Maana ya neno "ukaidi" kwa mtazamo wa Kikenya, tunaomba Watanzania mtuwie radhi

Maana ya neno "ukaidi" kwa mtazamo wa Kikenya, tunaomba Watanzania mtuwie radhi

MK254

JF-Expert Member
Joined
May 11, 2013
Posts
32,408
Reaction score
50,809
Siku kadhaa sasa nimeona kituo cha runinga cha Citizen TV Kenya kikipeperusha tangazo fulani la kumsifia rais wa Tanzania, kama njia moja ya kumkosha na kumpunguza hasira baada ya balozi wa Tanzania kuwalalamikia kwa wao kutumia maneno "ukaidi wa rais Magufuli" pale walipokua wanaeleza jinsi gani yeye amehamasisha Watanzania waendelee na maisha kama kawaida na kutegemea maombi kipindi hiki Corona inatesa dunia, kinyume na marais wote wa ukanda huu na duniani ambao kila mmoja alikua anatahadharisha wengine hata wakipiga lockdown kwenye mataifa yao.

Sisi Wakenya neno "ukaidi" hutumika pale mtu anakaidi na kupuuza ushauri wowote, shingo ngumu, yaani kwa kingereza tafsiri yake ni "stubborn - not to change one's attitude or position on something, especially in spite of good arguments or reasons to do so" kwa mfano, rais Magufuli alitanganza kanisani tena mbele ya vyombo vya habari kwamba yeye amekula mkate wa sakramenti bila kujali Corona maana corona itaungua kanisani.

Hivyo hapo tunasema alikaidi na kupuuza ushauri wa kitaalam na kuegemea kwenye mtazamo wa kidini, mimi binafsi ni Mkristo na ninamuelewa sana anaposema Corona itaungua kanisani, lakini hayo maneno yangetamkwa na rais Uhuru wa Kenya, yaani angetamani kuihama nchi maana angesemwa sana huku, tena zaidi ya "ukaidi wa rais Uhuru", maneno yangetumika makali sana na yenye hisia kali kali.

Sisi kwetu tunaamini urais ni taasisi, sio ofisi ya kuendeshwa kwa hisia za mtu au misingi ya kidini, maana nchi yetu hii tuna watu mamilioni ambao ni wafuasi wa dini zingine ambazo hazina habari na Yesu.

Raisi Uhuru hututangazia tuombe ila anahamasisha tahadhari tena kwa kusisitiza sana na kuongeza mikwara kwa wale watapatikana wakikiuka kanuni elekezi, ikiwemo utumiaji wa barakoa nchi yote, utakasaji wa mikono muda wote na mengine mengi.

Hivyo kwa rais kutangaza kinyume na tahadhari zinazohamasishwa na waziri wa afya, kawaida kwetu tunachukulia huo kama "ukaidi". Sasa Citizen wataendelea na hiyo misifa, lakini tatizo asilimia kubwa ya wanaoitazama ni Wakenya, wengi wanabaki kushangaa kipi kikubwa hapo na ndio maana wengi wanaeleza hisia zao kwenye Tweeter.

Kwa baadhi ya Wakenya kama mimi ambao tumewahi kuishi Tanzania, tutaelewa maana tunajua jinsi kule walivyo, yaani rais bado ana mamlaka makubwa na bado wanatumia katiba ya zamani na kumtaja rais lazima uwe makini sana, hata kwenye ulevi hauwezi kuthubutu, tumesoma habari za watu kutiwa lockup kisa tu walipiga picha kuta zenye nyufa kwenye majengo aliyozindua rais, hivyo ujasiri wa kutumia maneno kama "ukaidi wa rais" ni kitu kikubwa sana kwao.

Lakini kwa Wakenya ambao hawana habari na Tanzania na wamezoea uongozi wa kitaasisi chini ya katiba mpya, lazima washangae sana. Hivyo kwa tofauti hizi za kimtazamo, Watanzania mtuwie radhi, hilo neno "ukaidi" ni la kawaida sana huku kwetu pale unakaidi ushauri.

President Magufuli says coronavirus cannot survive in churches : The Standard
 
Sawa katibu muenezi ofisi ya raisi Kenya ila sasa ungeenda kuandika kule kwenye jukwaa la siasa ukapate maoni halisi ya wa bongo ingawa binafsi sikubali approach anayotumia kupambana na huu ugonjwa ila ilo neno ukaidi ijulikanavyo ni kukataa amri halali kutoka kwa waliokuzid mamlaka au kutotii sheria halali iliyowekwa au kukataa amri ya mtu yoyote aliekuzidi umri na mwenye mamlaka juu yako, the rest tunaita ni UBISHI.
 
Sawa katibu muenezi ofisi ya raisi Kenya ila sasa ungeenda kuandika kule kwenye jukwaa la siasa ukapate maoni halisi ya wa bongo ingawa binafsi sikubali approach anayotumia kupambana na huu ugonjwa ila ilo neno ukaidi ijulikanavyo ni kukataa amri halali kutoka kwa waliokuzid mamlaka au kutotii sheria halali iliyowekwa au kukataa amri ya mtu yoyote aliekuzidi umri na mwenye mamlaka juu yako, the rest tunaita ni UBISHI.

Ulichokieleza hapa kinaitwa "uasi", yaani kuasi dhidi ya maagizo ya wakuu wako, ila "ukaidi" kwa kingereza ni stubbornness, ile kuweka shingo ngumu dhidi ya ushauri wowote.
(KISWAHILI - KIINGEREZA)Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
 
Sisi Wakenya neno "ukaidi" hutumika pale mtu anakaidi na kupuuza ushauri wowote, shingo ngumu, yaani kwa kingereza tafsiri yake ni "stubborn - not to change one's attitude or position on something, especially in spite of good arguments or reasons to do so" kwa mfano, rais Magufuli alitanganza kanisani tena mbele ya vyombo vya habari kwamba yeye amekula mkate wa sakramenti bila kujali Corona maana corona itaungua kanisani.
Kwa tafsiri ya kiswahili, "ukaidi" ni neno zito na kali sana tofauti na linavyotafsiriwa "stubborn" kwa kiingereza.

Ukaidi ni ujeuri.

Kusema Rais wa nchi ni jeuri ni kumkosea heshima na hivyo ni kuikosea heshima nchi.

Heshima Tanzania ni kitu kikubwa sana, tofauti na Kenya ambako salamu haitolewi kwa heshima. Mkubwa na mdogo kenya wote ni sawa.

nice explanation. kiswahili unakimenya sawa sawa
Umekimanya!

Unakimenya - you're peeling.
 
Hako ka neno kanawanyima nyang'au usingizi wkt sisi venye tumetukanwa hatuku take any action.
Juu vile tunajua kabisa nyang'au mko na stress mingi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hako ka neno kanawanyima nyang'au usingizi wkt sisi venye tumetukanwa hatuku take any action.
Juu vile tunajua kabisa nyang'au mko na stress mingi.

Sent using Jamii Forums mobile app

Kha! Wakati balozi wenu mwenyewe alikwenda kulalamika kwenye kituo cha habari cha Citizen TV, wala hata haikua issue kwetu.
 
Sasa wakenya na Kiswahili wapi na wapi? Ni dhahiri shahiri hawakujua how heavy hilo neno lilivyo especially kwa mtu kama Rais wa nchi

Ndio maana hata kwa mara ya kwanza tu Ile video ilivyotoka kwenye social media, watanzania wali raise eyebrows kwenye utumizi wa hilo neno ukaidi, karejee comments za watanzania kwenye Ile video.
 
Kiufupi Magufuli ni Mkaidi na Short Minded president in Africa. Tanzania will sink, regardless all claps around him but situation on the ground is worst, he will now on ward start to blame C-19 because he cant finish his stupid useless mega project

Duh!
 
Halafu wakenya walivyo punguani wanamshambulia Magufulis badala ya kudeal na chang'aa media yao

Ila kiukweli tuweni wawazi, Tanzania Ina influence kubwa sana ukanda huu

LOL nikiangalia Kenya inavyoufyata kila time Tanzania ikikohoa ni mpaka huruma

Walirudisha dhahabu zetu

Walirudisha pesa zetu

Walimtia ndani mbunge wao alieongea shit kuhusu watanzania

Wanamuomba msamaha JPM week nzima

Gezaulole haya sio mambo madogo ujue
😅😅😅😅😅🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿
 
Back
Top Bottom