Mabadiliko haya TRA aliyoleta Rais Magufuli hata aondoke leo yatadumu milele

Mabadiliko haya TRA aliyoleta Rais Magufuli hata aondoke leo yatadumu milele

Magufuli is a president for life nani amesema ataondoka Leo au kesho?
 
mawazo mazuri sana haya mhusika lazima atayapata hebu tuyafanyie kazi tutoke hapa tulipotusonge mbele
 
Kuna jambo moja unapaswa kulijua, watanzania wengi wana nunua vitu wanavyo lipia VAT kuliko kuuza vitu vingi wanavyopaswa kukusanya VAT kwa niaba ya TRA.
Kuna hatari serikali ikajikuta inadaiwa madeni makubwa na raia ukisema watu wa kawaida sio bishara au kampuni wa-file VAT returns.

Kiujumla wake umetoa hoja na ushauri mzuri kwakweli.
 
Kuna jambo moja unapaswa kulijua, watanzania wengi wana nunua vitu wanavyo lipia VAT kuliko kuuza vitu vingi wanavyopaswa kukusanya VAT kwa niaba ya TRA.
Kuna hatari serikali ikajikuta inadaiwa madeni makubwa na raia ukisema watu wa kawaida sio bishara au kampuni wa-file VAT returns.

Kiujumla wake umetoa hoja na ushauri mzuri kwakweli.
Kama ajasajiliwa na VAT atadaije serikali.
Anaye claim VAT refund ni mtu aliyesajiliwa tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jamaa nazani anamaanisha return za income sio vat
Kuna jambo moja unapaswa kulijua, watanzania wengi wana nunua vitu wanavyo lipia VAT kuliko kuuza vitu vingi wanavyopaswa kukusanya VAT kwa niaba ya TRA.
Kuna hatari serikali ikajikuta inadaiwa madeni makubwa na raia ukisema watu wa kawaida sio bishara au kampuni wa-file VAT returns.

Kiujumla wake umetoa hoja na ushauri mzuri kwakweli.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unapongeza ,Unashauri,Unakosoa
Hii ndio Maana Nzuri ya Kuipenda nchi yako
Safi sana Ndugu huu ni Ushauri mzuri sana
Naimani wahusika wataupokea
Kama watasoma hii thread...
 
Mkuu kila mahali watu wanalalamika biashara hazitoki, Unemployment rate i am sure itakuwa inacheza above 12% maana kenya leo wametoa 10.8%

Sasa sijui ngombe akikamuliwa sana mwisho wake atafariki. Mkuu on the ground hali inatisha na huu ndio mwaka tulizoea wa uchaguzi labda vyuma vingepakwa grisi.

Mkuu wauza mihogo wameongezeka sababu ya kusaidia mlo kuwa mkuu. Unapiga mihogo ya kukaanga mpaka jioni.

Kodi zikizidi itakuwa hatari. Moja ya sababu za kuwa na NIda ID ni kutekeleza hayo uliyoyaongea. Ila wasisahau wao wako kwenye ma landcruiser V8 full viyoyozi sisi tunaitafuta corona kwenye mwendokasi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwanza kabisa nianze na swali, Kwa kasi hii ya mabadiliko katika mifumo mbali mbali hasa TRA, BRELA, BOT je kipindi cha nyuma tulikuwa hatuna watanzania wenye akili ? ama watu waliamua kuwa vipofu.

Kama msomi na mchumi katika vitu ambavyo amefanya Raisi Magufuli ambavyo sitasahau ni

1. MABADILIKO TRA
a) Asikuambie mtu sasa hivi TRA kuna vijana wadogo makini na wenye uchu wa kuimarisha uchumi wa nchi, MFUMO WA DIGITALI umerahishisha ukusanyaji wa kodi. Mfano sasa ukienda TRA lazima wahitaji mkataba wako, hapo inaamana direct mwenye nyumba nae atatafutwa kuhakiki amelipa kodi.


b) Process za Control Verfication ya VAT imemaliza tatizo la fake receipt na watu kutokulipa VAT

C) Process za Examination of returns and account ni kitu kilikuwa kinafanyika kwa makampuni makubwa naona sasa limerudi kwa makampuni yote Tanzania. Hii imesaidia sana TRA kupata pesa na wale wategaji, haya mabadiliko yatasababisha hata vijana kupata ajira sasa.


LAKINI BADO TRA MNA HAYA YA KUFANYA KUIMARISHA UKUSANYAJI WA KODI NCHINI
  • NINI KIFANYIKE KUKUZA TAX DATA BASE
Tanzania kwa sasa ina TAX BASE 12.8 kwa idadi ya watu 50m, ukilinganisha na Kenya in TAX BASE 18.5 kwa idadi ya watu 40m tu. Nini kifanyike

  • MFUMO WA UGAWAJI TIN KWA WATU WOTE WENYE MIAKA 18 NA KUFILE RETURN KILA MWAKA HATA KAMA MTU HAJAANZA BIASHARA
Nchi za wenzetu pale tu mtu anapofikia umri wa miaka 18 anapatiwa namba ya utambulisho wa mlipa kodi kipindi akipatiwa kitambulisho cha utaifa. Hii ni muhimu tuanzishe hapa Tanzania itasaidia sana ukusanyi wa kodi lakini pia kuleta hamasa kwa generation ijayo kujua kodi ni nini na ni lazima.

Kwa sasa hapa Tanzania unaweza ukakuta mtu aan mali za mpaka TSH 5 Billion lakini hana TIN number au analipa kodi ndogo sana au hajawahi kulipa kodi, hii inakuwaje chukulia mfano hapo chini wa MR X.

MR X amemaliza chuo lakini hajaingia kwenye ajira rasmi, ameachiwa mashamba na nyumba za kupangisha na baba ake, mashamba na nyumba zipo eneo ambalo halijapimwa, MR X anaweza amua uza mashamba kwa million 100 hadi 200 bila kulipa kodi, MRX atakuja kuchukua TIN number kwa ajili ya umiliki wa gari tu na sio TIN ya biashara. MRX atajenga nyumba atapangisha na ataendelea kuchukua kodi za wapangaji bila (WT) kwa kuwa ni ngumu kumpata. MRX anaweza akawa Tajiri bila kuwa na TIN ya biashara.


Lakini TRA ikianzisha mfumo wa kila mtu kuwa na TIN na kufile Return mwisho wa mwaka, ni rahisi kwa MRX kusema kwamba kwa mwaka huu nilipata pesa hiikutokana na kuuza shamba au kupangisha nyumba, nah ii inaweza kuwa rahisi TRA kuuliza MR X kama unaweza miliki gari na matretka mbon hulipi kodi.

Chukulia Mfano pia MRX amemaliza chuo amepata ajira isiyo rasmi, MRX anaweza fanya kazi kwa miaka 2 akapata mpaka million 30 akaamua kununua gari na kujenga nyumba lakini bila kulipa kodi yoyote, swali ni Je amewezaje kupata million 30 bila kulipia kodi, jibu ni rahisi, labda alifanya kazi akawa analipwa bila (WITHHOLDING TAX) au kulikuwa na WT sema yeye hajafile return za kila mwaka kuonesha sources za income.

Mwisho, Tax base itaongezeka endapo tutaweka mfumo wa kila mtu kufile return hata kama ni NIL return, hii itapelekea mapato mengi yakusanywe ambayo yalikuwa yanapotea.

Kwa kifupi ile notion kwamba hii ni TIN ya leseni tu sio ya Biashara lazima iondoke, mtu kama ana TIN lazima afile return kila mwaka hata kama ni NIL returns.

Kurahisha hili mfumo huo unaweza kuwa online.

  • MFUMO WA RETURN UWE HATA KWA WAFANYAKAZI WANAOLIPA PAYE
Ni desturi imejijenga kwamba kama mtu anafanya kazi ya ziada mapato yake anakuwa hayatolei taarifa kwa kuamini kwamba tayari analipa kodi PAYE kupitia kwa mwajiri wake. Mfumo wa kufile Return lazima uwe kwa wananchi wote hata kama mtu analipa PAYE, hii itarahisha mtu kuweza kulipa kodi kwa mapato ya ziada anayopata nje ya mshahara, mfano kama anapokea kodi ya nyumba au kama amefanya consultancy etc.

  • NIN KIFANYIKE KUBORESHA MFUMO WA UKUSANYAJI KODI

  • UJUZI WA WAFANYAKAZI NA MAFUNZO YA MARA KWA MARA KATIKA FIELD ZINGINE
Katika kila ofisi ujuzi wa wafanyakazi ndio tija muhimu katika kila jambo, kwa muda ambao nimefanya kazi na kuengage na wafanyakazi wa TRA nikiri kwamba kweli baadhi wana uelewa wa masuala ya kodi lakini wengi wako limited, mfano mfanyakazi wa department moja ukimpa scenario ambayo sio yake hawezi kukujibu. Swala la kodi ni swala Mtambuka ni vyema watumishi wa TRA wakawa na uelewa mtambuka pia, hii itawezakana kama kutakuwa na mafunzo ya mara kwa mara ya mwendelezo katika masuala tofauti mfano Corporate management and law, Land law and real estate, tourism etc.

Katika utafiti wangu katika baadhi ya ofisi, nimegundua baadhi ya watumishi kuwa wazuri lakini uelewa mpana wanakosa na hii ni kutokana na Mfumo ulivo TRA.

Mfano: Nilienda ofisi moja nkakutana na afisa senior tu, nkampa scenario kwamba nafanya Biashara, muda huhuo nafanya consultancy na muda huo huo na pokea kodi za nyumba za kupanga, nkamuuliza sasa je baada ya kupokea kodi ya nyumba na mpangaji amesha WT 10% mimi na haja ya kureporitia TRA, akajibu mpangaji akishalipa 10% ndo mwisho.

Ni muhimu sana kwa wafanyakazi waliopo na ambao wanaanza kupewa crach program kuhusu mambo mtambuka ya kodi, hii itawarahishia kuweza kufanya uchambuzi wa mambo.

Pia TRA ianzishe Continous learning programe mfano wafanyakakazi kujifunza mambo mapya kama Transfer pricing, Trade mark and royalties, land law and taxation, company management and Taxation etc. Na katika hili ni vyema wawezeshaji wawe ni watu kutoka private sector kuweza kubadilisha ujuzi.

  • KODI ZA MAJENGO HASA WITH HOLDING NA FINAL TAX
Tanzania hasa Dar es Salaam na mikoa iliyoendelea kuna nyumba nyingi sana za kupanga, lakini ni watu wachache sana wanalipa With holding Tax kama wapangaji na kama wenye nyumba kulipa final tax kutokana na mapato anayopata.

Kwa Dar mfano mtu anaweza akawa na nyumba za kupanga 20 zote anapokea kodi cash na hakuna WT wala final return anazofanya. Na wengi baada ya kuona ukimiliki nyumba kama individual hakuna wa kukusumbua wengi hawawezi kuanzisha kampuni ya real estate utakuta ana nyumba 10 zote amepangisha na hakuna mpangaji analipa WT wala yeye kufile final return, hili ni eneo ambalo TRA wakitilia mkazo na litaongeza Tax base na mapato.

ASANTENI
Mkuu Janja PORI umedadavua vizuri pia umekosoa,umeonya,umeshauri na umesifia.

Pia ungegusia na suala la ajira...kuwepo na balance hata watoto wa vigogo na wa wakulima/wafugaji wagawane Keki ya Taifa.

Kwa sababu:-

1: Kuna vijana huku mtaani wamehitimu Uhasibu more than 2years hawana ajira,wanazurura tuu na kukaa vijiweni.

2: Inasadikika ajira za TRA ni za kibaguzi,yaani kujuana.Vipi kuna uhalisia kwenye hili????? Na kama sivyo ni hatua gani mnachukua ili kuwapa ajira wale tunaowaona maofisini wakati tukilipa kodi.

3:Na pia Ajira za TRA hazitangazwi,hapa inakuaje?? Sasa hivi kuna system inatumika ndani ya TRA inaitwa Interns hii inakaaje???! Na jee? Vijana wale wa kitanzania wote wakimaliza mtawaajiri?na kama baadhi ya hawata ajiriwa si litakuwa ni suala la kupoteza muda wa vijana wetu???


Naamini mkuu Janja PORI wewe ni mtaalamu wa masuala ya uchumi na msomi mzuri,Hivyo sasa kwa busara zako ningependa kuona mchango wako kuhusu hili uliwa kama Expert member wa humu.

NAWASILISHA.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ushauri mzuri... Tatizo sio kukusanya mapato tatizo Ni matumizi...
TRa wanazidi kuongeza mapato lakini huku mbagala Ni heri ya jana kuliko leo... Sijui kesho Corona itakuwaje..
 
Huu ndo aina ya nyuzi tunazotaka humu.
Kwa kweli kuna umuhimu mkubwa mno wa tax base kuongezeka ili walau kila mwananchi anayepata chochote atoe return kwa mamlaka za nchi.

Lakini pia kuna umuhimu sana kusimamia na kuhakikisha kila kinachopatikana kinatumika vizuri kwa ajili ya wote.

Sasa hapo ni muhimu sana kwanza kulifanya suala kulipa kodi kama utamaduni au ibada. Pili tujifunze kuchagua viongozi waadilifu,wazalendo,wasio na tamaa,wabunifu na walio tayari kuitumikia nchi kwa uaminifu.
Tukikusanya kodi kwa mafanikio na bado tukawa na viongozi wa hovyo juhudi zote zinakuwa HOVYO na BURE.
 
Huu ndo aina ya nyuzi tunazotaka humu.
Kwa kweli kuna umuhimu mkubwa mno wa tax base kuongezeka ili walau kila mwananchi anayepata chochote atoe return kwa mamlaka za nchi.

Lakini pia kuna umuhimu sana kusimamia na kuhakikisha kila kinachopatikana kinatumika vizuri kwa ajili ya wote.

Sasa hapo ni muhimu sana kwanza kulifanya suala kulipa kodi kama utamaduni au ibada. Pili tujifunze kuchagua viongozi waadilifu,wazalendo,wasio na tamaa,wabunifu na walio tayari kuitumikia nchi kwa uaminifu.
Tukikusanya kodi kwa mafanikio na bado tukawa na viongozi wa hovyo juhudi zote zinakuwa HOVYO na BURE.
mkuu naona unatatafuta ugomvi na wakna tunda la masiara[emoji38]-jokes

Kiukweli mkuu umeongea jambo la maana sana unastahili pongezi!

Kama ulivyosema utoaji wa kodi uwe ni kama ibada ni kweli kabisa sipingani na wewe..na hii pia itapelekea uchumi wa Taifa kugrow zaidi.

NIMEYAPENDA MANENO YAKO ya“Pili tujifunze kuchagua viongozi waadilifu,wazalendo,wasio na tamaa,wabunifu na walio tayari kuitumikia nchi kwa uaminifu. ” sio viongozi tuu! Hata watendaji wa mamlaka yenyewe wapatikane watu wachapa kazi,waadilifu na wasio na tamaa Taifa litafika eneo..

Japo sina evidence za kutosha na zozote za Maofisa wa TRA,lakin suala la uadilifu na uaminifu kutokuwa na tamaa ni suala muhimu sana katika hii sector.Na ndio maana mchujo wa kuingia kwenye hizi mamlaka na kuwa mfanyakazi ni ngumu sana achilia mbali na yasemayo kuwa mamlaka hii kipindi cha nyuma ilifanya shughuli zake kwa kujuana hususani kwenye soko la ajira.

Lakini pia mkuu suala la kula keki ya taifa ni la kila mmoja wetu! Hivyo kama ulivyoshauri kuwa-“Lakini pia kuna umuhimu sana kusimamia na kuhakikisha kila kinachopatikana kinatumika vizuri kwa ajili ya wote.”

ni muhimu sana kwa ajili ya nchi yetu na tuzidi kulijenga TAIFA.

NAWASILISHA

Sent using Jamii Forums mobile app
 
KALIPE KODI TUJENGE TAIFA, LAZIMA TUWE NA STANDARD YA WENZETU, SIO NCHI UNA BIASHARA YA BILLION UNALIPA LAKI 2 A WENGINE NDO WANAUMIA
Dogo umetoka chuo juzi, bado una mihemuko ya ajira mpya, ukikua utajua kuwa mfumo mzuri wa TRA unategemea pia mifumo mingine,

Unaua sekta binafsi ambayo ndo engine ya uchumi alafu eti unaimarisha mifumo ya kodi hiyo kodi utatoa wapi? Acha kuwadanganya wajinga
 
Deni LA taifa limepaa mpaka tril.58.
Maana yake hiyo no indicator kuwa uchumi wetu umekufa, biashara zimekufa, maana yake hat ukiwa na mifumo mizuri ya kodi huwezi kupata kodi, kukopa Sana ni dalili ya kutokuwa mapato yanayo kidhi matumizi

Usidanganye tupo kwenye kipindi kigumu sana. Hiyo mifumo mizuri ya kukusanya kodi haitusaidii kwa sasa. Ikiwa hakuna walipa kodi

Tuko kwenye janga LA korona. Tumepoteza biashara ya utalii tumepoteza biashara ya airline mahoteli yamefungwa, sasa TRA na mifumo yao mizuri watatoa wapi kodi,?
 
Back
Top Bottom