Maajabu ya jiji la Kampala

Maajabu ya jiji la Kampala

K
1. Si kubwa kama jiji la Dar Es Salaam, lakini ningeambiwa nichague pa kuishi, ningepapendelea Kampala kutokana na hali yake ya hewa nzuri

2. Lugha ya Kiganda ndiyo imetawala kuanzia kwenye maredio na mitaani. Kizungu hutumika kinapohitajika

3. Kuna maeneo kuna Waswahili pia. Kuna mahali nimepita leo kwenye gesti moja nikakuta watu wanaongea Kiswahili. Nikipata muda nitaenda kuwauliza kama ni Watz au la. Kwenye ubao wa matangazo wa hiyo gesti, matangazo yamewekwa kwa lugha ya Kingereza na Kiswahili

4. Kuna mitaa pikipiki ni nyingi sana. Uliiona zikipita barabarani unaweza kufukiri zipo kwenye maadamano ya "chama"

6. Huenda boda boda wa huku nao wapo rafu katika uendeshaji pikipiki kama wa Bongo. Nimeshuhudia zikipuuzia kuzingatia taa za kuongozea magari. Ni tofauti na boda boda wa Kigali ambao inasemekana ni watiifu sana wa Sheria za barabarani

7. Inawezekana ndilo jiji la Afrika Mashariki linaloongoza kwa mabinti kuvaa vimini. Unakuta mwingine kimini chake ni kifupi sana kiasi kwamba akitaka kupanda boda boda inamlazimu awe na koti la kufunikia mapaja ili kujisitiri. Sijui ni utamaduni wao au ni "Uzungu" umewakolea?

8. Watu ni wachapa kazi. Ni kawaida kukuta maduka yaliyo pembezoni mwa mji yameshafunguliwa saa kumi na mbili Asubuhi, na muda huo mama lishe naye ameshaivisha chakula

9. Utamaduni wao kwenye matumizi ya Vyuo unaweza kuendana na Wakenya, ingawa Wakenya wanaweza wakawa "more advanced". Katika gesti kadhaa nilizolala, hakuna kopo la chooni wala toilet paper. Uzoefu wangu kwenye gesti za Kenya ni kwamba vyoo, hata vile vya umma(vya kulipa), lazima viwe na toilet paper. Lakini kwa Waganda sikuziona toilet paper wala kopo. Nazungumzia gesti za gharama nafuu na siyo mahoteli

10. Gesti za kawaida zinagharimu wastani wa Ugx 20,000 mpaka 30,000. Lakini ukienda nje ya mji, unaweza kupata mpaka Ugx 20,000 (self) na Ugx 13,000 (single)

11. Ndizi (matoke) ni chakula "common" huku

12. Wali wa huku ni kama pilau. Nimeshakula pilau zaidi ya mara moja, lakini mara zote nilipoagiza wali, nililetewa "pilau"

13. Kwa baadhi ya niliongea nao, hasa wale waliokwishafika Tanzania, wanaamini Serikali ya Tanzania inawajali raia wake kuliko ya Uganda😄. Mfano mojawapo waliotumia ni gharama za Internet. Wanadai internet ya Tanzania ni nafuu sana ukilinganisha na ya Uganda

14. Nimeshangazwa pia na chipsi mayai za huku. Chipsi kavu zilipashwa kivyake na mayai yakakaangwa kivyake. Sijui ndiyo kawaida ya huku au ni kwangu tu ndiyo waliamua kufanya hivyo!


NB. Ni "maajabu" kwangu tu ambaye bado "mgeni"
Izungu ndio lugha gani?
 
Tupe utofauti wa maisha kati ya kampala na Dar? (Lifestyle,maendeleo ,watu) etc
GoldDhahabu
Kwa jinsi nionavyo,
1. Dar kumeendelea zaidi ya Kampala, ingawa Kampala kumepangika vizuri zaidi. Labda kwa vile sijatembelea maeneo yote, ila mpaka sasa sijayaona mazingira ya "Uswahilini". Nafikiri naeleweka nikisema "Uswahilini"
2. Watu wa huku ni wachapa kazi. Wapo busy sana.
3. Sijui kama kuna watoto wa "mitaani", sijakutana nao huku. Labda sijafika mitaa wanapopendelea
4. Ni waelewa. Ukimwuliza mtu kitu, kama anafahamu, atakuelekeza vizuri
 
Kaulizie chakula kinaitwa Rolex, hakipatikan mgahawani ni vijana barabarani wanakaanga chapati Inakunjwa Kwenye mayai ni very cheap. Wape hi ba sebo na wanyabo
Rolex nilishasoma kwenye magazeti nikiwa "nyumbani". Nitaitafuta leo.

"Wa sebo na wanyabo" ni nini
 
Ndio saizi huwezi kupigwa, elfu 1 nadhani wanaita Lukumi. Polepole ni mpola mpola, hao boda usiku wengi wanakuwa maji unakuta anakuita sebo(mwanaume) tugende(twende). Wewe unamuita Janguu(njoo) sebo
Kwa nini hukuniambia hayo kabla sijaja huku?😀

Kuna raha kufahamu lugha ya wenyeji wako, alau misamiati ya muhimu kama salam na jinsi ya kuuliza au kuomba kitu.
 
Nilifanya kazi katika kampuni ambayo nilideal na waganda.

Nashindwa kuelewa mleta uzi anaposema waganda ni wachapakazi, nitatoa mfano: Ikinyesha mvua mganda haendi kazini wala shambani, wanahusudu kula bata mno, akiwa ana pesa anatakiwa kulipa deni au kula bata atachagua kula bata, mostly wanaishi kwa kumaanisha kesho itajitegemea
 
Nilifanya kazi katika kampuni ambayo nilideal na waganda.

Nashindwa kuelewa mleta uzi anaposema waganda ni wachapakazi, nitatoa mfano: Ikinyesha mvua mganda haendi kazini wala shambani, wanahusudu kula bata mno, akiwa ana pesa anatakiwa kulipa deni au kula bata atachagua kula bata, mostly wanaishi kwa kumaanisha kesho itajitegemea
Kwa kuwa ulishafanya nao kazi, siwezi kukubishia. Ila pia na Mimi nilishafanya kazi na mmoja miaka ya nyuma. Yeye peke yake ndiye aliyekuwa Mganda kwenye taasisi yetu. Alikuwa mchapa kazi sana japo sijui kama hiyo ilikuwa ni tabia yake binafsi au alinadilishwa na mazingira.

Kilichonifanya niwaone wa huku ni wachapa kazi ni baada ya kushuhudia maduka na mama lishe yamesahafunguliwa saa kumi na mbili Asubuhi, na mama lishe kuivisha chakula mapema sana Asubuhi.
 
Ni mji karibu na Ziwa Victoria kuna bandari kubwa inaitwa Port Bell, meli za kutoka Tanzania(Mwanza,Bukoba,Mara),Kenya( Kisumu) zinashusha mizigo na abiria hapo.

Sio mbali na Kampala, ukiwa na nafasi weekend ukatembee kuna waganda wanafanya booking boat za kuwatembeza ziwani na hapo ndio utakutana na wafanyabiashara kutoka Mwanza na Bukoba wakileta bidhaa na kutoa mizigo huko kuja Tanzania
Hivi kuna boti au meli za abiria za kwenda Tz kutokea Uganda?
 
Sijui nauli ya kutokea Dar. Kama unataka "kuja" Kampala, panda basi hadi Mwanza ukashangae kwanza miamba ya jijini Mwanza ndipo uendelee na safari ya Kampala.

Na kama utaanzia safari Mwanza kwa magari ya kuunga unga kama nilivyofanya, utapanda gari kutoka Mwanza hadi Katoro (Geita) Tsh 8,000/=.

Katoro hadi Bukoba Tsh 20,000/=

Kutoka Bukoba Mjini utachkua daladala hadi Mutukula Tsh 4,000/=.

Mutukula ukishagongewa mihuri, unaweza ukavuka mpaka kwa miguu kuingia upande wa Uganda kwenda ziliko hiace (Waganda huziita taxi), au uchukue bodaboda Tsh 1,000/= au Tsh 2,000/=, lakini wakikuona wewe ni wa kuja, bodaboda wanaweza wakakuambia hata Tsh 5,000/=.

Kabla ya kuvuka kwenda upande wa Uganda, ni vizuri ukabadilisha hela upate za Kiganda, na pia ukasajili line ya Uganda, mfano MTN (Vodacom). Kama una passport kubwa (siyo EMERGENCY TRAVEL DOCUMENT) unaweza ukasajili line yako kwa jina lako hapo hapo Mutukula upande wa Tanzania, gharama ni Tsh 3,000/=, lakini kama unatumia EMERGENCY TRAVEL DOCUMENT, watakupatia line iliyokwishasajiliwa kwa jina la mtu mwingine kwa Tsh 10,000/=, ila wakikuona wewe ni mtoaji mzuri watakuambia Tsh 15,000/=.

Ukishaingia upande wa Uganda, utapanda "taxi" kwa hela ya Kiganda Ugx 40,000 Mutukula hadi Kampala. Ingawa nauli ni Ugx 40,000/= , mimi nililipa Ugx 35,000/=, na mtu mwingine alilipa Ugx 30,000/=. Wakati wa kurudi nitabargain hadi na mimi nipande kwa Ugx 30,000/=.
Asante sana mkuu
 
Kitu kingine kuhusu waganda , hoja ya uchapakazi hii haipo kwa miaka miwili niliokaa kule kwani starehe kwao ni kipaumbele kikubwa ,wanaishi wakiwaza sana kutoka nchini kwao wakiamini kutoboa zaidi.Hawajitumi ila ni wajanja wajanja sana na ukikaa vibaya watakupiga ,tabia ya udokozi kwa vitu vidogo vidogo kwao ni kawaida.
Ngono ni kitu simple sana kwani wanakauzungu flani hata dem akikuelewa anakufata anakueleza uhalisia kua anakutaka .
Bidhaa zao sijui ni kwa nn ila nyingi ni org kwa asilimia 100, copy ni chache labda miaka hii ya sasa .Kama taifa kl Waganda ni kabila kubwa ila wanawabagua sana makabila mengine .
Kujiunga UPDF (jeshini ), kiswahili ilikua sifa ya ziada
 
1. Si kubwa kama jiji la Dar Es Salaam, lakini ningeambiwa nichague pa kuishi, ningepapendelea Kampala kutokana na hali yake ya hewa nzuri

2. Lugha ya Kiganda ndiyo imetawala kuanzia kwenye maredio na mitaani. Kizungu hutumika kinapohitajika

3. Kuna maeneo kuna Waswahili pia. Kuna mahali nimepita leo kwenye gesti moja nikakuta watu wanaongea Kiswahili. Nikipata muda nitaenda kuwauliza kama ni Watz au la. Kwenye ubao wa matangazo wa hiyo gesti, matangazo yamewekwa kwa lugha ya Kingereza na Kiswahili

4. Kuna mitaa pikipiki ni nyingi sana. Uliiona zikipita barabarani unaweza kufukiri zipo kwenye maadamano ya "chama"

6. Huenda boda boda wa huku nao wapo rafu katika uendeshaji pikipiki kama wa Bongo. Nimeshuhudia zikipuuzia kuzingatia taa za kuongozea magari. Ni tofauti na boda boda wa Kigali ambao inasemekana ni watiifu sana wa Sheria za barabarani

7. Inawezekana ndilo jiji la Afrika Mashariki linaloongoza kwa mabinti kuvaa vimini. Unakuta mwingine kimini chake ni kifupi sana kiasi kwamba akitaka kupanda boda boda inamlazimu awe na koti la kufunikia mapaja ili kujisitiri. Sijui ni utamaduni wao au ni "Uzungu" umewakolea?

8. Watu ni wachapa kazi. Ni kawaida kukuta maduka yaliyo pembezoni mwa mji yameshafunguliwa saa kumi na mbili Asubuhi, na muda huo mama lishe naye ameshaivisha chakula

9. Utamaduni wao kwenye matumizi ya Vyuo unaweza kuendana na Wakenya, ingawa Wakenya wanaweza wakawa "more advanced". Katika gesti kadhaa nilizolala, hakuna kopo la chooni wala toilet paper. Uzoefu wangu kwenye gesti za Kenya ni kwamba vyoo, hata vile vya umma(vya kulipa), lazima viwe na toilet paper. Lakini kwa Waganda sikuziona toilet paper wala kopo. Nazungumzia gesti za gharama nafuu na siyo mahoteli

10. Gesti za kawaida zinagharimu wastani wa Ugx 20,000 mpaka 30,000. Lakini ukienda nje ya mji, unaweza kupata mpaka Ugx 20,000 (self) na Ugx 13,000 (single)

11. Ndizi (matoke) ni chakula "common" huku

12. Wali wa huku ni kama pilau. Nimeshakula pilau zaidi ya mara moja, lakini mara zote nilipoagiza wali, nililetewa "pilau"

13. Kwa baadhi ya niliongea nao, hasa wale waliokwishafika Tanzania, wanaamini Serikali ya Tanzania inawajali raia wake kuliko ya Uganda😄. Mfano mojawapo waliotumia ni gharama za Internet. Wanadai internet ya Tanzania ni nafuu sana ukilinganisha na ya Uganda

14. Nimeshangazwa pia na chipsi mayai za huku. Chipsi kavu zilipashwa kivyake na mayai yakakaangwa kivyake. Sijui ndiyo kawaida ya huku au ni kwangu tu ndiyo waliamua kufanya hivyo!


NB. Ni "maajabu" kwangu tu ambaye bado "mgeni"
Hiyo namba 8, hicho chakula cha asubuhi asubuhi kinaitwa *akatogo"! Saa nne ndio Waganda wanakunywa chai.
 
Nimesoma huko Uganda shule moja inaitwa Eagle's Nest iko meko hapo Kati Kati ya jiji karibu na ikulu ya kabaka, miaka ya 2006 - 2009. Nilipapenda ug.

Kwangu Kampala ndo jiji namba moja. Manyabo wa kule Wana nyash za hataree.
Eagle's nest umenikumbusha mbali sana aisee. Nmesoma Ntinda View mitaa ya Ntinda. Nakawa unaingia kushoto.
 
Back
Top Bottom