Madaktari bingwa wafanikiwa kumpandikiza binadamu moyo wa nguruwe

Madaktari bingwa wafanikiwa kumpandikiza binadamu moyo wa nguruwe

Pigo kubwa sana kwa wapenda-kula nguruwe, because sasa haitakuwa kuwafuga kwa ajili ya bacon & pork, bali kwa ajili ya mioyo yao.
 
images (53).jpeg
 
Sijajua kama hapa Tanzania itakubalika labda Moshi.
--

Moyo wa nguruwe wapandikizwa kwa binadamu nchini Marekani​

View attachment 2077557

Katika picha hii iliyotolewa na Chuo cha kikuu cha Tiba cha Maryland, timu ya upasuaji inaonyesha moyo wa nguruwe tayari kupandikizwa kwenye mgonjwa

Kwa mara ya kwanza duniani, nchini Marekani, Madaktari wa upasuaji wamefanikiwa kupandikiza moyo kutoka kwa nguruwe aliyebadilishwa vinasaba hadi kwa binadamu mgonjwa, Chuo Kikuu cha tiba ya Maryland kimesema.

Operesheni hiyo ilitekelezwa siku ya Ijumaa. Ilionyesha, kwa mara ya kwanza, kwamba moyo wa mnyama unaweza kuendelea kufanya kazi kwa binadamu bila usumbufu wowote, Chuo Kikuu cha Maryland kimeongeza.

David Bennett, 57, ambaye alipokea moyo wa nguruwe, alitangazwa kuwa hastahili kupokea upandikizaji wa moyo wa binadamu. Sasa anafuatiliwa kwa karibu na madaktari ili kuhakikisha kiungo kipya kinafanya kazi vizuri.

"Yaani yalikuwa mambo mawili kwa binadamu huyo, ima kifo au upandikizaji wa moyo wa nguruwe. Nataka kuishi.

Ninajua ilinigusa sana, lakini ilikuwa chaguo langu la mwisho, "mkazi wa Maryland alisema siku moja kabla ya upasuaji wake, kulingana na chuo kikuu cha matibabu. "Siwezi kungoja niweze kuamka kitandani mara tu ninapokuwa mzima," David Bennett, ambaye amelala kitandani kwa miezi michache iliyopita na kutumia mashine inayomfanya aendelee kuishi.

Nguruwe aliyebadilishwa vinasaba
Mamlaka ya Madawa ya Marekani (FDA) iliidhinisha operesheni hiyo jioni ya siku ya kuamkia Mwaka Mpya. "Haya ni mafanikio makubwa ya upasuaji na ambayo yanatuwezesha kupata suluhisho dhidi ya uhaba wa viungo, " amebaini Bartley Griffith, aliyefanyiwa upandikizaji wa moyo wa nguruwe.

Nguruwe ambao moyo hutoka umebadilishwa vinasaba ili kutozalisha tena aina ya sukari ambayo kwa kawaida iko kwenye seli zote za nguruwe na ambayo husababisha kiungo kukataa kufanya kazi mara moja. Marekebisho haya ya jeni yalifanywa na kampuni ya Revivicor, ambayo pia ilitoa figo ya nguruwe ambalo madaktari wa upasuaji walifanikiwa kuunganisha kwa mishipa ya damu ya mgonjwa aliyekuwa mahututi huko New York mwezi Oktoba.

Takriban Wamarekani 110,000 kwa sasa wako kwenye orodha ya wanaosubiri kupandikizwa viungo na zaidi ya watu 6,000 wanaohitaji upandikizaji hufa kila mwaka nchini humo.
Inawezekana kabisa hii ikawa ni mojq ya mbinu ya udini. Ni kweli walikosa mnyama aina nyingine ambae anafanania zaidi na binadamu kama sokwe wakaamue wamtumie nguruwe ambae wanajua fika kuwa ni haramu kwa waislamu. Hii vita ya udini japo haipo waziwazi lakini inaonekana kuendelea chinichini.
 
Inawezekana kabisa hii ikawa ni mojq ya mbinu ya udini. Ni kweli walikosa mnyama aina nyingine ambae anafanania zaidi na binadamu kama sokwe wakaamue wamtumie nguruwe ambae wanajua fika kuwa ni haramu kwa waislamu. Hii vita ya udini japo haipo waziwazi lakini inaonekana kuendelea chinichini.

Hapana hakuna vita yeyote bali ni elimu tu na uvumbuzi
Uislam umeweka wazi kila kitu na suala la kuuliza na kujisomea tu

Zipo dawa ambazo hatuweza kutumia ila wengine wanatumia

Kuhusu hili jaribio hawakukurupuka tu bali ni la mda mrefu sana na Islamic council waliliongelea sana na tunajua ni Haram

Kwa hiyo acha wafanye majaribio yao na sisi kama kwetu haitufai tunaacha
 
Inawezekana kabisa hii ikawa ni mojq ya mbinu ya udini. Ni kweli walikosa mnyama aina nyingine ambae anafanania zaidi na binadamu kama sokwe wakaamue wamtumie nguruwe ambae wanajua fika kuwa ni haramu kwa waislamu. Hii vita ya udini japo haipo waziwazi lakini inaonekana kuendelea chinichini.
Mkuu, umenisoma uzuri hapo juu?
 
Mwanaume wa marekani amekuwa mtu wa kwanza kabisa duniani kupata moyo wa nguruwe aliyebadilishwa vinasaba(GMO).

David Bennett, mweNYE umri wa miaka 57, anaendelea vyema siku tatu baada ya upasuaji wa majaribio hayo uliofanyika katika mji wa Baltimore, wanasema madaktari.

Upandikizaji wa moyo huo unachukuliwa kama matumaini ya kuyaokoa maisha a Bw Bennett, ingawa haijawa wazi bado ni fursa ya kiasi gani aliyo nayo ya kuishi maisha marefu.

" Ulikuwa ni upandikizaji wa kufanya au afe," Bw Bennett alielezea siku moja kabla ya upasuaji.

''Ninafahamu kwamba ni jambo la kubahatisha, lakini ni chaguo langu la mwisho," alisema.

Madaktari wa Chuo Kikuu cha Maryland kito cha tiba walipewa idhini maalum na wasimamizi wa matibabu kuendelea na upasuaji huo, kwa misingi kwamba vinginevyo Bw Bennet angekufa.

Alikuwa ameonekana kwamba hakuwa na uwezo wa kupandikiziwa moyo wa binadamu, uamuazi ambao mara nyingi huchukuliwa na madaktari wakati mgonjwa anapokuwa na afya duni sana.

Kwa timu ya madaktari iliyofanya upandikizaji huo, mafanikio hayo yamehitimisha miaka kadhaa ya utrafiri na yanaweza kubadili maisha kote duniani.

Daktari wa upasuaji Bartley Griffith alisema upasuaji utaileta dunia katika "hatua moja ya kukaribia kutatua mzozo wa ukosefu wa kiungo cha mwili ",Chuo kikuu cha tiba cha Maryland kilisema katika taarifa yake kwa umma.

Kwamba mzozo huo unamaanisha kuwa watu 17 kwa siku hufariki nchini Marekani wakati wakisubiri kufanyiwa upasuaji wa kupandikiziwa viungo, huku zaidi ya 100,000 wakiripotiwa kungojea upasuaji.

Uwezekano wa kutumia viungo vya Wanyama kwa ajili ya kile kinachoitwa xenotransplantation ili kufikia mahitaji umekuwa ukifikiriwa kwa muda mrefu, na matumizi ya mishipa ya moyo wa nguruwe tayari limekuwa ni jambo la kawaida.

Mwezi Oktoba, 2021, madaktari wa upasuaji mjini New York walitangaza kwamba wamefanikiwa kupandikiza figo la nguruwe kwa binadamu.

Wakati huo, upasuaji huo ulikuwa ni jaribio la teknolojia ya hali ya juu zaidi kuwahi kufikiwa.

Hatahivyo, ubongo wa mtu alyepandikiziwa ulikufa na hakuna matumaini ya kupona.

Bw Bennett, hatahivyo , anamatumaini kuwa upandikizaji wake wa moyo wa nguruwe utamuwezesha kuendelea na maisha yake.

Alikuwa amelala kitandani kwa wiki sita mfulurizo kabla ya kufanyiwa upasuaji, na aliwekewa mashine ambayo ilimuwezesha kuendelea kuishi baada ya kupatikana na maradhi yanayoua ya moyo.

"Natazamia kunyenyuka na kuondoka kitandani baada ya kupona ," alisema wiki iliyopita.

Jumatatu, Bw Bennett aliripotiwa kupumua mwenyewe huku akiendelea kufuatiliwa kwa karibu.

Lakini kile kitakachotokea baadaye hakijawa wazi. Nguruwe aliyetumiwa katika upandikizaji alifanyiwa mabadiliko ya vinasaba ili kuondoa jeni kadhaa ambazo zingefanya kiungo hicho kikataliwe na mwili wa Bw Bennet, linaripoti shirika la habari la AFP.

Bw Griffith anasema wanaendelea kumfuatilia kwa makini na kwa uangalifu mkubwa, huku mwanae wa kiume David Bennett Jr akiliambia Shirika la Habari la ovAssociated Press kwamba familia yao iko "katika hali ya sintofamu wakati huu".

Lakini aliongeza : "Alitambua ukubwa wa kile kilichofanyika na anatambua umuhimu wake."

''Hatujawahi kufanya hili kwa binadamu na ninapenda kufikiria kwamba tumempatia chaguo bora kuliko kile ambacho kingetokea kama angeendelea kupewa matibabu aliyokuwa akiyapata," alisema Bw Griffith . Lakini iwapo [ataishi kwa] siku, wiki , mwezi, au mwaka, sijui."
IMG_20220113_151212.jpg
IMG_20220113_151158.jpg
 
Huyo bin adam atakufa tu wala huo moyo hautaleta matokeo kwake
 
Hivi nguruwe ana nini lakini? Chanjo ya corona nguruwe, chanjo ya tetenasi nguruwe, insulin nguruwe. Kwanini hawatengenezi kwa ngombe?
Hapo kwenye chanjo ya tetanus umetu piga changa la macho hakuna TT ya nguruwe bro
 
Hiyo ni kama medical trial na aliepandikizwa huyo moyo ni mgonjwa tayari wa moyo na anaweza kufa siku yoyote.

Pili, kabla hao madaktari hawajafanya huo upasuaji na kupandikiza huo moyo wa nguruwe waliomba kibali maalum kutoka serikalini na waliporuhusiwa ndo wamefanya hivyo.

Tatu, huyo nguruwe si nguruwe hawa tulozoea wa kuliwa kitimoto bali alipandikiwa maabara kwa ajili ya kujaribiwa katika upandikizaji yaani "genetically modified pig" hivyo si nguruwe wa kawaida.

Hivyo huyo mgonjwa baada ya kushindwa kumpata donor ambae yupo "healthy" ili kumsaidia kuendelea kuishi akaamua kukubali hiyo "experiment" ambayo ameambiwa haina uhakika wa kudumu yaani "guarantee".

Hitaji la viungo vya kupandikiza kama moyo ni kubwa sana nchini Marekani na mwaka jana pekee watu 3,800 walifanyiwa upasuaji wa moyo, na hiyo ni taarifa kutoka United network for Organ Sharing ambayo ni sehemu ya mfumo unosimamia upandikizaji wa viungo kwa mtu yoyote nchini Marekani.

Daktari bingwa wa upasuaji na mtaalam wa magonjwa ya moyo alofanya upasuaji kwa mgonjwa mzee David Bennett anaitwa Dr Muhammad Mohiuddin.

Dr Mohiuddin ndie alisimamia zoezi la kumtengeza nguruwe wa maabara na pia ni mtaalam wa upandikizaji wa viungo kutoka kwa wanyama kwenda kwa binadamu yaani "animal-to-human transplant".
Nguruwe hakutengenezwa maabara Bali amekuzwa chini ya uangalizi na wameondoa gene za kufanya asiweze kuzalisha antibodies za zitakazo sababisha organ rejection full stop! Yeye bado ni kitimoto halisi hakuna ku adjust story
 
Nguruwe hakutengenezwa maabara Bali amekuzwa chini ya uangalizi na wameondoa gene za kufanya asiweze kuzalisha antibodies za zitakazo sababisha organ rejection full stop! Yeye bado ni kitimoto halisi hakuna ku adjust story
Story hajawa adjsuted, nguruwe kabadilishwa dna maabara kawa kivingine hilo ndilo la msingi.

Yaani kafanyiwa matengenezo na si kuundwa. Nimetumia neno kapandikizwa nikimaanisha kabadilishwa, hivyo huyo hawezi kuwa nguruwe wa kawaida tena. Ndo maana wao wasema "genetic modified pig."

Hata ukimtumia kutaka piglets hutapata walo wazima kwa kila kinasaba.

Weye nguruwe huyo waweza kumla wakisema wanamrudisha mezani kutokea maabara?

Ndo maana wadau wa haki za wanyama welfare activits wanapinga masuala hayo ya "animal testing and modifications".
 
Back
Top Bottom