Maamuzi Magumu: Nimeamua kuwa baba wa mtoto wa rafiki yangu

Maamuzi Magumu: Nimeamua kuwa baba wa mtoto wa rafiki yangu

Kweli nimeamini wanga wapo.
Mleta mada keshasema na kaweka wazi.
Kuwa yeye ana hudumia kijacho na mtoto atamhudumia na kumtayarishia maisha ya badae mtoto atakayezaliwa.
Inaonekana wengi hawajui nini maana ya ubaba.

Mwanamke awe malaya arudi kwa baba mtoto yeye havimhusu.
Yeye analea mimba na mtoto tu.
Dunia ya sasa ni ngumu kiasi hiki mpaka msiamini haya?

Kuna wanaume kibao wanaolea, kusomesha na kuwajengea watoto ambao si wa kwao na hawajui hata wametokea wapi ni just wameamua kuwapa furaha watoto hao na kuwatayarishia maisha ya baadae.
 
Il in reality ni ngumu sana kufanya hayo bila mama kutaka mahusiano na wewe
Wanawake wengi tunashindwa kutenganisha hilo.
Mwanaume akimpenda mtoto na akiwa wa karibu na mtoto automatically unajikuta upendo umejengeka, upendo ukiwepo wivu lazima uwepo.
Ni ngumu sana kutenganisha mapenzi hayo.
Wewe utakuwa na msimamo huo mwenzako ataanza kucatch feelings.

Mitego itaanza.

Kama ulichoandika ndo utakachofanya simama kwenye nafasi yako ukirudia kula tunda tu utaharibu kila kitu na future ya huyo mtoto.
 
Mkuu bado huwa unategemea shukrani.
Niliwahi kumfadhili rafiki yangu mwanaume kiasi cha 10m na mkewe 2m, walikuwa wanapitia kipindi kigumu sana hata petrol walikuwa wanashindwa kuweka japo wana gari 3.
Basi nami kilikuja kipindi changu cha shida, mkataba wa kazi uliisha kwa kampuni kufilisika.
Walilijua hilo...kuna siku nilimpigia simu akajua labda naomba pesa...alijifanya hanifahamu kabisa.
Ukitenda wema kimbia au sahau kabisa...ukisubiri shukrani umekwisha
Amini kua,una seat yako mbinguni
Mungu akubariki mno
 
Kweli nimeamini wanga wapo.
Mleta mada keshasema na kaweka wazi.
Kuwa yeye ana hudumia kijacho na mtoto atamhufumia na kumtayarishia maisha ya badae mtoto atakayezaliwa.
Inaonekana wengi hawajui nini maana ya ubaba.

Mwanamke awe malaya arudi kwa baba mtoto yeye havimhusu.
Yeye analea mimba na mtoto tu.
Dunia ya sasa ni ngumu kiasi hiki mpaka msiamini haya?

Kuna wanaume kibao wanaolea, kusomesha na kuwajengea watoto ambao si wa kwao na hawajui hata wametokea wapi ni just wamehamia kuwapa furaha watoto hao na kuwatayarishia maisha ya baadae.
Watu wana roho mbaya sana
 
Ulivutiwa nae mlipokutana ofisi flan,mkatongozana na mkakulana.

Akaenda kwa mpenz wake nche ya nchi kakuacha unamsubiria arudi

Wakazinguana na mpenz wake akarud na kabla hajakufikia akakutana na njemba ikambandua na chata ikaacha.

Akarudi kwako na badae akakwambia ana ujauzito na umekubali kuulea na kua baba wa hiari na et hautakua na mahusiano nae kimapenzi tena...jombaa zinduka huko usingizini hii Mambo ata ungekua malaika ni ngumu kueleweka..ningeamin Kama tu hamkuwahi kua na mahusiano Cha mhimu akijifungua Lea mtoto na badae piga na wewe chata yako hapo Mambo yatabalance.
 
Nilikuwa na kawaida ya kwenda kwa bro weekend. Mke wa bro ambaye ni shemeji yangu tulikuwa marafiki San. Shem alkuwa na marafiki zake watatu walioshibana hasa.
Mimi nikamzoea sana mmoja, tumpe jina la Mwajuma. Alikuwa ni mkimya sana weekend hiyo tofauti na nilivyomzoea. kama mwenye mawazo sana. Nikamuita shem pemben kuteta, kumuuliza mbona mwajuma leo anaonekana hayuko poa.

Shem akaniambia dogo kaharibu kwao. Amefukuzwa ana mimba. Nikiri taarifa ya shem ilinimaliza kabisa, kwani nilishaanza mpango wa kuwa nae mwajuma.
Nikamuomba mwajuma anipe nafasi ya kuongea nae.
Alinielezea kuwa mpenzi wake amemfukuza sababu ya mimba. Hataki hata kumuona. Mwajuma akaanza kulia nikamuacha alie kwanza.

Nikawa najiuliza kwann jamaa amfukuze demu wake sababu ya mimba? Au huyu dogo mwingi? Nikamsubiri amalize kulia

Itaendelea
 
Nilikuwa na kawaida ya kwenda kwa bro weekend. Mke wa bro ambaye ni shemeji yangu tulikuwa marafiki San. Shem alkuwa na marafiki zake watatu walioshibana hasa.
Mimi nikamzoea sana mmoja, tumpe jina la Mwajuma. Alikuwa ni mkimya sana weekend hiyo tofauti na nilivyomzoea. kama mwenye mawazo sana. Nikamuita shem pemben kuteta, kumuuliza mbona mwajuma leo anaonekana hayuko poa.

Shem akaniambia dogo kaharibu kwao. Amefukuzwa ana mimba. Nikiri taarifa ya shem ilinimaliza kabisa, kwani nilishaanza mpango wa kuwa nae mwajuma.
Nikamuomba mwajuma anipe nafasi ya kuongea nae.
Alinielezea kuwa mpenzi wake amemfukuza sababu ya mimba. Hataki hata kumuona. Mwajuma akaanza kulia nikamuacha alie kwanza.

Nikawa najiuliza kwann jamaa amfukuze demu wake sababu ya mimba? Au huyu dogo mwingi? Nikamsubiri amalize kulia

Itaendelea
Itaendelea lini sasa
 
Alikuwa mjamzito mara ngapi..???
IMG_20200817_100332_077.jpg
 
Hujui ya ulimwenguni ndugu, damu ni nzito kuliko maji. Damu isiyo yako lazima uwe na kiasi na mipaka juu yake kwani mwisho wa siku lazima ujute sana.

Ninachoweza kusema hukujipa nafasi ya kutafakari kuhusu uamuzi wako, ama ulifanya maamuzi kwa mihemko yako ama kwa sababu kwa sasa unaona huna majukumu zaidi.

Mwisho wa siku vipi akipata ujauzito wa mtoto mwingine kwa MTU mwingine, pia utaendelea kulea ama umeamua awe mke wako!! Kuna mengi ya kutafakari na si kukurupuka. Si swala jepesi kama unavyoweza kufikiri.

Pia jiangalie sana huyo mwanamke ni mwepesi sana na wewe ni mgeni kwenye maswala ya mahusiano na malezi
 
Alikuwa mjamzito mara ngapi..???View attachment 1539890
Mbona inaeleweka? Kwenye paragraph ya mwanzo bidada alimjulisha tu kuwa ni mjamzito ila hakumpa habari nyingine na huenda mtoa mada alijua ametoka nayo kwa mchumba wake...baadae akaja akamsimulia jinsi mambo yalivyokuwa na hadi kupata ujauzito
 
  • Thanks
Reactions: amu
NI MAAMUZI MAGUMU LAKINI YAMETOKA MOYONI

Wapendwa wana jukwa hili la mahusiano, mapenzi na urafiki ninawasalimu nyote.

Kama habari ya awali inavyosemaka kuwa nimechukua uamuzi mgumu wa kuwa baba mtarajiwa wa mtoto mtarajiwa wa rafiki yangu kwa hiyari na kwa kupenda mwenyewe kwa sababu nitakazo zieleza hapa chini, lakini kabla ya hizo sababu naomba nitoe ufafanuzi wa urafiki wetu.

Kuna dada mmoja tulikutana ofisi flani ya serikali, ni dada flani mpole kiasi na mcheshi kiaina. Kwa muda mfupi sana nilivutiwa naye na ikafikia hatua ya kubadilishana naye namba za simu.

Zoezi la huduma lilienda vyema kwa yeye kufanya koneksheni na mtumishi flani na tukafanikiwa kupata hiyo huduma (pass ya kusafiria kwa haraka)

Baada ya hapo hatukuwasiliana haraka japo nilipanga lazima nimtafute. Ulifika wakati tukaanza kuwasiliana hapa na pale. Na ukafika wakati nikawa nachomekea viutani kuwa ninamhitaji awe rafiki yangu.

Baada ya muda mrefu tulifanikiwa kuwa marafiki hatimaye tukaanza kushirikiana....hapa wakubwa mmeelewa. Jambo nililompenda zaidi ni mwelewa na mwenye misimamo yake mizuri. Tuliwekana wazi kuhusu mahusiano yetu, kwake yeye mpenzi wake alikuwa ni raia wa kigeni na anaishi huko kwao huja mara chache hivyo alikuwa anajiandaa kwenda kumtembelea na walikuwa wamepanga kuoana.

Nini kilitokea kati yao?

Uliwadia wakati wa kusafiri alinijulisha nami nilimpa nafasi ya kuwa mbali naye kimawasiliano ili ajiweke sawa na akili yake iwaze juu ya mpenzi wake. Alifanikiwa kwenda na kurudi. Baada ya kurudi mawasiliano yetu yalikuwa hafifu kwani nilikuwa tight sana na kazi.


Baada ya miezi kama mitatu na nusu, tuliwasiliana na kupiga stori nyingi na mwishowe akanijulisha ni mjamzito. Nikampa hongera zake. Lakini mawasiliano yakazidi kuwa hafifu zaidi. Ukafika wakati nikamuuliza maendeleo na mipango ya ndoa na kama wamepanga lini wataanza kuishi pamoja?

JIBU LAKE NDILO HASA LILINIGUSA NA KUAMUA HAYA
Rafiki yangu huyu alinishtua aliponieleza kuwa walitengana na yule mchumba kwani walipokutana ughaibuni alimfanyia visa vingi vibaya mno..sitavitaja

Na alipotua nchini alimtumia ujumbe kuwa asimtafute tena. Akiwa katika hali ya kutafakari yaliyompata na jinsi gani atasonga mbele...ndipo alianza mahusiano na jamaa flani aliyeanza kumnyemelea kitambo na muda mfupi akapata ujauzito.

Baada ya kupata ujauzito alimjulisha mhusika lakini hakuwa tayari kuukubali bali alimwambia autoe kwani yeye anafamilia lakini aligoma kuutoa na akajiapiza ataulea na kwa vile jamaa ameukataa hata jina litakuwa la upande wa familia yake yaani ubini wa baba.

Habari hii iliniumiza sana na niliwaza haya yafuatayo;
1. Kuwa huyu dada ataishi kwa sonono kubwa wakati wa ujauzito na atamwathiri mtoto akiwa tumboni wazazi wanajua hili

2. Huyu atakayezaliwa hatakuwa na upendo katika jamii na anaweza kuja kuwa na tabia ya ajabu

MAAMUZI YANGU
1. Nikamwomba kama naweza kuwa baba wa wa hiyari na apewe ubini wa jina langu kama baba alikubali hili kwa mshangao mkubwa sana (Haya[emoji116]sijamshirikisha)

2. Nitamhudumia kipindi chote cha ujauzito

3. Nitamfanya mwenye furaha ili kulinda afya mama na ya mtoto atakaye zaliwa

4. Baada ya mtoto kukua yeye yuko huru kuwa na maisha yake bila mimi kumwingilia uhuru wake

5. Nitampa mtoto kiwanja na kumjengea kadri Mungu atakaponiweka hai na kunibariki, ili apate malazi na malezi bora.

Uamuzi huu nimeufanya mwenyewe japo sipangi kuishi na mtoto isipokuwa kumsapoti kimalezi tu.

Baada ya kukubaliana naye hasa kuhusu mtoto kuitwa kwa jina langu kama baba, alifurahi sana kiasi cha kulia machozi na nikamwahidi kuwa siku chache zijazo atakuja mkoa nilipo apate mapumziko ya muda mfupi sio nyumbani kwangu lakini. Amemweleza mama yake mzazi na hajaamini kuwa kuna mtu anaweza kufanya maamuzi magumu kiasi hiki.

Pamoja na hayo sijamweleza kwa undani namna nilivyojipanga kumsapoti mtoto hasa kumpa eneo na kumjengea, hili nimebaki nalo nikiomba Mungu aniwezeshe kulitimiza.

Wapendwa wana jf, inaweza kuonekana kuwa uamuzi wangu ni wa kijinga sana lakini kwangu mimi nitaona fahari kubwa kama hili litafaniniwa kwani;

Sisi wanaume tunapaswa kuwa chemichemi ya furaha ya wake zetu, mama, watoto na dada zetu lakini kinyume chake tumekuwa ni chanzo cha machozi.

Tujitahidi sana kuwafanya watu kuwa na furaha badala ya machozi. Muwe na wakati mwema wote.
dah asante sana kwa hii mada, maana mimi ni mtunzi wa simulizi, hiki kida chako kitafaa sana kuchezewa muvi ya bongo muvi

sipati picha wewe nafasi yako asimame ray ama gabo zigamba, nomaa bado staa wa kike awe huyo rafiki yako, nadhani hapo kajala atafaa sana
 
Back
Top Bottom