Maalim Seif akana kuitwa msaliti kwa kukubali SUK asema sio kila jambo unasusia!

Maalim Seif akana kuitwa msaliti kwa kukubali SUK asema sio kila jambo unasusia!

Wewe ndiyo lofa kwa kumuona Lipumba ni mungu wako hana Dhambi kumbe hukujua Lipumba ni mwizi zaidi aliiba pesa ya luzuku ya CUF kipindi Seif akiwa katibu mkuu
Sema shida yako ni kwamba kwa nyinyi CHADEMA Maalim ni mtu sahihi sana na mnajipendekeza kweke wakati hana mpango na nyie.

Maalim Seif alipomkandya Lipumba na kutoa ridhaa CUF kukubaliana na UKAWA kumsimamisha Lowassa kugombea urais mulimuona ni mtu wa maana sana! Lakini Maalim aliposusia uchaguzi wa mdogo wa madiwani 43 huku bara na kuiachia CHADEMA mkaona ni mtu bora sana.

Lakini kinyume chake Lipumba ni mbaya kwenu pale alipotumia pesa za ruzuku ya chama kusimamisha wagombea ubunge na udiwani kwenye uchaguzi mdogo wa baada ya uchaguzi mkuu wa 2015. Uchaguzi wenyewe hamkushinda hata kiti kimoja licha ya kuungwa mkono na genge la Maalim huku bara. na mliishia kama CUF tu. Maalim Seif ni "special mission" na hawezi kuwaletea neema CHAFEMA wala ACT.

Ndiyo maana na CHADEMA kwenye uchaguzi wa 2020 mkarudisha fadhila kwa Maalim Seif wa ACT kwa kumtangaza kuwa ndo mgombea wenu wa urais Zenji wakati wa chama chenu yupo! Maalim aliwateka nyie watoto wadogo wa siasa na sasa mmepotea boya! Ulofa huo!
 
Dogo ni mwanao sio mimi

Unaitaje an internet character you dont even know "dogo"?

Lipumba kavamia CUF kuua CUF baada ya kupewa hela na CCM

CUF ikapasuka katikati,everybody knows!

CUF wote waliohama CUF wakahamia ACT walitoka kwa sababu gani?

Sababu ni Lipumba,wewe kuja hapa na kuongea vitu unavyoona kichwani mwako ni sawa

Ila watu walihama,wakahamia ACT!

Thats a FACT!

Lipumba yupo kwenye payrol ya CCM....hutaki andamana!
Sasa kama wewe sio dogo basi niambie kwanini Seif na wafuasi wake hawakuamia CHADEMA licha ya wazee wa chama chenu kumkaribisha na kuahidi kumpa nafasi ya kugombea urais Zenji?

Kwanini Seif na watu wake hawakuahamia CHADEMA chama ambacho kilisimama upande wake kwenye mgogoro wa CUF na badala yake wakaingia ACT chama ambacho kilibaki "neutral" kwenye mgogoro huo?

Kwanini Maalim na watu wake hawakuahamia NCCR au NLD vyama ambavyo viliunda UKAWA na badala yake wakahamia ACT chama ambacho Tundu Lissu aliwahi kusema kiliundwa kimkakati na CCM kupambana na UKAWA?

Jibu maswali haya ili tuamini wewe si dogo bali mwanagu ndiye!
 
Hahaha Sasa jomba vyama ndio vinakuja kishika hatam ya Mamlaka ya serikali utaviachaje..Huo Ni ujuha..lazima vyama vitengenezwe vizuri na kuondoa matakataka yaliyomo ikiwemo ukiukwaji wa demokrasia Kama kwenye chama chako unachokitetea..kule ukihoji tu hata matumizi ya chama unafukuzwa, wanasema umetumwa..Huo ndio uhalisia..halaf utegemee chama hicho kije kishika dola, si mtakunya vima...hahaha..usione aibu kusema ukweli kwa sababu ukweli ndio utaponya vyama na wafuasi wao
Tumia elimu vzr Kiongozi, wazazi wako waliwekeza hela nyingi sana ili kukomboa fikra zako. Ebu watendee haki....!!

Sent from my SM-G920F using JamiiForums mobile app
 
Sema shida yako ni kwamba kwa nyinyi CHADEMA Maalim ni mtu sahihi sana na mnajipendekeza kweke wakati hana mpango na nyie.

Maalim Seif alipomkandya Lipumba na kutoa ridhaa CUF kukubaliana na UKAWA kumsimamisha Lowassa kugombea urais mulimuona ni mtu wa maana sana! Lakini Maalim aliposusia uchaguzi wa mdogo wa madiwani 43 huku bara na kuiachia CHADEMA mkaona ni mtu bora sana.

Lakini kinyume chake Lipumba ni mbaya kwenu pale alipotumia pesa za ruzuku ya chama kusimamisha wagombea ubunge na udiwani kwenye uchaguzi mdogo wa baada ya uchaguzi mkuu wa 2015. Uchaguzi wenyewe hamkushinda hata kiti kimoja licha ya kuungwa mkono na genge la Maalim huku bara. na mliishia kama CUF tu. Maalim Seif ni "special mission" na hawezi kuwaletea neema CHAFEMA wala ACT.

Ndiyo maana na CHADEMA kwenye uchaguzi wa 2020 mkarudisha fadhila kwa Maalim Seif wa ACT kwa kumtangaza kuwa ndo mgombea wenu wa urais Zenji wakati wa chama chenu yupo! Maalim aliwateka nyie watoto wadogo wa siasa na sasa mmepotea boya! Ulofa huo!
Wewe ndiyo lofa na umepotea boya wewe njaa zimekufanya ujitoe fahamu kutetea njaa za seif ukiwa uteuzi haramu wa njia za kishetani
 
Maalim siku zote focus yake ni Zanzibar tu na anavitumia vyama vya siasa vya bara kama vyombo vya kufikia lengo lake. Alikichukua chama cha wakina Aleck Che Mponda na kukigeuza kuwa chama ambacho priority yake kubwa ni masuala ya Pemba na Unguja. Ameingia sasa ACT-WAZALENDO na anarudia mchezo ule ule. Nasema hivi kwa sababu:
1. Anaposema wanachama wa ACT-WAZALENDO waliulizwa kuhusu hatua ya kuingia kwenye GNU sidhani kama anamaanisha wanachama walioko Kibondo au Newala. Kwake yeye mradi wanachama walioko Pemba na Unguja wameulizwa mchezo umekwisha.
2. ACT Wazalendo ni chama cha kitaifa na hivyo kabla ya uamuzi wowote kuchukuliwa walipaswa kuangalia athari au faida yake kwa Chama kwa ujumla na sio kwa upande mmoja wa Muungano. Mpaka sasa hivi tunachosikia ni faida tu kwa wanachama walioko Zanzibar lakini hatusikii lolote kuhusu faida ambazo mwanachama wa Kibondo atapata kutokana na hatua hii.
3. Lugha ya kuwa Zanzibar sio Tanzania Bara ni ya kuwakataza hata wanachama wenzake wasio wazanzibari kushiriki katika mjadala unaohusu uamuzi wao wa kujiunga katika SUK.
4. Kwa ACT-WAZALENDO ( Bara) uamuzi huu unaweza kuwaathiri sana maana wamejiweka wazi kwa tuhuma za kuwa wao sio sehemu ya upinzani makini bali ni sehemu ya utawala uliopo. Hali hii inaweza kukubalika Zanzibar lakini itawaathiri kwa wanachama wao waliokipigania chama chao kwenye mikoa kama Lindi na Mtwara.
5. Kwa matamshi yake tayari anajihesabu yeye ni sehemu ya utawala wa Zanzibar. Ameanza mpaka kutumia lugha za vitisho dhidi ya wale ambao hawakubaliani na uamuzi wake. Kwa kufanya hivi anaonyesha yeye by nature ni authoritarian na hataki watu watofautiane nae. Hii inasikitisha kwa sababu inaonyesha kuwa si muumini wa Demokrasia na kuna uwezekano mkubwa kama angekuwa na uwezo angefanya vitendo hivyo hivyo ambavyo alifanyiwa.

Hata hivyo pamoja na kusema hivi, ninawaombea heri ACT-WAZALENDO na viongozi wao katika safari yao ya kutuonyesha kuwa kuna njia mbadala. Mafanikio yao yatakuwa yetu sote. Na wakionyesha kuwa mawazo yangu ni potofu sitasita kurudi tena humu na kuwaomba msamaha.

Amandla...
Anzisha chama chako
 
Maalim bunya tu mafao na mwanao Mwami, Jussa amekuwa kiwete huku nyie mnajiona wajanja
IMG-20201213-WA0000.jpg
 
Back
Top Bottom