Maana ya Upendo ni hii

Maana ya Upendo ni hii

diamond d

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2018
Posts
812
Reaction score
2,048
1 Wakorintho 13 (Biblia Takatifu)

¹ Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao.

² Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote, nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, si kitu mimi.

³ Tena nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, tena nikijitoa mwili wangu niungue moto, kama sina upendo, hainifaidii kitu.

⁴ Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni;

⁵ haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya;

⁶ haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli;

⁷ huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote.

⁸ Upendo haupungui neno wakati wo wote; bali ukiwapo unabii utabatilika; zikiwapo lugha, zitakoma; yakiwapo maarifa, yatabatilika.

images%20(25).jpg
 
Mbona Biblia inakataa...Mathayo 2:191. Na wauweni popote mwakutapo, na muwatoe popote walipo kutoeni; kwani fitina ni mbaya zaidi kuliko kuuwa. Wala msipigane nao kwenye Msikiti Mtakatifu mpaka wakupigeni huko. Wakikupigeni huko basi nanyi pia wapigeni. Na hivi ndivyo yalivyo malipo ya makafiri.
 
Mbona Biblia inakataa...Mathayo 2:191. Na wauweni popote mwakutapo, na muwatoe popote walipo kutoeni; kwani fitina ni mbaya zaidi kuliko kuuwa. Wala msipigane nao kwenye Msikiti Mtakatifu mpaka wakupigeni huko. Wakikupigeni huko basi nanyi pia wapigeni. Na hivi ndivyo yalivyo malipo ya makafiri.
Hii biblia ni mpya yenye mathayo 2:191 [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Sent from my SM-J720F using JamiiForums mobile app
 
Hakika mkuu na pia Mungu hujitambulisha kwetu kuwa yeye ni PENDO basi ina maana unapokuwa na Roho wa Mungu ndani yako PENDO lake huumbika kwako,na vyote vilivyoolozeshwa kwenye hyo 1Wakorintho 13:4,10 uzaliwa ndani yako,na inaonekana kumbe pendo la mwanadamu lina ukomo lakini hili PENDO la Mungu halina ukomo kwa wanadamu hata ukiwa vipi Mungu utupenda vile tulivyo hata kama tuna madhaifu au mapungufu,GODISLOVE,LOVEISGOD🙏🏾
 
Mbona Biblia inakataa...Mathayo 2:191. Na wauweni popote mwakutapo, na muwatoe popote walipo kutoeni; kwani fitina ni mbaya zaidi kuliko kuuwa. Wala msipigane nao kwenye Msikiti Mtakatifu mpaka wakupigeni huko. Wakikupigeni huko basi nanyi pia wapigeni. Na hivi ndivyo yalivyo malipo ya makafiri.
Duuuh we jamaaa
 
Back
Top Bottom