Uchaguzi 2020 Maalim Seif: ACT Wazalendo hatuna mpasuko lakini Membe anataka kuwaaminisha Watanzania hivyo. Adai Mzee wa Ubwabwa ni bora kuliko Mgombea wao

Hapo naona Membe hataki awe wa mwisho, kuwa wa mwisho ni fedheha mjue.
 
Huyo Membe since day one nilijua ametumwa na CCM. Nilisema kabisa inyeshe mvua liwake jua, CHADEMA wasikosee wakajiunga na Membe na kufanya naye vikao vya siri. Hata Nyalandu ni wa kumuweka pembeni kwenye vikao vya siri vya CHADEMA. Haya ya Membe yanaanza kuwa wazi, uzuri ni kuwa wananchi wameshafanya maamuzi, vinginevyo ingekuwa tatizo hizi dakika za lala salama.
 
Mwenyekiti wa ACT Taifa anaongea na wanahabari jijini Dar es salam...
Maalif Seif huwa ninamuelewa sana , na Znz hawatakuja kupata mtu mvumilivu kama Mzee Seif. Mzee akisema amechoka kuibiwa kwa kweli amemaanisha na sasa mimi naona ni sawa kabisa aruhusu watu waingie road kuipambania demokrasia ambayo ccm wao wamekuwa wakiiminya kila iitwapo leo
 
Uwaneni,piganeni,chambaneni ila Magufuri anashinda kwa asilimia nyingi mnooo....


Ccm iliyumba wakati wa lowassa.
wapiga kura Og wako nje ya mitandao,vijijin ndo usiseme kura kama zote
Tunaopiga kelele ni huku mitandaoni kwa Id fake tena nyuma ya keybo'd .
 
Seif miaka yote kabla ya kura husemaga hivyo!

Hata baada ya matokeo ya uchaguzi wa marudio Zanzibar, seif alizunguka zunguka huko ulaya akaja kutwambia baada ya miezi 3 atakabidhiwa nchi yake. Mpka leo miak 4 imeshapita tunaingia kwenye uchaguz mwingine Seif akiwa yule yule.
 
Bora CHADEMA Lowassa kawafundisha akili, Membe yaani anaharibu mipango.
 
Jasusi is there to stay

Uchaguzi ukimalizika anaukurupusha mgogoro kama wa NCCR ya Mrema na Mabere Marando 1995~2000

Siku nyingine Ccm ikigombana na wanachama wake wapinzani wapunguze shobo
Uzuri Membe ataondoka yeye na mke wake kwenda ADC ya Hamad Rashid
 
Sawa kabisa. Kazi kubwa ni hiyo.
Usije shangaa ACT wakamvua uanachama Membe then uchaguzi ukaahirishwa kwa muda ili kuchapisha karatasi za kupigia kura upande wa Urais.
Au ACT ikamruhusu Membe kuendelea ili azigawe kura za WanaCCM na kumwacha Lissu akitamba, kitu ambacho hakiwezekani.
 
Membe alishapewa hela za kampeni kwa alio waahidi kuwa atakuwa rais wa JMT. Ni lazima wamuone amefanya kampeni ili ku halalisha matumizi ya pesa hizo. Hata mwenyewe anajua kuwa hawezi kuwa Rais nje ya CCM.
 
Maalim Seif, wewe ulikuwa ukishinda miaka yote ya uchaguzi Mkuu Zanzibar. Ulikuwa ukipokwa ushindi wako. Sasa basi. Safari hii uhuni huu basi.
 
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3] mkuu kunywa bia ntalipa. Umejua sana kuwanyoosha hao manyang'au.
Hahah daah ni mwana huko mitandaoni ndio aliamua kuwanyoosha hao jamaa.
 
Kabla ya kuchukua maamuzi hayo walimshirikisha Membe kwenye huo mkutano wao?
 
CCM walijua wameimaliza CHADEMA wakahisi ACT ndo itainuka wakamtuma membe bahati nzuri baada ya ACT kukubali kushirikiana na CHADEMA wakashtuliwa, na wasingekubali wangeishia kuzimu
 
Yani vitu vyengine havina kichwa wala miguu,hivi kweli haya mambo walijadili na kushindwa kufikia muafaka au wanatuletea mapicha picha tu?

Halafu kuna watu wanashabikia hii michezo ya wanasiasa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…