Uchaguzi 2020 Mabeberu wameitikisa nchi, ajenda yao kuu ni kumuweka Tundu Lissu madarakani

Uchaguzi 2020 Mabeberu wameitikisa nchi, ajenda yao kuu ni kumuweka Tundu Lissu madarakani

Kejuu

JF-Expert Member
Joined
May 20, 2020
Posts
645
Reaction score
906
Ndugu Watanzania,

Kipekee napenda kumshukuru Mungu kwa kuniamsha salama.

Sasa naanza kuona kwa vitendo kitu ambacho nilitumia my mental image na kuona kuwa nchi fulani zitaingilia uchaguzi wetu huu na viashiria vimeanza kuonekana sasa. Kitendo cha nchi yetu kukaa kwa takribani mwezi mmoja na kitu au miwili kwenye uchumi wa kati, ni njama tu ya kuitikisa nchi yetu kuelekea kwenye uchaguzi mkuu. Samba mba na hilo, na hii imetokea tu baada ya kuanza kusikika kwa tetesi za kwamba, jina la Tundu Lissu linaelekea kukatwa na tume ya uchaguzi, na tumeiona barua ya mabeberu wanaoumtetea Tundu Lissu Amsterdam and Partners LLP.

Kama ulikuwa unamfuatilia Tundu Lissu tangu arudi nchini, amekuwa akitoa maneno ya kutisha na kuonyesha jeuri kubwa sana kwa serikali. Kwa mfano, kama TL ameweza kuwapata wadhamini kutoka Zanzibar bila ya kwenda kufanya mikutano ya hadhara visiwani kule, swali la kujiuliza hapa ni kwamba, mikutano aliyokuwa anaifanya huku Tanzania bara ilikuwa na lengo gani zaidi ya kuonyesha ubabe zidi ya NEC? Hii jeuri aliyonayo huyu ndugu inatoka kwa hawa mabeberu na si vinginevyo.

Aidha, kutikiswa huku kumeanza kuweka wazi wazi kuwa Tundu Lissu ni mgombea wa namna gani na mabeberu wanataka nini hasa kwenye uchaguzi huu. Naona mambo haya: (1) Tundu Lissu ni mgombea aliyeandaliwa na mabeberu ili aweze kumng’oa madarakani Mh. Magufuli; (2) hata kama Mh. Magufuli atashinda, Chadema hawatakubali, na mabeberu watawasaidia kwa namna yoyote ile ili kuleta taharuki baada ya uchaguzi mkuu.

Katika bara la Afrika, maraisi wa namna ya Mh. Magufuli ambao ni wazalendo kweli kweli katika nchi zao, na hufanya kila namna kulinda maliasili za nchi zidi ya uporaji wa mabeberu, huchukiwa sana na watu hawa. Tumeziona juhudi za Mh. Raisi kwa miaka hii mitano katika kuipigania nchi hii. Katika uchaguzi huu, jamaa hawa watafanya kila mbinu ili wamung’oe Mh. Raisi madarakani na kumuweka Tundu Lissu ili kuitumiza malengo yao. Ndugu watanzania wenzangu, nchi yetu imeanza kutikiswa, nawasihi tuiombee nchi yetu na Mh. Raisi pia ili Mungu ampe hekima na busura na nguvu ya kutuvusha salama dhidi ya mpango huu ovu. Kama Mungu alituvusha salama kwenye janga la Korona, naamini atatuvusha tena kwenye uchaguzi huu.

Asante sana,
Nawasilisha,
Kejuu.
 
Duh...!.
P
Pascal Mayalla unaona hoja za vijana?

Utawala uliopo ndio umemfanya Tundu Lissu awe jitu la kutisha.

Amenusurika kifo, ana kesi lukuki zisizo na kichwa Wala miguu, amedhulumiwa haki na stahiki zake za kibunge, yaani hakika matendo ya serikali dhidi yake ndio yamemfanya asiwe muoga Tena.

Leo mnaanza kulialia, mlizuia siasa miaka mitano, Leo tuna kiu ya kuwasikiliza mliowaziba midomo.
Hi ndio karma yenyewe
 
Ukiwa na kesi unatafuta mwanasheria aliyebobea mwenye uwezo wa kuisimamia kesi yako. Lissu amemtafuta Robert Amsterdam kuwa mwanasheria wake, Mr Amsterdam angeweza kuwa Mjamaica au Mmarekani mweusi lakini imetokea tu amekua mzungu. Punguza ubaguzi.
 
Wakati mnarukaruka na kukanyagana hapo Lumumba, chondechonde mtuachie nchi yetu salama. Naona kabisa hamjui kutofautisha kati ya nchi na ccm 😆

Mmezoea kumwaga mboga kila uchaguzi bila kuwajibishwa! Safari hii mkimwaga mboga tutawaadabisha na ugali tutaula kwa kurumanga
 
Magufuli siyo mzalendo pekee nchi hii
Hata siye tupo.
Tanzania aliiikuta na ataiacha,amekufa Mkapa sembuse yeye!
The bottomline is mwacheni Lissu agombee,wananchi kama hawampendi vichinjio wanavyo watamkata
Kama kweli nyinyi CCM mnajiamini kuwa mmewafanyia maendeleo makubwa wananchi wa nchi hii, basi waachieni wenyewe wananchi waamue kwenye sanduku la kura.........

Lakini hizi tetesi zilizoenea hivi sasa kuwa nyinyi CCM mnapanga njama za kulikata jina la Tundu Lissu, zitaliingiza Taifa hili katika machafuko makubwa, ambayo hayajawahi shuhudiwa nchi hii
 
Kuna watu mnafanya analysis very emotionally driven, Sasa TAL hana ubavu wa kushika hii nchi na kamwe hawezi kuwa Rais, Afu tu nikujuze sambamba na Vyombo vya dola kutokulala kuhakikisha wewe unakuja kuhara apa safely, Watanzania tuna desturi ya kupenda amani utatugawa kwa lipi kama udini na ukabila kwetu sisi sio inshu kabisa
 
Ndugu Watanzania,

Kipekee napenda kumshukuru Mungu kwa kuniamsha salama...

Kwani haya yakifanyika serikali kama nia yao ni uchaguzi huru na wa haki wataathirika wapi?

1. Futa kesi zote zanazomkabili Lissu au ziahirishe hadi baada ya uchaguzi.

2. Acha hatima ya Lissu kiuchaguzi iamuriwe na wapiga kura kwa kuhakikisha uhuru na uwazi kamili katika kampeni, kupiga kura, kuhesabu kura na kutangaza matokeo.

Hao mabeberu unaowaongelea wewe wanatokea wapi katika hatua hizo mbili?

Bandugu mnatuchanganya. Mabeberu wanataka haki na nyie mnataka kuminya haki.

Kwa mtaji huu yaonesha yupi ni mbaya (zaidi) baina ya mabeberu na mkoloni mweusi nyie.
 
Back
Top Bottom