Madaktari bingwa wafanikiwa kumpandikiza binadamu moyo wa nguruwe

Madaktari bingwa wafanikiwa kumpandikiza binadamu moyo wa nguruwe

Huyo bin adam atakufa tu wala huo moyo hautaleta matokeo kwake
Wanafahamu atakufa kwani hakuwa ame-qualify kupata moyo mwingine wa binadamu, na wakaona anafaa kufanyiwa majaribio.

Hata hivyo huyu mgonjwa aliwahi kutumikia kifungo jela kwa kumchoma kisu mwanamme mwingine ambae alimhisi alikuwa na mahusiano na mkewe.

Hivyo alitumikia kifungo cha miaka 10 jela na alipotoka akawa na hilo tatizo.

Hili suala la kutumia mioyo ya wanyama limekuwa likifanyika nchini Marekani kwa siri.

Mwaka 1980 madaktari walipandikiza moyo wa sokwe kwa mtoto inasemwa ni (mtoto mwenye asili ya Afrika) aliezaliwa na moyo wenye tundu (congenital heart defect) na akafariki baada ya mwezi kutokana na mfumo wake wa kinga kukataa moyo huo wa sokwe.

Baada ya hiyo failure ndo wakaendelea na kumshughulikia zaidi nguruwe ili kupata moyo ambayo wafaa zaidi.
 
Moyo unatolewa yanayobaki yanaliwa🤣🤣
Si kweli.

Hawa nguruwe waitwa "GalSafe Pigs" hutayarishwa na kampuni moja yaitwa Revivicor ni regenerative medicine company.

Hii kampuni kazi yake ni kuwandaa hawa nguruwe na kisha kupata kibali kutoka FDAS ili watumiwe kwenye "Pharmacology".

Hivyo si nguruwe wa kawaida kiasi cha kumkarangiza na kumla.
 
Wanafahamu atakufa kwani hakuwa ame-qualify kupata moyo mwingine wa binadamu, na wakaona anafaa kufanyiwa majaribio.

Hata hivyo huyu mgonjwa aliwahi kutumikia kifungo jela kwa kumchoma kisu mwanamme mwingine ambae alimhisi alikuwa na mahusiano na mkewe.

Hivyo alitumikia kifungo cha miaka 10 jela na alipotoka akawa na hilo tatizo.

Hili suala la kutumia mioyo ya wanyama limekuwa likifanyika nchini Marekani kwa siri.

Mwaka 1980 madaktari walipandikiza moyo wa sokwe kwa mtoto inasemwa ni (mtoto mwenye asili ya Afrika) aliezaliwa na moyo wenye tundu (congenital heart defect) na akafariki baada ya mwezi kutokana na mfumo wake wa kinga kukataa moyo huo wa sokwe.

Baada ya hiyo failure ndo wakaendelea na kumshughulikia zaidi nguruwe ili kupata moyo ambayo wafaa zaidi.
Ngoja tuone matokeo ya kisayansi vs Muumba
 
Si kweli.

Hawa nguruwe waitwa "GalSafe Pigs" hutayarishwa na kampuni moja yaitwa Revivicor ni regenerative medicine company.

Hii kampuni kazi yake ni kuwandaa hawa nguruwe na kisha kupata kibali kutoka FDAS ili watumiwe kwenye "Pharmacology".

Hivyo si nguruwe wa kawaida kiasi cha kumkarangiza na kumla.
Ofcourse hata huo moyo umeeditiwa genes. Hapa tunaleta utani tu
 
Story hajawa adjsuted, nguruwe kabadilishwa dna maabara kawa kivingine hilo ndilo la msingi.

Yaani kafanyiwa matengenezo na si kuundwa. Nimetumia neno kapandikizwa nikimaanisha kabadilishwa, hivyo huyo hawezi kuwa nguruwe wa kawaida tena. Ndo maana wao wasema "genetic modified pig."

Hata ukimtumia kutaka piglets hutapata walo wazima kwa kila kinasaba.

Weye nguruwe huyo waweza kumla wakisema wanamrudisha mezani kutokea maabara?

Ndo maana wadau wa haki za wanyama welfare activits wanapinga masuala hayo ya "animal testing and modifications".
Unajua tofauti ya antigen na DNA?
 
Sijajua kama hapa Tanzania itakubalika labda Moshi.
--

Moyo wa nguruwe wapandikizwa kwa binadamu nchini Marekani​

View attachment 2077557

Katika picha hii iliyotolewa na Chuo cha kikuu cha Tiba cha Maryland, timu ya upasuaji inaonyesha moyo wa nguruwe tayari kupandikizwa kwenye mgonjwa

Kwa mara ya kwanza duniani, nchini Marekani, Madaktari wa upasuaji wamefanikiwa kupandikiza moyo kutoka kwa nguruwe aliyebadilishwa vinasaba hadi kwa binadamu mgonjwa, Chuo Kikuu cha tiba ya Maryland kimesema.

Operesheni hiyo ilitekelezwa siku ya Ijumaa. Ilionyesha, kwa mara ya kwanza, kwamba moyo wa mnyama unaweza kuendelea kufanya kazi kwa binadamu bila usumbufu wowote, Chuo Kikuu cha Maryland kimeongeza.

David Bennett, 57, ambaye alipokea moyo wa nguruwe, alitangazwa kuwa hastahili kupokea upandikizaji wa moyo wa binadamu. Sasa anafuatiliwa kwa karibu na madaktari ili kuhakikisha kiungo kipya kinafanya kazi vizuri.

"Yaani yalikuwa mambo mawili kwa binadamu huyo, ima kifo au upandikizaji wa moyo wa nguruwe. Nataka kuishi.

Ninajua ilinigusa sana, lakini ilikuwa chaguo langu la mwisho, "mkazi wa Maryland alisema siku moja kabla ya upasuaji wake, kulingana na chuo kikuu cha matibabu. "Siwezi kungoja niweze kuamka kitandani mara tu ninapokuwa mzima," David Bennett, ambaye amelala kitandani kwa miezi michache iliyopita na kutumia mashine inayomfanya aendelee kuishi.

Nguruwe aliyebadilishwa vinasaba
Mamlaka ya Madawa ya Marekani (FDA) iliidhinisha operesheni hiyo jioni ya siku ya kuamkia Mwaka Mpya. "Haya ni mafanikio makubwa ya upasuaji na ambayo yanatuwezesha kupata suluhisho dhidi ya uhaba wa viungo, " amebaini Bartley Griffith, aliyefanyiwa upandikizaji wa moyo wa nguruwe.

Nguruwe ambao moyo hutoka umebadilishwa vinasaba ili kutozalisha tena aina ya sukari ambayo kwa kawaida iko kwenye seli zote za nguruwe na ambayo husababisha kiungo kukataa kufanya kazi mara moja. Marekebisho haya ya jeni yalifanywa na kampuni ya Revivicor, ambayo pia ilitoa figo ya nguruwe ambalo madaktari wa upasuaji walifanikiwa kuunganisha kwa mishipa ya damu ya mgonjwa aliyekuwa mahututi huko New York mwezi Oktoba.

Takriban Wamarekani 110,000 kwa sasa wako kwenye orodha ya wanaosubiri kupandikizwa viungo na zaidi ya watu 6,000 wanaohitaji upandikizaji hufa kila mwaka nchini humo.

Ivi hii inawezekana? Na unakuwa na akili ya kawaida au kuna namna unaweza kuathirika nakuwa na akili za nguruwe nguruwe
 
Kuna jamaa aliwahi kuandika kitabu chake cha dini, ambapo dini hiyo ndio mpaka sasa inakitumia kama kitabu cha kiada in every respect

Kwenye kitabu hicho aliweka mila ya watu wa middle east ya kutokula mdudu na kusema ni haramu

Kwa kuwa aliandika kitabu hicho kwa mafumbo na mfumo wa ushahiri wenye lugha za picha , wengi hawakumuelewa hasa kwenye bara la wenye nywele zinazofanana na lami.

Wengi wakimwona mdudu hata anajipitia zake huanza kumtoa nduki na kudhani ndio yule mwovu abaye kabla hawajaanza toba yoyote husema " tuepushe na mwovu........"

Madhalani , kama mimi ndio ningekuwa mwandishi wa kitabu hicho ningesema wazi " msimle mdudu kwani nyama yenu na yake zinafanana na nilikuumbeni kwa donge moja la udongo ila kila mmoja nikampa namna tofauti..Msiwale hao ni ndugu zenu na watawasaidia viungo tiba kwani hata mifumo niliokuwekeeni na wao nilibadilidha kidogo. Mwisho wa kunukuu
 
Swali la msingi ni umri wa nguruwe kuishi..
Nguruwe anaishi miaka minne maximum..
Je moyo wake utaendelea kuishi baada ya hapo?

Ila huyu mtu hatakiwi kula nyama ya nguruwe, wameshakuwa ndugu
Hahaaahaaaa nimecheka sana mpaka simu yangu imeporomoka,,akila kitumoto kamla ndugu yake teteeeeheteeee jf ukiwa na mawazo yanakuzongo we log in jf mambo yanakua poa
 
Back
Top Bottom