MADA: Tatizo la Watoto kuchelewa kuongea. Ni kipi chanzo chake? Je, nawezaje kutatua tatizo hili?

Mtoto wangu yeye ana miezi 17,akitAKa kitu anakushika mkono anakuvuta mpaka kilipo kitu anachokihitAji kama anataka maji atakupelekA kwenye ndoo yA maji, na akitaka kunyonya anakuvutA mpaka kwenye kiti ili ukae anyonye .

Mpeleke kwenye hospital yoyote yenye audiologist mzuri amkague kwanza. Majibu atakayokupa unaweza kushare na mimi kupitia 0765886191. Lakini pia, unaweza kunitumia video clip ambayo mtoto anaongea, anaongeleshwa na kuagizwa kitu au kupewa maelekezo fulani. Ni ngumu kwa mimi kukwambia chochote bila kulijua tatizo la mtoto wako.
 
Kwangu Mimi hi ni mada ya maana kuliko zile zilizozoeleka humu ....
 
Unaanzaje kupata usingizi mzuri au kufanya kazi vizuri endapo ukaona damu yako ina shida?

Unaweza ukawa na furaha ila kuna muda ukikaa unaona kuna uchungu unaingia ndani kuhusu mtoto.

Hongera kwa bandiko lenye elimu pana, huyo jamaa mpuuzie tu na kisha umsamehe.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
TV inarudisha sana maendeleo ya ukuaji wa ubongo wa watoto. Nimefanya diagnosis kwa watoto wengi wenye tatizo hili, chanzo kwa wengi nimebaini ni TV. Nitaandika makala juu ya hili nikipata wasaa.
Inaweza ikawa ni kweli, pamoja na kuwapa simu watoto kutazama makatuni kwa muda mrefu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Habarini za Kazi.

Naombeni msaada wa ushauri hapa. Nina mwanangu ana miaka mitatu na miezi sita na mwaka huu nimemuanzisha shule. Tatizo lake ni kwenye kuwasiliana imekuwa changamoto sana. Anaweza kuimba nyimbo za shule toka asubuhi hadi jioni, anaweza kuhesabu, kuandika na kusoma 1-20, Anaweza kusoma herufi zote A-Z.

Randomly kuna maneno mengi anatamka shida ni kwamba hawezi kujibu chochote utakachomuuliza labda ukimuambia afanye kitu flani ndo anaweza. Ila ukimwambia aseme neno flani au kitu flani anakuangalia tu. Hapa shida inaweza kuwa nini na suluhisho lake ni nini? Kama kuna mtu ana namba ya mtaalamu naomba anisaidie.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyu Mwanangu Wa Kiume , Ana Umri Wa miaka miwili na Miezi Miwili, lakini Ajabu Hadi Sasa hajui kutamka Mama Wala baba Yeye Akishamka Ni kuguna Tu Na Kuimba hadi Siku Inaisha Ni Mhhh..... Aahhhh
.... Eeeeh.......!!!

Majirani Wanamsema Vibaya Kuwa Mtoto Mkubwa lakini Anazidiwa Hata Na Wadogo wenzie yaani Hajui kuongea chochote, hii Inanipa Stress Mimi Kama Mzazi Najisikia Vibaya Sana Na Sijui Nifanyeje Ili Mwanangu Aongee

Naombeni Mnisaidie Jinsi gani Nitamfanya mwanangu Ajue Kutamka Maneno kama baba n.k
 
Habari wakuu..

Mtoto wangu ana miaka minne na miezi miwili hajajua kuongea vizur..wala hawez kuunganisha maneno vizuri yaeleweke..ushauri nifanyeje wakuu.

Mtoto ni wa kike
 
Mwanangu wa sita kuzaliwa alikua anasubiri nikirejea anaanza kutoa mashtaka...
Aaa baba.....
Kisha naitika, then anasema
Aaa mama akuma chini...🤣🤣
Kisha namuuliza, ikawaje
Then anajibu, akuma aaamimi achafuka sana....😂😂
Then baada ya hapo, namuuliza tena unasemaje??😆😆
Wakati huo alikua anaumri wa mwaka mbili na nusu....😅😅
 
Mzee stress kisa majirani wamesema?

Unataka tukuambie uende kwa mganga?

Kama ana afya, uzito unaohitajika, anatembea kwa umri wake mi sioni shida.
 
Usisikilize maneno ya hovyo na kukatisha tamaa ya majirani. Huyo mtoto bado mdogo kwa umri huo kumhukumu. Hata hivyo watoto hawafanani katika hatua za makuzi. Wengine wanawahi kuongea wengine wanachelewa. Sasa majirani wanataka mtoto wa miaka 2 awe anaongea kama chiriku!!!
 
Ni Kati ya sababu ya kum bembenda mtoto waulize watu maana ya kubemenda mtoto halafu ndio utajuwa kama ulifanya kosa
Hiizi ni fikra za hovyo sana mkuu, bila shaka wewe ni msikiliza maneno ya majirani na kitaa sana
 
Sina uzoefu sana na hili ila jaribu kumpeleka shule za vidudu akachanganyike na wenzie, wataalam wanadai inasaidia
Siungi mkono huu ushauri aiseeee....
Mtoto wa kiTanganyika inapendeza akianza shule akiwa na umri wa walau miezi 30
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…