Tetesi: Mabadiliko ya Vifurushi yanakuja Tarehe 18.08.2022: Tutegemee unafuu au maumivu zaidi?

Iyo 32mbs unaunga bando ya milioni ngapi?
 
Aisee! 32MB/SEC? Hapo bando la mwezi si linaisha ndani ya siku?πŸ˜‚

Mimi natumia Voda, wana option ya kupunguza na kuongeza speed. Ukiongeza speed inafikia hadi 12MBps. Ukipunguza inaishia kwenye 1MBps.

So nimepunguza speed na bado naperezi kwa mtelezo kabisa. Pia imepunguza speed ya bando kuisha..
 
Ni mwendo wa makampuni kubadilisha vifurushi jinsi wanavyotaka sasa
 
Unapunguzaje/Unaongezaje speed kwenye voda mzee
 
Mi sipo voda sijapata msg yeyote ya mabadliko labda voda wameanza ustaarab wa kuwaambia wateja wao huku kwingine ukiamka asubuhi unakutana tu na za uso.
 
Mkuu unapunguzaje speed?
 
naona kama zinaweza zikawa za maumivu kwani takwimu zinaonyesha kuwa Tanzania ni moja ya nchi ambazo bundle za internet zipo chini sana.

ila huenda pia "sirikali" watakuwa wamewaagiza washushe maana hii miezi 9 tumekuwa tunapigwa kushoto na kulia na vimakato mbali mbali!
 
Tegemea maumivu zaidi, maana ninachoona ni kuthibiti matumizi ya kimtandao kwa wananchi wa kawaida kama njia ya kiusalama zaidi, maana mitandao imeonekana kuwa na nguvu sana........ni mtazamo wangu tu.
 
Tuamini kwa sasa Serikali yetu haina meno wala uwezo wa kutuondolea kero.

Wanaotuongoza unaweza kukuta wana hisa kwenye hayo makampuni. Hakuna pa kuponea.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…