Maamuzi ya kesi ndogo katika Kesi ya Mbowe na Wenzake kutolewa Oktoba 19, 2021

Maamuzi ya kesi ndogo katika Kesi ya Mbowe na Wenzake kutolewa Oktoba 19, 2021

Nilichojifunza kupitia kesi hii ni

1.kuwa Ujaji si kazi rahisi,inahitaji umakini na active mind muda wote!
2.Jambo jingine ni kuwa jeshi la polisi wanafanya kazi kama wapo juu ya sheria!
3.Mawakili wa serikali sio vilaza ila wanapewa mazingira magumu ya kufanya kazi yao mpaka wanaonekana watupu vichwani!Kutetea uovu si kazi rahisi,mwenye urahisi ni yule ambaye yupo upande wa haki japo wakati mwingine competence ya wakili inaweza kufanya haki kupatikana kwa ugumu!
 
Kwa hiyo Samia kwanini asitoe amri ya kufutwa hii case?
Hivi ni nani alisema kule BBC kuwa watuhumiwa wengine wa hii case walisha kiri makosa na kuhukumiwa?
Angekuwa haitaki hii case angeifuta toka mwanzo wakati Mbowe ana kamatwa.
Lazima tukubali hii case imechangiwa sana na vugu vugu la katiba mpya.....
Hii case ina ushawishi wa Rais aliyeko madarakani wala usitetee....
Samia ameishi kwenye uovu kwa miaka mitano. Ameuishi uovu kwa miaka 5. Ameufurahia uovu kwa miaka mitano. Hata akitaka kutoka, hawezi kutoka ghafla kwa 100%. Ni lazima ile roho ya uovu itaendelea kuwa ndani yake.

Hata pale anapokuwa na dhamira ya kutenda mema, kuna wakati atatumia uzoefu alio nao, ambao ni uovu.

Kwa hiyo kwenye hili kuna mkono wake na ile roho ya uovu aliyoiishi kwa miaka 5.
 
P
haya ni maneno ya faraja sana toka kwa Jaji, Ubarikiwe Jaji kwa kumtia nguvu shahidi, maana wamama huwa wana majonzi sana - anaweza kuanza kulia na kushindwa kutamka neno lolote lile
Pamoja na pongez kwa Jaj, ata huyu mama amekuwa jasiri. Yaan ushahid wa uongo na wa ukweli ni haraka kuwatambua...
 
Hapa nimejifunza kwamba polisi ndio hatari kuliko jambazi.
Ipo siku watalipia huo uhuni wao
IMG_20210922_171548.jpg
 
Yeye Kama Raisi na Kama mama mzazi, na Kama mke mwenye kuwa na watoto...

Sijui kwakeli ushahidi wa huyu mwanamke mwenzake alioutoa leo, anajisikiaje????

Naamin Atasikia huruma sana. Mumeo apotee, uanze kumtafuta adi mochwale, mizunguko yote hela ya Nauli ikuiishie, hapo hapo nyumbani umeacha mtoto mdogo.... Kwakwel apa Mungu mwenye haki asimame tu.
Samia ameishi kwenye uovu kwa miaka mitano. Ameuishi uovu kwa miaka 5. Ameufurahia uovu kwa miaka mitano. Hata akitaka kutoka, hawezi kitoka ghafla kwa 100%. Ni lazima ile roho ya uovu itaendelea kuwa ndani yake.

Hata pale anapokuwa na dhamira ya kutenda mema, kuna wakati atatumia uzoefu alio nao, ambao ni uovu.

Kwa hiyo kwenye hili kuna mkono wake na ile roho ya uovu aliyoiishi kwa miaka 5.
 
Siro na Samia walikosea sana kujitokeza hadharani na kuizungumzia hii kesi kua ushahidi upo,. Sijui walijiona akina nani kwamba watanzania na ulimwengu mzima unaweza kuhamini kauli zao, ona wanavyoumbuka


Unamkamata unaficha taarifa zake wakati ana familia, mke mtoto,wazazi kaka na eadogo zake, bado unaenda kwake unasachi bila yeye kuwepo u aondoka na hati ya nyumba pamoja na kadi ya pikipiki,. Bado mateso mliyompa, hati na kadi ya pikipiki havijulikani vilipo,

Bahati mbaya mtoto augue apoteze maisha kwa kukosa gharama za kulipia huduma, mke afariki kwa msongo wa mawazo, mwisho wa kesi adamoo aachiwe kwa kuonekana hana hatia, aisee

Akina Hamza mnawatengeneza wenyewe wakifanya tukio mnawatukana mpaka wazazi wao kua wana uzao wa hovyoo
 
Karibuni hapa kwa updates kutoka mahakama ya uhujumu uchumi kwenye kesi namba 16 ya mwaka 2021 inayomuhusu mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe na wenzake watatu...

Watuhumiwa tayari wamefikishwa mahakamani, leo shahidi wa tatu upande wa utetezi ataanza kutoa ushahidi wake.

View attachment 1956923


Mawakili upande wa Utetezi tayari wapo katika ukumbi wa Mahakama. Mawakili upande wa Mashtaka bado wapo Nje.

-------------------------------------------------------------------------​


Jaji ameshaingia Sasa Mahakamani, kesi inatajwa.

Wakili wa Serikali: naomba radhi tumeingia wakati umeshaingia

Jaji: sawa

Wakili wa Serikali: Kidando Wakili wa Serikali anatambulisha wenzake
1. Robert Kidando​
2. Nassoro Katuga​
3. Ignas Mwanuka​
4. Esther Martin​
5. Tulimanywa Majigo​

Kibatala: anatambulisha Wenzake
Adv. Peter Kibatala​
Adv. Jonathan Mndeme​
Adv. Fredrick Kiwhelo​
Adv. John Malya​
Adv. Sisty Aloyce​
Adv. Alex Masaba​
Adv. Idd Msawanga​
Adv. Gaston Garubindi​
Adv. Evaresta Kisanga​
Adv. Faraj Mangula​
Adv. Maria Mushi​
Adv. Bonifasia Mapunda​

Wakili Dickson Matata: anaombewa Ruhusa Mdogo wake anafanyiwa Operesheni Hospitali ya Lugalo

Jaji: Wakili wa Serikali

Wakili wa serikali: Tumekuja kwa ajili ya kesi ndogo ambapo Shahidi wa tatu yupo tayari kuendelea Kutoa Ushahidi wake

Jaji: John Mallya

Mallya: Tunaye, na Shahidi yupo tayari kutoa Ushahidi

Jaji: anaandika Kidogo na Ukimya wa Mahakama

Jaji: Shahidi wa 3 upande wa Utetezi ambaye ameandaliwa Tafadhali anaweza Kuja

Shahidi Mdada anatokea Nyuma kabisa ya Chumba Cha Mahakama anaenda Kizimbani

Jaji: Shahidi upo Mahakamani ondoa Hofu, nitakuuliza Majina yako na Nitakuapisha, Wakili wa Utetezi atakuongoza na Mawakili wengine watakuuliza Swali na Mawakili wa Serikali watakuuliza Maswali, pia huna Haja ya Kuogopa, tupo hapa kutafuta Haki.

Jaji: Shahidi unaitwa nani

Shahidi: Lilian Kibona, Dini Mkristo Shahidi Naapa Mbele ya Mahakama hii kuwa Ushahidi nitakao toa utakuwa Ukweli na Ukweli Mtupu, Mungu ni Saidie.

Jaji: Liliani utachagua Kukaa au Kusimama, Hata Ukikaaa nitakuona.

Jaji: wakili Mallya endelea

Mallya: Shahidi Unaishi wapi

Shahidi: Chalinze Mkoa wa Pwani

Mallya: sehemu gani huko Chalinze

Shahidi: Ramboni

Jaji: ni Mtaa.?

Shahidi: Ndiyo

Mallya: Unaishi na nani..?

Shahidi: Na mme wangu na Watoto ambaye kwa Sasa Mme wangu ameshikiliwa.

Jaji: ni Miongoni Mwa washitakiwa?

Shahidi: Ndiyo

Mallya: Mme wako anaitwa nani?

Shahidi: Adamu Khalfani Kasekwa

Mallya: hapa nitakuwa namuita Mshitakiwa wa Pili nitakuwa namaanisha pia ni yeye

Shahidi: ndiyo

Mallya: Mmeoana lini, 05/08/2016, Ndoa Ya Kiserikali

Shahidi: Ndiyo

Mallya: Mlikuwa mnaishi wapi

Shahidi: Pale pale Chalinze

Mallya: unaweza Kukumbuka Mme wako alikuwa anafanya kazi gani wakati huo

Shahidi: Askari Jeshi la JWTZ, kikosi cha 92 Ngerengere

Mallya: alikuwa anafanya kazi gani Nyingine

Shahidi: alikuwa hana kazi Nyingine zaidi ya hiyo ya Serikali

Mallya: naruka nakuja 2020 Mme wako alikuwa anafanya kazi gani

Shahidi: alikuwa anafanya shughuli zake za Biashara

Mallya: Mwanzoni Mwa Mwezi wa Nane Mwaka 2020 unakumbuka Kilitokea Kitu gani kati yako na Mme wako

Shahidi: Mme wangu alikuwa Moshi, tulikuwa tunawasiliana naye Vizuri

Mallya: Kabla ya Kwenda Moshi mlikuwa na Hali gani kati yako na Mme wako

Shahidi: Palikuwa na Mawasiliano

Mallya: kabla hajaenda Moshi kitu gani kilitokea

Shahidi: Rafiki yake Ling'wenya waliwasiliana kuwa kuna Kazi imepatikana Moshi

Mallya: Unaweza Kukumbuka Siku na Saa ya hayo mawasiliano

Shahidi: Hapana sikumbuki

Jaji: unasema palikiwa na Mawasiliano Kati ya Mme wako na Ling'wenya .?

Shahidi: Ndiyo Kwamba Ling'wenya alimpigia Simu kuwa kuna kazi Imepatikana Moshi

Jaji: Ndiyo

Mallya: Simu zilikuwa zinapigwa kati ya Ling'wenya na Mme wako, wewe ulijuaje

Shahidi: Mimi Kama Mke wake alinishirikisha, Mimi kama Mke nilimruhusu

Mallya: Jambo gani lilifanyika, kabla ya Mme wako kwenda Moshi

Shahidi: Nakumbuka walikutana na Ling'wenya wakaenda Kwanza Morogoro, Wakarudi, Waliporudi wakajiandaa Wakaenda Moshi

Mallya: Hali ya Mme wako kiAfya Wakati anaenda Moshi hali yake ilikuwaje

Shahidi: Ilikuwa Nzuri inamruhusu kwenda Kufanya kazi

Mallya: Hali Nzuri unamaanisha nini ,Mwambie Mheshimiwa Jaji

Shahidi: haumwi na Kwamba anaweza Kwenda Moshi

Mallya: kitu gani kilifuata baada ya Kwenda Moshi

Shahidi: alinitaarifu kuwa amefika Moshi

Mallya: mlikuwa mnatumia Njia gani kufanya mazungumzo

Shahidi: kwa Njia ya Simu

Mallya: Siku ya Tarehe 05/08/2020 kitu gani kilitokea

Shahidi: alinipigia na akaongea na watoto, tulipokuwa tunaongea akasema Hebu subiri nikamsubiri

Mallya: ilikuwa Saa ngapi

Shahidi: Kama Saa Moja

Mallya: alipokwambia Subiri kidogo nitakupigia Kidogo kitu gani Kilifuata

Shahidi: Nilipoona Muda umeenda ilipofika Saa 10 ilibidi nimpigie, Simu iliita ikawa imepokelewa lakini Kila nikisema Hallo Sisikii Mtu akiongea

Mallya: Unaweza Kukumbuka namba ya Simu uliyopiga, ambayo ulipiga Ikapokelewa.?

Shahidi: Sikumbuki Kichwani lakini ipo kwenye Simu yangu

Mallya: Baadae kilifuata nini baada ya Simu kutokupokelewa

Shahidi: baadae Ikawa haipatikani

Mallya: kitu gani Kilifuata

Shahidi: kwa kuwa nilikuwa na namba ya Mwenzake Ling'wenya nikampigia Ling'wenya

Mallya: baada ya Kumpigia Ling'wenya.?

Shahidi: Ikawa inaita Mpaka jioni, Mpaka Usiku, Mpaka Kesho yake inaita haipokelewi

Mallya: Sasa wewe ulipata hisia gani baada ya kuona Inaita hadi Kesho yake haipokelewi

Shahidi: niliona labda ni Mambo ya Kazi, sikuwa na wasiwasi wowote

Mallya: Wewe ulichukua hatua gani..?

Shahidi: Sikuwa na namna yoyote zaidi ya Kusubiri simu kutoka kwao

Mallya: umesema una mtoto, anaumri gani

Shahidi: Miaka 3 na Miezi 9

Mallya: Nataka kukupeleka Tarehe 09 Mwezi 08 kitu gani Kilitokea

Shahidi: nakumbuka ilikuwa tarehe 09 mwezi 08 Mwaka 2020 niliamka Asubuhi ikiwa siku ya Jumapili, Mtoto alikuwa anasumbuliwa na tumbo

Jaji: Mtoto wa Jinsia gani

Shahidi: Wa kike

Mallya: kwanini Unakumbuka kuwa ilikuwa Siku ya Jumapili

Shahidi: Sababu ilikuwa Siku ya Ibada

Mallya: Ikawaje

Shahidi: Sikwenda Ibadani badala yake nikaenda Hospitali

Mallya: ikawaje huko Hospitali

Shahidi: Nilipokelewa

Mallya: Hospitali gani

Shahidi: Hospitali ya Serikali pale pale Chalinze

Mallya: baada ya Kupokelewa Hospitali

Shahidi: nilipatiwa Huduma nikarudi Nyumbani

Mallya: baada ya Kurudi Nyumbani

Shahidi: niliona Miguu ya watu kama Imekanyaga, Wakati natoka Nyumbani nilifunga Mlango lakini niliporudi nikakuta Milango ipo wazi

Mallya: Ule Mlango ulikuwa katika hali gani

Shahidi: Mlango ulikuwa wazi na Kitasa nikakuta kimevunjwa

Mallya: kitu gani kikatokea

Shahidi: kwa akili ya haraka haraka nilijua Wezi, Cha ajabu kila kitu nilikuta Vipo, Kitu kama Tv lakini vipo

Mallya: enheeee ikawaje

Shahidi: Nikaingia Chumbani nikakuta Nguo zimemwagwa Chini

Jaji: Za Mme wako

Shahidi: zote zimemwaga,na Mabegi yamefunguliwa

Shahidi: Kuna begi la jeshi alinunua Congo nilipokuja nikakuta halipo

Jaji: ukisema begi la jeshi alinunua Congo unamaanisha nini

Shahidi: Alinunua Congo Begi lenye Mabaka Mabaka ya Jeshi

Mallya: Kitu gani kilifuata

Shahidi: Nilienda Kuuliza Majirani zangu

Mallya: Jirani yako anaitwa nani.?

Shahidi: Judith Charles

Mallya: lengo la kwenda kwa Jirani lilikuwa nini

Shahidi: nilienda Kuuliza kama Mme wangu amekuja Nyumbani.? wamemuona.? kwamba kuna kitu huenda alikuja Kukitafuta kwa haraka haraka

Mallya: Jirani alikwambiaje

Shahidi: Kuna Magari yalikuja hapa Ya Kipolisi, Moja walikuwa wamevaa Sare na Wengine walikuwa Wamevaa Kiraia

Mallya: Taarifa Nyingine alikupa Jirani yako ni Ipi

Shahidi: kwamba Mapolisi walimuita kwa lengo la Kuniulizia Mimi. baada ya hapo Mapolisi walishuka kwenye gari wakaingia Ndani

Mallya: yeye Jirani alikuwa anafanya nini wakati huo

Shahidi: alikuwa anashuhudia wakati wanaingia ndani ya Nyumba yako

Mallya: Kitu gani kingine walikufahamisha au Kumpatia

Shahidi: walisema walichukua Begi, Vyeti vyake vya Kijeshi vya Adamu, Walichukua Hati ya Uwanja, Kadi ya pikipiki

Mallya: Kitu gani Kingine alikwambia

Shahidi: aliongozana na Mkuu wa Upelelezi wa Chalinze

Mallya: aliyeongozana na Mkuu wa Upelelezi wa Chalinze alikuwa ameongozana na akina nani

Shahidi: Jirani yangu aliongozana na Mkuu wa Upelelezi na aliacha namba ya Simu kwa Jirani.

Jaji: kwa ajili ya Nini

Shahidi: alisema Kama Kuna Lolote ambalo hajalielewa ampigie

Mallya: Siku ya Jumapili 08 Mwezi 09 Nyumba imesachiwa na Umekuta namba ya simu ya Mkuu wa Upelelezi Chalinze, kitu gani Kilifuata baada ya hapo

Shahidi: nilimpigia Simu,yeye aliniambia kuwa alipigiwa tu simu kuwa inabidi waongozane kwenda Kusachi kwenye Nyumba ya Adamu Kasekwa

Mallya: alikufahamisha kuwa alipigiwa Simu na nani..?

Jaji: Mnasikia au Mvua inasababisha Kupoteza Usikivu tuhairishe kidogo.?

Jaji: labda nisikilize Mawakili

Mallya: Mheshimiwa Jaji naomba tubreak Kidogo kwa Sababu Shahidi akitumia Sana Nguvu anaweza kupoteza Energy na huenda akawa na siku Ndefu

Jaji: upande wa Serikali

Wakili wa Serikali: hatuna Pingamizi

Jaji: kama Mvua imeacha Kidogo, Hebu tuendelee Kidogo, Ikirudi na tukashindwa ,Tutaahirisha

Jaji: uliishia Kuhusu kumpigia simu Mkuu wa Upelelezi Chalinze

Mallya: nilimuuliza Mkuu wa Upelelezi alijibu Kitu gani

Shahidi: alisema amepigiwa simu Kutoka Moshi

Jaji: naona Mvua haitupi Muda wa kuendelea, siwezi Kukadiria kwa muda gani. Kwa muda Mchache nahairisha Shauri, Jaji anatoka Nje.

--------------------------------------------------------​


Jaji amerejea Mvua Imekatika Sasa Kesi inatajwa Kesi namba 16 ya Mwaka 2021,Jamuhuri dhidi ya Halfan Bwire, Adam Hassan Kasekwa (Adamoo), Mohammed Abdalah Ling'wenya na Freeman Aikael Mbowe

Jaji: wakili John Mallya tuendelee

Mallya: Baada ya Kuwa ameshakwambia kuwa alipigiwa simu Kutoka Moshi kitu gani kilifuata

Shahidi: Muda ulikuwa umeshaenda , nikasema itabidi Kesho yake niende kwa sababu sikuamini alichoniambia

Mallya: Kesho yake ikawaje

Jaji: Tunasikilizana, kama Mvua Inanisubiri Mimi, (Imeanza Kunyesha)

Mallya: Ulisema Ulienda Kituoni kesho yake wapi

Shahidi: Kituo cha Chalinze

Jaji: sasa ilikuwa Jumatatu

Mallya: tarehe 05 Umepigia Umemkosa, Tarehe 09 ukakuta kumesachiwa, Kitu gani kilitokea Tarehe 10 Ya Jumatatu pale Kituoni

Shahidi: Nikaomba Kuonana na Mpelelezi, Nilipo muona nikajitambulisha Kuwa Mimi ni Yule Dada ambaye Mmekuja Nyumbani Kusachi

Mallya: akakwambiaje

Shahidi: akasema kama nilivyokueleza sina ambacho nakijua zaidi ya Kuchukuliwa na kuwasindikiza Kwenda Nyumbani Kwako Kusachi,Sina ninachokijua Zaidi

Mallya: Wewe ulikuwa unafanya Jitihada gani zingine

Shahidi: nilianza kutafuta namba za Mke wa Ling'wenya

Mallya: awali ulituambia namba za Ling'wenya ulikuwa nazo na Ukampigia, za Mke wake unazitafuta, Za Ling'wenya ulitoa wapi

Shahidi: ni Mtu wa Karibu wa Mme wangu, Rafiki yake, tuseme siku wanaondoka walikuwa naye

Mallya: ulitumia Njia gani za Kupata namba za Mke wa Ling'wenya

Shahidi: nilimtafuta Mwenzao SHIKUNZI aliyekuwa anaishi nao Kimara

Jaji: Mwenzao, Kwamba alikuwa Askari Jeshi

Shahidi: Ndiyo

Mallya: alikuwa kimara anakaa na nani

Shahidi: alikuwa anakaa karibu na Ling'wenya

Mallya: kikichokufanya Umtafute SHIKUNZI ili umtafute Mke wa Ling'wenya ni nini.?

Shahidi: Nilitaka kumuuliza Mke wa Ling'wenya ili Kumuuliza huko kwake ni nini kilikuwa kinaendelea.?

Jaji: Kwanini hukumtafuta SHIKUNZI.?

Shahidi: walikuwa ni Majirani

Mallya: SHIKUNZI akafanyeje..?

Shahidi: alinipatia namba ya Mke wa Ling'wenya

Mallya: ulifanya hatua gani..?

Shahidi: nilimpigia Mke wa Ling'wenya Ilikuqa siku ya Jumatatu, na yeye akaniambia Siku ya Jumapili ambayo ni Jana yake walienda Nyumbani Kwake wakafanya Upekuzi

Mallya: nini kilifuata baada ya hapo

Shahidi: akaniambia baada ya hapo walienda Kwa Mwingine anaitwa Bwire, tumtafute Mke wa Bwire. nikamwambia wewe huko ni Jirani Mtafute Mke wa Bwire

Mallya: Kitu gani alikueleza Mke wa Ling'wenya

Shahidi: kwamba nilitaka Kujua kama kwake walienda kusachi akaniambia Wameenda kusachi, akaniambia pia tutafute Mke wa Bwire

Mallya: ulipata namba ya Mke wa Bwire na Unaweza kukumbuka Majina yao

Shahidi: Mke wa Bwire anaitwa mama Itham na Mke wa Ling'wenya anaitwa Mama Somoye

Mallya: nini Kinafuata

Shahidi: Mke wa Bwire alikuwa Dar es salaam anakasema Inabidi nitoke Chalinze nije Dar es salaam

Jaji: alisema utoke wapi.?

Shahidi: Chalinze nije Dar es salaam

Mallya: hii sintofahamu yote ilitokana na nini

Shahidi: Kutokana na kutokujua Mwenza wangu yupo wapi, namtafuta simpati alafu Nyumbani wamekuja Kusachi

Mallya: baada ya Kushauriwa Ulichukua hatua gani

Shahidi: Nilitafuta Nauli nikaja Dar es salaam

Mallya: ilikuwa lini.?

Shahidi: Sikumbuki

Mallya: Baada ya Kufika Dar es salaam nini Kilifuata

Shahidi: tulishauriana tuanze Kutafuta Vituo Vyote vya Polisi

Mallya: unaweza Kujua Nyumbani Kwake Bwire

Shahidi: Maeneo ya Temeke

Mallya: Unaweza kukumbuka mlianzia Wapi

Shahidi: Kituo cha Polisi CHANG'OMBE

Mallya: halafu

Shahidi: Tukajitambulisha kuwa sisi Waume zetu Wamekamatwa hatujui wamepelekwa Kituo gani

Mallya: mlimkuta Polisi gani

Shahidi: Polisi wa zamu

Mallya: Mkajitambulishaje..

Shahidi: Kwa Majina yetu na Waume zetu

Mallya: baada ya hapo yule Askari alifanyeje

Shahidi: akaanza kupekua Kitabu kwa kuangalia yale Majina ya waume zetu hatukuyaona

Mallya: Baada ya Kutoyaona Majina ya Mnaowatafuta Kitu gani Kilifuata

Shahidi: tulienda kituo Kingine

Mallya: Kituo gani

Shahidi: Central Police Dar es salaam

Mallya: Ikawaje

Shahidi: vile vile tukajitambukisha ya kwamba, sisi waume zetu wameletwa polisi na hatujui Kituo gani

Mallya: baada ya Kujitambulisha kwa Askari nini Kilifuata

Shahidi: aliangalia kile Kitabu hakuona yale Majina yetu

Mallya: wakati anaangalia Majina ya waume zenu Nyie Mlishiriki Vipi

Shahidi: Wakati anaangalia Kitabu, Wote tuliinama kuangalia Majina ya Waume zetu kwa usahihi

Mallya: Mmeangalia pamoja na Askari Majina ya wenza wenu hamjayaona, nini Kiliendelea baada ya hapi

Shahidi: tulitoka Kituo vha Polisi Central Police tukaenda Oysterbay, Tukajitambulisha kwa Askari wa zamu akaangalia kwenye kitabu, Majina yao, hayakwepo

Mallya: baada ya Kuwakosa Central nini kilifuata

Shahidi: tulienda Tazara

Mallya: unaweza Kueleza Kwanini Mlienda Tazara

Shahidi: tulienda kwa Sababu tulikuwa kwenye Kuendelea kuwatafuta Kituo gani cha Polisi wamepelekwa

Mallya: Unaweza Kuiambaia Mahakama mara zote mlipokuwa mnatafuta mlikuwa mnawatafuta kwa Namna gani

Shahidi: mara zote tunataja Majina na Mimi nilitaja Jina la Mme wangu Adamu Khalfani Kasekwa

Mallya: Kitu gani Kilifuata

Shahidi: Hatukuyaona Majina yao

Mallya: Mmeshaenda Vituo Vinne Kutafuta wenza wenu, hatua gani ilifuata baada ya hapo

Shahidi: Tulirudi Nyumbani kwa sababu Muda ulikuwa umeenda na tuliacha watoto wadogo

Mallya: Nyumbani kwa Maana Wapi

Shahidi: Kwa Mke wa Bwire

Mallya: kwa Mazungumzo yako na Mke wa Bwire alikwambia nini kimetokea Kule Moshi

Shahidi: akaniambia Kule Moshi kuna wifi yake ambaye ni Dada wa Mohammed Abdilah Ling'wenya

Jaji: twendeni Taratibu, Mmeshazunguka Vituo Vyote ilikuwa siku gani..?

Shahidi: Tarehe 13

Jaji: ooohhh tunakosa Mtiririko kwa sababu nilikuwa bado nipo kwenye Vituo Vya Polisi

Mallya: Samahani Mheshimiwa Jaji nilirudi Nyuma Kumuuliza kama waliongea na Mke wa Bwire

Mallya: alikwambia nini sasa

Shahidi: Kwamba Wifi yake amempigia Simu Kuwa Adam wakiwa Moshi na Mohamed, akiwa anakunywa Chai Adamu alikuwa anazungumza na Simu, ikawa kama kelele za Mvutano, Niache niache baada ya hapo wakawa wanamvuta Kumleta Sehemu za Vyakula sasa.

Mallya: Nini kilifuata

Shahidi: Kwamba alikuwa amepigwa akawa anavuja Damu

Jaji: hii ni Habari ambayo umesema Umeambiwa na Mke wa nani..?

Shahidi: Mke wa Ling'wenya Tukiwa kwa Mke wa Bwire

Mallya: huyo wifi yake anaitwa nani.?

Shahidi: anaitwa Athima

Jaji: nafikiri tulirudi kwenye Mstari hapo tunaanza kuzungumzia "Here say" yeye kaambiwa na Mke wa Ling'wenya na Mke wa Ling'wenya kaambiwa na Wifi nafikiri Mkiona Kuna Umuhimu mumwite Wifi yake aje kutoa Ushahidi ila Hatuwezi Kwenda hivyo.

Mallya: sawa Mheshimiwa Jaji

Mallya: Mliporudi Nyumbani ikawaje

Shahidi: tulikubaliana tupite Hospitalini

Mallya: Mlikuwa na Nyenzo gani katika Kuwatafuta

Shahidi: Tulikuwa na Picha zao

Mallya: Mlianzia Wapi

Shahidi: tulianzia Hospitali ya Muhimbili

Jaji: Kwanini Mlianza Kuwatafuta Kwenye Mahospitali

Shahidi: Ni baada ya Kuwakosa Kwenye Vituo vya Polisi

Jaji: Kwa Off Record tu, Moshi waliwambiaje

Shahidi: kwamba huku hawapo wameletwa Dar es salaam tukahisi labda wamepata Ajali

Mallya: Mlipofika Muhimbili ikawaje

Shahidi: Tukajitambulisha na Kueleza kuwa tunawatafuta Waume zetu, tulizunguka Kwenye wodi na Monchwari hatukuwaona

Mallya: nini Kikafuata

Shahidi: Tukaenda Hospitali ya Amana, Tukajitambulisha na Kuingia Kwenye Mawodi na Monchwari hatukuwaona pia

Mallya: baada ya Amana .?

Shahidi: tulienda Mwananyamala tukajitambulisha na Kuwatafuta waume zetu kwenye Mawodi na Mochwari hatukuwaona

Mallya: Siku ya tatu Sasa Mmeanda Muhimbili, Amana na Mwananyamala mkawakosa, Ulichukua hatua gani

Shahidi: ilibidi nirudi Chalinze kwa Sababu nauli ilikuwa imeshaaanza kuisha na Kwa sababu nina wawasiliano ikabidi nirudi Chalinze

Mallya: baada ya Kurudi Nyumbani, kwa Mara ya kwanza Ulipata Taarifa ya Mume wako yupo wapi

Shahidi: Ilikuwa kwenye Taarifa Ya Habari ya Jioni

Mallya: uliwaona wakiwa wapi

Shahidi: Mahakamani Kisutu Mallya Kituo gani Cha Habari

Shahidi: ITV

Mallya: Uliwaona au Ulisimuliwa

Shahidi: niliona

Mallya: wanatuhumiwa kwa Makosa gani

Shahidi: Anashitakiwa kwa Ugaidi na uhujumu Uchumi

Mallya: mara Ya Mwisho Mme wako wakati anakuaga alikwambia anaenda Moshi Kufanya nini

Shahidi: kwamba Kuna kaz Imepatikana anaenda kuifanya

Mallya: ikawaje

Shahidi: Niliwasiliana na wenzangu

Mallya: Uliona hiyo Taarifa ya Habari ITV saa ngapi

Shahidi: Ilikuwa Saa 2 za Usiku

Mallya: mkafanya Mawasiliano, Mawasiliano gani

Shahidi: tulikubaliana Twende Mahabusu kwa Sababu hatukujua wamepelekwa Mahabusu gani

Mallya: Baada ya hapo nini kilifuata

Shahidi: Mzee Ling'wenya alikuja kutoka Mtwara

Mallya: kitu gani alifanya baada ya Kutoka Mtwara Mzee Ling'wenya

Shahidi: Tulikuwa hatuelewi wapo Mahabusu gani, Tulianza kutafuta Mahabusu waliopo

Mallya: mlianza kutafuta Mahabusu gani

Shahidi: Mimi sikwepo nilikuwa Chalinze, Tulifanya Mawasiliano

Mallya: wakakwambiaje

Shahidi: Kwamba wameenda Keko wamewakosa ila Segerea Wamewakuta wapo

Jaji: ni akina nani

Shahidi: Mke wa Mohammed Abdilah Ling'wenya na Mzee Ling'wenya

Jaji: Mke wa Ling'wenya na nani..?

Shahidi: Na Baba Mkwe wake, Mzee Ling'wenya

Mallya: sasa Ushajua Mwenza wako yupo Segerea hatua gani ilifuata

Shahidi: Nilikuja Jumapili kutoka Chalinze, Jumatatu tuliamka wote Mke wa Bwire, Ling'wenya tukaenda Wote Segerea

Mallya: Mlipofika Segerea ikawaje

Shahidi: Tulipokelewa na Askari wa Jinsia ya kike akatueleza leo siyo siku ya kuwaona Mahabusu Mje Jumamosi au Junapili

Mallya: baada hapo ulifanya Hatua gani

Shahidi: Nilienda Jumamosi

shahidi: nilisikia Ma ASKARI wakisema ndiyo Yule Jamaa ambaye yupo Kabatini

Mallya: ni nani aliteyaongea hayo

Shahidi: ni Ma Askari niliowaleza Majina kuwa namtafuta Mme wangu

Mallya: hatua gani ilifuata

Shahidi: Wakachukua funguo wakasema tunaenda kumleta

Mallya: unaweza Kutuambia hapo ulipokuwepo pana taswira gani ili Mheshimiwa jaji apate Picha

Shahidi: Ukiingia Segerea maeneo ambayo kuna Meza ya Kuwekea Chakula na Kuna Chuma kama Grill lililotenganisha

Mallya: Kitu gani kilifuata

Shahidi: nilimuona Mume wangu akitembea Kwa tabu kama Vile inaonekana ameteswa

Mallya: Unaeeza Kukumbuka Mume wako alikuwa amevaaje

Shahidi: Alikuwa amevaa kama Singlendi

Mallya: hali yake ilikuwaje

Shahidi: Amedhoofika, alikuwa amekonda Sana

Mallya: Mwendo wake ulikuwaje, alivyokuwa anatembea.?

Shahidi: alikuwa anachechemea

Mallya: Ulichukua hatua gani

Shahidi: Kama Utaratibu ulivyo wa pale, Nilibeba vitu kwa ajili yake

Jaji: ukikuwa umeleta Vitu gani

Shahidi: Chakula, shuka na Sababuni

Jaji: Vitu ulimkabidhi nani.?

Shahidi: Askari akishakagua anachukua ukiwa unamuona

Mallya: ulisema ulikuwa unamuona Mume wako anaelekea sehemu, Ni sehemu gani

Shahidi: Eneo la Nyavu ambalo mnaweza Kuzungumza

Mallya: ilikuwaje Mazungumzo kati yenu

Shahidi: Nilimuuliza Hali yake na Kilichotokea

Mallya: alikujibu nini

Shahidi: HaLi yangu ni hivyo hivyo ila siyo Nzuri

Mallya: alikwambia kwanini hali yake siyo Nzuri

Shahidi: aliniambia Kuna Mateso alipitia wakati yupo Moshi, alipigwa sana Ndiyo Maana Unaniona nipo Kwenye hali hii

Mallya: Baada ya Hapo.?

Shahidi: alichukuliwa akapelekwa Mahabusu

Mallya: nitakurudisha Nyuma Kidogo, Kilichokufanya utamtafute Vituo vya Polisi na Mahospitali Mume wako ni Kitu gani

Wakili wa Serikali: OBJECTION wakili ameshauliza

Mallya: Sikuuliza, Kama aliulizwa ni Off Records nataka sasa iingie kwenye Records

Wakili wa Serikali: Ameshaliuliza hilo swali

Jaji: Sijachoka Kuandika, Muuulize tena

Mallya: nitakurudisha Nyuma Kidogo, Kilichokufanya umtafute Vituo vya Polisi na Mahospitali Mume wako ni Kitu gani.

Shahidi: Kwa sababu tuliambiwa kuwa Walitolewa Moshi Kuja Dar es salaam na tulienda Vituo Vya Polisi Kwa Sababu tuliamini Kama wangetusaidia

Mallya: Vipi Kuhusu Ushiriki wa Ndugu zake Mwanamme

Shahidi: alikuja Mama yake, tukaenda naye Moshi

Mallya: Kwanini wewe namba ya Mume wako umesema huikumbuki kwa kichwa miye ya Mke wangu naikumbuka

Shahidi: Kwa sababu alikuwa na line Mpya aliyotoka Kuisajili

Mallya: Kwanini Unasema Ulipoenda Segerea hali yake ilikuwa tofauti

Shahidi: alikuwa amekonda sana na Macho yameingia Ndani Kama Yameganda, amekonda kwa kweli na Pia Nilimuona akiwa na alama Kwenye Mkono wakati anaenda Moshi alikuwa hana

Jaji: ulisema Uliona nini Kwenye mkono

Shahidi: alama ya Kovu kwenye Mkono, Awali alikuwa hana wakati anaenda Moshi

Mallya: ya kwangu ni hayo

Jaji: Asante sana Mallya

Jaji: pamoja na Mvua kutuharibia ratiba yetu, lakini tutabreak tena kidogo tutarejea Saa 6 Kamili, Jaji ananyanyuka anatoka.

------------------------------------------------------------------​

Jaji amerejea

Shahidi anapanda tena Kzimbani

Kesi inatajwa na Washitakiwa wanakaa Kizimbani Kwao

Jaji: Wakili Nashon kama Unaswali lolote

Nashon: Sitokuwa na Swali Kwa Shahidi

Jaji: Wakili Fredrick Kihwelo kama Unaswali.?

Fredrick Kihwelo: sitokuwa na Swali kwa Niaba ya Mshitakiwa wa tatu

Jaji: Wakili Kibatala kwa niaba ya Mashtakiwa wa Nne

Kibatala: Shahidi Ulijisikiaje uliporudi Nyumbani Kukuta Nyumba yako Imevunjwa na Mume wako alikuwa hapatikani Muda wote

Shahidi: Niliogopa Kwanza Nilihisi ni wezi

Kibatala: Ulitegemea kuwa Polisi wanaweza kufanya hivyo.?

Shahidi: Hapana sikuwahi Kutegemea Polisi wanaweza Kufanya tendo hilo

Kibatala: Umeongelea kwamba Ulikuta Tv na Vingine Vipo, ila Kadi ya Pikipiki na Hati ya Kiwanja Vilikuwa Vimechukuliwa

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Mpaka leo hii hujawahi kuambiwa kuwa nani anahivyo hivo vitu, Kituo cha Polisi Chalinze au afisa yoyote wa Polisi

Shahidi: Hakuna aliye wahi Kuniambia

Kibatala: Mpaka leo hii hujui nani wa Kumdai hivyo Vitu

Shahidi: Sahihi sijui nani nimdai

Kibatala: Kuna Mgogoro wowote wa Kiwanja sehemu unayoishi au Kupelekwa hata Kwa Mjumbe

Shahidi: Hapana

Kibatala: Ushawahi Kujua Kwanini Adamoo alisimamishwa kazi au Utumishi wake wa Kijeshi Ulivyokomea

Shahidi: Nafikiri huko kwenye Mambo ya Kijeshi tusiende Sana Miye sijui lolote kuhusu Jeshi

Kibatala: Sawa tuachane na hilo

Kibatala: nimesikia kuwa ulienda Kumtafuta Mumeo Vituo Vya Polisi, Naomba Nikuonyeshe Kielelezo Namba 1 Kitabu fulani Mahakama inampatia Kibatala Kielelezo DETENTION REGISTER

Kibatala: unasema ulienda Polisi ukaoneshwa Kijitabu kama hiki au Kinachofanana na Hiki na bado baada ya Kupekua hukuona Jina la Mumeo

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: unasababu yoyote ya Kutunga Story ya Uongo kuwa Hukwenda Polisi Central alafu leo Uje useme ulienda Polisi Central, Je unasababu yoyote ya Kutunga.?

Shahidi: Hapana sina Sababu yoyote

Kibatala: Nimesikia Kuwa kilichowafanya Muanze Kutafuta Dar es salaam baada ya Mke wa Ling'wenya, Kuwasiliana na Dada yake Ling'wenya Kule Moshi, akasema kuwa Adamoo na Ling'wenya Wameletwa Dar es salaam, je nilikusikia Sahihi

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Nimekusikia Sahihi Kuwa Mlipita Kote ikiwemo Chang'ombe, Central Station, na Tazara pamoja na Vyumba Vya Kuhifadhia Maiti kwa sababu ya Kukosa Taarifa.?

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Mlilazimika Kufunguliwa Mwili Mmoja baada ya Mwingine Kwenye vyumba vya Kuhifadhia Maiti

Shahidi: Ndiyo Nililazimika Kufungukiwa Mahiti Moja baada ya Nyingine ilikuweza kuthibitisha kama Mume yupo huko

Kibatala: Ni sahihi Kwamba wakati unapitia hali hii ulikuwa na Miaka 25 tu.?

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: na Wakati huo ulikuwa na Mtoto Mdogo

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: wakati huo Ulikuwa kwenye Ndoa kwa muda gani Mpaka unapitia Matukio haya Mazito

Shahidi: Mitatu

Jaji: Hesabu zenu zipo Vizuri.? kutoka 2016 August Mpaka 2020 ni Miaka Mingapi

Kibatala: Minne

Jaji: naona hakuna tatizo Mtu kukosea hesabu Mahakamani, Hilo swali tunaweza Kuliacha

Kibatala: ni Sahihi wakati nakuja kupekuliwa Ilikuwa ni Kabla ya Tarehe 09 au ni baada ya tarehe 09

Shahidi: ni baada ya Tarehe 09

Kibatala: Asante Mheshimiwa Jaji ni hayo tu

Jaji: Shahidi una nguvu za Kuendelea Kujibu?

Shahidi: Ndiyo tuendeleee

Jaji: wakili gani Serikali ataanza Kuuliza Maswali

Wakili Kidando: ataanza Jenitreza Kitali

Wakili wa Serikali: Ni sahihi Shahidi Umesema Adamu ni Mume wako

Wakili wa Serikali: Ni sahihi ujatoa Cheti Cha Ndoa

Wakili wa Serikali: Ni sahihi umesema Kuwa Adamu walikuaga wakati wanaenda Moshi Mwanzoni Mwa Mwezi wa nane

Shahidi: ni sahihi

Wakili wa Serikali: ni kweli umeeleza Kuwa walikuaga wakati wanaenda Kwa Mheshimiwa Mbowe

Shahidi: Sahihi

Wakili wa Serikali: ni kweli au Si Kweli Mume wako na Ling'wenya walikuwa marafiki sana

Shahidi: Ni kweli

Wakili wa Serikali: Mume wako pamoja na Ling'wenya waliondoka Pamoja Chalinze, Sahihi.?

Shahidi: Sahihi

Wakili wa Serikali: wakati Mume wako anajianda Kwa ajili ya Safari, Mazingira ya Nyumba yenu yakoje

Shahidi: Nyumba ya Vyumba Vinne, Kuna Sebule, Dinning na Choo

Wakili wa Serikali: Wakati Mumeo anajiandaa na Safari nitakuwa sahihi nikisema Kuwa Adamu alikuwa ndani ya Chumba wakati Mgeni akiwa Sebuleni

Shahidi: Sahihi Mgeni alikuwa sebuleni

Wakili wa Serikali: Katika Ushahidi wako Mwanzo Mpaka Mwisho ujasema ni lini walianza Safari

Shahidi: Sikusema, Sikumbuki ilikuwa tarehe ngapi

Wakili wa Serikali: nitakuwa sahihi nikisema kama ukumbuki tarehe na unachokisema siyo sahihi

Shahidi: sikumbuki tarehe lakini walianza Kusafiri pamoja Mwishoni mwa Mwezi wa Saba

Wakili wa Serikali: baada ya Adamu na Ling'wenya Kufika Moshi ulipewa taarifa kwamba Wamekamatwa.?

Shahidi: Niliambiwa

Wakili wa Serikali: aliyekwambia ni Mke wa Ling'wenya, nitakuwa sahihi kuwa Mtu aliyekwambia wamekamatwa Moshi siyo Mtu aliyekwepo wakati wanakamatwa Moshi

Shahidi: ni sahihi

Wakili wa Serikali: Naomba Nikurejeshe Nyuma, Wakati Mumeo anajianda na Safari, Ling'wenya aliakuwa sebuleni, Ni kweli Ling'wenya hakujua Vitu gani Vimewekwa Katika begi

Shahidi: ni sahihi hawezi Kujua

Wakili wa Serikali: Ni sahihi Kwamba hujaiambia Mahakama kwamba wakati Mumeao anapakia Vitu vyake alibeba Vitu hivi na hivi

Shahidi: Si kweli

Wakili wa Serikali: Ni kweli umesema Kwamba Adamu alipigwa Moshi Mpaka akatoa damu

Mallya: OBJECTION hicho anachouliza Tayari Mahakama ishatoa Malekezo kuhusu Here say

Jaji: Wakili wa Serikali

Wakili wa Serikali: labda Mahakama ituonyeshe kama Ilitoa Muongozo huo

Jaji: ngoja niseme kuwa wakati tunaanza zoezi nilisema Vitu ambavyo Shahidi anaweza asiulizwe ni Vile Vinavyotezwa Utu wake

Jaji: sasa Vingime Vyote unaweza Kuuliza na anaweza Kujibu

Wakili wa Serikali: ulisema ulisikia kuwa Adamuu amepigwa Mpaka Kutoa Damu

Shahidi: kweli

Wakili wa Serikali: Umesema Ulisema kuwa baada ya Kuwa hapatikani kwenye simu mlianza kumtafuta Vituo vya Polisi

Shahidi: Sahihi

Wakili wa Serikali: Mlianza kituo gani cha Polisi

Shahidi: Kituo cha Polisi Chang'ombe

Wakili wa Serikali: Mlipofika Kituo cha Polisi wewe na wenzako mlianza Kuomba Huyo Mtu aangaliwe kama yupo Kituoni hapo

Shahidi: Ndiyo Wakili wa Serikali: ilikuwa tarehe ngapi

Shahidi: tarehe 13 Mwezi wa 09

Jaji: Mwenzi wa Ngapi.?

Shahidi: Mwezi wa 08

Jaji: sasa niandike lipi Mwezi wa 08 au 09

Shahidi: Mwezi wa 08

Wakili wa Serikali: Utakubaliana na Mimi kuwa wakati Nyumba inasachiwa hukuwepo

Shahidi: ndiyo nimeeleza

Wakili wa Serikali: Kwa hiyo Maneno ya kwamba Kuna Vitu vimechukuliwa ni Maneno ya Kuambiwa

Shahidi: Ndiyo

Wakili wa Serikali: Baada ya Kukosekana Adamu Mpaka wakati unamtafuta hukuwahi Kumtafuta Mheshimiwa Mbowe mbali na Kwamba walikwambia wanaenda Moshi kufanya kazi kwake

Shahidi: Ndiyo sikumtafuta

Wakili wa Serikali: ujaieleza mahakama kwamba Wakati Mnaenda Mochwari mlifuata Utaratibu wa kukagua

Shahidi: Nilifuata Utaratibu

Wakili wa Serikali: Lakini wakati unatoa Ushahidi Hukusema ni Taratibu zipi ulizifuata.?

Shahidi: Ndiyo

Wakili wa Serikali: Wakati wote wa Shauri hili linaendelea Mahakamani ulipata kulifuatilia.?

Shahidi: Ndiyo

Wakili wa Serikali: Kwa Njia gani

Shahidi : vyombo vya habari

Wakili wa Serikali: Kwa kuwa ulikuwa unafuatilia Kesi hii kwenye vyombo Vya Habari na Kwa kuwa Ushahidi uliokuwa Unaendelea Kuwa Adam Kasekwa kateswa, Ni sahihi Ulisikia

Shahidi: Nilisikia kupitia Vyombo vya Habari na Yeye pia aliniambia

Wakili wa Serikali: Ni sahihi kwamba Wakati Mumeo anaelekea Moshi alikuwa ni Mzima wa Afya na hakuwa na Majeraha

Shahidi: Ni sahihi

Wakili wa Serikali: wakati unamtembelea Segerea Uliona Makovu, Je uliyaona wapi

Shahidi: Niliona Kwenye Mikono

Wakili wa Serikali: Kwenye Mikono yote Miwili

Shahidi: Ndiyo

Wakili wa Serikali: Wewe kama Mke wa Adamu kasekwa utakubaliana na Mimi kuwa Unaieleza Mahakama kama Adam Kasekwa aliwahi Kuwa na Makovu Mengine kabla ya wewe Kumkuta na hayo segerea

Shahidi: Ni sahihi

Wakili wa Serikali: Adamu Kasekwa alipokuwa Segerea, Mshitakiwa alimweleza kuwa amepigwa

Shahidi: Ndiyo baada ya kuona anachechemea

Wakili wa Serikali: lakini hukueleza Mahakama kama alipigwa Wapi na lini

Shahidi: Sikueleza lini

Wakili wa Serikali: Unaifahamu sana Dar es salaam

Shahidi: Kiasi Kidogo

Wakili wa Serikali: Ulisema Ulitembelea Vituo vya Tazara, Chang'ombe, Central na Oysterbay

Shahidi: Ndiyo

Wakili wa Serikali: Hukuiambia Mahakama Sababu ya kwanini hukutembelea Vituo Vingie vidogo

Shahidi: Ni sahihi sikusema Sababu

Wakili wa Serikali: Ni sahihi ulimuona Adamu amakonda sana

Shahidi: ni Sahihi

Wakili wa sarikali: hukuieleza Mahakama kwanini alikonda

Shahidi: Ni sahihi sikueleza Sababu za Kukonda

Wakili wa serikali: naomba Niwachie wenzangu

Anasimama Wakili Robert Kidando

Wakili wa Serikali: Mpaka siku Nyumba yako inafanyiwa Upekuzi, Ni kweli ulikuwa ujui Adam yupo wapi.?

Shahidi: Ndiyo

Wakili wa Serikali: Uwezi Kujua kama alikuwa ameridhia

Shahidi: Sijui

Wakili wa Serikali: Mpaka sasa Askari waliovaa Uniforms Ujui walikuwa ni akina nani.?

Shahidi: Sijui

Wakili wa Serikali: na Mpaka sasa wale waliovalia Kiraia hujui walikuwa wakina nani

Shahidi: Ndiyo sijui kwa sababu Sikwepo

Wakili wa Serikali: na pale Chalinze Mtaa wako Unapoishi unasema unaitwaje

Shahidi: Ramboni

Wakili wa Serikali: Na Nyumba yako bila shaka itakuwa na Grill/Geti

Shahidi: Ndiyo

Wakili wa Serikali: ulikuwa umelifungwa

Shahidi: hapana huwa naurudishia, Mlango ndiyo huwa nafunga

Wakili wa Serikali: Baada ya kwenda kwa Jirani yako Kuuliza alikwambia Mwenyekiti wa Mtaa alikwepo.?

Shahidi: Hapana alikwepo Mjumbe wa Nyumba 10

Wakili wa Serikali: Mpaka sasa yupo pale Chalinze

Shahidi: Ndiyo

Wakili wa Serikali: Unasema uliambiwa Kuwa Wamechukua begi la Adamu alilotoka nalo Congo, Je lipo tofauti na Sare za Jeshi la JWTZ

Shahidi: Lipo tofauti na Mabaka Mabaka ya Tanzania

Jaji: weke Vizuri mabaka mabaka ya Nini, Isije kuwa unasema Watanzania Wanamabaka Mabaka

Mahakama Kichekooooooo

Shahidi: Mabaka Mabaka ambayo ni Maua ya Sare za JWTZ yapo tofauli na Mabaka mabaka ya lile begi

Jaji: hapo Umeweka Sawa

Wakili wa Serikali: Ni sahihi Ukumbuki tarehe ambazo waliondoka Kwenda moshi

Shahidi: Ndiyo Sikumbuki

Wakili wa Serikali: Kwa hiyo Inaweza ikawa hata Mwishoni mwa Mwezi wa 07

Shahidi: Ndiyo inawezekana

Wakili wa Serikali: hujaieleza mahakama kama Mumeo aliondoka na kiasi gani cha fedha

Shahidi: Sijaeleza

Wakili wa Serikali: hujaeleza Kwamba wakati wanaenda Moshi Walitumia usafiri gani.?

Shahidi: Sijaeleza Ila walitumia Usafiri wa Basi

Wakili wa Serikali: umeeleza Polisi walichukua Kadi ya Pikipiki na Hati, ila hujasema Ni Pikipiki ya aina gani wala namba gani, Ujasema

Shahidi: Ndiyo Sijasema

Wakili wa Serikali: turudi kabla hawajaondoka Kwenda Moshi, ulisema walienda Kwanza Morogoro wakarudi

Shahidi: Ndiyo

Wakili wa Serikali: Ila hujasema kwamba Morogoro walienda kufanya Nini.?

Shahidi: Sijasema

Wakili wa Serikali: kwa Sababu ulisema kadi ya Pikipiki ilichukuliwa, hujasema pikipiki hiyo ipo wapi

Shahidi: Sijasema

Wakili wa Serikali Tuje tarehe 05 Mwezi 08 2020 Kwamba Uliwasiliana na Adam Kasekwa kuwajulia hali wewe na Watoto, akasema subiri nitakupigia, Lakini Hakukupigia tena

Shahidi:Hakunipigia

Wakili wa Serikali
: na hakukupigia

Shahidi: Ndiyo

Wakili wa Serikali: Ilipofika Jioni wewe Mwenyewe uliamua kumtafuta

Shahidi: Ndiyo

Wakili wa Serikali: hujasema mahakamani kwamba Kazi hiyo ya Ulinzi alikuwa ameianza

Jaji: Wakili tubreak Kidogo Kwa Saa 1

Jaji: tutaendelea Saa 8 Na Dakika 15 Kwa hiyo naharisha Shauri hili Mpaka Saa 8 na Dakika 15.
Kazi IPO..Mimi binafsi yangu nauona ukweli kuwa hawa mabwana wametungiwa KESI.. Hakika kuna watu hawana hofu ya Mungu kabisa.
 
Samia ameishi kwenye uovu kwa miaka mitano. Ameuishi uovu kwa miaka 5. Ameufurahia uovu kwa miaka mitano. Hata akitaka kutoka, hawezi kitoka ghafla kwa 100%. Ni lazima ile roho ya uovu itaendelea kuwa ndani yake.

Hata pale anapokuwa na dhamira ya kutenda mema, kuna wakati atatumia uzoefu alio nao, ambao ni uovu.

Kwa hiyo kwenye hili kuna mkono wake na ile roho ya uovu aliyoiishi kwa miaka 5.
Nilikutambua toka siku ya kwanza nilipokusoma humu JF, kuwa kati ya 'GTs' waliosalia JF.
Ni fikra chache zilizobaki zinazoendelea kuibeba JF kubaki 'relevant.'
 
Siro na Samia walikosea sana kujitokeza hadharani na kuizungumzia hii kesi kua ushahidi upo,. Sijui walijiona akina nani kwamba watanzania na ulimwengu mzima unaweza kuhamini kauli zao, ona wanavyoumbuka


Unamkamata unaficha taarifa zake wakati ana familia, mke mtoto,wazazi kaka na eadogo zake, bado unaenda kwake unasachi bila yeye kuwepo u aondoka na hati ya nyumba pamoja na kadi ya pikipiki,. Bado mateso mliyompa, hati na kadi ya pikipiki havijulikani vilipo,

Bahati mbaya mtoto augue apoteze maisha kwa kukosa gharama za kulipia huduma, mke afariki kwa msongo wa mawazo, mwisho wa kesi adamoo aachiwe kwa kuonekana hana hatia, aisee

Akina Hamza mnawatengeneza wenyewe wakifanya tukio mnawatukana mpaka wazazi wao kua wana uzao wa hovyoo
LOoooh, mkuu umefanya 'summary' inayohudhunisha sana!

'Mama Mizinguo' kwenye hotuba yake kule UNGA anasifu uwepo wa utawala bora nchini mwake. Ni kama anaizungumzia nchi ambayo yeye haijui ipoje!
 
Huyo gaidi wanamchelewesha tu kama alifikia hatua ya kutapeli familia yake kwa kujimilikisha mali zote za urithi wampige haraka mvua 50
Kama wewe ni mtoto wa mcheuko wa Mzee Aikaeli na hukuambulia urithi kutoka kwake mlaumu mamako Kwa kushangilia mshedede na kusahau kuomba urithi wako Kwa Mzee! Vinginevyo, endelea kupiga miayo na yowe but huna utakachoambulia kwani akili zako ni za urithi kutoka Kwa mamako
 
HIVI VYOMBO VYA DOLA HAVIJAGUNDUA TU KWAMBA HII KESI INAIVUA NGUO SERIKALI MBELE YA DUNIA NA KUFUNUA WAZI SIRI ZA SERIKALI NA NCHI? NAWAAMBIA HAO WATU WA KILA AINA WANAOIFUATILIA HIYO KESI WANAPATA TAARIFA MUHIMU MNO AMBAZO NI HATARI KWA NCHI KIUSALAMA. UTENDAJI WA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA UNAANIKWA WAZI. IPO SIKU TUTASHANGAA KITABU KINAANDIKWA MAMBO YA AJABU KUHUSU TANZANIA. JE, MNAWAFAHAMU VIZURI HAO WANAOHUDHURIA HAPO MAHAKAMANI? WENGINE NI KUTOKA NJE YA NCHI. HAO MAKOMANDOO WA JESHI WANAFUNUA SIRI AMBAZO HAZISTAHILI KUTOKA NJE YA JESHI LENYEWE. KWANINI SERIKALI INAKUBALI MAMBO YA SIRI ZA NCHI YAANIKWE HADHARANI?
Siri gani watu wanatupwa angetupwa mjomba ako ungesema mambo ya siri za Nchi ni kikundi cha watu wachache wameharibu taswaira ya Taifa wacha watu wajue ikiwezekana wachukuliwe hatua..
 
Back
Top Bottom