MADA YA WEEKEND: Wazee wa Dar na Benz la Mwinyi

MADA YA WEEKEND: Wazee wa Dar na Benz la Mwinyi

Tatozo la Waafrika ni Elimu zetu za Kikoloni.
Elimu inayowafanya wasomi kujiona ni wazungu kwa sababu ya kahitaji ya kizungu.
Uafrika wetu tumeuondoa na kukimbia uzungu kwa nguvu zote.Wakati wazungu wakitendeana utu mkubwa sana wao kwa wao.

Kila msomi wa Kiafrika anaamini na kuwaza kuwa ipo siku ataingia kwenye nafasi ya ulaji tuu, na sio kutumikia wananchi na kutumia elimu yake kuwasaidia wengine.

Ndani ya mwaka mmoja Bilionea Mzee Ruksa amekabidhiwa mali za mabiloni kwa kodi za watu maskini sana.

Kikwete yeye aliamini kuwa maisha bora yanamfaa kila mtu awe nayo . Akasema maisha bora kwa kila mtanzania yanawezekana.

Mama ameanza kumgawia Bilionea Gari la mamilioni.
Bila shaka maskini wanasubiri mgao wao kutokana na Rasilimali walizopewa wote na Mungu.

Mungu ana Hekima kubwa sana.
Ingekua Hewa ya Oxygen inagawanywa na watawala leo hii mgawanyo ungekuwa kwa Upendeleo na kujuana na sio kwa haki .
Ingekua kifo kingepangiwa Ratiba na watawala wetu wa kiafrika na dunia basi ratiba ya kifo isingeonekana kutemblea maeneo ya wakubwa wala magonjwa.

Kuua Demokrasia ilikua ni jambo baya sana katika nchi hii.
Waoua demokrasia wamepoteza utu na uwajibikaji wa viongozi wetu kwa karne ijayo.
Walaaniwe wakurugenzi na wote walioshiriki kuua Demokrasia katika nchi hii.

Nchi yenye Demokrasia wapiga kura wanaheshimiwa kwa kupewa keki ya taifa mana wanahoji na wanawakataa viongozi wanaotumia vibaya rasilimali za umma kwa manufaa yao.

Nchi siyo na Demokrasia Wapiga kura hawana thamani mana hawawezi kubadili utawala na uongozi.

Tanzania tulipotezwa sana kwa kupumbazwa na watu wa chache kwa manufaa yao huku Demokrasia ikiuawa sasa matokeo yake ni haya.
Watumishi wanaolipwa mshahara laki nne kwa mwezi huku wakiwa wanajitafutia wenyewe mahitaji yao yote mpaka nauli za kufika ofisini na nyumba ya kuishi na chakula wanaambiwa mishahara yao inatosha na serikali haitaongeza mishahara mana sio kipao mbele chake.
Huku watawala wakiwa wanajipa kila kitu kwa kodi za wananchi. Wafanyakazi hawana tena thamani mana waliambiwa kura zao hazifiki hata laki 5 hivyo hazina maana. Na atakayethubutu kumpigia kura mpinzani atakiona cha mtema kuni.

Kazi inaendelea.
 
Tofauti ni moja wale ni wananchi wa kawaida walioenda kumsikiliza rais... Na yule ni rais mstaafu mwenye mtoto rais, aliyeenda kuzindua kitabu cha maisha yake
Kila mmoja hapo anakula kwa urefu wa kamba yake..
Hii ni kwa Afrika tu chief.
Kugawana mali ya umma kisa urefu wa kamba.
 
Wakati wa uzinduzi wa kitabu cha maisha ya mstaafu mzee Ally Hassan Mwinyi mambo mengi yamesemwa na hata baadaye kuonekana issue hii kuibukia kwa Simba na Yanga.

Twende kwenye hoja.
Wazee wa Dar waliofika kumsikiliza mama kama walikuwa 1000 basi kwa bei ya gari linalotakiwa anunuliwe mstaafu Rais Mwinyi kila mzee angeweza kurudi na tshs 250,000 nyumbani lakini akasema hana hata elfu 30!.

Mfano angalia prices ya hii benz,
View attachment 1778314
Hii ndio maana halisi ya mwenye nacho huongezewa zaidi,.
 
Wamempa gari mtu asiyehitaji gari, yaani hata mwanae Rais wa Znz angeweza mmnunulia gari , ila wake wazee walikuwa wanahitaji wamepewe hata elfu 30 tu kwa mwezi wametoswa
Hivi nchi hii nani katuroga? wazee wanataka wawe wanalipwa kila mwezi alfu 30 kwa maisha yao yote na wazee hawaishi vijana wa leo kesho wazee na utatumia kigezo kipi kusema huyu sasa mzee jana alikuwa bado apewe alfu 30 wanasema kuna wazee 2.5 million hiyo kila mwezi billion 75 kwa mwaka katibia trillion acheni utani kila aliyefanya kazi kuna fao la uzeeni hayo ndio malipo ya kisheria. Kelele zote hizi gari na gari zenyewe unasikia watu kodi zetu utasema hata hiyo kodi wanalipa. haya magari walipewa zawadi wa mfalme wa Morocco acheni roho za chuki yuke mzee alikuwa Rais nchi hii na anamiaka 96 anastahili. Mimi nilikuwa nawaunga kiasi mkono wapinzani lakini hii tabia ya kudandia kila jambo na kuwa negative nimewashusha utasema Mzee kapewa bombadier kelele za watu.
 
Eeh.. kumbe alishapewa na nyumba tena..? 🙄
Nyumba wanapewa kisheria imetungwa maraisi wastaafu wote wanajengewa na sheria waliopitisha ni hao hao tunaowachagua bungeni na Rais anahudumiwa mpaka usafiri na ulinzi wake na serikali.
 
Mbona marehemu ruge mutahaba alipewa mil 50 na mzee wakati anaumwa afrika kusini lakini hamjaongea?
 
Tofauti ni moja wale ni wananchi wa kawaida walioenda kumsikiliza rais... Na yule ni rais mstaafu mwenye mtoto rais, aliyeenda kuzindua kitabu cha maisha yake
Kila mmoja hapo anakula kwa urefu wa kamba yake..
Mshana itakuwa ulisoma African literature kabisa
 
Bora huyu alikua anagawia masikini wenye uhitaji. Hilo benzi Mwingi ataendesha anaenda wapi?
Benz hilo linatufaa vijana na kwenda kung'ata papuchi na kula bata na watoto, sasa huyu mzee sijui la Nini?
Ushauri wangu mwinyi auze hiyo Benz anunue nguo apeleke kwenye vituo vya watoto yatima nchi nzima au madawati na vitabu apeleke shuleni, hizo ela za wanyonge ,
Mzee alipige mnada atengeneze pesa nyingi akasaidie watu maskini, njaa Mbaya sana,

Kuna wenyeviti huku mtani wanatusumbua kuhusu ela za kujenga vyoo mashuleni, michango ya zahanati na madawati , Sasa sijui tugome kuchangia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
  • Thanks
Reactions: mmh
Mshana itakuwa ulisoma African literature kabisa

Hivi akili zako zinafanya kazi vizur wewe? Ruge alikua mahututi na alikua anahitaji msaada kwa ajili ya matibabu, au ulidhan alipewa akanunue Land cruiser?
 
Umri wenyewe ushaenda, Benz la nini , huyu mama anajifanya mother Theresa , kitamkuta kitu


Enz za magu Tz ilikua inaheshimika sana duniani, sasa hiv tumerud kuwa mazuzu, hapa raisi hatuna, miaka yake iishe tupige kura
 
Hivi nchi hii nani katuroga? wazee wanataka wawe wanalipwa kila mwezi alfu 30 kwa maisha yao yote na wazee hawaishi vijana wa leo kesho wazee na utatumia kigezo kipi kusema huyu sasa mzee jana alikuwa bado apewe alfu 30 wanasema kuna wazee 2.5 million hiyo kila mwezi billion 75 kwa mwaka katibia trillion acheni utani kila aliyefanya kazi kuna fao la uzeeni hayo ndio malipo ya kisheria. Kelele zote hizi gari na gari zenyewe unasikia watu kodi zetu utasema hata hiyo kodi wanalipa. haya magari walipewa zawadi wa mfalme wa Morocco acheni roho za chuki yuke mzee alikuwa Rais nchi hii na anamiaka 96 anastahili. Mimi nilikuwa nawaunga kiasi mkono wapinzani lakini hii tabia ya kudandia kila jambo na kuwa negative nimewashusha utasema Mzee kapewa bombadier kelele za watu.
Shida ni Kuwa ,serikali ya CCM wanakula nchi peke yao , saa mzee Mwinyi alikuwa na shida ya gari kweli?!
 
Mambo ya Tanzania yanachekesha sana, tulianza kumsema Mwendazake alipokuwa anawapa Mkapa, Kikwete, Mwinyi majumba ya fedha nyingi na leo tunahama ukurasa mwingine aaaiiii..!
 
Umri wenyewe ushaenda, Benz la nini , huyu mama anajifanya mother Theresa , kitamkuta kitu


Enz za magu Tz ilikua inaheshimika sana duniani, sasa hiv tumerud kuwa mazuzu, hapa raisi hatuna, miaka yake iishe tupige kura
Inasikitisha Sana, halafu kuna mijitu inakuja na nyimbo na vigelegele vya kusifu upuuzi. Tulikuwa tunaanza kupiga hatua sasa hivi twarejea tulipotoka, business as usual.
 
Shida ni Kuwa ,serikali ya CCM wanakula nchi peke yao , saa mzee Mwinyi alikuwa na shida ya gari kweli?!
Nadhani Mama aliongea sababu ya kumpa gari ndogo, Huyu mzee ana miaka 96 na amekuwa anaitwa katika shughuli mbalimbali za kiserikali kama Rais mstaafu, kasema tunamuona shida anayopata wakati wa kupanda gari na kushuka tunampa gari ndogo asipate tabu huyu ni mtu mzima 96 years old na mtu aliyewahi kushika nafasi kubwa katika nchi hii. Jamani hata mzee wetu tunamsakama utasema kapewa Boeng gari zenyewe zilikuwa zawadi tu toka Morocco.
 
Back
Top Bottom