Mada maalum ya magari: Uzoefu, ushauri na maswali

Mada maalum ya magari: Uzoefu, ushauri na maswali

Ila kama kuna mtu anaweza kunisaidia naomba anipe majibu samahani kama nimemlenga yeye tu
 
Msaada wenu gari timing belt ilikatika nikaivuta mpaka mjini sasa nimebadili hiyo timing belt gari imewaka ina misi ya hatari kabisa sasa hawa mafundi wananiambia itakuwa imeharibu vitu vingi sana kwenye engine maana ilipo nizimikia nilijaribu kuiwasha sasa fundi anasema ndio nilifanya makosa hapo sasa amenitajia vitu vingi Mimi sio fundi sivijui ghalama yake anasema inafika 500000 na gari ni cresta gx100 vvti
Nimesoma kuanzia mwanzo mpka hapa ulipoiandika hii. Nilichojifunza ni kuwa gari likifikia km laki moja ni vzr kubadili timing belt, si busara kusubiri mpaka ikatike, madhara yake ndio kama haya, gharama zinaongezeka ktk utengenezaji as kuna hatari mifumo mingine ikaharibika.
 
Sawa mkuu. Nitajuaje kama taa ya timing belt ni nzima? Mfano kama hiyo taa ilisha haribika ina maana haiwezekani kujua kama timing belt inahitaji kubadilishwa!!

Hasa kwa gari ambalo umenunua kwa mtu na hujui kilomita alizobadilishia timing belt

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa diploma ya hapa hapa jukwaani ni vzr unaponunua gari kwa mtu akakupa service history yake ili kukusaidia kumaintain gari hilo. Ni vzr ikawa kwenye maandishi.

Pia wenye magari, ni vzr kuandika service history ili tunapoamua kuyauza tusiwape tabu kama hii wateja tarajali
 
habari zenu wakuu??
ipi ni gari nzuri kununua kati ya TOYOTA AURIS na TOYOTA VOLTZ?? interms of gharama ya spare na upatikanaji wake,,ubora wa gari,,fuel consumption pamoja na bei
pia naomba msaada kwa anayefahamu bei ya hizo gari hadi kufika tz pamoja na kuingia barabarani
 
Aisee nimesoma kuanzia mwanzo na sasa nimemaliza!

Nitarudia tena once my car reaches me from Japan.

Very educative! Asanteni sana wooote!!! Sijaacha comment ya mtu!

Barikiwa Mshana Jr kwa kuanzisha uzi huu murua!!
 
Wadau nina Passo piston 3 nataka kubadili engine kuweka ya piston 4. Naomba kujua gharama ya tukio zima kuanazia manunuzi kwa wanaoju. Thanks
 
Wadau nina Passo piston 3 nataka kubadili engine kuweka ya piston 4. Naomba kujua gharama ya tukio zima kuanazia manunuzi kwa wanaoju. Thanks
Is it possible kuswitch hiyo engine bila kuathiri vitu kama engine mountings? Wajuzi wa mambo njooni huku...
 
Kwa wamiliki wa magari engine oil ni kitu muhimu sana kwa uhai wa gari lako. Bila engine oil au ukitumia engine oil isio sahihi kwa gari lako,unaweza kuliua haraka sana au likwa linakufa taratibu bila wewe kujua,ndio unaona mara kwa mara mara hiki kimekufa mara kile hatimae inakubidi ubadili engine nzima.

Kuna aina mbili za oil[well zinazotumika sana kwa magari]:
1.mono grade eg SAE 40
2.multi grade eg 5W40

Mono Grade:
Hizi huwa zinakuwa na viscocity moja,ikipoa au ikipata moto,zinatumika sana kwa magari ya kawaida hasa toyota,kama ukiona SAE40, SAE 60 ndio hizo

Multi Grade:
Hizi zina grade mbili kulingana na joto la engine eg 5W40, 5W30,10W60 etc. Hizi zinatumiwa sana na european cars. BMW,AUDI,MERCEDES BENZ,VW,RR.DISCOVERY 3/4 etc

mfano 5W30
5 inawakilisha viscocity engine ikiwa baridi kabla haijapata moto, W inawakilisha neno 'weight' wengine wanasema winter.
30 inawakilisha viscocity engine ikishafika optimum operating temperature,ukiangalia gauge yako pale mstari wa temp unapokaa kati ndio operating temperature.

Multi grade huwa zinatumika sana kwa european cars na wameweka hivyo kusudi kwasababu ya baridi,oil inakuwa nzito sana kwahio inabidi iwe nyembamba ili iweze kuzunguka kwenye engine na ubaridi wake mpaka ikipata moto ndio inakuwa nzito inavyotakiwa na kuzunguka kwa urahisi.

Kama unamiliki euro cars nakushauri tafuta specific number kwa ajili ya gari yako. Gari nyingi zinatumia 5W30 au 5W40. Usipotumia oil sahihi utaua vitu vingi taratibu kikubwa turbo kwa gari za diesel. Na asikudanganye mtu kuwa kuna oil ya VW/BENZ/AUDI etc muhimu ni namba ya engine oil specific kwa gari fulani,halafu ndio uchague kampuni nzuri ununue hio oil.

Natumaini kuna wataalam wa lubricants humu wanaweza kuingia deep zaidi na kutupa darasa zaidi.
 
nina Gari aina ya Toyota spacio old model,Jana nimebadili oil ya gearbox nashangaa imebadili tabia,ili kuwa inabadili gear kwenye spidi ya 13km/h,baada ya kubadili mpka ifike 16km/hr je ni sahihi?nilistuka Na kumuuliza fundi ananambia itarudia hali yake oili bado inazunguka je ikoje Hapana Naomba msaada wenu
 
nina Gari aina ya Toyota spacio old model,Jana nimebadili oil ya gearbox nashangaa imebadili tabia,ili kuwa inabadili gear kwenye spidi ya 13km/h,baada ya kubadili mpka ifike 16km/hr je ni sahihi?nilistuka Na kumuuliza fundi ananambia itarudia hali yake oili bado inazunguka je ikoje Hapana Naomba msaada wenu
Mafundi wetu sio mahiri kabisa
 
nina Gari aina ya Toyota spacio old model,Jana nimebadili oil ya gearbox nashangaa imebadili tabia,ili kuwa inabadili gear kwenye spidi ya 13km/h,baada ya kubadili mpka ifike 16km/hr je ni sahihi?nilistuka Na kumuuliza fundi ananambia itarudia hali yake oili bado inazunguka je ikoje Hapana Naomba msaada wenu
Ilitakiwa uongeze oil na sio kubadili, mie ilinitokea kwenye prado sx, ilikuwa kubadili gear mtihani inabd ukanyage kwel, lakin baada ya kufanya safar ndef ikarudi kawaida, baada ya kuanza kudadisi shida ilikuwa kutoa oil yote. Hivyo vizur kuongeza na sio kubadiisha yote.
 
Habari za week end wandugu? Naomba kupata uzoefu kwa mwenye Nissan murano, Nimezifatilia hizi gar nimependa ukubwa wake na nafasi ilonayo ndani. Ila nilisoma uzi mmoja wa nje kuwa zina shida sana katika gear box na umeme yani haziko reliable kama prado au x trail. Mwenye uzoefu nazo tafadhali anijuze natanguliza asante, pia nasema asante kwa bwana lege alinisaidia baada ya brevis kunizimikia ghafla
 
Habari za week end wandugu? Naomba kupata uzoefu kwa mwenye Nissan murano, Nimezifatilia hizi gar nimependa ukubwa wake na nafasi ilonayo ndani. Ila nilisoma uzi mmoja wa nje kuwa zina shida sana katika gear box na umeme yani haziko reliable kama prado au x trail. Mwenye uzoefu nazo tafadhali anijuze natanguliza asante, pia nasema asante kwa bwana lege alinisaidia baada ya brevis kunizimikia ghafla
Ziko vizuri sana kwa kila kitu ila zingatia masharti ya kuitunza... Hasa hiyo gearbox weka hydraulic stahiki usidanganywe na fundi ukaweka inayofanania utaumia
 
Back
Top Bottom