The best 007
JF-Expert Member
- Oct 6, 2019
- 41,015
- 93,277
Nimepenpda huu msemo "kacute kumbe ka killer" umenitia hofup sn huu msemo.Siku zote najua Komodo wanapatikana Indonesia na maeneo mengine ya Asia pekee, sikujua kama wapo Australia.
Afrika na Asia lazima tuwe na death toll kubwa kutokana na umbali wa vituo vya afya, upatikanaji wa anti venom na gharama yake.
Kuna ndege anaitwa Cassowary, yupo Australia pia, picha yake ukimuona ni kacute kumbe kakiller.
Yeah watu wamejitahidi kuelezea.
Kwanini? Umeuhamisha katika maisha ya kila siku?Nimepenpda huu msemo "kacute kumbe ka killer" umenitia hofup sn huu msemo.
Sent using Jamii Forums mobile app
Wakati ni haram kumlaHuyu ni mmoja ya wanyama wenye akili sana duniani. Kwenye top four kuna sokwe mtu, mbwa, pomboo(dolphin) na huyu jamaa. Pia ni bosi mmoja msafi sana. Kama umewahi mfuga utakuta anajisaidia mbali na anapokula.
Nimetokea kukaogopa sn haka ka ndege, kumbe ni kacute lkn ni kakiller.Kwanini? Umeuhamisha katika maisha ya kila siku?
Siyo ka ndege ni lindege. haya madege yanaweza kuwa makubwa kama punda...Nimetokea kukaogopa sn haka ka ndege, kumbe ni kacute lkn ni kakiller.View attachment 2030830
Sent using Jamii Forums mobile app
Huyu ni noma. Niliona video kuna cayman (aina ya mamba wa south america) alijaribu kumfanya mmoja lunch akapigwa shoti hadi kufa.Kuna samaki anaitwa electric eel, huku kwetu bongo tunamwita mkunga anapatikana katika mabwawa na mito mingi Africa na America ya kusini. Huyu samaki ana uwezo wa kuzalisha nguvu za umeme mpaka kufika Volts 600 kwaajili ya kuliua windo lake au kuwaweka adui zake mbali na yeye au kushambulia pale anapohisi kuna hatari.
Binafsi nishawavua sana hawa samaki nikiwa teenager katika makuzi ya kuvua vua samaki katika mabwawa lakini sikujua kama ana uwezo wa kukupiga shoti ambayo inaweza kukusababishia shock nakuwa drown hata katika kina kifupi cha maji. Kuna cases chache mpaka sasa za vifo vya binadamu vilivyosababishwa na huyu mjuba.
Mzee ni warefu.Nimetokea kukaogopa sn haka ka ndege, kumbe ni kacute lkn ni kakiller.View attachment 2030830
Sent using Jamii Forums mobile app
Kuna samaki wa ziwa Tanganyika naye ana hii tabia. Anakusanya makombe ya konokono na kuyapanga. Jike anaangali mzigo upi ni mwingi. Viumbe vyote wanawake wanamkubali mwenye uwezo.Bowerbird, huyu ndege vijana wa JF wanaweza kumuita baharia wa ndege. Wa kiume wanajenga viota na kuvipamba vizuuri ili kuvutia mpenzi. Wa kike wanakagua na kuchagua kiota kipi kimependeza ndo anaingia/kubali kuwa na huyo dume. Wako vizuri sana katika kupangilia rangi na wanatumia kila aina ya vitu kupamba kiota kama vile mawe, maua, vitu vya kibinadam kama vifuniko vya chupa, vipande vya glass...
Kibongobongo huyu ndege ni baharia mwenye ghetto lenye carpet la manyoya na bonge la sofa, huenda na subwoofer pia
Noma sana. Surely wale samaki wengine wasio na mawe na walikosa majike kwa kuwa na collection ndogo watakuwa wanaishia kulalamika eti 'mademu wanathamini utajiri kuliko utu (usamaki?)Kuna samaki wa ziwa Tanganyika naye ana hii tabia. Anakusanya makombe ya konokono na kuyapanga. Jike anaangali mzigo upi ni mwingi. Viumbe vyote wanawake wanamkubali mwenye uwezo.
HahaaaaaaNoma sana. Surely wale samaki wengine wasio na mawe na walikosa majike kwa kuwa na collection ndogo watakuwa wanaishia kulalamika eti 'mademu wanathamini utajiri kuliko utu (usamaki?)
Orca (killer whale) naweza kusema ni kama genge la wahuni wa baharini. Pamoja na kuitwa killer whale, wao ni ana ya dolphin, ndiyo dolphin mkubwa katika jamii ya dolphins. Wanasayansi wanaamini hawa majamaa wana akili sana. Wanawinda kwa makundi na pia wanajua kutumia miili yao na movement ya kutengeneza mawimbi yanayoweza kumtungua seal aliye juu ya barafu majini. Pia wanaweza kujisogeza hadi ufukweni kiasi fulani kuwinda seal.Nyoka mwenye sumu kali duniani yupo Australia. Anaitwa Inland Taipan ndugu yake wa karibu ni Coastal Taipan wana death toll kubwa kwakua hakuna antivenom bado.
Hata hivyo ukiwa Australia hao siyo wanyama pekee wa kuwahofia. Utatakiwa uwahofie Stone fish, Box Jellyfish ambao wana sumu kali isiyo na tiba kokote. Kangaroo inabidi uwakimbie achana na muvi adult kangaroo is deadly, na Great White Shark hawa papa hukua mpaka kufikia futi 25.
Hata hivyo chakula cha papa kikuu ni seal, papa hawindi binadamu actively. Ikatokea papa amekutana na binadamu hufanya ile kumzunguka zunguka kujaribu kung'amua hiki ni kiumbe gani. Akiona haelewi anang'ata kisha anagundua huyu siyo seal anaachana na wewe. Ndiyo maana wanaokufa kwa ajili ya papa hua ni majeraha yanayotokana na kung'atwa vital organs.
That aside I wish niseme nothing can stop Great White Shark ila hapana hawa papa huuawa na Orcinus Orca au Killer Whale. Wote tunajua whales hawali papa hivyo kuwaua papa hawa itakua wanachukulia mchezo anyway, these whales have learn't kwamba papa wanahitaji kua in a movement muda wote so wanachaofanya ni kumvizia papa wanamtokea kwa chini kisha wanakua kama wanamnyanyua hivyo kuzuia movement.
hivi tagi la mbwa mwitu linawz kuua binadamu?Hawa wanaogopwa na kuheshimiwa kama watawala wa nyika.
Ila kama wewe ni mnyama wa kuwindwa (mf. punda milia), ukiwaona hawa wazee wanakufuatilia, we pambana na kimbia maana unaweza ukapona maana inasemekana simba wanashindwa kukamata mnyama mara nyingi zaidi kuliko kupata (success rate 25%).
Ila ukiona unawindwa na kundi la hawa jamaa wengine, mbwa mwitu, get your affairs in order na sali toba na sala zako za mwisho maana unaweza kuwa na uhakika wa kifo. Hawa jamaa ndo vinara wa successful hunt nyikani (85%). Wakikuamulia hawa jamaa jua umekwisha.
sidhani kama imewahi kutokea ingawa sina imani na hawa jamaa kabisa. nafikiri ni bora kukaa mbali tu