Maalim Seif achukua fomu ya Uenyekiti ACT-Wazalendo

Cheo cha mkuu wa chama mbona hakichukuliwi fom

Sent using Jamii Forums mobile app
Maajabu halafu Zitto anajitia mpigania Demokrasia.

Cheo Cha mwenyekiti ni boya tu mwenyekiti wa Sasa was ACT wazalendo anaitwa Jeremiah Maganja Lakini wengi hata hawamjui sababu kazinzake Zitto Kabwe mkuu wa Chama kabeba zote.

Hicho cheo ndio Maalim Seif anagombea ili amtoe huyo.mwenyekiti ws Sasa taifa Maganja ambaye hata humu.jamii forums wengi hawamjui
 
Zitto atabakia kuwa mbunge hata wakuteuliwa na maisha yataendelea vilevile
Wa kuteuliwa ambao sio viti maalum lazima wateuliwe na Raisi wa nchi.
Viti maalum wana ruhusiwa wanaume ambao hawapo ktk kundi la watu maalum kama walemavu?
Uhakika wa ubunge wa kuteuliwa Zitto anautoa wapi?
 
Hapo sawa na kusema Maalim atakuwa Zitto's puppet [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Don't hunt what you can't kill.
 
Halafu anajifanya mwanademokrasia,ngoja membe aje achukue chama chake
 
Kuna picha la kutisha sana Octoba 2020. Mfano CCM ikagoma kuunda tume huru ya uchaguzi inamaana CCM itashinda bara na kujitangazia ushindi. Lakini haki ya kisiasa Zanzibar safari hii mrithi wa Jecha hawezi kuiba tena hivyo ACT itachukua serikali Zanzibar. Jee nini hatma ya uongozi wa Jiwe kimuungano? Serikali ya Zanzibar chini ya ACT haiwezi kukubali ukandamizaji wa upinzani huku bara maana na wao ni washirika wa serikali ya muungano, huyu naye kiburi!
Sasa tutegemee moto kuwaka!

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Jamaa zetu upande wa pili wakiona na kuskia habari kama hizi mavi kitambaani
 
Meko si alitanabahisha kwamba ameongea na Vice President wa WB kuhusu mkopo wa $500 mil.
Vipi alishakabidhiwa?

Zitto ni mtoto wa mjini. Hawezi kuzidiwa ujanja na huyo mlima matikiti wa Chato.
Sent using Jamii Forums mobile app
 
NI KIONGOZI WA CHAMA SI KIONGOZI MKUU WA CHAMA!
Kama ilivyo kwa vyama vingine duniani vinavyofuata mfumo huu, Kiongozi wa Juu huitwa Kiongozi wa Chama (Party Leader) na si Kiongozi Mkuu Wa Chama (Supreme Party Leader) Kama ambavyo baadhi ya watu huita kimakosa. Dhana “Mkuu(Supreme)” huambatana na utukufu/kutopingika. Hakuna sehemu yoyote Kwenye Katiba ya ACT Wazalendo ambako kuna rejea ya ‘Kiongozi Mkuu’.
Tuhitimishe Mjadala wetu kwa kuona nafasi ya Kiongozi wa Chama ndani ya ACT Wazalendo;
Kiongozi wa Chama atakuwa ndiye Msemaji Wa Kisera. Katika kutekeleza wajibu huu, Kiongozi wa Chama atawajibika kutoa mwongozo na mwangaza kuhusu maeneo mbalimbali ya kisera. Baada ya mwongozo wake kusemwa, ni wajibu wa Wenyeviti Wa Kamati (Wasemaji Wa Kisekta) na Msemaji Wa Chama (Msemaji Wa Jumla) kuendeleza na kueneza kwa umma.
Mkuu Wa siasa. Katika kutekeleza wajibu huu, Kiongozi wa Chama anapaswa kuwa kielelezo cha kuimarisha taswira ya Chama na kukiuza ndani na nje ya Bunge na kwenye Jamii kwa ujumla
Kiongozi wa Chama hataongoza vikao vya Chama, isipokuwa Mkutano Mkuu Wa Kidemokrasia. Vikao vya Maamuzi Kama vile Kamati Kuu, Halmashauri Kuu na Mkutano Mkuu vitaongozwa na Mwenyekiti. Wajibu wa kusimamia utekelezaji Wa maamuzi ya vikao vya Chama pia upo kwa Mwenyekiti.

Na ufahamu tu kiongozi wa chama huchaguliwa kwa kura.
 
Acha kupotosha watu humu, katiba ya ACT sura ya 29 ibara 25 kipengele kidogo Cha 1 inamtambua kiongozi kama kiongozi mkuu wa chama ( supreme party leader)

Na miaka ya baadaye katiba ya ACT itamtambua Zitto kwa jina lake kabisa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…