Maamuzi ya kesi ndogo katika Kesi ya Mbowe na Wenzake kutolewa Oktoba 19, 2021

Maamuzi ya kesi ndogo katika Kesi ya Mbowe na Wenzake kutolewa Oktoba 19, 2021

Huyo gaidi wanamchelewesha tu kama alifikia hatua ya kutapeli familia yake kwa kujimilikisha mali zote za urithi wampige haraka mvua 50
 
Karibuni hapa kwa updates kutoka mahakama ya uhujumu uchumi kwenye kesi namba 16 ya ugaidi inayomuhusu mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe na wenzake watatu...

Watuhumiwa tayari wamefikishwa mahakamani, leo shahidi wa tatu upande wa utetezi ataanza kutoa ushahidi wake.

Mawakili upande wa Utetezi tayari wapo katika ukumbi wa Mahakama. Mawakili upande wa Mashtaka bado wapo Nje.

Jaji ameshaingia Sasa Mahakamani. kesi inatajwa.

Wakili wa Serikali: naomba radhi tumeingia wakati umeshaingia

Jaji: sawa

Wakili wa Serikali: Kidando Wakili wa Serikali anatambulisha wenzake
1. Robert Kidando​
2. Nassoro Katuga​
3. Ignas Mwanuka​
4. Esther Martin​
5. Tulimanywa Majigo​

Kibatala anatambulisha Wenzake
Adv. Peter Kibatala​
Adv. Jonathan Mndeme​
Adv. Fredrick Kiwhelo​
Adv. John Malya​
Adv. Sisty Aloyce​
Adv. Alex Masaba​
Adv. Idd Msawanga​
Adv. Gaston Garubindi​
Adv. Evaresta Kisanga​
Adv. Faraj Mangula​
Adv. Maria Mushi​
Adv. Bonifasia Mapunda​

Wakili Dickson Matata: anaombewa Ruhusa Mdogo wake anafanyiwa Operesheni Hospitali ya Lugalo

Jaji: Wakili wa Serikali

Wakili wa serikali: Tumekuja kwa ajili ya kesi ndogo ambapo Shahidi wa tatu yupo tayari kuendelea Kutoa Ushahidi wake

Jaji: John Mallya

Mallya: Tunaye, na Shahidi yupo tayari kutoa Ushahidi

Jaji: anaandika Kidogo na Ukimya wa Mahakama

Jaji: Shahidi wa 3 upande wa Utetezi ambaye ameandaliwa Tafadhali anaweza Kuja

Shahidi Mdada anatokea Nyuma kabisa ya Chumba Cha Mahakama anaenda Kizimbani

Jaji: Shahidi upo Mahakamani ondoa Hofu, nitakuuliza Majina yako na Nitakuapisha, Wakili wa Utetezi atakuongoza na Mawakili wengine watakuuliza Swali na Mawakili wa Serikali watakuuliza Maswali, pia huna Haja ya Kuogopa, tupo hapa kutafuta Haki.

Jaji: Shahidi unaitwa nani

Shahidi: Lilian Kibona, Dini Mkristo Shahidi Naapa Mbele ya Mahakama hii kuwa Ushahidi nitakao toa utakuwa Ukweli na Ukweli Mtupu, Mungu ni Saidie.

Jaji: Liliani utachagua Kukaa au Kusimama, Hata Ukikaaa nitakuona.

Jaji: wakili Mallya endelea

Mallya: Shahidi Unaishi wapi

Shahidi: Chalinze Mkoa wa Pwani

Mallya: sehemu gani huko Chalinze

Shahidi: Ramboni

Jaji: ni Mtaa.?

Shahidi: Ndiyo

Mallya: Unaishi na nani..?

Shahidi: Na mme wangu na Watoto ambaye kwa Sasa Mme wangu ameshikiliwa.

Jaji: ni Miongoni Mwa washitakiwa?

Shahidi: Ndiyo

Mallya: Mme wako anaitwa nani?

Shahidi: Adamu Khalfani Kasekwa

Mallya: hapa nitakuwa namuita Mshitakiwa wa Pili nitakuwa namaanisha pia ni yeye

Shahidi:ndiyo

Mallya: Mmeoana lini, 05/08/2016, Ndoa Ya Kiserikali

Shahidi: Ndiyo

Mallya: Mlikuwa mnaishi wapi

Shahidi: Pale pale Chalinze

Mallya: unaweza Kukumbuka Mme wako alikuwa anafanya kazi gani wakati huo

Shahidi: Askari Jeshi la JWTZ, kikosi cha 92 Ngerengere

Mallya: alikuwa anafanya kazi gani Nyingine

Shahidi: alikuwa hana kazi Nyingine zaidi ya hiyo ya Serikali

Mallya: naruka nakuja 2020 Mme wako alikuwa anafanya kazi gani

Shahidi: alikuwa anafanya shughuli zake za Biashara

Mallya: Mwanzoni Mwa Mwezi wa Nane Mwaka 2020 unakumbuka Kilitokea Kitu gani kati yako na Mme wako

Shahidi: Mme wangu alikuwa Moshi, tulikuwa tunawasiliana naye Vizuri

Mallya: Kabla ya Kwenda Moshi mlikuwa na Hali gani kati yako na Mme wako

Shahidi: Palikuwa na Mawasiliano

Mallya: kabla hajaenda Moshi kitu gani kilitokea

Shahidi: Rafiki yake Ling'wenya waliwasiliana kuwa kuna Kazi imepatikana Moshi

Mallya: Unaweza Kukumbuka Siku na Saa ya hayo mawasiliano

Shahidi: Hapana sikumbuki

Jaji: unasema palikiwa na Mawasiliano Kati ya Mme wako na Ling'wenya .?

Shahidi: Ndiyo Kwamba Ling'wenya alimpigia Simu kuwa kuna kazi Imepatikana Moshi

Jaji: Ndiyo

Mallya: Simu zilikuwa zinapigwa kati ya Ling'wenya na Mme wako, wewe ulijuaje

Shahidi: Mimi Kama Mke wake alinishirikisha, Mimi kama Mke nilimruhusu

Mallya: Jambo gani lilifanyika, kabla ya Mme wako kwenda Moshi

Shahidi: Nakumbuka walikutana na Ling'wenya wakaenda Kwanza Morogoro, Wakarudi, Waliporudi wakajiandaa Wakaenda Moshi

Mallya: Hali ya Mme wako kiAfya Wakati anaenda Moshi hali yake ilikuwaje

Shahidi: Ilikuwa Nzuri inamruhusu kwenda Kufanya kazi

Mallya: Hali Nzuri unamaanisha nini ,Mwambie Mheshimiwa Jaji

Shahidi: haumwi na Kwamba anaweza Kwenda Moshi

Mallya: kitu gani kilifuata baada ya Kwenda Moshi

Shahidi: alinitaarifu kuwa amefika Moshi

Mallya: mlikuwa mnatumia Njia gani kufanya mazungumzo

Shahidi: kwa Njia ya Simu

Mallya: Siku ya Tarehe 05/08/2020 kitu gani kilitokea

Shahidi: alinipigia na akaongea na watoto, tulipokuwa tunaongea akasema Hebu subiri nikamsubiri

Mallya: ilikuwa Saa ngapi

Shahidi: Kama Saa Moja

Mallya: alipokwambia Subiri kidogo nitakupigia Kidogo kitu gani Kilifuata

Shahidi: Nilipoona Muda umeenda ilipofika Saa 10 ilibidi nimpigie, Simu iliita ikawa imepokelewa lakini Kila nikisema Hallo Sisikii Mtu akiongea

Mallya: Unaweza Kukumbuka namba ya Simu uliyopiga, ambayo ulipiga Ikapokelewa.?

Shahidi: Sikumbuki Kichwani lakini ipo kwenye Simu yangu

Mallya: Baadae kilifuata nini baada ya Simu kutokupokelewa

Shahidi: baadae Ikawa haipatikani

Mallya: kitu gani Kilifuata

Shahidi: kwa kuwa nilikuwa na namba ya Mwenzake Ling'wenya nikampigia Ling'wenya

Mallya: baada ya Kumpigia Ling'wenya.?

Shahidi: Ikawa inaita Mpaka jioni, Mpaka Usiku, Mpaka Kesho yake inaita haipokelewi

Mallya: Sasa wewe ulipata hisia gani baada ya kuona Inaita hadi Kesho yake haipokelewi

Shahidi: niliona labda ni Mambo ya Kazi, sikuwa na wasiwasi wowote

Mallya: Wewe ulichukua hatua gani..?

Shahidi: Sikuwa na namna yoyote zaidi ya Kusubiri simu kutoka kwao

Mallya: umesema una mtoto, anaumri gani

Shahidi: Miaka 3 na Miezi 9

Mallya: Nataka kukupeleka Tarehe 09 Mwezi 08 kitu gani Kilitokea

Shahidi: nakumbuka ilikuwa tarehe 09 mwezi 08 Mwaka 2020 niliamka Asubuhi ikiwa siku ya Jumapili, Mtoto alikuwa anasumbuliwa na tumbo

Jaji: Mtoto wa Jinsia gani

Shahidi: Wa kike

Mallya: kwanini Unakumbuka kuwa ilikuwa Siku ya Jumapili

Shahidi: Sababu ilikuwa Siku ya Ibada

Mallya: Ikawaje

Shahidi: Sikwenda Ibadani badala yake nikaenda Hospitali

Mallya: ikawaje huko Hospitali

Shahidi: Nilipokelewa

Mallya: Hospitali gani

Shahidi: Hospitali ya Serikali pale pale Chalinze

Mallya: baada ya Kupokelewa Hospitali

Shahidi: nilipatiwa Huduma nikarudi Nyumbani

Mallya: baada ya Kurudi Nyumbani

Shahidi: niliona Miguu ya watu kama Imekanyaga, Wakati natoka Nyumbani nilifunga Mlango lakini niliporudi nikakuta Milango ipo wazi

Mallya: Ule Mlango ulikuwa katika hali gani

Shahidi: Mlango ulikuwa wazi na Kitasa nikakuta kimevunjwa

Mallya: kitu gani kikatokea

Shahidi: kwa akili ya haraka haraka nilijua Wezi, Cha ajabu kila kitu nilikuta Vipo, Kitu kama Tv lakini vipo

Mallya: enheeee ikawaje

Shahidi: Nikaingia Chumbani nikakuta Nguo zimemwagwa Chini

Jaji: Za Mme wako

Shahidi: zote zimemwaga,na Mabegi yamefunguliwa

Shahidi: Kuna begi la jeshi alinunua Congo nilipokuja nikakuta halipo

Jaji: ukisema begi la jeshi alinunua Congo unamaanisha nini

Shahidi: Alinunua Congo Begi lenye Mabaka Mabaka ya Jeshi

Mallya: Kitu gani kilifuata

Shahidi: Nilienda Kuuliza Majirani zangu

Mallya: Jirani yako anaitwa nani.?

Shahidi: Judith Charles

Mallya: lengo la kwenda kwa Jirani lilikuwa nini

Shahidi: nilienda Kuuliza kama Mme wangu amekuja Nyumbani.? wamemuona.? kwamba kuna kitu huenda alikuja Kukitafuta kwa haraka haraka
Mbona advocates wanaomtetea makengeza ni vyasaka na vishoia wenzake
 
Muda sio mrefu mawakili wa jamhuli wataweka pingamizi hawana Imani na mh mtukufu jaji.
Mshua yupo poa Hana upendeleo haegemei upande wowote.MUNGU ambariki Mr jaji.
Hii kitu hata wakiweka pingamizi Jaji yeyote atakayefuata bado atakuwa na kazi ngumu Sana maana hapa ni kifungu kwa kifungu hakuna janja janja[emoji16][emoji16]
 
Back
Top Bottom