The Phylosopher
JF-Expert Member
- Mar 11, 2015
- 1,968
- 2,957
Rasmi naomba kutoa kusudio langu la kuitisha maandamano makubwa ya kunusuru hifadhi ya taifa ya Ngorongoro.
Nimeanza mchakato wa kuomba kibali polisi na mamlaka zingine husika ili kuitisha maandamano makubwa yatakayofanyika hivi karibuni ili kuishinikiza serikali iwaondoe binadamu wote waliomo ndani ya hifadhi ya taifa ya Ngorongoro kwani ni dhahiri wakiachwa humo hifadhi hiyo itakufa. Nimefikia uamuzi huo baada ya kuona licha ya nguvu zoote ilizonazo Serikali lakini inasita kuzitumia kuwatoa hao jamaa.
Kama Serikali imeweza kuwatoa machinga waliokuwa wamezagaa kwenye miji yote nchini, kama serikali iliweza kuvunja makazi ya watu pale kimara Mbezi naamini hata hawa waliomo ndani ya hifadhi wataondolewa na hakutatokea madhara yoyote zaidi sana tutainusuru hifadhi yetu kwa ajili ya vizazi vijavyo.
Naomba watanzania wote wenye uzalendo na nchi hii mniunge mkono pindi nikikamlisha maandalizi yote muhimu ya maandamano hayo.
Nimeanza mchakato wa kuomba kibali polisi na mamlaka zingine husika ili kuitisha maandamano makubwa yatakayofanyika hivi karibuni ili kuishinikiza serikali iwaondoe binadamu wote waliomo ndani ya hifadhi ya taifa ya Ngorongoro kwani ni dhahiri wakiachwa humo hifadhi hiyo itakufa. Nimefikia uamuzi huo baada ya kuona licha ya nguvu zoote ilizonazo Serikali lakini inasita kuzitumia kuwatoa hao jamaa.
Kama Serikali imeweza kuwatoa machinga waliokuwa wamezagaa kwenye miji yote nchini, kama serikali iliweza kuvunja makazi ya watu pale kimara Mbezi naamini hata hawa waliomo ndani ya hifadhi wataondolewa na hakutatokea madhara yoyote zaidi sana tutainusuru hifadhi yetu kwa ajili ya vizazi vijavyo.
Naomba watanzania wote wenye uzalendo na nchi hii mniunge mkono pindi nikikamlisha maandalizi yote muhimu ya maandamano hayo.