Madai ya Lissu kutoa tuhuma za rushwa ndani ya CHADEMA, Mnyika asema “Yeyote mwenye tuhuma aziwasilishe zishughulikiwe”

Madai ya Lissu kutoa tuhuma za rushwa ndani ya CHADEMA, Mnyika asema “Yeyote mwenye tuhuma aziwasilishe zishughulikiwe”

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Katibu Mkuu wa CHADEMA, John Mnyika amezungumza na Waandishi wa Habari, Jijini Dar es Salaam, leo Desemba 16, 2024.

Akijibu swali kuhusu Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu kutoa tuhuma za uwepo wa mazingira ya Rushwa na kukosekana kwa Uadilifu, amesema:

“Kuhusu tuhuma ambazo Makamu (Lissu) amezitoa kuhusu uadilifu, nisisitize kwa nafasi yangu ya utendaji mkuu wa Chama ikiwa kuna Kiongozi au Mtu yoyote wa CHADEMA ana tuhuma dhidi ya yoyote aziwasilishe ili zishughulikiwe kwa mujibu wa Katiba, Itifaki na maadili ya Chama na sio kutoa tuhuma za jumlajumla bila kusema hapa kuna huyu anatuhumiwa na huyu na hili na hili.”

“Tukipata tuhuma zenye ushahidi zitapelekwa kwenye Kamati Kuu ya Chama ambayo itaamua kushughulika nayo au kupeleka Kamati ya Maadili, kama kuna jambo liletwe.”
 
Mnyika mkamate wenje,mkamate sugu,mkamate kigaila,mkamate mrema
Mbona Yericko alieleza hili swala vizur jana?

Kwamba walikuwa wanatafuta namna alipwe hela zake... Kuna mtu akasema atamsaidia na ni rafiki wa Jamaa mmoja ambae yupo kamati kuu kwakuwa wanafanya biashara pamoja .

Sasa jamaa katuma vielelezo hata havijajibiwa kaja kulimwaga hadharani...

Naweza nikawa sikubaliani na kina Kigaila lakini TL ana issues za kukosa busara mara nyingi...

Hizo shutuma zenyewe aliambiwa azithibitishe mpaka leo kimya...

Apewe Chama muone atakapoanza kulaumu watu..
 
Mbona Yericko alieleza hili swala vizur jana?

Kwamba walikuwa wanatafuta namna alipwe hela zake... Kuna mtu akasema atamsaidia na ni rafiki wa Jamaa mmoja ambae yupo kamati kuu kwakuwa wanafanya biashara pamoja .

Sasa jamaa katuma vielelezo hata havijajibiwa kaja kulimwaga hadharani...

Naweza nikawa sikubaliani na kina Kigaila lakini TL ana issues za kukosa busara mara nyingi...

Hizo shutuma zenyewe aliambiwa azithibitishe mpaka leo kimya...

Apewe Chama muone atakapoanza kulaumu watu..

..Abduli ana nafasi gani wizara ya fedha mpaka awe na uwezo wa kufanikisha malipo ya stahiki za Tundu Lissu?

..huo ulikuwa mpango wa kumtumbukiza Tundu Lissu katika genge lao, ili awe compromised.

..Na Lissu angekubaliana na matakwa ya hao vibaka wangeanza kum-blackmail ili aachane na misimamo yake.

..tukio kama hilo liliwahi kumtokea Christopher Mtikila. Na ndio ukawa mwanzo wa mwisho wa Mtikila.
 
..huyo Abduli ana nafasi gani wizara ya fedha mpaka awe na uwezo wa kufanikisha malipo ya stahiki za Tundu Lissu?

..huo ulikuwa mpango wa kumtumbukiza Tundu Lissu katika genge lao, ili awe compromised.

..Na Lissu angekubaliana na matakwa ya hao vibaka wangeanza kum-blackmail ili aachane na misimamo yake.

..tukio kama hilo liliwahi kumtokea Christopher Mtikila. Na ndio ukawa mwanzo wa mwisho wa Mtikila.
Ila mkuu ninavyojua kibongo bongo Connection ni muhim sana kwenye aina ya madai yaliyokuwa ya TL...

Lakini hiyo huwezi ita rushwa moja kwa moja?
Kama ni Rushwa mbona email alituma?

Utume na email kabisa baadae uite wenzako wala rushwa kwel?

Kwamba kufanya biashara na watu wengine wasio na mrengo wako imekuwa ni rushwa?

Pengine ukasema black mail, sasa unaweza kuwa black mailed na malipo ni yako kihalali kabisa?

Alichokusudia TL ni kujijenga binafsi kisiasa, na amefanikiwa kwa kiasi.

Balaa ni kwamba deep part owners wa chama chake wakimkataa atapata taabu sana kuelekea 2030...

Kuwa mgombea urais tu kama Membe then golden career yake iwe imeishia hapo...

Ninachojua Siasa na Biashara zenye mafanikio duniani huwa zinafanywa back door na sio front office kama anavyofanya TL .

Hizi Character za Front office politics zilikuwa za Mrema na Mtikila.... Sina kumbu kumbu nzuri kwenye mafanikio ya vyama vyao....

Muda utasema...
 
Mbona Yericko alieleza hili swala vizur jana?

Kwamba walikuwa wanatafuta namna alipwe hela zake... Kuna mtu akasema atamsaidia na ni rafiki wa Jamaa mmoja ambae yupo kamati kuu kwakuwa wanafanya biashara pamoja .

Sasa jamaa katuma vielelezo hata havijajibiwa kaja kulimwaga hadharani...

Naweza nikawa sikubaliani na kina Kigaila lakini TL ana issues za kukosa busara mara nyingi...

Hizo shutuma zenyewe aliambiwa azithibitishe mpaka leo kimya...

Apewe Chama muone atakapoanza kulaumu watu..

Namtaka Lissu Chadema sababu ya ujeuri na kukosa Busara kwake. Lissu ana Jazba na hana subira lakini mi ninavyoona tunahitaji kweli mtu kutoka upinzani ambae atakemea vitu vya upuuzi ambavo watanzania wengi tumejisahau.

Tunahitaji mtu wa kuongelea sheria,kujitegemea,kuendana na Technology na Science based on facts and philosophy.

Tanzania is one of the biggest,populated,cultural diverse country in East Africa lakini tumebaki pale pale sababu wananchi wetu tumepewa maarifa ya dunia na utawala wetu kwa kiasi kidogo cha kujitosheleza sisi tu kwa miaka mingi tumebakia tunaachwa na majirani na kua incompetent kwenye kila tunachokifanya.

Watu kama Lissu sidhani kama atachukua nchi lakini ni mtu mzuri sana kuwakumbusha waTanzania na CCM kuhusu namna bora ya kuendana na wakati pamoja na Technology.

Tanzania inategemewa na kuhitajika East Africa ila tunajichukulia poa sana.
 
Namtaka Lissu Chadema sababu ya ujeuri na kukosa Busara kwake. Lissu ana Jazba na hana subira lakini mi ninavyoona tunahitaji kweli mtu kutoka upinzani ambae atakemea vitu vya upuuzi ambavo watanzania wengi tumejisahau.

Tunahitaji mtu wa kuongelea sheria,kujitegemea,kuendana na Technology na Science based on facts and philosophy.

Tanzania is one of the biggest,populated,cultural diverse country in East Africa lakini tumebaki pale pale sababu wananchi wetu tumepewa maarifa ya dunia na utawala wetu kwa kiasi kidogo cha kujitosheleza sisi tu kwa miaka mingi tumebakia tunaachwa na majirani na kua incompetent kwenye kila tunachokifanya.

Watu kama Lissu sidhani kama atachukua nchi lakini ni mtu mzuri sana kuwakumbusha waTanzania na CCM kuhusu namna bora ya kuendana na wakati pamoja na Technology.

Tanzania inategemewa na kuhitajika East Africa ila tunajichukulia poa sana.
Kwenye kugombea urais nakubaliana na wewe..
Ila kuendesha CDM kwa hiz ropo ropo bila kifua kuna balaa naiona...

Watu watakufa na hakuna kitu atafanya.
 
Ila mkuu ninavyojua kibongo bongo Connection ni muhim sana kwenye aina ya madai yaliyokuwa ya TL...

Lakini hiyo huwezi ita rushwa moja kwa moja?
Kama ni Rushwa mbona email alituma?

Utume na email kabisa baadae uite wenzako wala rushwa kwel?

Kwamba kufanya biashara na watu wengine wasio na mrengo wako imekuwa ni rushwa?

Pengine ukasema black mail, sasa unaweza kuwa black mailed na malipo ni yako kihalali kabisa?

Alichokusudia TL ni kujijenga binafsi kisiasa, na amefanikiwa kwa kiasi.

Balaa ni kwamba deep part owners wa chama chake wakimkataa atapata taabu sana kuelekea 2030...

Kuwa mgombea urais tu kama Membe then golden career yake iwe imeishia hapo...

Ninachojua Siasa na Biashara zenye mafanikio duniani huwa zinafanywa back door na sio front office kama anavyofanya TL .

Hizi Character za Front office politics zilikuwa za Mrema na Mtikila.... Sina kumbu kumbu nzuri kwenye mafanikio ya vyama vyao....

Muda utasema...

..Amiri Jeshi Mkuu si alishapitisha Lissu alipwe mafao yake?

..Sasa huyo bwana mdogo Abduli ana mamlaka kuliko Amiri Jeshi Mkuu?

..wakati vijana wadogo wanachama wanapotezwa kuna kikundi ndani ya chama kinakata madili na Abduli.

..very stupid people, and I'm glad Lissu has exposed them.
 
Kwenye kugombea urais nakubaliana na wewe..
Ila kuendesha CDM kwa hiz ropo ropo bila kifua kuna balaa naiona...

Watu watakufa na hakuna kitu atafanya.

..kwanini watu wafe?

..nani atauwa watu?

..kwanini mmeyafanya maisha ya Watanzania kuwa na thamani ndogo kiasi hiki?

..tuwaambie tu wenye silaha nchi hii waache kuuwa wananchi.
 
Kwenye kugombea urais nakubaliana na wewe..
Ila kuendesha CDM kwa hiz ropo ropo bila kifua kuna balaa naiona...

Watu watakufa na hakuna kitu atafanya.
Ropo ropo yake ndio Tanzania inahitaji kwa sasa hivi. Kuna roporopo nyingi sana sasa hivi lakini hakuna roporopo ya kutuamsha na kutukumbusha sisi ni nani. Roporopo za sasa hivi ni za kutukuza cheo,mamlaka na mpira tunahitaji roporopo za kuhusu sisi ni nani na kama mtanzania una uwezo gani ili uchangie pato la taifa. Hii population bila kuipa kitu cha msingi(purpose) cha maendeleo na kushughulika nacho huku tukiwapa habari nyepesi nyepesi na mpira itakuja kutukost kama taifa. Kama millenial wa 94 nimejionea vya kutosha.
 
Back
Top Bottom