo nimewaona. Kuna watu wasikie tu, sijaona body stamina yao katika kizazi hiki cha chips mayai.

Mzee , takwimu hazidanganyi..

Nambie kizota alifunga goli ngapi akiwa yanga?

Nambie, alishinda vikombe vingapi katika maisha yake ya SOKA!

Ukisema hujui, basi sitaamini kuwa huu mpira ulifuatilia kama unabyojinasibu
 
Back
Top Bottom