Mabasi ya 'Dar Express' yanahujumiwa?

Jamani watu hutumia simu kupost issues zao kwenye mtandao sasa si mnajua hizi simu zetu hasa hizi za touch screen ambazo hazina viandikio utakuta ubabonyeza W badala ya E ,kwa hiyo kukosea ni kama kawa
 
mkubwa!
Yani humu ndani tuna raia ambao ni mizigo flu!
Na kwa kuwa tupo nao hakika tuenende na hivi hivi bila shaka wanaweza elimika hapo mbeleni.

Ama vipi tutamwomba mods aangalie hili upya!

Happy new year 2012!

what d'u mean!?
Umetumia kipimo
gan kumuona mtu
mwingine ni mzigo!?
How far are you sure
ur perfect?!
Kila mtu anatoa maon yake yale yanayokufaa yafanyie kazi yasiyokufaa yapotezee!!!

Toa boriti jichon mwako ndipo uone kibanz jichon mwa mwenzioa!!!!!
 
Naomba unisaidie haya maswali:
  1. Huduma za mabasi mengine zikoje?
  2. Je huduma zao(Dar express) zilikuwa nzuri kipindi cha nyuma?
 
Tatizo hujui hata unasema nini...familia yangu inahusika moja kwa moja na hiyo kampuni..Filisika?? Unacheza kweli....

Pesa ni maua!! Acha upuuzi ww usifikiri huyo na DR EXPRSS na vibasi vyake atashindwa kufilisika,anaweza kufilisika vile vile, wamefilisika wakina NJIWA atashindwa yeye.
 
Ndugu yangu, mtoa mada hajatia juhudi kutupa ushahidi wa Dar express kufilisika, hii haimuhusu cos ametumwa na wale mafisadi wanaonyemelea northern circuit, waache waje, sisi wateja twamjua mtoa huduma.

Hakuna aliye2mwa mkuu ni kweli DR EXPRSS huduma zao ni mbovu hasa vile vidada vinanyofanya kazi kw kukatia tiketi vinaongea nyodo halafu vina dharau mbhaaya,mimi nilikua msafiri mzuri sana wa hayo mabasi ila tokea siku hiyo niende kukata tiketi pale ubungo nimefika namuongelesha kidada kimoja chenyewe ndio kwanza kinaendelea kuandika sms kwnye simu!! nahisi yule mzee anakula vifanyakazi vyake. miye nimehamia KLM ........ Halafu nikujulishe 2 northern zoze hajaikamata DR EXPRSS peke yake kuna mabasi yanayotoa huduma nzuri zaidi y huyo DR EXPRSS so sioni sababu ya kusema kwamba anapigwa majungu!!
 
Ujumbe hauwezi kufika kama lugha iliyotumika si fasaha.
Hivyo tumia lugha sanifu usijifanye mkal wakati umekosea.
 
Hii ni moja ya kampuni kongwe kabisa ya usafiri nadhani wao na HOOD ndio wako toka 1980. Si mara nyingi kampuni za mabasi kudumu kama hizi. nadhani mtoa mada ni mtu wa kutumwa na DAR LUX BUS SERVICE ambayo tuliijadili kitambo hapa.
 

Mimi hoja yako siioni. Una"raramikia" kubadilishiwa gari? Ingekuwa umepewa tiketi na ukakosa kusafiri ningeelewa. Kama unaamini wana mabasi machache mbona waliweza kukupa "alternative bus" na ukasafiri? Basi kufika saa 3 usiku inaweza kutokea once in a while, na ni jambo la kawaida kama kweli wewe ni msafiri wa mara kwa mara utalijua hilo
Hakuna kampuni duniani itakayokwepa magari yake kuharibika au kuchelewa mara moja moja.

"Mararamiko" yako hayana mantiki unless unapigia debe mtu au watu wanaohangaishwa na ushindani wa Dar Express.
 
Kiswahili jamani Kiswahili!!! hizi shule za academy zinatuharibia watoto. Hivi kweli R na L zina sauti moja kweli?? utaona mtu anasema "Kufirisika", mwingine naye anauliza at alisafiri "Mala" Ngapi"" we beeed to go back to school. Lol
 

Usiwe mbishi kaka KULA si sawa na KURA
 
Mkuu RR sijaelewa umeandika nini "kuraramika" kiswahili cha wapi unashindwa kuandika kulalamika ? kama hiyo haitoshi umerudia tena makosa yale yale "mala ngapi" unashindwa kuandika mara ngapi ?.Tafadhali usituharibie lugha yetu adhimu.

Read mzee...soma sentensi yangu vizuri....

Hahaha...dalili za jazba maana kwake matumizi ya L na R ni kiboko

Umenielewa....:lol:

hili tatzo la heruf 'l' badala ya 'r' litaisha lini?

Umakini wa kuandika.....sina shida na kuongea (labda ni beyond repair)

laia kama hawa ndio mabingwa wa kuraramika wakati hata gali renyewe langi zake hazijui.

Hahaaaa....

msome mtoa mada utajua nani kaharibu kiswahili

Sawa BW.....(mzima weye?)



Mkuu ni vema kukubali makosa na ujirekebishe...sidhani kama kanda ya ziwa ndio inayokufanya uchanganye 'r" na 'l'....ingekua ni kuongea ningekubali kwamba umeathiriwa na lugha mama (japo unachanganya).....sioni uhusiano wa kukosea kuchapa (kwa vidole) na utamkaji....ni umakini tu unakosa.... (btw: wahindi ama wamasai kukosea haikupi uhalali wa wewe kukosea).
Jambo lingine hujapangilia vizuri hoja zako.....tulia panga!


Heri ya mwaka mpya wadau......
 
Nami nichukue fursa hii kuchangia thread hii,
Ni kweli magari ya Dar Express huduma zake zimepungua, sana na kutoridhisha. Sitapenda kuongelea kiushabiki kwa sababu sifaidiki na chochote kama watu wakipanda au wasipopanda magari hayo.

Magari hayo ukiyaangalia hata kwa nje yana muonekano mbaya, jana nilikuwa stand kumpokea mgeni stand ya Dar Express karibu magari yote matatu yaliyokuwepo pale vioo vya dereva ni kama vilikuwa vimeng'oka na kuungwa kienyeji enyeji! Nikajiuliza magari kama haya yanapoharibika ina maana yanapelekwa garaji zisizo na kiwango, hivyo nikatilia shaka hata SERVICES ya magari hayo. Hii inathibitishwa na kuharibika kwa magari ya Dar Express njiani mara kwa mara.

Usafi na huduma kwa ujumla hazikidhi haja, wameanza kuwa kama mabasi ya Ngorika yanavyofanya au Happy Nation!!! Wahudumu wake hawapo seriously na huduma ni kama wanafanyia mazoea na watu walisha claim ukitaka kuja Arusha ni usafiri ni Dar Express. Kwa huduma inazotoa Dar Express saizi naanza kuifananisha na iliyokuwa Scandinavia ilipozidiwa na wateja ikaanza kuvurunda!!!

 


Pamoja na ushauri wako mzuri kwake, tatizo halipo kwenye kupangilia hoja na lugha tu, hoja yake si hoja. Utamwitaje mtu tapeli wakati amekupa huduma uliyoilipia? Kama uliambiwa utasafiri na gari X lakini muda wa kusafiri ukaambiwa ingia gari Y lenye sifa ile ile utakuwa umetapeliwa nini?
 
Tatizo hujui hata unasema nini...familia yangu inahusika moja kwa moja na hiyo kampuni..Filisika?? Unacheza kweli....

Then kwa atitude hii kama familia yako inahusika moja kwa moja then mtafilisika kweli. Kwanini usiichukue hii kama positive challenge? Ni kweli usiopingika kama kweli tunataka kuwa fair kwamba huduma za Dar Express za say 3 years ago na sasa haziko sawa, zimeporomoka hasa. Sasa whether hili limetokea kwa makampuni mengine pia mimi sijui ninachojua ni kwamba huduma zenu (kama unasema ukweli) zimeshuka chini. Of course sikubaliani kwa kiwango fulani na mtoa mada, mfano neno kufilisika limetumika ndivyo sivyo, ni kama vile kuua sisimizi kwa bunduki. Lakini mapungufu yake ya mawasiliano likiwemo matumizi ya R na L yangewekwa kando na tujudge content kitu ambacho ndicho kinacho matter zaidi.
 

Mzee wa Rula, ukijiuliza maswali wewe mwenyewe juu ya issue inayomhusu a third party na ukayatafutia majibu wewe mwenyewe almost always utakuwa na wrong conclusions.
Kama wewe mimi sina personal interest na kampuni ya Dar Express, ila kwa kuwa nasafiri nao mara kwa mara ninaweza kukujibu. Wana mabasi brands tatu, Scania, Iriza na Mercedes Benz. Zile Scania Marco Polo karibu zote vioo vyake vime crack, na kwa kuwa magari karibu yote ya brand hiyo yana tatizo hilo hilo ni wazi kuwa ni defects toka kwa watengenezaji (kumbuka Dar Express huagiza at least mabasi 10 kwa wakati mmoja). Bahati mbaya kampuni inayotengeneza magari ya Scania (Saab) imekuwa na matatizo makubwa kiasi cha kusimamisha operations. Dar Express wamelazimika kutoa special order ya kutengenezewa vioo kuvibadilisha hivyo vibovu maana havipatikani nchini wala mahali popote pengine.

Magari yao ni under guarantee, kwa hiyo kusema wanapeleka gereji za uchochoroni si sahihi. Halafu sidhani kuwa "muonekano" mbaya wa gari ni tatizo, labda uniambie performance maana muonekano mbaya kwako waweza kuwa mzuri kwa Bujibuji, Sikonge na kadhalika na kadhalika.

Heri ya mwaka mpya!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…