Mnyama huyo usimwache tatizo lake ambalo laweza kuwa sio tatizo iko chini sana kwahiyo rough road inabidi kuwa mpole otherwise ni gari ya kijamaaa sehemu kubwa na ubepari kidogo yaani 75/25%
Njia rahisi kabisa ni kwenda naye hapo nilipokuelekeza kwakuwa siku hizi watu wanapigwa sana
Iko hivi ni nina gari anakuja mshkaji kuniazima let's say akimbie Tanga mara moja kumbe fix
Namkabidhi gari na vitu vyote muhimu ikiwemo copy certified ya gari, yeye anaenda kutengeneza kitambulisho bandia kwa jina langu anaenda polisi kuripoti wizi/upotevu wa kadi halisi ya gari,anapewa loss report
Akitoka hapa ni TRA, akifika anaonyesha police loss report anapewa kadi duplicate ya gari ikitoka siku ya pili anatengeneza mkabata wa mauziano ya gari, anajiuzia kwa jina lake halisi na kupata kadi duplicate yenye jina lake
Huku nikijua mshkaji yuko mkoa kumbe yupo TOWN anadalalia gari yangu, akifanikiwa kuiuza mimi nikaja kugundua nikifika TRA na kukuta hizo habari na kadi original wanaifungia gari kwenye system na kuanza kuitafuta
Ukikamatwa nayo wewe ndio mwizi
Na mara nyingi TRA hawahangaiki kutafuta gari wanakusubiri kwenye road licence ukishalipia unaenda dirishani kuchukua sticker yako....habari mbaya huanzia hapo
Habari za asubuhi wanaJF,
Naomba nielekezwe utaratibu wa kufuata baada ya kudilisha mashine ya gari.
Mathalani baada ya kufunga mashine ya Toyota katika Escudo nawajibika chochote labda TRA?polisi? au ni mwendo mdundo?
Duu umeponea tundu LA sindano kupigwa hizo case zipo nyingi sana pale TRA makao makuu ghorofa ya nne chumba cha kwanza kushoto ukitoka kwenye lift, pameandikwa Investigation, kwenye post za mwanzo angalia nimeizungumzia hiyo kitu kwa undani
Mshana jr mimi nataka kununua gx 100 cresta wiki tatu zijazo,hilo nalo vp?
Mnyama huyo usimwache tatizo lake ambalo laweza kuwa sio tatizo iko chini sana kwahiyo rough road inabidi kuwa mpole otherwise ni gari ya kijamaaa sehemu kubwa na ubepari kidogo yaani 75/25%
Inategemea gari na gari na ukubwa wa tank! Kwa mfano reserve ya Duet haiwezi kuwa reserve ya Mark X au Brevis! Magari yenye engine kubwa huwa na tank kubwa na automatically reserve pia huwa kubwa
Vyovyote viwavyo taa ikishawaka moja kwa moja bila kuzima una uwezo wa kwenda km 30 ndio izime kabisa, kwahiyo hapo unaweza kufanya mahesabu kulingana na ulaji wa mafuta wa gari lako
MADHARA YA KUTEMBELEA EMPTY TANK/MAFUTA KIDOGO
kwenye tank la gari kuna pump inayochuja na kusukukuma mafuta yaende kwenye mfumo wa engine, ile pump hulala kwenye sakafu ya tank na huinuka kadiri mafuta yanavyokuwa mengi (ina boya)
Mafuta ambayo hayajadhibitiwa vema huingia na chembechembe za michanga, ambazo hutuwama chini ya tank, hivyo ukitembea mafuta kidogo kila wakati pump badala ya kuvuta mafuta inavuta uchafu na hatimaye kuziba na kushindwa kupeleka kiwango cha kutosha kwenye mfumo wa engine
Haya madhara si kitu cha maramoja bali huja taratibu mno, kwahiyo kwa USHAURI
-Epuka mafuta ya videbe/drip
-Epuka kuendesha gari mara kwa mara likiwa halina mafuta ya kutosha
-Epuka kuweka mafuta kwenye vituo vya kienyeji
Jaribu hii technique! Taa ikiwaka tu nenda station jaza full tank (hata km ni town trips). Tumia mpk iwake tena weka full tank, hiyo mm inanisaidia sana kuepuka kuua pump
Nakubaliana sana na wewe broo... Ukitaka kununua gari kwa mtu hakikisha mnaenda TRA kwanza la sivyo kuna kulia. Mi niliwahi kununua gari mwaka 2012 nikapewa kadi na document zote muhim , tatizo likaja wakato road licence imeisha nataka kulipia tena nikakuta kumbe aliyekuwa na gari alienda sijui wap akachukua Road lisence fake na stika kabisa ikawa inaonyesha haijalipiwa muda mrefu. Kwanza ikabidi nilipe karibu laki tisa pamoja na faini. Pili TRA wakataka niwapeleke kwa aliyeniuzia gari ili wamkamate kwa kosa la kufoji. Nilivyoenda kwa aliyeniuzia akaniambia huo ni msala wako ukinisanua nakumaliza(machalii wa Arusha tena) nikawahonga TRA laki tatu wapotezee. Kwa kweli sishauri mtu atoe hela mfukoni kununua gari bila kupita TRA na pale TRA hawatakuchaji kitu.
Mghosi
Wandungu ahsanteni kwa maelezo mazuri yaliyonyooka. Basi mimi hapo nilikuwa najuaga labda kuna some general formula kuwa some % ya tank huwa reserved kwa magari yote. Ila nimefurahi kuwa whatever taa itakavyowaka una uwezo wa kuchanja mbuga for 30km ahead mpk gari kuzima. Mana mm kichwa huwaga kinapata moto pale taa ya mafuta inapoanza kuwaka,kublink. Ila cjawahi iacha ing'ang'anie kuwaka.
Nimesoma kitu hapa nadhani sijaelewa vizuri, ina maana mtu akibadilisha engine ya gari akaweka ya aina ya gari ile ile anatakiwa kutoa ripoti polisi na TRA?
Ndio kwakuwa makadirio ya road licence hutumia vigezo vya ukubwa/ uwezo wa engine, lakini pia hata unapobadili rangi ya gari inabidi TRA na JESHI LA POLISI wajulishwe, update ruhusa/kibali cha kubadili rangi na nafikiri na kadi mpya
Wakuu naomba kujulishwa hivi ile hydraulic ya kwenye gear box za automatic huwa inabadilishwa baada ya muda gani au baada ya kms ngapi?Mm nimetumia gari yangu sasa ni miezi 7 tokea nitoe bandarini nimekuwa nabadilisha engene oil peke yake.Nimeshatemebea kama 10,000kms kwa huo muda.Ila nikiicheki hiyo hydraulic ya gear box naona bado ipo poa tuu na gear zinabadilika bila shida yoyote.Gari yangu ni premio new model ya 2003.
MANI ebu msikilize huyu jamaa aseee, DAH.