Pre GE2025 Maajabu ya Walimu: Wachangishana kumchukulia Rais Samia form lakini wameshindwa kuwachangia viti walimu wenzako, wanakaa chini

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Hapo sio kujipendekeza bro! Inawezekana wamelazimishwa, kama wanavyolazimishwa kuchangia mwenge, au kuna kenge wawili wamepewa mpunga,wawe chawa, wajitokeze, wawashwawishi baadhi ya, wenzao, waseme wanatoa mchango, ila ki ukweli pesa imetoka hazina! Waalimu ni wengi Sana, na wananjaa(wanafanywa wawe na njaa), hakuna mwalimu wa kutoa pesa achangie huu upuuzi!
Ni kama wale kenge wenngine wanaojiita vyama vya siasa waliokuwa wanapinga maandamano, unaweza ukafikiri wana maaana kumbe wajinga,na njaa ndio inawasumbua.
 
Mkuu

Uwe unawaza nje ya boksi!

Unaamini kweli Kuna mwalimu kamchangia Samiah Hela ya form!!?

Hao wakuu was shule waliochanga unaamini ni Tz nzima!!?

Hizo no propaganda za kampeni baada ya serikali kujua imepuuza madai ya walim,yaani spining ya madai walim Kwa serikali !!!
 

View: https://m.youtube.com/watch?v=fwJ6x3hpDss
Wanaomuda wa kujali shida zao saa ngapi au hata hao wazazi wanajali mazingira ya shule zao. Wazazi wengi washakubali kufeli kwa watoto zao kwa sababu ni vilaza tu. Hakuna uhusiano wowote na quality ya elimu au mazingira ya kufundishia kama chagizo la matokeo mabaya.

Siasa za nchii pasua kichwa, ebu angalia watu wazima wanasherekea birthday ya raisi huko Arusha, mtu ambae yupo nje ya nchi.

Hayo mambo ya jamii na madhara wanafikiria saa ngapi.

Hii nchi bora ufanye biashara au mambo mengine ya maisha, kuliko kufuatilia vituko vya watu wazima wanavyojidhalilisha only god knows what for. Yaani hapo kuna mtu akiangalia clip anasema baba yule.

Sijapata kuona, sisi watanzania ni wakipekee kwa kweli akija raisi anapenda raha tunaenda na mdundo wake, akija raisi mkali tunaenda na mdundo wake.

Yaani anachohitaji raisi wa Tanzania ni kuonyesha tu mtu wa aina gani, wapambe wanamaliza shughuli bila ya kuwatuma.

Tarehe 27 January imekuwa siku ya kitaifa, bado Ikulu kuturushia picha akiwalisha cake.
 
Mwalimu alikuwa akifanikiwa kupata mtoto anapata kazi anakuwa mwalimu.
Siku hizi laana imewakuta walimu watoto wao wakimaliza chuo wanakoelekea ni mungu anajua.
 
Labda aliwaambia hana pesa za fomu !πŸ˜…
Hao watu ndio tunawategemea watutengenezee msingi wa raia bora na viongozi bora wa Nchi yetu !!
Je unaweza ukasikia hii kitu inatokea huko Duniani ??!
Haya maigizo hayafai Bandugu !
 
Walimu wamejaa unafiki. Ukiangalia viongozi wao ni matokeo ya Upe na Nemkwa
 
Sio walimu wote wenye mawazo kama hayo. Walio wengi wanajielewa. Ila hao kwa kweli wamechemka, kama ambavyo kada zingine wanazingua vilevile. Tuwasamehe bure
 
lengo la ccm huwa ni mtazamo kama huu wako.

lina mtaji wa kutosha maana mpo wengi.

hivi kwa akili za kawaida wale waalimu wa CWT ndio hawa hawa unaowafahamu??wanaolia maisha ni magumu???
 
Wale waliochanga sio Walimu..... Ni chawa tu
 
Walimu nadhani wanafurahia hizi dharura, mtu akukalishe chini then uje ukubali kupigwa picha ili uzidi kudhalilika?!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…