Mabishano kati ya medical professionals yanayolenga interests za mgonjwa ni jambo la kawaida na ni ethical

Mabishano kati ya medical professionals yanayolenga interests za mgonjwa ni jambo la kawaida na ni ethical

It 100% unethical. You dont argue on the patient's fate right in frintt6of them. Unakuja mbele ya mgonjwa when decisions are made. Worst of all arguments on matters of opinion can be tolerated but not on matters of fact . The latter portrays incompetence.
 
Nani kakufundisha kwamba wauguzi hawana ufahamu wo wote wa mambo ya maabara? Unajua wanajifunza nini katika hiyo kozi ya miaka 4 ya diploma in clinical nursing au ile kozi ya BSc in clinical nursing?
Ainisha kazia kukosea kwa yule nurse na kisha weka bayana ufahamu wenu na speculate why ajizime data? Na pia kuna wahitimu ambao ni vilaza kwenye baadha ya masomo na baadhi kupita kwa rushwa au hongo, sio ajabu kuwa network kichwani hana, chetu fake alonunua cheti na kama mwenye cheti sio mwajiriwa bado wapo kazini
 
Nani kakufundisha kwamba wauguzi hawana ufahamu wo wote wa mambo ya maabara? Unajua wanajifunza nini katika hiyo kozi ya miaka 4 ya diploma in clinical nursing au ile kozi ya BSc in clinical nursing?
diploma nursing miaka 3 sio minne, wanasoma basics za lab sio deep kama unavyodhani na by the way hata wanaosoma maabara kuna vitu wanasoma lakini mipaka ipo.

wao kuchoma sindano ya kutoa damu kuna mishipa hawaruhusiwi unless otherwise amekuwa trained..hata chanjo tu haruhusiwi kuchoma..haohao wanaosoma maabara wanasoma pia kuhusu dawa zinazoweza kumsaidia mgonjwa endapo mgonjwa anaumwa na dawa zingine zimeshindwa kumsaidia.

kwa maana hiyo sio kwamba wa maabara hawajui vya famasia wanajua lakini mipaka ya kazi hairuhusu kuvuka hapo na kugawa dawa au kuandikia mtu dawa hata kama anajua unless ipite tena kwa daktari aipitishe..iweje aliyesoma nursing aje akupangie kutumia kifaa kilichokwisha muda wake?

Taaluma ziheshimiwe na jamaa wa maabara aliyerekodi kakosea kurekodi angetakiwa apeleke malalamiko hayo kwenye uongozi endapo anaona hilo suala limemshinda na sio kupost mtandaoni.

yote tisa kumi mtu mwenye akili timamu huwezi kutumia kipimo kilichokwisha muda kumpimia mtu.Sio unethical tu hata kiubinadamu japo haimletei madhara kwenye mwili kwa sababu sio dawa ila nafsi yako haikusuti hata kidogo ukifanya hivyo kweli?

Haya umpime aonekane anaumwa kumbe kifaa hakipo sawa uanze kummezesha mtu dawa huoni ni dhambi zingine unazitafuta kwa nguvu??
 
Hapo kuna uovu gani umetendeka? Unajua maana ya expirely date? Unadhani hizo chemicals zina exact date ya kuharibika? For your information hiyo expirely date iliyooneshwa na manufacturer ni ya makisisio tu ambayo manufacturer anajitoa responsibility kwa kile kitakachotokea baada ya tarehe hiyo. Mara nyingi huwa ni plus or minus three months.

Maana yake ni kuwa chemical hiyo inaweza expire miezi 3 kabla ya tarehe iliyooneshwa au miezi 3 baada ya tarehe iliyooneshwa kutegemea na aina ya chemical hiyo na mazingara iliyotunzwa. Zinatakiwa kufanyiwa quality testing za mara kwa mara kubaini ubora wake.
Kama ni Ni 3+ or 3-D common sense would tell you that presumption should be in favour of -3.
 
Ni uzembe wa wasimamizi wa huduma hizi yaani DHMTs (district health management teams) zinazoongozwa na waganga wakuu wa wilaya (DMOs) na RHMTs zinazoongozwa na waganga wakuu wa mikoa (RMOs). Timu hizi zinatakiwa kuzifanyiwa quality testing maabara hizo za mara kwa mara. Yaani hata wewe jaribu tu hata siku moja badala ya mkojo wapelekee maji yaliyochanganywa na fanta au wapelekee mkojo wa ng'ombe au mbuzi. Utashangaa majibu utakayopewa. Utaambiwa una UTI sugu au kisonono. Wapelekee damu ya kuku, utaambiwa una malaria tatu au typhoid au HIV.
My friend, chain ya kiutawala taasisi, wakuu wa vitengo, idara hawana uhuru wa kitaaluma, uhuru wa weledi, kulindwa na uonevu, kulindwa na viapo, kulindwa na sheria, Amri amri na ukionekana unatumia kanuni za kitaaluma unaonekana hufai, huo ukaguzi ukifanyika upigaji haupo, kila mmoja ni mfalme wa mwenzake kwa faida zake.

Watu wanashudia kupitia bima ya afya na malipo cash mahospitalini tunaandikiwa dawa lukuki bila hofu ili tu dawa ziishe hospital iagize zingine na pesa iingie, kwa sasa hakuna Kada ya watu waovu na mashetani kama sekta ya Afya.
 
Mabishano kati ya medical professionals yanayolenga kupata huduma sahihi na safi kwa wagonjwa wao ni kitu cha kawaida na cha kila siku. Mabishano au mijadala ya namna hiyo kuna wakati mwingine inakuwaga mikali sana (heated). Mijadala hii hufanyika aidha kati ya mtu mmoja mmoja au kivikundi. Mabishano kama hayo ni very medically ethical kwani yanalenga kutoa huduma bora kwa mteja/ mgonjwa. Cha muhimu tu ni kwamba mabishano kama hayo hayapaswi kufanyika mbele ya mteja/ mgonjwa.

Mabishano yaliyotokea kati ya muuguzi na mmaabara huko Tabora yalikuwa ya aina hiyo. Muuguzi alikuwa anataka mteja wake mwenye mimba afanyiwe kipimo cha malaria ya MRDT ambacho mmaabara alikuwa amekataa kwa sababu kipimo hicho hakitatoa majibu sahihi kwa kuwa diagnostic kits alizokuwanazo za kipimo hiko zilikuwa zime expire. Muuguzi hakukubaliana na sababu hizo na alitaka mmaabara afanye tu kipimo hicho hata kama expirely date ya kits hizo ilishavukwa. Mteja hakuwepo eneo la mabishano.

Tatizo liko kwa yule aliyeamua kuwarekodi wawili hao walipokuwa wanabishana na kuyarusha mabishano hayo kwenye mitandao ya kijamii kwa manufaa anayeyajua mwenyewe. Kama mtu huyu naye ni medical professional, basi atakuwa na kesi kubwa ya ki medical ethics ya kujibu.

Tatizo suala hili limechukuliwa kisiasa baada ya video hiyo kuonekana na wanasiasa. Wale innocent persons wametimuliwa kazi. Yule culpit aliye record na kusambaza hizo picha anapeta. Eti anaitwa whistle blower. Ana blower kitu gani ambacho hakiko sahihi ki medical?
Hii unayoita ni kawaida, inatokea wapi?
Nimefanya kwenye sekta ya afya kipindi fulani, sio Tz, huko wote kuanzia tabibu, mkunga na wasaidizi wake, watu wa madawa, wa mazoezi ya viungo wanajitambua kama ni kikundi (team).
Hawabishani, bali kuna vikao vya mara kwa mara na mgonjwa fulani atajadiliwa tatizo lake, maendeleo yake, mbinu gani itumike/ inayomletea ahueni, ikiwa ni pamoja na madawa au mazoezi. Kila mmoja ya watoa huduma hutoa maelezo yake, hawabishani!
Sasa hao unaowatetea, wanabishana juu ya dawa zilizoisha muda wake wa matumizi, na mkunga anataka zigawiwe kwa wajawazito!! Unaona ni Sawa hilo??!!
 
Nani kakufundisha kwamba wauguzi hawana ufahamu wo wote wa mambo ya maabara? Unajua wanajifunza nini katika hiyo kozi ya miaka 4 ya diploma in clinical nursing au ile kozi ya BSc in clinical nursing?
Ndio anawapa wajawazito dawa zilizoisha muda wake?
 
Binafsi nitakwambia kuwa huwa ninachoshwa sana nikienda benki, kuweka au kuchukua pesa ambayo ni pesa yangu mwenyewe, lakini ninakutana na mtu mwenye 'attitude', anayejifanya kana kwamba ananifanyia fadhila kunihudumia!

Nina hakika hiyo ni sehemu moja tu, zipo sehemu nyingi sana zisizotoa huduma ipasavyo.
Tz kila sekta, linapokuja huduma kwa wateja ni bure kabisa!
 
Mdogomdogo tutaelewa kuwa wale wahudumu hawakufanya kosa na watarudishwa kazini
 
Hata yule mmaabara yuko sahihi. Kilichotakiwa baada ya kutoelewana wangalifikisha suala hilo kwa mganga mfawidhi na kupata suluhu.
Dr Akili, usahihi unaohusisha madawa yaliyoisha muda kwa wajawazito uko wapi?
 
Nani kakufundisha kwamba wauguzi hawana ufahamu wo wote wa mambo ya maabara? Unajua wanajifunza nini katika hiyo kozi ya miaka 4 ya diploma in clinical nursing au ile kozi ya BSc in clinical nursing?
Wewe siku zote nilijua ni kiazi kweli. Kama una MD kama unavyodai hapa, nadhani uliipata kwa mizengwe sana.
Nesi na vipimo vya maabara wapi na wapi; na hata wewe hapo utaanza kujidai miaka mitano ilikupa uwezo wa kujua kazi ya maabara, si ujinga huo?

Kila mtu anayo kazi yake katika fani hizo, hakuna mwenye ujuaji zaidi ya mwenzie katika fani isiyomhusu.
 
Mabishano kati ya medical professionals yanayolenga kupata huduma sahihi na safi kwa wagonjwa wao ni kitu cha kawaida na cha kila siku. Mabishano au mijadala ya namna hiyo kuna wakati mwingine inakuwaga mikali sana (heated). Mijadala hii hufanyika aidha kati ya mtu mmoja mmoja au kivikundi. Mabishano kama hayo ni very medically ethical kwani yanalenga kutoa huduma bora kwa mteja/ mgonjwa. Cha muhimu tu ni kwamba mabishano kama hayo hayapaswi kufanyika mbele ya mteja/ mgonjwa.

Mabishano yaliyotokea kati ya muuguzi na mmaabara huko Tabora yalikuwa ya aina hiyo. Muuguzi alikuwa anataka mteja wake mwenye mimba afanyiwe kipimo cha malaria ya MRDT ambacho mmaabara alikuwa amekataa kwa sababu kipimo hicho hakitatoa majibu sahihi kwa kuwa diagnostic kits alizokuwanazo za kipimo hiko zilikuwa zime expire. Muuguzi hakukubaliana na sababu hizo na alitaka mmaabara afanye tu kipimo hicho hata kama expirely date ya kits hizo ilishavukwa. Mteja hakuwepo eneo la mabishano.

Tatizo liko kwa yule aliyeamua kuwarekodi wawili hao walipokuwa wanabishana na kuyarusha mabishano hayo kwenye mitandao ya kijamii kwa manufaa anayeyajua mwenyewe. Kama mtu huyu naye ni medical professional, basi atakuwa na kesi kubwa ya ki medical ethics ya kujibu.

Tatizo suala hili limechukuliwa kisiasa baada ya video hiyo kuonekana na wanasiasa. Wale innocent persons wametimuliwa kazi. Yule culpit aliye record na kusambaza hizo picha anapeta. Eti anaitwa whistle blower. Ana blower kitu gani ambacho hakiko sahihi ki medical?
Rubbish, wenzetu wanaweka CCTV camera kila mahala ili kuwaumbua watumishi wapuuzi, wazembe, wenye viburi na lugha chafu wewe unataka hayo mambo yafukiwe chini ya meza. Hivi mngekuwa kwenye maofisi ya wazi kama ma benki na kwingineko ambako hakuna siri mngeweza kweli? Halafu mkitoka hapo mnailaumu serikali kwa kufanya mikataba mbalimbali kuwa siri, mikopo kuwa siri etc really??
 
Kwenye sekta ya afya serikalini ndio sehem pekee iliyojaa wajuaji , academic arrogance na limited vision ya hali ya juu mno....

hela zenyewe kiduchu unamchomea mwenzako Mambo ya kuzungumza kwenye vikao....
Niondolee shobo, kwenda hukooo, unataka kuwa mfanyakazi bora?? Na meengii ya kudhalilisha... Kumbuka haya ni ya kwenye video clip je huko nyuma amewahi kumtakia au kumtukana mangapi? Huyu kama ni private hospital hata mwezi mmoja hamalizi, sijui hata hii kazi aliipataje, maana haimfai hata kidogo.
 
Niondolee shobo, kwenda hukooo, unataka kuwa mfanyakazi bora?? Na meengii ya kudhalilisha... Kumbuka haya ni ya kwenye video clip je huko nyuma amewahi kumtakia au kumtukana mangapi? Huyu kama ni private hospital hata mwezi mmoja hamalizi, sijui hata hii kazi aliipataje, maana haimfai hata kidogo.
Sasa hapo tusi ni lipi masta.. ukienda jeshini si naacha kabisa narud na nyumban.. hahaha
 
Ni uzembe wa wasimamizi wa huduma hizi yaani DHMTs (district health management teams) zinazoongozwa na waganga wakuu wa wilaya (DMOs) na RHMTs zinazoongozwa na waganga wakuu wa mikoa (RMOs). Timu hizi zinatakiwa kuzifanyiwa quality testing maabara hizo za mara kwa mara. Yaani hata wewe jaribu tu hata siku moja badala ya mkojo wapelekee maji yaliyochanganywa na fanta au wapelekee mkojo wa ng'ombe au mbuzi. Utashangaa majibu utakayopewa. Utaambiwa una UTI sugu au kisonono. Wapelekee damu ya kuku, utaambiwa una malaria tatu au typhoid au HIV.
Garbage in, garbage out.
 
Wewe siku zote nilijua ni kiazi kweli. Kama una MD kama unavyodai hapa, nadhani uliipata kwa mizengwe sana.
Nesi na vipimo vya maabara wapi na wapi; na hata wewe hapo utaanza kujidai miaka mitano ilikupa uwezo wa kujua kazi ya maabara, si ujinga huo?

Kila mtu anayo kazi yake katika fani hizo, hakuna mwenye ujuaji zaidi ya mwenzie katika fani isiyomhusu.
Ngoja nikufundishe kidogo layman wangu upate uelewa angalao kidogo wa haya masayansi na matekinolojia:

Vipimo vingi vya maabara sasa hivi viko simplified and automated. Vingi hata mgonjwa au wewe unaweza kujipima ukielekezwa kidogo tu. Nitakupa mifano:

- Blood sugar: Nunua GlucoPlus meter na glucose test strips kwenye duka la dawa. Gharama yake ni ndogo tu na utaweza kupima mwenyewe sukari yako ya mwili ili mradi tu uwe una uwezo wa kusoma na kuandika. Wagonjwa wa kisukari hu monitor blood sugar ya kila siku kwa bei isiyozidi Sh 200 kila kipimo. Hauhitaji mmaabara wala muuguzi kukupima sukari yako.

- Kipimo cha malaria cha MRDT (Malaria Rapid Diagnostic) Kit: Hichi hata wewe layman unaweza kujipima mwenyewe ukiwa nyumbani kwako. Unaweka tone moja dogo la damu na matone matatu ya assay fluid na baada ya dakika chache unapata majibu. Hauhitaji muuguzi wala mmaabara. Kipimo hiki ndicho walikuwa wakibishana kwenye hiyo video clip kati ya muuguzi na mmaabara. Wote wanaweza kukifanya na hata mgonjwa akioneshwa anaweza kukifanya.

- HIV blood test kit: Kipimo hiki unaweza na unashauriwa kukifanya mwenyewe nyumbani au guest ukiwa na mpenzi wako. Kinafanyika kama kile cha MRDT, unapata majibu yako na ya mpenzi wako baada ya dakika kumi. Kipimo kimoja hata Sh 200 hazifiki.

- HIV saliva test kit: Hiki kinatumia mate badala ya damu. Yaani kabla ya huo mchezo wa wawili kila mmoja anaweka mate kidogo kwenye kit, mnasubiri dakika 20 mnayaona majibu na kuamua mchezo utachezwa kwa namna gani. Kits hizi zinapatikana kwenye maduka ya dawa kwa bei ya chee. Tatizo wizara ya afya haijazikazania. Zilipaswa kumwagwa kwa wingi hadi machinga wazisambaze kwani ndiyo mwarobaini wa kudhibiti janga hili la UKIMWI. Kondomu wengi hawazitumii kwa sababu mbali mbali zikiwamo zenye mashiko na zisizo na mashiko.

- Kipimo cha mkojo: Hiki nacho ni rahisi sana na unaweza kujipima mwenyewe. Kinapatikana kwenye maduka ya dawa kwa bei chee. Kinatumia urinary strips. Unachukua mkojo wa katikati (mid urinary stream), unachovya hiyo strip kwenye mkojo huo. Itakupa majibu kama una UTI, kisukari, protein, albumin, bilirubin, red blood cells na kadhalika.
Cha muhimu sana ni kwamba tumia mkojo wa katikati. Ule wa mwanzo na wa mwisho huwa ni mchafu kwa kawaida. Hasa kwa wanawake, mkojo wa kwanza kwenye stream huweza kuchanganyika na uchafu wa ukeni ikiwamo seminal fluid, blood cells kwa walio kwenye hedhi na kadhalika. Tatizo la wanamaabara wengi huwa hawawaelekezi wagonjwa mkojo wa kuchukuliwa ie mid stream urine. Hiki ndicho chanzo cha wagonjwa wengi kuonekana wana tatizo la UTI wakati hawana bali walipima mkojo wa kwanza au mwisho ya stream.

- Pregnancy test strips: Kujua kama umeshanasa mimba ni rahisi tu. Unanunua pregnancy test strip moja kwa bei ya jero. Unachovya strip hiyo kwenye mkojo wako wa asubuhi. Yaani hata mimba ya wiki moja kipimo hiki itakiona. Huhitaji usubiri hadi ukose hedhi ya mwezi ujao au hadi uanze kutapika tapika ovyo. Yaani ndani ya siku 3 hadi 7 tu utajua kama mimba imeingia na hivyo utajua ni ya mwanaume yupi aliyesababisha hilo. Hauhangaiki kwenda maabara au kwa daktari.

- Kipimo cha pressure ya damu: Unahitaji kununua tu digital blood pressure machine. Unajifunga mwenyewe, unabonyeza kitufe na baada ya muda mfupi unapata unapata pressure yako na pulse rate yako.
- Huko kwenye maabara vipimo karibu vyote hufanywa na automated machines. Kazi ya mmaabara ni kutumbikiza tu hizo samples kwenye machines. Yaani ni kama kutumbukiza nguo kwenye mashine ya kufua nguo na kuwasha. Ujuzi wake aliosoma chuoni hautumiki kwani muuguzi au hata layman wa medicine yo yote anaweza kutumbukiza hizo samples na kuwasha mashine. Yaani kwa sasa laboratory technicians hawahitajiki sana kwenye vituo vya kutolea huduma za afya. Ujuzi wao unahitajika kwenye viwanda vya kutengeneza vitendanishi, kwenye taasisi za utafiti, vyuo vya kufudisha taaluma. Ni kama ilivyo kwa sasa kwa wafamasia. Ujuzi wao ni wa kutengeneza dawa na utafiti wa dawa. Hapo zamani kazi yao hospitalini ilikuwa ni kutengeneza au ku compound dawa mbali mbali. Sasa hivi dawa zote zinakuja hospit ziko fully compounded toka viwandani. Hivyo kazi ya pharmacist hospitalini imebaki ku dispense tu dawa kwa wagonjwa na kutunza store ya dawa, kazi ambayo haihitaji kisomo cha miaka 4 chuo kikuu au zaidi kwa wale walio na master degrees or PhD in pharmacy ambao kwa sasa tunao wengi tu wakidispense dawa mbili mara mbili wakiwa na PhD in pharmacy!

Kwa kifupi tunawa under utilize sana hawa watalaamu wetu wa maabara na wana famasia. Ndiyo maana huyo mmaabara wa kwenye hiyo video clip kwanza hakuwa amevaa laboratory coat yake na hakuwa kwenye chumba chake cha maabara. Alikuwa kamfuata huyo muuguzi mrembo kwenye kituo chake cha kazi kupiga soga. Muuguzi alikuwa bize na kazi yake huku hilo linjemba la maabara likimsumbua kwa soga zake zisizo na mashiko.
 
Back
Top Bottom