Mabadiliko Jeshini: Mpambe wa Rais apandishwa cheo na kupangiwa kazi nyingine, Kanali Mulunga awa mpambe mpya

Mabadiliko Jeshini: Mpambe wa Rais apandishwa cheo na kupangiwa kazi nyingine, Kanali Mulunga awa mpambe mpya

Nasikia ADC mpya ni Msukuma, hadi sasa major general 5 Wasukuma.......Wasukuma mwaka wenu huu.....
Mkuu wa Majeshi ya ulinzi, Jenerali Mabeyo amefanya teuzi kadhaa ndani ya Jeshi la wananchi. Kanali M.E. Kaguti ambaye kwa sasa ni mkuu wa wilaya ya Buhigwe, Kigoma amepandishwa cheo na mkuu wa majeshi, Jenerali Mabeyo amemuomba Rais amtumie kwa kazi nyingine.

Mabeyo amesema amefanya teuzi 28 na kwa ujumla wao na amemuomba Rais awatumie ili aimarishe safu ya uongozi katika Jeshi na anaamini kwa viongozi waliopo safu ya uongozi itaimarika.

Sambamba nao hao, Mabeyo amemuomba Rais aridhie kupandishwa cheo Luteni kanali D.P.M Mulunga kuwa Kanali na kwa cheo hicho Rais ameridhia awe mpambe wa Rais kuanzia leo.

Meja Generali PP Masau amepandishwa kuwa Ruteni generali atakuwa Mkuuwa Mafunzo Chuo cha Monduli

HS Kamunde amepandishwa kuwa Meja Generali na atapangiwa kazi baadae.

Pia Makanali 28 wamepandishwa vyeo kuwa Mabrigedia Generali ambao ni;

J.J Maseba, Madugu,

A. S Mwami aliyekuwa Mwambata India,

R. K Kapinga,

C.D Katenga,

Z.S Kiwenge,

M.A Mugambo,

A.A Alfonsi, alikuwa Mwambata Zimbabwe

A.P MUTA, alikuwa Mwambata Marekani

A. Chakila,

M.G Mhagama,

V.M Kisiri,

C.E Msola,

S.M Mzee,

C.J Njiege,

A. Muhona,

R.C Mumbi

SJ Mkande,

Sibuti,

M.M Mwanga,

I.S Ismail.

Mwingine ni M.N Mkelemi ambae kwa sasa ni mpambe wa Rais na kwa cheo hicho Jenerali Mabeyo amemuomba Rais ampangie kazi nyingine.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 12 Aprili, 2018 amewapandisha vyeo maafisa wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) katika vyeo mbalimbali.

Taarifa iliyosomwa na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Jenerali Venance Salvatory Mabeyo, Ikulu Jijini Dar es Salaam imeeleza kuwa Mhe. Rais Magufuli amempandisha cheo Meja Jenarali Peter Paul Massao kuwa Luteni Jenerali.

Meja Jenerali Massao ni Mkuu wa Chuo cha Mafunzo ya Maafisa Wanafunzi wa Jeshi Monduli (TMA) na kwa uteuzi huo, sasa JWTZ itakuwa na Luteni Jenerali wawili.

Mhe. Rais Magufuli amempandisha cheo Brigedia Jenerali Henry Kamunde kuwa Meja Jenerali.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli amewapandisha vyeo maafisa 27 wa JWTZ kutoka cheo cha Kanali na kuwa Brigedia Jenerali na Afisa 1 kutoka Luteni Kanali na kuwa Kanali.

Waliopandishwa vyeo hivyo ni D.D.M Mullugu, J.J Mwaseba, A.S Mwamy, R.K Kapinda, C.D Katenga, Z.S Kiwenge, M.A Mgambo, A.M Alphonce, A.P Mutta, A.V Chakila, M.G Mhagama, V.M Kisiri, C.E Msolla na S.M Mzee.

Wengine ni C.J Ndiege, I.M Mhona, R.C Ng’umbi, S.J Mnkande, A.C Sibuti, M.M Mumanga, I.S Ismail, M.N Mkeremy, G.S Mhidze, M.A Machanga, S.B Gwaya, P.K Simuli na M.E Gaguti.

Halikadhalika Mhe. Rais Magufuli amempandisha cheo Luteni Kanali Bernard Masala Mlunga kuwa Kanali na ameteuliwa kuwa Mpambe wa Rais (Aide de Camp – ADC)

Kanali Mlunga ameteuliwa kuwa Mpambe wa Rais akichukua nafasi ya Kanali Mbaraka Naziad Mkeremy ambaye amepandishwa cheo kuwa Brigedia Jenerali.
Gerson Msigwa

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Dar es Salaam

12 Aprili, 2018

Soma: Mpambe wa Rais Magufuli abadilishwe
 
Kumbebea makabrasha raisi ,kumshikia mwamvuli pindi mvua ikinyesha,kwenda kuchukua karatasi na kumpa rais atie saini na kama kuna mzigo anabeba ..msaidizi wa raisi
Ni kweli. Ila kuna lingine kubwa zaidi ya hayo.
 
Wadau kwahiyo mlitaka afande Mkelemi aendelee kuwa ADC! Mungu anawaona jaman khaaaa. Ile kazi iskieni tu jaman muoneeen huruma mwenzenu akapumzike
 
Kanali mkelemi sio tena ADC wa mukulu,anakuja kanali mwingine" sawa, kwani ukiwa brigedia general huwezi kuwa ADC wa presidar?
Wanaofahamu mambo ya inteligencia watujuze
cc. Brother GENTAMYCINE,na wengineo
Hata Rais wa Zanzibar yeye anapambiwa na Luteni Kanali na si Kanali. Hayo ni mambo ya itifaki, na Brigedia mtu mzito, mpaka gari yake inavaa nyota !
 
Hivi CDF huwa anateuliwa kutoka kwenye rank ipi ya jeshi?
Kwa kawaida Brigadier, Major na Luten General anaweza kuwa CDF

Mara nyingi, Luten General ndio anakuwa kwenye nafas nzur ya kuwa CDF kutokana na seniority

Hata hivyo, Rais anaweza kuteua yoyote kati ya General niliyetaja hapo paragraph ya kwanza baada ya kupitia hatua mbalimbali za uteuzi
 
Hilo neno "mpambe" lina ukakasi mjue?
Maana tunaambiwa na wahenga "MPAMBE NUKSI" sasa sielewi wanavosema ati "mpambe wa Rais"
 
Mwambata wa kijeshi katika Ubalozi wa Tanzania - Abuja. It is self-explanatory Mkuu.
Sasa "mwambata" inajiexplain vp apo?
Viswahili vyenu vya BAKITA havieleweki!
Codify the language na sio kujitungia misamiati kutokana na akili zenu finyu
 
Ni vizuri muwe mnafanya tafiti kabla hamjapotosha humu Canada amiri jeshi mkuu ni tofauti kabisa na kiongozi wa nchi/serikali Yaani madaraka yote ya kiserikali yapo kwa waziri mkuu ila Governor general ambaye ndio mwakilishi wa malkia Canada amepewa nguvu juu ya majeshi sasa unaposema nchi zote una maana gani
Atakua anamaanisha "Nchi Jirani"
 
Back
Top Bottom