Habari wakuu,
Naomba msaada wa mawazo kuhusu hili.
Mwanangu ana umri wa miaka 3 na miezi 8 ila bado hajaweza kuongea vizuri anaongea baadhi ya maneno kama baba, mama, bibi yaani kwa kuyahesabu hayafiki hata 30.
Nimejaribu kumpeleka Muhimbili kitengo cha speech ila tofauti haionekani sasa mitaani nakutana sana na ushauri kwamba nimpeleke kwa watalaam akaangaliwe kama ana UDATA.
Mama yake anasema ameshachunguza watoto wawili na anaona kuna tofauti kubwa katika ndimi zao kwa chini ila sasa hofu yangu ni kweli hili jambo lipo?
Naomba kama kuna ambaye aliishamfanyia mwanae hiki kitu aniambie pia anipe na risk zake.
Asante.