Mada maalum ya ndege toka FB

Mada maalum ya ndege toka FB

Hili ndiyo eneo aliloketi Mhandisi wa Ndege "Flight Engineer" nyuma ya marubani ndani ya ndege ya DC-10.
Huwezi amini, hivi vyote sasa vimechukuliwa nafasi na "Computer Automations" na kumuondoa mhandisi nje ya chumba cha marubani (Cockpit)
FB_IMG_1707598460200.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
"𝗕𝗜𝗥𝗗 𝗦𝗧𝗥𝗜𝗞𝗘"

𝗡𝗱𝗲𝗴𝗲 𝗸𝘂𝗴𝗼𝗻𝗴𝗮𝗻𝗮 𝗻𝗮 𝗡𝗱𝗲𝗴𝗲.

Katika usafiri wa anga neno "#birdstrike" lina maana ya ndege hai kugongana na ndege chombo.
Hali hii inaweza kutokea wakati wa ndege kupaa, kuwa angani au kutua.

Muda mwingine hali hiyo ikitokea inaweza kupelekea ndege (chombo) kupata ajali (ingawa ni mara chache), kuharibika sehemu husika kama pua, kupasua kioo na kujeruhi rubani, kuharibu injini, mbawa n.k

Kiwango wa uharibifu huo kinategemea kasi, ugumu na uzito wa ndege hai na ndege chombo, pembe inayokutana wakati wa kugongana n.k

Wanahisabati na fizikia wanakokotoa hali hilo kwa njia ifuatayo;
F=MA (Force = Mass × Acceleration)

Kwa kiswahili,
#Nguvu ni sawasawa na Ujazo wa kitu zidisha na Kasi yake.

Ndege nyingi zinaundwa na malighafi za #Aluminium au mchanganyiko wa plastiki na nyuzi za kaboni (carbon_composite) "epoxy" ili kuifanya kuwa nyepesi.

Wepesi wa ndege ni pesa katika usafiri wa anga, kwakuwa itabeba abiria wengi, mafuta zaidi, mizigo ya ziada na kwenda mbali pasipo kutumia nguvu kubwa ya injini.

Kwahiyo kitu chochote kikiwa na kasi na uzito huwa kinasababisha uharibifu pale kinapogongana na kitu kingine.

Mfano, endapo kama risasi ingekuwa inarushwa na mkono isingeleta madhara tunayoyaona leo, lakini inapofyatuliwa na bunduki, kasi huwa kubwa na madhara yake inapogongana na kitu hufanya uharibifu zaidi..

Ikiwa kasi ya ndege chombo ni kilomita 200-900 kwa saa, jumlisha na kasi ya ndege hai, basi madhara au uharibifu hutokea pale vinapokutana.
Kishindo/nguvu ya mgongano huo unaweza kufikia tani au zaidi kutegemea kasi na uzito.

Ndege nyingi zinaundwa kwa viwango maalumu vya kukabiliana na hali hiyo lakini si mara zote zinaweza kuhimili kishindo hasa pale kasi inapokuwa kubwa pamoja na uzito/ugumu wa ndege kiumbe.

Mfano,
Wanasema, mbegu ya ubuyu inaweza kupasua kichwa endapo itarushwa kwa kasi inayozidi 900km/h.
Kwa waendesha pikipiki, wanafahamu maumivu ya punje ya mchanga inapogonga usoni barabarani kwa kasi ndogo tu isiyozidi hata 100 kilomita Kwa saa.

#Admin
FB_IMG_1708335145550.jpg
 
𝗠𝗲𝗹𝗶 𝘆𝗮 𝗸𝗶𝗷𝗲𝘀𝗵𝗶 𝗛.𝗠.𝗦 𝗦𝘂𝘀𝘀𝗲𝘅 𝗶𝗸𝗶𝘄𝗮 𝗻𝗮 𝗮𝗹𝗮𝗺𝗮 𝘆𝗮 𝗻𝗱𝗲𝗴𝗲 𝘂𝗯𝗮𝘃𝘂𝗻𝗶 𝗺𝘄𝗮𝗸𝗲 𝗯𝗮𝗮𝗱𝗮 𝘆𝗮 𝗷𝗮𝗿𝗶𝗯𝗶𝗼 𝗹𝗮 𝗸𝘂𝗷𝗶𝘁𝗼𝗮 𝗺𝘂𝗵𝗮𝗻𝗴𝗮 𝗺𝗮𝗮𝗿𝘂𝗳𝘂 𝗸𝗮𝗺𝗮 "𝗞𝗮𝗺𝗶𝗸𝗮𝘇𝗲" 𝗹𝗶𝗹𝗶𝗹𝗼𝗳𝗮𝗻𝘆𝘄𝗮 𝗻𝗮 𝗺𝗮𝗿𝘂𝗯𝗮𝗻𝗶 𝗸𝘂𝘁𝗼𝗸𝗮 𝗝𝗮𝗽𝗮𝗻, 𝘄𝗮𝗸𝗶𝘁𝘂𝗺𝗶𝗮 𝗻𝗱𝗲𝗴𝗲 𝘇𝗮 𝗠𝗶𝘁𝘀𝘂𝗯𝗶𝘀𝗵𝗶 𝗞𝗶-51 '𝗦𝗼𝗻𝗶𝗮' 𝗺𝗻𝗮𝗺𝗼 1945.

[emoji991]
𝗠𝘁𝗮𝗻𝗱𝗮𝗼𝗻𝗶.
FB_IMG_1708450758730.jpg
 
Nani anafahamu sifa japo mbili za ndege hii, DHC-6 Twin Otter..?

[emoji991]
RRegional Air TanzaniaTanzania
FB_IMG_1708577769433.jpg
 
"Nguo huwa zinastiri"
Mig-15 Trainer ikiwa imefunuliwa mfuniko wa mkia.
FB_IMG_1708630025226.jpg
 
𝗔𝗶𝗿 𝗧𝗮𝗻𝘇𝗮𝗻𝗶æ, 𝗕𝗼𝗲𝗶𝗻𝗴 𝗕787-8 #𝗗𝗿𝗲𝗮𝗺𝗹𝗶𝗻𝗲𝗿 𝗶𝗸𝗶𝘄𝗮 𝗶𝗻𝗮𝗽𝗼𝘇𝗮 𝗷𝗼𝘁𝗼 [emoji3587] 𝗹𝗮 𝗗𝗮𝗿 𝗵𝘂𝗸𝗼 𝗚𝗮𝗿𝗱𝗲𝗿𝗺𝗼𝗲𝗻 (15/02/24).

𝗣𝗶𝗰𝗵𝗮/𝗖𝗿𝗲𝗱𝗶𝘁:
𝗚𝗹𝗲𝗻𝗻 𝘀𝗰𝗵𝗼𝗻𝗻𝗶𝗻𝗴 𝗸𝗿𝗶𝘀𝘁𝗼𝗳𝗳𝗲𝗿𝘀𝗲𝗻
FB_IMG_1708644085547.jpg
 
Kwanini ndege inaporuka kwa mara ya kwanza kwenye majaribio mara nyingi tairi husalia nje?
Na mara nyingine 'Flaps' pia hazipandishwi juu..(retracting)

Wataalamu, tunaomba darasa.
FB_IMG_1708710345368.jpg
 
Back
Top Bottom