Mabasi aina ya Scania na Mercedes Benz vs Yutong na Zongtong: Mchina ameuza ramani ya vita kwa adui

Mzee hizo body unazoongelea ni kutoka mombasa hazina kiwango mwaka tu zinachakaa..fananisha sauli DRH au Dpn na zhongtong yeyote DHA
Au newforce DJQ na hizo rungwe utapata jibu...
Advantage ya sauli ni terias ipo karibu na mfumo wa booster ke bet king'amuzi basi uscania hauusiki hapa
 
Kuna basi za Scania, walikuwa nazo wakina Nganga, Ottawa na Luwinzo. Zile nadhani zilichongwa South Africa ndani zilikuwa nafasi kubwa Kati ya seat ya abiria na abiria. Pia hata speed na nguvu ilikuwa kubwa. Basi ya Nganga Express niliiona ingawa ina miaka zaidi ya 10 lakini body bado haijachoka.
 
If I had $1,000,000 USD to invest, I could have approached you for a deep consultation and offer you a 1%. Nothing is so important than information.
Leo nimejikuta nalisindikiza 143M 450 V8 mpaka lilipotokomea. Kufika mbele kidogo, lingine pia hilo. Kumbe kuna wanazi wanavyo hivi vyuma hapa bongo! maana hii nchi imefurika ma 124L 420.
Kuna siku nimepakia mzigo wangu kutoka nyanda za juu kusini, kuleta town ndani ya G440, aiseee! utasema tulikua hatujabeba chochote huko nyuma, na mnyama anaondoka utasema tunasafiri na gari binafsi wakati nyuma tuna tani 32 za mzigo. Niko kwenye cab mule ndani nafikiria shughuli ya R620 V8 ( my dream truck) itakuaje, nabaki tu kuitimisha tu...NITAJICHANGA.
 
Mkuu ujue Newforce wale ni wachina ,ukizingalia New force bado zipo mkwaju kwenye bodi mpaka mashine kwa sababu zinatunzwa sana na wamiliki,ila si unajua sisi ngozi nyeusi kutunza vitu hatutaki tunajali hela tu.
 
143 ni vintage kwa sasa , ndio the longest serving truck diesel engine kwa sasa , mengi yana 30+ years of service ,na yapo mengi tu hapa kwetu the last 143 kutengenezwa ilikuwa ni mwaka 96 .
 
Sio mjuzi wa magari ila najua Sauli zina busta na madereva vichaa.
Hivi suspension ya zhongtong ni ipi???

Na kwann haiwezi kupita kwenye tuta kama bwana mkubwa acha iende au mjeshi?...
Turudi kwenye mada
Al saedy wenyewe walishakiri kwamba sauli kashindikana
Nao wana gemi on the way...
 
Hivi suspension ya zhongtong ni ipi???

Na kwann haiwezi kupita kwenye tuta kama bwana mkubwa acha iende au mjeshi?...
Turudi kwenye mada
Al saedy wenyewe walishakiri kwamba sauli kashindikana
Nao wana gemi on the way...
Zhongtong anatumia leaf steel suspension mbele na nyuma
Sauli anatumia leaf suspension mbele lakini nyuma kwenye diff na terias ni air ride (busta )

Lakini Kama Kuna gari inajua kupiga tuta ni zile Man za taqwa , zenyewe ni full air ride , busta kuanzia mbele, diff na terias .
 
Sema mkuu nakuona humu unatema nondo sana nakurespect mno
Nashukuru kwa jibu zuri la kueleweka sasa mkuu naomba tena kuuliza
Maana hio leaf suspension na busta
Kwa mm ninavyoelewa air ride ni kwamba gari inanyanyuka juu ila tairi zinabaki chini sio? Hio busta ndo inafanya gari kurudi chini bila impact sio??
Na hio ya leaf inamaana gari inapoenda juu na tairi zinaenda angan sio???
Sasa kwann zhongtong haina air ride???
Is it costful ??
Halafu mkuu nisamehe kama maswali mengi ila kwani hio full air ride inaweza kuwekwa kwenye scania?
Na kati ya man na scania kama gemi hivi ipi ina uwezo zaidi
Kwann wasitumie man hapa tz??
 
Leaf spring ni traditional , yaan yale maspringi ya vipande vipande ya chuma , leaf steel imetumika kwa Miaka mingi sana na mchina anatumia Hadi leo kwenye gari zake, leaf ina mazuri yake na ni gharama nafuu , shida yake ni kuwa zenyewe huwa Zina uzito fixed wa kubeba , uzito ukizidi ni tatizo hakuna mneso na ukipungua ni tatizo pia zinakuwa zinarusha , hii ndo sababu gari ya leaf spring haziwezi kupiga tuta vizuri

Busta ni neno la mitaani tu hata sijui lilitokea wapi , lakini kimsingi ni Air suspension, hii ni models ya kisasa Zaid nafikiri ilianza kutumika marekani Miaka ya 80, hii ni aina ya mpira unaojazwa hewa na piston kwa ajili ya kubeba mzigo, ni complex Kushinda leaf , maana inajumlisha vitu vingi Kama control valve , uzuri wa aina hii ni kwanza ni nyepesi, pili zenye huwa Zina maintain level kwa mzigo wowote zinaobeba , na zinamaintain mneso pia kea mzigo wowote zinaobeba , aina hii pia kwa sasa imekuwa linked na vitu Kama Abs Ebd and the likes
Scania full air ride zipo ,zile K series za kina air msae , kiswele Tawaqal, Matema beach and the likes zilikuwa full air ride , hata hizi 4 series zipo nyingi tu tena Hadi malori yapo , huzioni nyingi kwa sababu moja tu ni optional extra at extra cost ,
Man hazipo nyingi kwa sababu ya maintenance costs ,
Man or scania gemi?? Inategemeana na malengo yako , Kama ni Mbio na comfort Man all the way , Kama unataka compact power for life gemi all the way , kwa Mbio scania haiwezi Kamata Man , kwa segment yoyote inayojulikana.

Air ride ni neno la kutamba tu hapo zamani wakati aina hii ya suspension inaanza haikuwa kwa kila gari , ilikuwa ni optional , at extra cost , nafikiri kwenye magari madogo ipo hivyo hadi leo , kwa maana hiyo watunwalitumia Air ride Kama kitu exceptional , maana sikuwahi kusikia steel ride .
 
Ni moto balaa
 
Fact, we ushaona Dar -Tdm Abood kaweka Yutong? Ni zile zile marcopolo Dar Mbeya au Dar Tunduma
 
Man kwenye kupandisha milimani inapitwa Sana na scania
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…