Uchaguzi 2020 Maalim Seif: ACT Wazalendo hatuna mpasuko lakini Membe anataka kuwaaminisha Watanzania hivyo. Adai Mzee wa Ubwabwa ni bora kuliko Mgombea wao

Hahaha ma CCM sasa yamepata mwanya wa kutuibia.

Huyu Membe huyu anajidai anawatu, mbona hawaji kumuunga mikono?!

Ndio maana anafukuzwa kumbe, sasa anataka na huko ACT afukuzwe?!
 
Namhurumia sana Membe, nauhurumia sana upinzani. Je, ni Membe huyu aliyefuatwa Rondo na kupokelewa na chama kwa shangwe?! Leo hii anatupwa na kudhihakiwa?

Afadhali angebaki huru bila chama kama mimi. Pengine mabadiliko hayataletwa na vyama na wasaka vyeo kupitia vyama vya siasa, bali sisi wananchi tukiungana pamoja bila kuegemea chama chochote isipokuwa taifa letu.
 
Membe alipitishwa na kamati kuu na mkutano mkuu wa chama
Hivyo vikao havikufanyika hadi leo .Hivyo Membe ni mgombea halali aliyepitishwa kihali na vikao.Kumtengua kulitakiwa vikao vile vile vikae vitengue sio kigenge cha watu wawili watatu wakae waseme tumeamua.Membe shikilia hapo hapo ili vyama viwe na nidhamu ya kuzingatia katiba zao

Hata CHADEMA kusema wanamuunga mkono mgombea Uraisi Zanzibar ni uamuzi batili sababu wana mgombea Urais wao kule Zanzibar waliyemchagua kwa vikao halali. Na yeye asiogope ajitokeze kama Membe aseme yeye mgombea Urais wa Zanzibar kupitia CHADEMA
 
Umesema kweli kabisa!
 
Maalim mkorofi sana huyu babu,kaingia ACT juzi tu keshaanza migogoro,kwanini walimpa baraka zote Membe za kupeperusha bendera ya Urais ilhali wanajua kabisa hafai!?

Sasa wameona hauziki, ndio maana wamebadilisha Gia angani

Kama kweli lengo la Membe ni kuitoa CCM basi imefeli
 
Hongera CDM kwa kushutka mapema, vinginevyo, angekuwa nawapiga kutoea ndani. Ni afadhali ss anatokea nje.
 
The game is over
 
Maalim mkorofi sana huyu babu,kaingia ACT juzi tu keshaanza migogoro,kwanini walimpa baraka zote Membe za kupeperusha bendera ya Urais ilhali wanajua kabisa hafai!?
Walikuwa hawajamjua, ukitaka kujua kina cha maji ya bahari sharti uzamie.
 
Ninachojiuliza ni kwamba, Membe yupo hapo Dar. inamchukua gharama gani kwenda kuwanadi hata wagombea ubunge wa chama chake hapo Dar? Maana nauli ni sh. 400 kutoka anapoishi hadi kwenye mikutano ya kampeni!!!
Jasusi kanyanganywa taulo, na amegoma kuchutama, huyu angepewa nafasi ya uenyekiti angekipasua ACT kabisa
 
Sawa kabisa, lakini hawasikii mpaka nilinyosha mikono!
Mimi huwa nashangaa sana mpaka leo vyama vya upinzani vinapokea wanasiasa kutoka ccm., Ni lazima upigwe mstari mwekundu hawa watu ata wakija vipi muachane nao, muachane nao ni virusi kuliko ata korona
 
Uko sahihi
Jasusi is there to stay

Uchaguzi ukimalizika anaukurupusha mgogoro kama wa NCCR ya Mrema na Mabere marando 1995~2000

Siku nyingine Ccm ikigombana na wanachama wake wapinzani wapunguze shobo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…