Mada maalum ya magari: Uzoefu, ushauri na maswali

Mada maalum ya magari: Uzoefu, ushauri na maswali

Tofauti hapo ni cabins na bei kama unanunua lori jipya. , ie, Kama unanunua used kwa ajili ya kazi zako , nunua cabin yoyote unayoona budget yako inaweza,

Top line ni kwa ajili ya safari ndefu kwa madereva Wawili , zina vitanda viwili, makabati Mengi kwa ajili ya kuhifadhia vitu , reserve kwa ajili ya kuweka freezer ,cofee maker na microwave.

Highliner hii ni ya pili kwa ukubwa inatumika katika mazinyira Kama ya top liner ila Ina nafasi kidogo.

Stream liner hii hasa sio cabin type , ila ni jinsi gani cabin inawezo wa kupenyesha Upepo ili kupunguza ukinzani , na hivyo kupunguza matumizi ya mafuta, kwa maana hiyo streamline inaweza kuwa Highline , top line au normal cabin.

Hii ni kiufundi zaidi nami nimeelimika hapa
 
Nina swali la ufahamu hapo mkuu mshana jnr na wengine wenye majibu. Kwa kuangalia tu kwa macho na hata kwa mbali waweza tofautisha kati ya carina ti na si? Na je zina tofauti gani kitaalam? Nauliza kwa sababu nilienda kutafuta taa ya carina ti kwenye duka la spea used na gari nilikuwa nalo, nilipomwuliza muuzaji nahitaji taa ya carina ti akaniuliza gari ndo ile?, akasema ile siyo ti ni si wamepiga chata tu.... Kweli sijajua hadi leo hii yangu ni ti au si. Kwenye kadi ya gari imeandikwa carina ti.

Nafikiri moja ya tofauti Kati ya Si na Ti iko kwenye engine, Si huwa na engine ya 5a -1490 cc na Ti huwa na engine ya 7a -1790cc
Ni kweli Kuna watu wanajua kuzitofautisha kwa kuziona tu .
 
Nafikiri moja ya tofauti Kati ya Si na Ti iko kwenye engine, Si huwa na engine ya 5a -1490 cc na Ti huwa na engine ya 7a -1790cc
Ni kweli Kuna watu wanajua kuzitofautisha kwa kuziona tu .

Naomba kurekebisha kidogo.Kinyume cha hicho ulicho andika ndio ukweli.Carina Ti ina Cc 1500 na Si ina Cc 1800.Na watu wengi wa taxi wanazipenda Ti kuliko Si kwa sababu ya engene ndogo iliyopo kwenye Ti.
 
Naomba kurekebisha kidogo.Kinyume cha hicho ulicho andika ndio ukweli.Carina Ti ina Cc 1500 na Si ina Cc 1800.Na watu wengi wa taxi wanazipenda Ti kuliko Si kwa sababu ya engene ndogo iliyopo kwenye Ti.

Yeah nimekosea, kweli huwa zinanichanganya Sana Ti na Si,lakini huwa nafahamu tofauti yake ni ukubwa wa engine,
 
Tofauti hapo ni cabins na bei kama unanunua lori jipya. , ie, Kama unanunua used kwa ajili ya kazi zako , nunua cabin yoyote unayoona budget yako inaweza,

Top line ni kwa ajili ya safari ndefu kwa madereva Wawili , zina vitanda viwili, makabati Mengi kwa ajili ya kuhifadhia vitu , reserve kwa ajili ya kuweka freezer ,cofee maker na microwave.

Highliner hii ni ya pili kwa ukubwa inatumika katika mazinyira Kama ya top liner ila Ina nafasi kidogo.

Stream liner hii hasa sio cabin type , ila ni jinsi gani cabin inawezo wa kupenyesha Upepo ili kupunguza ukinzani , na hivyo kupunguza matumizi ya mafuta, kwa maana hiyo streamline inaweza kuwa Highline , top line au normal cabin.

Thanxx so much na Je hizi gar za Kichina kama Howo sinotruk faw zinaweza leta competition kwa european Truck hasa hapa Tz mana naona europe wanakuja na tecnolojia za ajabu mfano euro 6 trucks ni hali ya Juu sana
 
Nilikuwa na nia ya kununua gari hilo ila kwa sasa umebadili mawazo yangu. Asante kwa reply yako kaka.
Usikuli kila story mkuu,utakuta tofauti yake ktk ulaji mafuta na hizo unazodhani hazili ni less than 2km kwa kila lita ktk maeneo yenye jam. Ebu linganisha na ubora wa gari ktk aspect nyingine afu uhitimishe. Kwangu mimi CRESTA bado nichaguo sahihi
 
Mkuu mshana ebu tupe ubora wa gari aina ya harrier maake bei zake zimeshuka kidogo sokoni na wengi tunampango wa kuhamia huko! Mfano mimi nina rav 4 new model lakini Kiukweli naizimia sana harrier.
 
Mkuu mshana ebu tupe ubora wa gari aina ya harrier maake bei zake zimeshuka kidogo sokoni na wengi tunampango wa kuhamia huko! Mfano mimi nina rav 4 new model lakini Kiukweli naizimia sana harrier.

Baki na rav4 yako harrier zina ugonjwa sugu wa gearbox na ni gari mayai sana ambayo ni handle with care
 
Baki na rav4 yako harrier zina ugonjwa sugu wa gearbox na ni gari mayai sana ambayo ni handle with care

Usemalo ni kweli mkuu, frnd wangu aliuza Harrier 5s cc 2.2 (2163) baada ya gari kutokuwa /kushindwa kubadilisha gear , mafundi walihangaika ikatengamaa kidogo lakini atlast jamaa aliuza
 
Nawashukuru sana mshana jnr na ansah miles , rav4 shida yake space ndogo sana! Mbona kuna wengine wanadunda nazo sana hizo hizo harrier?
 
Nawashukuru sana mshana jnr na ansah miles , rav4 shida yake space ndogo sana! Mbona kuna wengine wanadunda nazo sana hizo hizo harrier?

Handling with special care! Ni chache sana barabarani zenye namba A
 
Mshana mpaka huku upo ?ok naswali sample ya engine oil inavuja na niliweka oil ya total sasa imepungua nawezakuweka oil ya pb kama kuongezea?
 
Mshana mpaka huku upo ?ok naswali sample ya engine oil inavuja na niliweka oil ya total sasa imepungua nawezakuweka oil ya pb kama kuongezea?

Nipo pote dagii Kiutaalam haishauriwi mwaga yote hiyo ya total weka hiyo mpya kwa vipimo vyake! Lakini kwanini imepungua kiasi hicho? Je kuna leakage? Ni hatari kwa uhai wa gearbox pata fundi haraka kabla hujafanya mwenyewe
 
Last edited by a moderator:
Nawashukuru sana mshana jnr na ansah miles , rav4 shida yake space ndogo sana! Mbona kuna wengine wanadunda nazo sana hizo hizo harrier?

Inaonekana unaipenda Harrier, licha ya gear box hata system suspension haitaki sana rough road na kama ni kuhitaji nafasi(space) ya ndani ya gari nenda kwa kluger 2AZ engine cc 2.4 (2360) 4cylinder with VVTi, kwa maoni yangu ni gari nzuri, very smooth kupata speed unayotaka hasa kama una safari za mikoani na resonable fuel consumption.
Lakini hapana!!! hapana!!! kwa kluger yenye V6 ya cc 3.0 hii lazima uwe vzr mfukoni,
Yote hayo ni maoni tu
 
Idea nzima ya kunyanyua matairi ni kupunguza matumizi ya matairi hayo kipindi ambacho gari halijabeba mzigo, kumbuka malori yana matairi Mengi si kwa ajili ya urembo ,ni kutokana na mizigo mizito yanayobeba. ,ilikiwa tupu kunakuwa hakuna umuhimu wa kuyatembeza yote,

Mifumo ya kunyanyua matairi iko miwili , kutegemeana na aina ya suspension zilizotumika , kwa steel suspension mfumo unaotumika ni hydraulic , kwa air suspension mfumo unaotumika huwa ni wa electronic solenoid ambayo kimsingi huwa ni hewa . kwa bahati mbaya sina uwezo wa kuielezea humu jamvini, ila ni mifumo rahisi Sana Kama unaielezea kwa vitendo .
Kwa kuongezea tu , kuna aina mbili za kunyanyua matairi,mid lift na tag axle
mid lift , hii hunyangua tairi za mbele ya diff,
Tag axle ,hunyanyua tairi za nyuma ya diff,
Mid lift huwa inanyanyua tairi ikiwa empty tu, Tag axle huwa inanyanyua hata Kama Ina mzigo , idea ni kuongeza mkandamizo kwenye diff, Kama itatokea kuteleza .nk, na ndio sababu tag axle huwa zinatumika Sana kwenye rough roads.

Mkuu Asanteh kwa kunielewesha maana nilikuwa natamani kujua juu ya hili
 
Back
Top Bottom