Mabilioni ya shilingi yamwagwa kujenga barabara Kigoma

Mabilioni ya shilingi yamwagwa kujenga barabara Kigoma

Dah huu Mkoa waukumbuke tu.
Mwaka juzi nilienda huko ni tabu tupu, yaan kutoka kigoma mpaka Kasulu ni vurugu tupu, iwe kiangazi iwe masika!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sio mjuzi wa hii barabara ila ndio inayounganisha mkoa wa kigoma na jiji LA Mwanza Kwa njia ya Lami kupitia nyakanazi? Sababu navyojua hiyo bara bara ilikuwa na mkandarasi tayari, au ni nyingine?

Nyanza Road ways co. Ltd miaka nenda rudi.

Kampuni ya wenyewe.
 
View attachment 1365779

SERIKALI ya Tanzania imetiliana saini mkataba na wakandarasi wanne wa kampuni ya ujenzi ya China kwa ajili ya barabara ya kiwango cha lami kutoka Kabingo wilayani Kakonko hadi Manyovu wilayani Buhigwe yenye urefu wa kilometa 260 kwa gharama ya Sh bilioni 584.7.

Waziri wa Ujenzi, Isack Kamwelwe aliongoza viongozi wa Serikali ya Tanzania kushuhudia utiaji saini huo ambao Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara (Tanroads), Patrick Mfugale aliongoza utiaji saini huo kwa Serikali ya Tanzania ambao unafanyika kutokana na mkopo wa riba nafuu kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) huku Serikali ya Tanzania ikitoa kiasi cha Sh bilioni 58 kuchangia ujenzi huo.

Akizungumza kabla ya utiaji saini, Kamwelwe alisema ujenzi huo wa barabara ni matokeo ya ahadi aliyotoa Dk John Magufuli wakati wa kampeni za urais mwaka 2015. Alisema aliona ukanda wa magharibi una changamoto kubwa. Akitoa taarifa kabla ya utiaji saini huo, Mfugale alisema mradi huo wa ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami umegawanywa kwenye vipande vinne kuwezesha ujenzi wake kufanywa kwa haraka na katika kipindi cha miaka mitatu barabara hiyo inapaswa ianze kutumika.

Aliwataja wakandarasi hao kuwa ni Zhejiang Communication Construction Group Co. Ltd iliyopewa kipande cha Manyovu hadi Kasulu kilometa 68.2 kwa gharama ya Sh bilioni 76.1 na Sinohydro Corporation Ltd iliyopewa kipande cha kuanzia Kasulu Mjini hadi Mvugwe wilayani Kasulu kilometa 70.5 kwa gharama ya Sh bilioni 83.7.

Wengine ni STECOL Corporation iliyopewa kipande cha kuanzia Kijiji cha Mvugwe hadi eneo la njia panda ya Kambi ya Wakimbizi Nduta wilayani Kibondo kilometa 59.3 kwa gharama ya Sh bilioni 84.7 na China Hennan International Cooperation Group (CHICCO) kilometa 62.5 iliyopewa kipande cha kuanzia njia panda ya Kambi ya Wakimbizi ya Nduta hadi Kijiji cha Kabingo kwa gharama ya Sh bilioni 95.5.

Kwa upande wake, Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango alisema atasimamia kwa karibu kuhakikisha fedha za utekelezaji wa mradi huo zinatolewa kwa wakati ili kuwezesha kutekelezwa kwa muda huo uliopangwa.

Dk Mpango alisema ujenzi wa barabara hiyo siyo muhimu kwa uchumi wa Mkoa wa Kigoma na watu wake pekee, bali kwa Taifa kutokana na mkoa kuwa kitovu cha uchumi kwa nchi za Afrika Mashariki na Kusini mwa barabara la Afrika; na kuongeza kuwa lazima Tanroads waoneshe weledi wao katika kusimamia utekelezaji wa mradi huo kwa viwango na wakati huku akionya wakandarasi kutoyumbisha na kuomba kuongezewa muda bila sababu.

Naye Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako alisema barabara hiyo ni tukio muhimu kwa mkoa huo kwani kuna watu ambao hawajawahi kuona lami hivyo kwao jambo hilo lilileta manung’uko makubwa na kujiona kama siyo sehemu ya Tanzania.

Akitoa neno kwa niaba ya wananchi wake, Mkuu wa mkoa, Emmanuel Maganga alisema kwao mradi huo ni moja ya miradi iliyokuwa ikisubiriwa kwa muda mrefu kutokana na umuhimu wake kiuchumi kwa wananchi wa mkoa huo kwani ni mkoa wa kimkakati kwa ajili ya soko la Ukanda wa Nchi za Maziwa Makuu. Aliwataka wakandarasi kuzingatia kuajiri vijana kutoka mkoani humo katika kazi ambazo hazihitaji utaalamu.
Yote haya yananikumbusha maneno ya mbunge wa KILWA..Mr. Bwege... alisema, nanukuu.... 'CCM TUNAWAJUA, WATABANAA LAKINI KULEE MWISHOOOONIIIII WATAACHIA'... mwisho wa kunukuu
 
Wawalipe.thatha thio kama wale wa mikoa mingine miradi imethimama

Don't make a promise you can't fulfill...
 
akili za kijinga sana hizi. Yaani kila mradi wanajenga wageni wakati vijana wetu hawana kazi, why?

Nchi zote duniani zinategemeana kwa kazi Mkuu
Wazawa wana fursa pia ya kupata kazi katika kazi hizo
Hata Ulaya pia sio kila kitu wanafanya wao mengine mengi yanafanywa na kampuni za nje



Sent from my iPhone using Tapatalk
 
Hapo sawa jambo jema,mambo ya kutapakanya fedha zetu kwenye biashara kichaa ya midirimulaina na mibombadiyee hatutaki.
 
Sio mjuzi wa hii barabara ila ndio inayounganisha mkoa wa kigoma na jiji LA Mwanza Kwa njia ya Lami kupitia nyakanazi? Sababu navyojua hiyo bara bara ilikuwa na mkandarasi tayari, au ni nyingine?
Ninatamani sana pangekuwa na ramani za barabara hizi, lakini sijui kwa nini hilo huwa ni gumu kulifanya!
 
Zitto lazima atapinga mradi huu!

siwezi kupinga kwa sababu ni moja ya miradi nimepigia kelele maisha yangu yote ya Ubunge na ipo kwenye ilani ya ACT mwaka 2015 na pia African Development Bank niliwasumbua sana kuhusu Mradi huu.
Wala Mradi huu hautakuwa sababu ya watu wa Kigoma kuipa kura CCM kwani sio hisani bali ni Haki yetu
 
ZITO, Ninachochua nikuwa Barabara na madaraj ni maendeleo ya Vitu amabvyo upinzani na baadhi wa wnaccm wanataka maendeleo ya watu. Kwani ni leo unasupport maendelo ya vitu kama Barabara na madaraja au kwa kuwa yanajengwa kwenda Kigoma il yakijengwa pengine inakuwa siyo maendeleo ya watu. Hebu dadavua

siwezi kupinga kwa sababu ni moja ya miradi nimepigia kelele maisha yangu yote ya Ubunge na ipo kwenye ilani ya ACT mwaka 2015 na pia African Development Bank niliwasumbua sana kuhusu Mradi huu.
Wala Mradi huu hautakuwa sababu ya watu wa Kigoma kuipa kura CCM kwani sio hisani bali ni Haki yetu
 
Sio mjuzi wa hii barabara ila ndio inayounganisha mkoa wa kigoma na jiji LA Mwanza Kwa njia ya Lami kupitia nyakanazi? Sababu navyojua hiyo bara bara ilikuwa na mkandarasi tayari, au ni nyingine?
Zana Za Kilimo aliitisha wazee wake ili mradi usifanikiwe , na akishindwa kwa njia za asili ataandika barua kwa "Mabeberu"
 
View attachment 1365779

SERIKALI ya Tanzania imetiliana saini mkataba na wakandarasi wanne wa kampuni ya ujenzi ya China kwa ajili ya barabara ya kiwango cha lami kutoka Kabingo wilayani Kakonko hadi Manyovu wilayani Buhigwe yenye urefu wa kilometa 260 kwa gharama ya Sh bilioni 584.7.

Waziri wa Ujenzi, Isack Kamwelwe aliongoza viongozi wa Serikali ya Tanzania kushuhudia utiaji saini huo ambao Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara (Tanroads), Patrick Mfugale aliongoza utiaji saini huo kwa Serikali ya Tanzania ambao unafanyika kutokana na mkopo wa riba nafuu kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) huku Serikali ya Tanzania ikitoa kiasi cha Sh bilioni 58 kuchangia ujenzi huo.

Akizungumza kabla ya utiaji saini, Kamwelwe alisema ujenzi huo wa barabara ni matokeo ya ahadi aliyotoa Dk John Magufuli wakati wa kampeni za urais mwaka 2015. Alisema aliona ukanda wa magharibi una changamoto kubwa. Akitoa taarifa kabla ya utiaji saini huo, Mfugale alisema mradi huo wa ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami umegawanywa kwenye vipande vinne kuwezesha ujenzi wake kufanywa kwa haraka na katika kipindi cha miaka mitatu barabara hiyo inapaswa ianze kutumika.

Aliwataja wakandarasi hao kuwa ni Zhejiang Communication Construction Group Co. Ltd iliyopewa kipande cha Manyovu hadi Kasulu kilometa 68.2 kwa gharama ya Sh bilioni 76.1 na Sinohydro Corporation Ltd iliyopewa kipande cha kuanzia Kasulu Mjini hadi Mvugwe wilayani Kasulu kilometa 70.5 kwa gharama ya Sh bilioni 83.7.

Wengine ni STECOL Corporation iliyopewa kipande cha kuanzia Kijiji cha Mvugwe hadi eneo la njia panda ya Kambi ya Wakimbizi Nduta wilayani Kibondo kilometa 59.3 kwa gharama ya Sh bilioni 84.7 na China Hennan International Cooperation Group (CHICCO) kilometa 62.5 iliyopewa kipande cha kuanzia njia panda ya Kambi ya Wakimbizi ya Nduta hadi Kijiji cha Kabingo kwa gharama ya Sh bilioni 95.5.

Kwa upande wake, Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango alisema atasimamia kwa karibu kuhakikisha fedha za utekelezaji wa mradi huo zinatolewa kwa wakati ili kuwezesha kutekelezwa kwa muda huo uliopangwa.

Dk Mpango alisema ujenzi wa barabara hiyo siyo muhimu kwa uchumi wa Mkoa wa Kigoma na watu wake pekee, bali kwa Taifa kutokana na mkoa kuwa kitovu cha uchumi kwa nchi za Afrika Mashariki na Kusini mwa barabara la Afrika; na kuongeza kuwa lazima Tanroads waoneshe weledi wao katika kusimamia utekelezaji wa mradi huo kwa viwango na wakati huku akionya wakandarasi kutoyumbisha na kuomba kuongezewa muda bila sababu.

Naye Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako alisema barabara hiyo ni tukio muhimu kwa mkoa huo kwani kuna watu ambao hawajawahi kuona lami hivyo kwao jambo hilo lilileta manung’uko makubwa na kujiona kama siyo sehemu ya Tanzania.

Akitoa neno kwa niaba ya wananchi wake, Mkuu wa mkoa, Emmanuel Maganga alisema kwao mradi huo ni moja ya miradi iliyokuwa ikisubiriwa kwa muda mrefu kutokana na umuhimu wake kiuchumi kwa wananchi wa mkoa huo kwani ni mkoa wa kimkakati kwa ajili ya soko la Ukanda wa Nchi za Maziwa Makuu. Aliwataka wakandarasi kuzingatia kuajiri vijana kutoka mkoani humo katika kazi ambazo hazihitaji utaalamu.
Hii ndiyo faida ya wananchi kuwa na utayari na uthubutu wa kuchagua na kuishi na "strong opposition parties". Katika maeneo hayo chama tawala kinakosa namna zaidi ya kuanza kuwekeza miradi mikubwa ya maendeleo ili kuwafanya wavutiwe na sera zao.

Maeneo mengi ambayo upinzani ni dhaifu huishia tu kuyasikia ktk vyombo vya habari maendeleo kama haya. Kupanga ni kuchagua, kwa hiyo kazi ni kwao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sio mjuzi wa hii barabara ila ndio inayounganisha mkoa wa kigoma na jiji LA Mwanza Kwa njia ya Lami kupitia nyakanazi? Sababu navyojua hiyo bara bara ilikuwa na mkandarasi tayari, au ni nyingine?
Hiyo nyingine
 
siwezi kupinga kwa sababu ni moja ya miradi nimepigia kelele maisha yangu yote ya Ubunge na ipo kwenye ilani ya ACT mwaka 2015 na pia African Development Bank niliwasumbua sana kuhusu Mradi huu.
Wala Mradi huu hautakuwa sababu ya watu wa Kigoma kuipa kura CCM kwani sio hisani bali ni Haki yetu
Wewe zitto kweli unatabia za umaraya maraya , juzi hapa umepinga tanzania tusipewe mkopo! Umaraya wa kupiga kelele ili serikari ya ccm ipewe huu mkopo wa kujenga hii barabara ulitoka wapi.
Nyie wa tatu mmejimariza wenyewe! Mwenzio Tundulisu anatafutwa na mahakama aje ale mshono!
Mbowee nae chama kina mfia , umesikia makatibu wa kanda alochagua leo! Ni dariri ya chama kufa
Wewe nawe ulishanyea kambi.
 
Back
Top Bottom