Mada maalum ya ndege toka FB

Mada maalum ya ndege toka FB

JINSI HELIKOPTA INAVYOPAA

(Ufafanuzi mwepesi)

#Helicopter ni ndege inayotumia mbawa zinayozunguka juu (panga) kutengeneza '#lift' ili iweze kunyanyuka kupaa.
Kumbuka ndege ya kawaida inategemea kusukumwa na injini kwenda mbele ili mbawa zake zipitiwe na hewa ya kutosha kuweza kutengeneza mkandamizo wa hewa chini ya mbawa utakaosababisha kunyanyuka 'lift' na kupaa.

Kwa Helikopta hali ni tofauti kidogo, kwani panga ndiyo zinakimbia/kuzunguka (rotation) ili kuzalisha 'lift' kwa kusukuma hewa chini.

Lakini pia ina panga ndogo nyuma {mkiani} ili kuzuia bodi {#fuselage} kuzunguka pamoja na panga kubwa inapozunguka (torque effect)

'Helicopter' kiasili ni ndege isiyotaka kupaa kwasababu vidhibiti vyake (contros) lazima vifanye kazi kwa kupingana ili iweze kwenda sawa.
Hiyo ndiyo sababu 'Helicopter' inahitaji hesabu kubwa zaidi kupaisha.

Hii ndiyo sababu hata baadhi ya Helikopta zinazotoka na mfumo wa kujiendesha yenyewe {autopilot} ni gharama kiasi.
Rubani wa Helikopta muda wote hufanya kazi ya kuipa milinganyo tofauti {balance} kati ya panga kubwa na ndogo itakayomwezesha kupaa alivyokusudia.

UPAAJI
{Endapo kila kitu shwari}
Rubani huwasha mzunguko wa injini #rpm hadi ifike kiwango kinachohitajika kwa kutumia '#throttle' {inafanana na mkono wa #acceleretor ya pikipiki}

Baada ya hapo huvuta juu taratibu '#collective' {inafanana na #handbrake ya mkono ya gari za zamani}
Kazi ya 'collective' ni kubadili 'angle' ya mapanga ya juu {rotor blades angle} ili iwe na umbile linaloweza kukandamiza hewa chini na kupaa {mfano wa panga za feni zilivyokunjwa ili kuweza kusukuma upepo}.

Wakati wa kunyanyuka ina tabia ya kiwiliwili kutaka kuzunga na panga kubwa {#torque effect} hivyo rubani huzuia hali hiyo kwa kukanyaga pedeli ya kulia au kushoto kuiweka sawa, kutegemea bodi inazunguka upande gani.
Pedeli hizi zina'control panga ndogo mkiani kama ilivyo kwenye ndege ya kawaida pedeli zinavyo'control' kielekezi (#rudder) mkiani ili kukata kona.

Ikifika kimo anachohitaji kwenda juu hutumia "#cyclic" ambayo ni 'control stick' iliyopo katikati ya miguu ya rubani na kazi yake kuinamisha panga kubwa iwe kulia, kushoto, mbele au nyuma ili helikopta ielekee upande ambao panga litainamia.

Kama ni kwenda mbele atasukuma mbele taratibu "cyclic" ambayo itasababisha mzunguko wa panga la juu {#main_rotor_disk} kuinama kidogo mbele na kusababisha helikopta kufuata kuelekea huo.
Hii ni kwasababu panga kubwa litaanza kukandamiza hewa kwenda chini na nyuma na kusababisha helikopta kunyanyuka juu na kwenda mbele (lift & Thrust)

Rubani pia anaweza kuongeza nguvu ya injini kidogo kwenye 'throttle' yake au kuvuta "collective" ili kuongeza kasi ya panga kuzalisha nguvu hizo mbili kutegemea na haraka au uzito wa Helkopta wakati huo akikanyaga kiumakini pedeli kusahihisha uelekeo.

Zipo 'Helikopta ambazo hazina panga ndogo nyuma, ila panga mbili kubwa zilizo katika nguzo moja (rotor must) ambazo zinazunguka kinyume ili kuondoa tatizo la kiwiliwili kuzunguka na panga wanaita 'Coaxial rotor' au 'Counter rotating Blades' mfano Kamov #Ka52.
Pia kuna Helkopta nyengine yenye panga zote kubwa mbele na nyuma zinazozunguka kinyume mfano #Chinook CH-47 ili kuondoa hali ya 'torque'effect.

Helkopta ni mashine ya kufanya kazi nyingi ambazo ndege ya kawaida haiwezi kufanya.
Na hii kutokana na uwezo wa wa kuganda sehemu moja hewani (hovering), kugeuka papo kwa papo, kwenda ubavu au kurudi kinyume na kutua sehemu ambazo ndege ya kawaida haiwezi.

Kutokana na ugumu wa kupaisha Helikopta wanaanga wanatumia usemi ufuatao;
"kupaisha ndege ya kawaida ni kama kuendesha baiskeli ya tairi mbili, lakini kupaisha Helkopta ni kama kuendesha baiskeli ya tairi moja.

#Like & #share!
#AdminsView attachment 2622812
Kumbe kuendesha helikopta ni mziki mnene?
 
KWANINI NDEGE HUMWAGA MAFUTA ANGANI?

Ndege kumwaga mafuta angani kitaalamu #FuelDump au #Jetsoning ni utaratibu wa dharura unaofanywa na rubani kupunguza mafuta nje ya tanki za ndege angani kupitia tundu maalumu '#Nozzel' zilizo karibu na ncha nyuma ya mabawa.

Ndege nyingi kubwa zimeundwa na uwezo wa kupaa na uzito mkubwa kuliko kutua kwasababu misukosuko ya mkandamizo wa umbo 'Airframe Stress' wakati wa kutua ni mkubwa kuliko wakati wa kupaa kwahiyo, ndege kutua na uzito mkubwa wa mafuta inapitiliza mipaka ya usalama wake (structural limits)

Ndege ipatapo dharura hasa muda mfupi baada ya kupaa, huwa na ujazo mwingi wa mafuta, kujaribu kutua na uzito huo huweza kupelekea hatari ya ndege kupinda, kuvunjika maungio, kutosimama mapema, kupitiliza nje ya barabara, kupasua tairi, breki kushika moto na pia mafuta mengi ni tishio endapo itapasua tanki na kukutana na moto.

Ndege kubwa hujazwa mafuta kama ifuatavyo:
Mafuta ya safari husika,
Mafuta ya kuzunguka angani kusubiri kama kuna dharura kiwanjani
Mafuta ya kwenda kutua uwanja wa ndege mwengine endapo kuna dharura katika uwanja uliopangwa kutua awali n.k

Uzito wa mafuta hupungua kwa kuunguzwa na injini katika safari yake, kwahiyo endapo ndege husika inapata dharura inayohitaji kutua kabla mafuta hayajapungua uzito rubani hufuata taratibu za kupunguza mafuta angani katika eneo salama atakaloona au kuelekezwa na waongoza ndege ili kuweza kutua na uzito salama.

Humwagaji mafuta mara nyingi hufanyika katika kimo fulani ambacho mafuta huweza kutawanywa na upepo angani hasa nje ya makazi ya watu.
Baadhi ya ndege za kivita pia humwaga mafuta angani na mara nyingi hufanya kitu kiitwacho 'Dump & Burning' kumwaga na kuunguza ambapo mafuta huunguzwa baada ya kutoka nyuma ya injini.
Hii ni tofauti na kitu kinachoitwa 'Afterburner'

Katika maenesho ya anga awali marubani wa kijeshi walikuwa wakionesha kitendo hiki kabla ya kukatazwa na baadhi ya nchi.

Kwa ndege za abiria au mizigo, tafadhali usifananishe umwagaji mafuta "#fuel_dump" na kitendo cha injini kuacha wingu la moshi mweupe nyuma "#Contrails" ikiwa kimo cha juu.

'Contrails au condensation trail' ni mvuke-joto hutokao nyuma ya injini na kuganda kuwa michirizi ya wingu jeupe kutokana na ubaridi ulio kimo cha juu.
Wengi huita roketi kimakosa.

Kama hujawahi kuona ndege ya kijeshi au kiraia ikimwaga mafuta bofya link ifuatayo:



'Salute' sana kwa wanao'subscribe Youtube Channel yetu.

Tukipata like 2K na Share za kutosha, tunaendelea na Somo lijalo litahusu kwanini ndege kubwa za abiria au mizigo zinapendelea kupita juu sana.

Admin
Hisani:
#CaptainJoe
#Boldmethod
FB_IMG_1684406435518.jpg
 
KWANINI NDEGE NYINGI KUBWA ZINARUKA USAWA WA JUU SANA?

PIA KWANINI NYUMA HUACHA MOSHI?

Sababu ya ndege kubwa za abiria au mizigo kuruka juu sana ni ufanisi wa mafuta na kupunguza ukinzani wa hewa.

Katika kimo cha mbali hewa ni nyembamba hivyo upinzani mdogo wa hewa, ikiruhusu ndege kuruka haraka kwa kutumia mafuta kidogo maana yake nguvu zaidi kwa juhudi ndogo.

Kuruka juu ya futi 30,000 pia kuna faida kwa ndege kupaa juu ya hali za hewa nyingi mbaya mbaya na kuifanya iwe salama zaidi.
Wakati ardhini mkipigwa na mvua ya jero, wengine wanaruka juu ya wingu la mvua na kupata jua.

Pia kunasaidia rubani na ndege yake kupata muda wa kutosha kutatua tatizo litalojitokeza au kutafuta sehemu salama ya kutua kabla ndege haijapungukiwa kimo (gliding distance)

Hasara ni pale injini ikizima rubani hulazimika kushusha ndege kimo cha chini kwenye hewa nyingi ya oksijeni kisha kuwasha tena ikukubali anarudi juu.

SABABU ZA KUACHA MOSHI MWEUPE NYUMA

Michirizi ya moshi mweupe au mistari ya wingu nyuma ya ndege angani maarufu "#Contrails au #condensation_trails" inatokana na mvuke joto kutoka kwenye injini ya ndege kukutana na hali ya ubaridi wa angani na kusababisha mvuke huo kuganda mfano wa chenga za barafu.

Hali hiyo inafanana kidogo na mawingu yanavyojitengeneza, mvuke ukipanda juu huganda na kuunda wingu.
Pia mfano mwingine mzuri ni kiumbe hai anapokuwa mkoa wenye baridi utakugundua anapoachama kinywa, hewa yenye joto kutoka mdomoni hugeuka kuwa mfano wa moshi.

Njia rahisi ya kufahamu idadi ya injini za ndege ikiwa katika kimo cha mbali ni kuhesabu idadi ya michirizi. Endapo ikiwa mistari miwili nyuma basi ndege ya injini Mbili,, ikiwa injini 03 mistari mitatu, na injini 04 mistari itakuwa minne.

Kumbuka, michirizi hii haifanani na kile kitendo cha umwagaji mafuta wa ndege kama tulivyoelezea kwenye chapisho lililopita.

#Admin,
#aircrafttechnik
FB_IMG_1684485113180.jpg
 
#UPDATES Waliofariki dunia katika ajali ya ndege iliyotokea katika kiwanja kidogo cha Matambwe Selous hii leo ni mtumishi mstaafu wa maliasili na utalii, Rubani Bernard Shayo, kutoka kampuni ya Frankfurt Zoological Society (FZS), Aman Mgogolo na Theonas Nota

Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili imeeleza Rubani Shayo pamoja na Mgogolo walifariki papo hapo, huku Askari Mhifadhi Nota, akifariki wakati ndege iliyokuwa ikimkimbiza hospitali kutua katika uwanja wa ndege wa Dar es Salaam.

#AjaliYaNdege
#EastAfricaTV
FB_IMG_1684485327336.jpg
 
JE, KWANINI TANKI ZA MAFUTA YA NDEGE ZIPO KWENYE MABAWA?

Ndege huwa zinabeba mafuta mengi sana na wakati mwingine uzito wa mafuta ni karibu theluthi ya uzito wote wa ndege.
Lakini umewahi kufikiria ni wapi uhifadhiwa?

Ukiacha ndege nyingi za kijeshi hasa za kivita ambazo tanki za mafuta mara nyingi huwa ndani ya kiwiliwili cha ndege (Fuselage),
Ndege nyingi za kawaida ndogo na kubwa mafuta uhifadhiwa ndani ya mabawa.

Kwanini? Hapa kuna sababu kadhaa muhimu:

UZANI WA UZITO (weight balance)

Katika ndege ni muhimu kuzingatia sio tu upangaji wa viti na eneo la mizigo, lakini kikubwa mahali mzigo mzito wa mafuta yatapokaa.

Ili kuwa na uzani ulio karibu sawa kwa ndege nzima, ni muhimu tanki za mafuta kusimikwa katikati ya uzito wa ndege (Centre of gravity) kwa maana ya mabawa hata tumbo la kati (Centre Tank) ili kuepuka uzani kuzidi nyuma au mbele.

Lakini pia kwa ndege nyingine ni rahisi rubani kuhamisha mafuta angani kutoka bawa moja kuelekea nyingine pale anapohitaji uwiano sawa wa ndege (balance) inapotokea kwa namna yeyote uzito kuelemea upande mmoja.

KUONDOA MISUKOSUKO YA MNESO

Mafuta kukaa kwenye mabawa husaidia kufanya kama mkazo kukabiliana na misukosuko ya mneso wa mabawa hasa wakati wa kupaa (counter stress)
Kumbuka mabawa huzalisha mnyanyuko (lift) na kubeba uzito wa ndege nzima mara tu inapoacha ardhi.
Katika ndege kubwa iliyopakia mzigo mzito, kuacha mbawa zikiwa tupu/nyepesi wakati wa kupaa inaweza kusababisha mabawa kupinda juu nje ya mipaka ya uhimili wake au kusababisha kukatika.

KUPUNGUZA MITETEMO

Uzito wa mafuta husababisha ugumu kwenye mabawa na hivyo kupunguza kupepea (fluttering).
Mtetemo wa mabawa au 'vibration' husababishwa na mtiririko wa hewa.

Mtetemo mkubwa ni hatari sana hata inaweza kusababisha kuweka nyufa au kukwanyuka kabisa kwa bawa.
Kwa hivyo, kuhifadhi mafuta katika mabawa ni uamuzi wa busara sana ambao hufanya ndege kuruka salama.

Kwa ujumla, kuna sababu nyingi zaidi za kutaja..
Je, unaweza kuorodhesha angalau moja zaidi..

Kwa wafuatiliaji wanaopenda kujifunza zaidi, bofya link chini kutazama video ya jetblue jinsi ya kuweka mafuta kwenye ndege na dakika ya pili utakutana na mhandisi akikwea ndani ya tanki tupu za mafuta.



Shukrani 'Subscribers' wetu.

Credit:
#BAflighttraining
#KLMsyllabus
FB_IMG_1684657150406.jpg
FB_IMG_1684657145608.jpg
 
"ALBATROSS" XWB/DREAMLINER YA ASILI

Maendeleo ya teknolojia yanatuwezesha kujifunza kwamba ndegehai wanaweza kusafiri umbali mkubwa chini ya uwezo wao wenyewe.

Vifaa vyepesi sana vya kufuatilia GPS - chini ya gramu 1.5 - vinaweza kutumika kufuatilia ndege bila kutatiza safari zao.
Wanabiolojia walioweka vifuatiliaji vya GPS kwenye albatrosi wanaotangatanga wamegundua kwamba ndege hao wakubwa wanaweza kusafiri angalau kilomita 15,000 (chini ya maili 10,000) juu ya bahari kabla ya kurudi nchi kavu.
Hiyo ni kama kuruka bila kusimama kutoka Houston, Texas hadi Perth, Australia.
Ni ndege chache sana za abiria zinaweza kufanya hivyo!

Chanzo:
FB_IMG_1684675163629.jpg
 
"Mkuu wa Starlux Airlines anaweza kupigwa faini kubwa baada ya kumruhusu Mtumia YouTube kwenye chumba cha marubani cha ndege yake kufuatia safari ya kwanza ya njia mpya'

"Wanachama wa vyombo vya habari na washawishi pia walikuwa ndani ya ndege hiyo na Mwaustralia #SamChui, ambaye ana zaidi ya watu milioni tatu waliojisajili kwenye chaneli yake ya "usafiri wa anga ya " YouTube"

"Kesi hiyo inachunguzwa na Utawala wa Usafiri wa Anga nchini, huku mkurugenzi mkuu wa shirika hilo, Lin Kuo-shian, akiripotiwa kumwita mkurugenzi wa shughuli za ndege wa Starlux kwa maelezo"

Chanzo:
@aviationbreakingnews/tweeter
FB_IMG_1684678921944.jpg
 
Je, Umegundua kitu gani katika mbawa ya Mbuyu huyu ambacho kwenye baadhi ya ndege pia unaweza kukuta?

[emoji991] Cdt:
Respective Owner.
FB_IMG_1684682013738.jpg
 
Muundo wa awali wa P-51 Mustang wenye alama za RAF za Uingereza na gurudumu la mbao lililoambatishwa ili iweze kusogezwa juu na chini kwa urahisi ngazi kwenye North American Aviation, Inglewood California, 1942. Ukiangalia kwa makini, kwenye gurudumu la mbao mtu ameandika 'Fanya. si inflate'. https://planehistoria.com/p-51-mustang/
FB_IMG_1684819007259.jpg
 
"Saa chache zilizopita"
Safari za mwisho za ukaguzi (functional check) ya ndege ya mizigo "Air Tanzania Cargo" aina ya #Boeing767 5H-TCO kutoka uwanja wa ndege wa kiwanda cha Boeing #PaineField.

Mkakati wa kusafirishwa hadi Uwanja wa Ndege wa GMTT (Tang Ibn Battouta-Morocco) imeratibiwa kufanywa Mei 31.
Kumbuka Ndege iliyoundwa maalumu kwa kupakia Mizigo huwa hazina madirisha tofauti na yale ya mbele kwa rubani.

Chanzo:


[emoji991]
Paine Field
FB_IMG_1684913056928.jpg
 
KWA UCHACHE KUHUSU BOEING 767

Boeing 767 ni ndege ya Kimarekani yenye umbo pana inayotengenezwa kiwanda cha Boeing Commercial Airplanes.
Ndege hii ilizinduliwa kama mpango wa Boeing 7X7 mnamo Julai 14, 1978, na ndege ya kwanza ya majaribio iliruka kwa mara ya kwanza mnamo Septemba 26, 1981, na ilithibitishwa mnamo Julai 30, 1982.

Boeing 767-200 ya kwanza, ilianza kutoa huduma mnamo Septemba 8, 1982 na United Airlines na 767-200ER ya masafa marefu mwaka wa 1984. Ikafuata Boeing767-300 mnamo Oktoba 1986, ikifuatiwa na 767-300ER mwaka wa 1988 ambayo ndiyo toleo maarufu zaidi.
Toleo la kubeba mizigo Boeing 767-300F (Freighter) lilianza Oktoba 1995 na baadae ikazalishwa Boeing 767-400ER Septemba 2000.

Kimo cha kupaa: hadi futi 43,000
Umbali wa safari: kilomita 7200 hadi 11,000.
Mwendokasi: 851 km/h
Abiria: 210 hadi 269 kulingana na aina ya toleo.

Kwa toleo la kubeba shehena (mizigo) Boeing 767-300ER (Extended Range) hubeba hadi tani 52.4 za Bei inayotajwa mtandaoni kwa ndege moja ya B767-300F ni dola milioni $220.

Watumiaji wakubwa ndege hii kwa takwimu iliyochapwa na jarada la Simple flying ya mwaka 2021 kwa idadi ya ndege,
Delta AirLines - 72
FedEx Express- 96
UPS - 75
United Airlines-54
Hadi kufikia Aprili 2023 jumla ya ndege 1,273 zilitengenezwa.

Vyanzo:
Simpleflying
Wikipedia
Learntofly

[emoji991]
Jennifer Schuld/Tweeter
FB_IMG_1684940145022.jpg
 
Msamiati wa neno "Aviation" limetokana na neno la Kilatini "avis" linalomaanisha "ndege" hai.
Kwa tafsiri ya leo "Aviation" ni usafiri wa anga.

Vocabulary.com
FB_IMG_1684946314084.jpg
 
Comac #C919 / China Eastern Airlines, mteja wa kwanza wa C919, atazindua safari ya kwanza ya kibiashara ya ndege hiyo siku ya Jumapili.
Ndege ya MU9191 itapaa saa 10:45 asubuhi kwa saa za Beijing (0245 GMT) kutoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Shanghai Hongqiao na kuwasili katika Uwanja wa Ndege Mkuu wa Beijing saa 1:10 asubuhi.

Ndege itaruka mara ya pili Jumapili alasiri kurudi kutoka Beijing hadi Shanghai.
Kampuni hiyo kutoka nchini China ya #Comac imedhamiria kushindana kwenye soko la mapapa wawili, #Boeing na #Airbus katika ndege zao za matoleo ya #Boeing737MAX na #Airbus320Neo.

Chanzo:
@Aeronews
FB_IMG_1685119092470.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom