Mada maalum ya magari: Uzoefu, ushauri na maswali

Mada maalum ya magari: Uzoefu, ushauri na maswali

Mkuu Mshana Jr gari yangu ni Nisan Xtrail inawaka taa ya check engine. Na wakati naendesha wakati mwingine inakosa nguvu kabisa na engine rotation kuwa kubwa. Baada ya diagnosis wanasema solenaid valve ya gear box imekufa.

Hiki ni kitu gani na kinapatikana wapi kwa bei gani? Natanguliza shukrani
 
Jamani namtafuta fundi wa Fuel System ya SUBARU FORESTER,nikikanyaga accelerator hadi mwisho kwennye Mwendo inaanza miss,inajivuta vuta.Ni plugs?na inawaka CHECK ENGINE.Nipo DAR
 
Mkuu mshana jr nashukuru sana kwa thread yako hii, kuna vitu vimenisaidia. Mimi naomba tu kujua mafundi wazuri, kwa service ya gari hizi Raum new model na Toyota Voltz. Kwa Dar, fundi wa mwanzo niliyekuwa naye now hayupo.
 
Last edited by a moderator:
Kumekuwa na mada nyingi kuhusu mambo yote yahusuyo magari, nikaona basi na sisi tuwe na Uzi huu ambapo habari zote zihusuzo magari kuanzia kuchagua, kuagiza, kuuza, kubadili nyaraka, matengenezo utunzaji na kadhalika.

Watu wengi wametapeliwa kwenye mauzo na manunuzi, kwenye nyaraka, kwenye vipuri kwenye matengenezo na hata matumizi.

Kwa Uzi huu basi kila mwenye ujuzi, uzoefu, ushauri au mwenye maswali na tatizo lolote linalohusiana na magari hapa ndio pawe uwanja wake

Karibuni sana


View attachment 225786

Nisaidie kutofautisha Suzuki escudo 2.0 vs V6.Ni hayo tu
 
wakuu nielewesheni jinsi ya kutumia auto/manual transimission system kwenye Toyota Mark x, pia kwenye gear leaver kuna D na S + na - nini kazi zake, D ni drive ila S+ na S- sizielewi, nawasilisha.
 
Mkuu mshana jr nashukuru sana kwa thread yako hii, kuna vitu vimenisaidia. Mimi naomba tu kujua mafundi wazuri, kwa service ya gari hizi Raum new model na Toyota Voltz. Kwa Dar, fundi wa mwanzo niliyekuwa naye now hayupo.

Sehemu za uhakika za kufanyia service ni kwenye petrol station zinazotoa hiyo huduma, inaweza kuwa a bit expensive lakini ni afadhali kuliko
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Mshana Jr gari yangu ni Nisan Xtrail inawaka taa ya check engine. Na wakati naendesha wakati mwingine inakosa nguvu kabisa na engine rotation kuwa kubwa. Baada ya diagnosis wanasema solenaid valve ya gear box imekufa. Hiki ni kitu gani na kinapatikana wapi kwa bei gani? Natanguliza shukrani

Nashauri ukafanye tena diagnosis D.T. DOBIE ujiridhishe kisha spare agiza Nairobi utaokoa pesa nyingi na utapata genuine parts
 
wakuu nielewesheni jinsi ya kutumia auto/manual transimission system kwenye Toyota Mark x, pia kwenye gear leaver kuna D na S + na - nini kazi zake, D ni drive ila S+ na S- sizielewi, nawasilisha.

Kwenye Mark X engage manual transmission then button zagear zipo chini ya steering, lakini tumia tu auto ndio kisasa S+ na S- nafikiri ni D1 na D2, D1 ya mwinuko na tifutifu D2 utelezi
 
Jukwaa zuri sana hili. Ingefaa tukatajiwa maeneo au garage ambazo angalau ni wataalam kwa aina husika za magari. Hapa hii siyo promo ila ni msaada tu. Maana huko mitaani mafundi wanatupiga za uso sana.
 
Kwenye Mark X engage manual transmission then button zagear zipo chini ya steering, lakini tumia tu auto ndio kisasa S+ na S- nafikiri ni D1 na D2, D1 ya mwinuko na tifutifu D2 utelezi


ahsante mkuu.
 
Hapana mimi sio fundi, runx si ndio kizazi cha ist, Allex, duet nk? Ni gari ambazo hazitaki shida wala mikikimikiki, kwa ushauri nunua gari yeyote kizazi cha corolla100, 110 au hata GX 100 kavu! GX vvti itakutesa

Nimekuelewa mkuu, sawasawa!!
 
HAKI ZA DEREVA ANAPOKAMATWA NA TRAFFIC
- Trafiki hana idhini ya kukulazimisha kumkabidhi leseni yako
-Akikukuta na kosa na kukuandikia notification na ukalipa ni lazima akupe risiti ya serikali
-Hana haki ya kukuulizia kuhusu road licence hiyo ni kazi ya TRA kwakuwa siku utakapoenda kulipa utalipia na faini
-kama huna leseni una haki kisheria kuipeleka kituoni ndani ya Massa 72 ya kazi tangu ulipotakiwa kufanya hivyo
-Akikusimamisha una haki ya kusimama sehemu ile ambayo utaona ni salama na si lazima usimame anapotaka yeye
- Sio kila kosa ni la kuadhibiwa, mengine ya kuonywa au kuelimishwa

Mkuu mshana Jr kwanza nakupongeza kwa hii brilliant idea ya kuanzisha huu Uzi..! Sasa tafadhali tuelimishe kuhusu makosa yanayostahili faini na yale yanayostahili kuonywa au kuelimishwa, pia na vifungu vyake vya sheria.
 
Hapana mimi sio fundi, runx si ndio kizazi cha ist, Allex, duet nk? Ni gari ambazo hazitaki shida wala mikikimikiki, kwa ushauri nunua gari yeyote kizazi cha corolla100, 110 au hata GX 100 kavu! GX vvti itakutesa

Nimekuelewa mkuu, sawasawa!!
 
Hivi kwa nini House Girl kuachiwa mtoto sio ishu lakini huwezi kusikia House girl kaachiwa gari?

Binafsi sioni kama swali lako ni la kiufundi bali swali lako ni la kisaikolojia na kimajukumu...! Kimajukumu kwamba yeye house girl ameajiriwa kwa kumlea mtoto sio kuendesha gari...! Mbona huulizi kuwa kwanini madereva walioajiriwa majumbani wanaachiwa magari lakini hawaachiwi watoto? Think big mkuu
 
Sehemu za uhakika za kufanyia service ni kwenye petrol station zinazotoa hiyo huduma, inaweza kuwa a bit expensive lakini ni afadhali kuliko

Okay nitafanya hivyo kwa kweli, nashukuru sana Mshana ubarikiwe.
 
Mkuu mshana Jr kwanza nakupongeza kwa hii brilliant idea ya kuanzisha huu Uzi..! Sasa tafadhali tuelimishe kuhusu makosa yanayostahili faini na yale yanayostahili kuonywa au kuelimishwa, pia na vifungu vyake vya sheria.

Makosa yanayostahili faini ya moja kwa moja ni pamoja na kuendesha mwendo kupita spidi iliyowekwa, kuendesha gari bila leseni, gari kukosa break fire extinguisher, bima, indicators, triangles, ulevi nk nk! makosa yapaswayo kuonywa kutofunga mkanda,kuwa na shida na matatizo madogomadogo kwenye gari kama bulb kuungua vioo kupasuka nk nk
 
Jamani namtafuta fundi wa Fuel System ya SUBARU FORESTER,nikikanyaga accelerator hadi mwisho kwennye Mwendo inaanza miss,inajivuta vuta.Ni plugs?na inawaka CHECK ENGINE.Nipo DAR

Mkuu kasongo chukua namba hii 0717 369 183. yupo dar. karibu na Karume. ni fundi mzuri sana
 
Invisible na team yake wanegoma kutuwekea jukwaa letu sisi wapenda magari
labda aombe mwanamke, maana mwanamke akilegeza sauti..."jamani invidhiboo, tunaomba jukwaa la mapishii, na la mmu..ah, usisahau na chitchat jamani dia", hapo Invisible mwili wote unamlegea legelege, faster anamake sure.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom