MABABU ZETU WATAENDA MOTONI WOTE?

Soma maandiko uelewe kwa kifupi hawataenda moyoni kwa kwa kuwa hawakuhubiriwa biblia na ndo maana maandiko yanasema injili ikihubiriwa duniani kote na hapo ndo mwisho wa dunia utafika ili kila mtu atahukumiwa kwa makosa yake.wajuvi wa biblia mtusaidie
 
Kama wewe ni muislam kasome suratul bayyina ( quran 98) utapata majibu ya swali lako kwa biblia sijui sikupitapita huko
 

Mbona hilo swali lilishajibiwa mara nyingi hapa hapa ukwaani?
Hao watahukumiwa kutokana na nyakati zao kadri Mungu atavyo ona inafaa.
Mfano; hata bila kuwepo na muongozo wa dini, Kuchukua kitu cha mwenzako bila ruhusa (kuiba) ni kosa; kuua mtu ni kosa; kunyima mtu haki yake ni kosa; Kuloga mtu ateseke bila sababu ni kosa, Kula mali waliyo achiwa watoto yatima ni kosa; Kupunja watu kwenye vipimo (mizani) unamwambia mtu ni kilo kumbe umepunguza, ni kosa nk nk nk hivyo hukumu itakuwa pale pale na wale waliokuwa wanafanya matendo mema watapata pepo.
Hata kwa kipindi hiki, wapo wengi tu ambao wanaishi bila kufuata mafundisho ya Yesu wala ya Muhamad na watakuhumiwa kwa matendo yao!
 
Ila wao watakuwa hawana nafasi ya kutubu kama sisi kwa mjibu wa mandiko. Maana leo nawezaiba miaka 30 ila nikatubu na nikawa kiumbe kipya na mwisho wangu ukawa mwema. Je wao aliyeacha wizi akawa mwema ataokolewa vipi. Maana makosa yake ya nyuma yatamhukumu maana hajapata elimu ya toba
 
Hakuna mzazi anayeweza kumchoma moto mtoto wake hata kama kamkosea namna Gani labda awe amerukwa akili, Je Inawezekana vipi Mungu mwenye upendo kuliko mzazi aruhusu wewe kuchomwa moto?.
 
Nani kakudanganya kuwa kuna moto? Huo ni ujinga tu wa kutishana. Kiukweli hakuna moto, hakuna peponi hakuna kuonana na Mungu, Yesu harudi tena, hakuna Sheitwani wala Malaika wewe ukishakufa umekufa hakuna chochote kinachokuhusu anavyokufa mbwa, kuku, nyau, simba, tembo, nyoka nk hakuna tofauti na wewe. Hakuna maisha baada ya kufa mtu awaye yote asikudanganye
 
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ ila inatia hasira bado kuna watu watumwa kifikra mpaka kesho.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…