Madai ya jukwaa la wakristo hayana ukweli

Madai ya jukwaa la wakristo hayana ukweli

Tena wewe ndo mento namba moja usietaka kuelewa ukweli wa uzuri wa Katiba pendekezwa.

Katiba ya pendekezwa ni ya ccm ile ya wananchi ndio tunayoitaka sisi tulimpa mrejesho jaji warioba ili ikienda bungeni ikaongezwe makali zaidi sio kwenda kutoa maoni yetu na kuweka ya mazebe wachache sasa tutaona kati ya hao waroho wa madaraka wenye hofu ya maisha na sisi wananchi tuliowatama nani zaidi.
 
mmebaki wachache sana, na mtajikuta jangwani peke yenu. Watanzania tumeshaamua 'katiba ya chenge hapana!. Matusi ya mwendawazimu huwa hayaumi kwa sababu ni sehemu ya wehu wake na hayabadilishi ukweli.

huna jipya kalale
 
katiba ya pendekezwa ni ya ccm ile ya wananchi ndio tunayoitaka sisi tulimpa mrejesho jaji warioba ili ikienda bungeni ikaongezwe makali zaidi sio kwenda kutoa maoni yetu na kuweka ya mazebe wachache sasa tutaona kati ya hao waroho wa madaraka wenye hofu ya maisha na sisi wananchi tuliowatama nani zaidi.

too late my friend, ngoma inapita hii, kama umeishiwa hoja kalale.
 
Jukwaa la Wakristo Tanzania madai yenu kuhusu suala la ulinzi na usalama nawashauri muipate Katiba Inayopendekezwa na muisome kwa makini Katiba hiyo katika SURA YA 17 mtapata majibu mazuri ya wasiwasi wenu kuhusu usalama wa nchi.


Kuhusu suala la Muundo wa Serikali, wajameni SURA YA 7 ya Katiba Inayopendekezwa imeeleza wazi wazi juu ya Muundo wa Jamhuri ya Muungano katika IBARA YA 73.


Kuhusu masuala ya mauaji ya watu wenye ualbino, nadhani kila siku mnasikia wahusika wanavyokamatwa haswa waganga wa jadi pamoja na wauaji, lakini pia kuna kesi mbalimbali zinaendelea na nyingine zimeshatolewa hukumu kali.


Kuhusu kuwataka waumini wenu wote wajitokeze kwa wingi kujiandikisha katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura, kuisoma Katiba Inayopendekezwa na kushiriki kikamilifu vipindi vya elimu juu ya Katiba Inayopendekezwa na kisha wajitokeze kwa wingi kupiga kura ya hapana kwa Katiba Inayopendekezwa kwa sababu mlizozitaja hapo mmechemsha, kwasababu msidhani kuwa waumini wote watafanya hivyo, nina amini wapo waumini wenye busara na wenye uelewa juu ya ukweli wa mambo mazuri yaliyoelezwa ndani ya Katiba Inayopendekezwa ambao hawatapoteza haki yao ya kufanya hivyo mlivyopanga.


Lakini pia hivi hamuoni kuwa mtakuwa mmemkosea Mwenyezi Mungu kwa kuwashinikiza waumini wenu waipinge Katiba hiyo? Kwani hata Biblia yenyewe inasema “ya Kaisari mpeni Kaisari nay a Mungu mpeni Mungu”, sasa udikteta huo mnaowafanyia waumini mmeupata wapi? Dini mnaiingiza na siasa tena jamanai? Tanzania ni nchi isiyokuwa na dini, kuweni makini msije mkaulizwa na Muumba wenu je kwanini mliwanyima haki waumini wenu katika Mamlaka ya Dunia. Kuwenu mfano wa mbele katika kuelimisha waumini badala ya kuwashinikiza waikatae. Huo sio uungwana kabisaaaaa!.

Nani aliandika katiba inayopendekezwa?
 
naukiza katiba pendekezwa ina kipengele cha mahakama ya kadhi??

Haina kipengele cha mahakama ya kadhi....ila inatoa haki ya kila raia kuabudu...kumbuka Tanzania ts a seculer state....itakuwa ngumu sana kuweka kipengele hicho ndan ya Katiba Inayopendekezwa...
 
Mmebaki wachache sana, na mtajikuta jangwani peke yenu. Watanzania tumeshaamua 'KATIBA YA CHENGE HAPANA!. Matusi ya mwendawazimu huwa hayaumi kwa sababu ni sehemu ya wehu wake na hayabadilishi ukweli.

Hivi unadhani kuwa mwenyekiti wa Kamati ya Maandishi ndio kigezo cha kuwa yale ndo maoni yake....kwa kukuelimisha tu hatuna katiba ya aina hiyo tunayo katiba inayopendekezwa iliyoandikwa na wajumbe wa BMK waliochaguliwa kuwawakilisha wananchi bungeni.....mchakato ulimshirikisha kila aliyeona ana haja ya kumchagua mjumbe atakayeenda kumtetea ndani ya bunge lile...Ningependa kumshukuru chege for the assist katika uandishi
 
toa hoja acha matusi, hakuna snake hapa
SNAKE wewe ndio unakuja na jazba, mm mwenzako nilikuwa km wewe nililielewa lile tamko juu juu.
Unachokieleza ni changa la macho limekupitia kwani kuna kasoro zaidi ya 100 zilizoainishwa kwa kuukataa mchakato huo
ntakueleza chache tu
  1. Tanzania si Nchi ya kidini hivyo si sahihi kuanza kuyaingiza mambo ya kidini katia Bunge eti kujadili Mahakama ya Kadhi (Mbunge wa Nkasi Mh Ally Keyssi amekataa kabisa mambo ya kadhi kujadiliwa na Serikali au Bunge kwani sio katika NGUZO ZA UISLAMU
    Mbunge wa Nkasi Kaskazini (CCM), Ally Keissy alisema hakubaliani na suala la kuitambua Mahakama ya Kadhi kisheria akisema hiyo si miongoni mwa Nguzo Kuu za Uislamu
    Mahakama ya Kadhi yawavuruga wabunge - Kitaifa - mwananchi.co.tz
  2. CCM katika Kampeni zake tangu 205, 2010 kiliahidi kama kitapewa Kura kitaweka Mahakama ya Kadhi, na bado kikitarajia hata kura za 2015, (tafuta DVD ya MADHARA YA MAHAKAMA YA KADHI) anaoneka Mwenyekiti wa CCM ndani ya Msikiti wa Gadaffi Mjini Dodoma akiwahakikishia Waislamu kuwa sasa kazi imekwisha bado sehemu ndogo tu itamaliziwa na Mahakama hizo kuwepo
  3. Kuipigia Katiba pendekezi KURA YA HAPANA ni kwamba irudiwe tena kwani
    • Spika aliyeiongoza aliiburuza sana na kufunika mambo mengi katika mchakato huo.
    • ikiwemo wabunge wasiwajibishwe na Wapiga Kura wao
    • theluthi ya wawakilishi wa wananchi walitoka nje, wakiwemo UKAWA
    • Siku zilizopangwa za kuwaandikisha Wapiga kura kwa Nchi nzima hazitosho kwani zimebaki siku 30 tu na bado tupo Mkoa wa Njombe, Kura hii bora isipigike.
  4. Kumbuka Rais mwenyewe kakataa hakuna Mahakama ya KADHI lakini Waziri Mkuu kalazimisha kuiingiza Bungeni kwa kuwaogopa Waisalamu na jana tu ngumi kidogo ziwake Bungeni hadi akawasihi Wabunge suala la MAHAKAMA ya KADHI halitaingizwa bungeni,
kama KATIBA mpya itapendekezwa itaanza kutumika 2018
sasa ukipiga kura ya HAPANA maana yake Rais ataitisha Bunge na mchakato mwingine, aidha wa kuongeza au kupunguza vipengele hivyo zaidi ya 100, na kumbuka hawatatakiwa Wabunge wale wa mwanzo, iwe kwa kuondolewa Ubunge aua kuteuliwa kurudi Ukumbini.
Ikipigwa tena ya HAPANA basi itaendelea iliyokuwepo
wakati wote a Mchakato
SI DHAMBI UKISEMA HAPANA na bila tishio hilo la Maaskofu WABUNGE WAKO WASINGECHAFUANA JANA

kadhi+picha.gif

Mahakama ya Kadhi yawavuruga wabunge - Kitaifa - mwananchi.co.tz
 
naukiza katiba pendekezwa ina kipengele cha mahakama ya kadhi??
Kwa hiyo na sisi ni mambumbu pamoja na wabunge wanaotaka kupigana leo kuhusu Mahakama ya KADHI
Kama katika Katiba pendekezwa hakuna mahakama ya kadhi kwanini ijadiliwe leo na Rais keshakanusha hakuna kitu hicho Kila DINI ishighulike na masuala hayo.
Kitende tu cha kuuingiza MUSWADA HU WA MAHAKAMA YA KADHI hapo kesho ni jibu tosha kwako nani ni mwerevu
na kikishapitishwa utakiondoaje na umeshasema MAHAKAMA YA KADHI IWEPO?
Na ikishakuwepo Katiba itakiingiza aua kukikataa wakati imeshakuwa Sheria
Dada yangu Mkirsto kaolea na Mwislamu halafu kafumaniwa na kaka wa huyo Mumewe adhabu ya mawe inawahusu wote Dada ngu Mkristo na huyo Mwislamu au
umeiba Kuku kwa jirani unakatwa mkono na huyo Ruge anayegawa hela za Escrow wanakamatwa waliopewa tu
Ni bora wewe uliyekatwa mkono wa kulia kwa kuipa Kuku na unamaliziwa wa kushoto kwa kukutwa na mbuzi?
wakati watu wana malizana na PAP, Mabibo, Meremeta wanashangiliwa
 
Kwa hiyo na sisi ni mambumbu pamoja na wabunge wanaotaka kupigana leo kuhusu Mahakama ya KADHI
Kama katika Katiba pendekezwa hakuna mahakama ya kadhi kwanini ijadiliwe leo na Rais keshakanusha hakuna kitu hicho Kila DINI ishighulike na masuala hayo.
Kitende tu cha kuuingiza MUSWADA HU WA MAHAKAMA YA KADHI hapo kesho ni jibu tosha kwako nani ni mwerevu
na kikishapitishwa utakiondoaje na umeshasema MAHAKAMA YA KADHI IWEPO?
Na ikishakuwepo Katiba itakiingiza aua kukikataa wakati imeshakuwa Sheria
Dada yangu Mkirsto kaolea na Mwislamu halafu kafumaniwa na kaka wa huyo Mumewe adhabu ya mawe inawahusu wote Dada ngu Mkristo na huyo Mwislamu au
umeiba Kuku kwa jirani unakatwa mkono na huyo Ruge anayegawa hela za Escrow wanakamatwa waliopewa tu
Ni bora wewe uliyekatwa mkono wa kulia kwa kuipa Kuku na unamaliziwa wa kushoto kwa kukutwa na mbuzi?
wakati watu wana malizana na PAP, Mabibo, Meremeta wanashangiliwa

Mahakama ya kadhi haina muda hapa, this is a secular State,
 
Back
Top Bottom