Mada maalum ya magari: Uzoefu, ushauri na maswali

Mmmh!kuna fundi nilishamskia akisema gearbox oil huwa haibadilishwi coz ipo unique na ukibadili hupati iliyo bora kama hiyo.

Mungu wangu ile ni lubricant ndio inafanya gear zisogeze gari kuanzia Spidi 0 na kuendelea na kinyume chake, inafika mahali unapoteza uimara kwasababu ya msuguano wa vyuma
Alitakiwa kukuambia kuwa unapotaka kubadili hakikisha unapata iliyo bora
 
RANGE ROVER vogue!

Kwa macho yangu nimeshuhudia gari tajwa hapo juu zikiungua na kuteketea kabisa!

Dar Maeneo ya Cocacola, Dar Maeneo ya Ocean Rd, Mbele kidogo ya vigwaza baada ya kupita mizani mipya...

Pia kwa kuhadithiwa zipo nyingine zilizoteketea kwa moto jumla kama gari 6 au 7 hivi.

Awali nilifikiri ni mchezo wa insurance!...

Lakini baada ya kuliona hilo la Vigwaza (ilikuwa saa kumi alfajiri kati ya tar 5 na 6 Feb 2015) nimeanza kuwa na waswasi wa magari hayo...

Je kuna shida gani inayosababisha magari hayo kuwaka moto? au ni mchezo ule ule wa bima?
 

Yana hilo tatizo ni kweli lakini yale magari ni full umeme na full sensors na hutakiwi kupuuzia hata warning indicator moja lakini ambazo nyingi wamiliki/madereva hawajui kuzi tafsiri
Yale madude si sawa na kuendesha matoyota yetu haya unaingia unapiga starter unachapa mwendo, lile mpaka kufungua milango kuna masharti kuswitch on na kuondoka inachukua muda yani inabidi ulisubiri lisome mambo yake yote mpaka iwake taa ya READY ndio uondoke, halifai kwenye dharura za kufumaniwa (joke)nk labda kama uiache on
Hizi hazitaki mikono mingi ndio maana wamiliki huteua dereva mmoja anayepewa mafunzo maalum ya kuliendesha na kusoma alama zote na kuzitafsiri
 
Mungu wangu ile ni lubricant ndio inafanya gear zisogeze gari kuanzia Spidi 0 na kuendelea na kinyume chake, inafika mahali unapoteza uimara kwasababu ya msuguano wa vyuma
Alitakiwa kukuambia kuwa unapotaka kubadili hakikisha unapata iliyo bora

Well noted!
 

habari mkuu Mshana,naomba unijuze kwa faida ya wengi card orijino na duplicate utaitambuaje?
 
habari mkuu Mshana,naomba unijuze kwa faida ya wengi card orijino na duplicate utaitambuaje?

Duplicate ina maneno yaliyofifia kwenye kadi yake ya DUPLICATE, yanajukana kama water mark, original haina hiyo
 
Habari mshana jr,bado sijapata fundi wa kunibadrishia freelander kwenda rav4,wale vijana ulionielekeza wa toyota hawawezi mzee
 
Habari mshana jr,bado sijapata fundi wa kunibadrishia freelander kwenda rav4,wale vijana ulionielekeza wa toyota hawawezi mzee

Hebu cheki namimi jumatatu hata kwa pm tafadhali
 
Hivi ukiagiza gari na ukaitoa bandarini inabd uifanyie services i mean ubadilishe oil filter na oil yake. Au inabd utumie mpaka km3000
 
Hivi oil ya aina gani ni bora kwa gari? Nimetumia oil za nchini Australia yani zile za kawaida ni km10,000 ndipo unamwaga wakti za Tz ni km3000-5000.

Wapi ntapata 10,000 km engine oil #40 ? Brand name??
 
Hivi oil ya aina gani ni bora kwa gari? Nimetumia oil za nchini Australia yani zile za kawaida ni km10,000 ndipo unamwaga wakti za Tz ni km3000-5000.

Wapi ntapata 10,000 km engine oil #40 ? Brand name??

Castrol ni brandname inayoaminika thou zipo brands nyingi kv valvoline nk but ukitaka ni oil za uhakika ni Synthetic oils (artificially made)tofauti na hzi ordinary ambazo wengi tunatumia,check na vituo vya puma wana varieties za oil nzuri
 
Utavihitaji vitu hivi wakati utakapotakiwa kusafiri zaidi ya km 500,,,Hakikisha unavyo garini wakati unapoanza safari:-
1.Tochi
2.Kisu
3.Waya mita mbili.
4.Tools kit
5.Jeki
6. Jerry can 5lts
7.Kamba
8.Adhesive glue
9.Mwamvuli
10. Silaha eg kisu,bunduki,jambia,...UNAWEZA KUONGEZA VINGINE...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…