Mabati bora ya kuezeka nyumba

Mabati bora ya kuezeka nyumba

kumbe wanakata hadi mita 12 vipi kuhusu kofia walikukatia ndefu?yah

kumbe wanakata hadi mita 12 vipi kuhusu kofia walikukatia ndefu?
Ndiyo wanakata, hata mafundi walikuwa hawajawahi kukata mita 12+ . Kuhusu kofia nadhani hawakati, nilikuta zipo tayari nadhani ni ft 12 (sina uhakika sana) ila za valley hazikuwepo wakatuambia tuchukue bati za kawaida za rangi km ile ya bati mafundi wakakunje maan zinakaa ndani tu zinafaa, na fundi alikubali na kusema hufanya hivyo mara nyingi wakikuta valleys zimeisha.
 
Ndiyo wanakata, hata mafundi walikuwa hawajawahi kukata mita 12+ . Kuhusu kofia nadhani hawakati, nilikuta zipo tayari nadhani ni ft 12 (sina uhakika sana) ila za valley hazikuwepo wakatuambia tuchukue bati za kawaida za rangi km ile ya bati mafundi wakakunje maan zinakaa ndani tu zinafaa, na fundi alikubali na kusema hufanya hivyo mara nyingi wakikuta valleys zimeisha.
ndio naskia kofia zao n mita 3 mwisho.
 
ALAF amezidiwa quality na mchina shunshare,binafsi nimetumia wote na utofauti nimeona ,hilo bati la mchina ni litamu kiasi kwamba unatamani utowezee mkate.Ila bei imechangamka kuliko ALAF
 
ALAF kiboko yao. Unaenda na vipimo vyako wanakufyatuli kwa kadri unavyotaka. Inapunguza uharibifu wa mabati.
 
ANDO.


Naomba ufafanuzi kwa wazoefu juu ya Mabati kwaajili ya kuezeka nyumba. Ni mabati gani ambayo ni bora zaidi ambayo hayana changamoto za kupauka na gharama zake. Maana sasa hivi viwanda ni vingi sana na kila mtu anavutia kwake.
 
Kwanza sio kweli bat nzuri zinatola alaf pekee bali yapo makampuni zaidi ya Saba yenye quality sawa na hata kupitishwa na serikali kutumia katika majengo yake.

Kinachowasumbua wengi ni vitu viwili
Moja ni unene wa Bati(gauge). Kwa mikoa ya pwani yote(karibu na bahari) na hata sehemu zenye hali ya hewa inayobadilika mara Kwa mara joto Kali na mvua gauge 30 hazifai kabisa Kila miaka 7 hadi 15 utabadili Bati. Hivyo Kwa pwani usinunue geji 30. Walau 28 na kuendelea.

Tatizo la pili ni rangi: Kuna rangi hata iwe nzuri kiasi gani zitapauka TU. Mojawapo ya rangi hizo ni blue(blue bahari), deep red, na rangi zingine zote zinazong'aa sana. Pia marneo ya pwani sio salama joto Kali na mvua za ghafla, chumvi n.k vyote hupelekea rangi hizo kufubaa haraka na kuonekana.

Ndio maana alaf hazalishi Bati zenye rangi hizo.

Rangi zisizong'aa kama grey, brick red, etc hutumia muda mrefu sana mpaka kuona kama imebadilika. Hivyo Kwa pwani rangi nyekundu, blue na zile zote unazoona zimepauka haraka usinunue hata Kwa Bati zenye ubora.

Mwisho.
Kiwango cha ubora kinapimwa na maisha ya Bati ambao gauge 30 ni kati ya miaka 10 hadi 15 warranty utapewa walau 5yrs

28G ina maisha kati ya miaka 20 na 40yrs na warrant ya miaka 10.

26G warrant yake ni kati 40 na 60yrs warant yake ni 15yrs.

Hakuna atakayekupa warrant ya rangi. Maana joto likiwa Kali Bati linatanuka ikipoa linasinyaa hivyo hali hewa ikiwa mbaya lazima rangi itapauka TU. Hivyo hakuna warrant, ukiona wanakuambiabni Ile TU wamefanya kautafiti kamahali kulingana na hali ya hewa na rambi zisizong'aa ni ngumu kuona Kwa haraka.

Kama utahitaji nikusaidie ipate Bati Bora Kwa reasonable price karibu pia nafahamu watu wanafanya karibu viwanda vyote na hizo taarifa ni kutoka kwao
 
Kiwango cha ubora kinapimwa na maisha ya Bati ambao gauge 30 ni kati ya miaka 10 hadi 15 warranty utapewa walau 5yrs
Siyo kweli mkuu, labda useme matunzo nayo yanaongeza maisha ya bati. 30G no zaidi ya hiyo uliweka hapo. Ninayo leo mwaka wa 18 huu na sifikrii kubadilisha hivi karibuni!
 
Siyo kweli mkuu, labda useme matunzo nayo yanaongeza maisha ya bati. 30G no zaidi ya hiyo uliweka hapo. Ninayo leo mwaka wa 18 huu na sifikrii kubadilisha hivi karibuni!
Mkuu hayo mabati unayatumia mkoa gani? Lakini nenda kasome standard za bati utajua ninachosema.

Pili Bati kuisha ubora sio lazima livuje
 
Mkuu noamba uelezee zaidi kuhusu hili bati.



ANDO ROOFING PRODUCTS LIMITED
0769 529 392

ANDO ROOFING PRODUCTS LIMITED - Google Search

Ndio mabati imara na bora zaidi kwa zama hizi.
Kama unataka unaweza kuwatembelea kiwandani kwao pia.
Ni kampuni ya hapa hapa Tanzania
Fuata hiyo link na ukitaka unaweza kugoogle ukafungua option ya images utaona aina tofauti za mabati yao na pia mawasiliano yao yako hapo juu.
 
Tahadhari Ogopeni matapeli wanaojiita mawakala, wengi wao siyo waaminifu, wanachanganya bati za kampuni tofauti tofauti halafu wanakuizia bei kubwa km bati za ALAF.

Kwa uzoefu wangu km nyumba yako ni kubwa na unahitaji bati nyingi bora uende kiwandani mwenyewe.

Siri ni moja tu waliyoniambia ALAF kipindi nanunua kiwandani kwao, walisema bati lao original lina mhuri wa moto, na kweli bati zote nilizobeba pale zilikuwa na mhuri wa moto, Toka 2020 Dec hadi Leo watu wanapita wanashangaa hayapauki, utafikiri nimeweka jana. Ila kwa bei ndo habari nyingine, ukizingtia nilichukua yale ya muundo wa vigae, na ubebaji wake nilitumia semi maana kulikuwa na marefu hadi mita 12 na point. Ila namshukuru sana Mungu mambo siyo mabaya
Mita moja sh ngapi?
 
Naomba ufafanuzi kwa wazoefu juu ya Mabati kwaajili ya kuezeka nyumba. Ni mabati gani ambayo ni bora zaidi ambayo hayana changamoto za kupauka na gharama zake. Maana sasa hivi viwanda ni vingi sana na kila mtu anavutia kwake.
Usihofu, mabati ya nyasi yako poa sana
 
Mita moja sh ngapi?
Sikumbuki vizuri ni muda kidogo 2020, ila iliikuwa haipungui elf 27. Maana bati aina hii pamoja na ROMANTILE ndo zenye bei kubwa kuliko zote. Nilikamuliwa kisawasawa sina hamu ila ndo hivyo usipende vizuri lazima ugharamie. Na hizi bei hubadilika kwa sasa zinaweza kuwa tofauti, ni wewe tu kwenda kiwandan kuulizia
 
Back
Top Bottom