Madaktari hasa wa Tanzania rudini maabara tena kuhusu ugonjwa wa U.T.I

Hauko sahihi hata chembe , ni vema labda wewe mwenyewe kabla ya kuja hapa ungejiridhisha Kwa kujaribu kujua U.T.I ni kitu gani na kama kweli ni ugonjwa wa kuambukizwa kutoka chooni au kwingineko ( ni rahisi sana kujua hili ) , ukifanya uchunguzi utagundua kwamba watoto wadogo sana ndio wahanga wa huu ugonjwa , lakini mbona hawajawahi kuingia kwenye vyoo vya wakubwa ? hivi ni kweli wanawake hao uliowataja wanaumwa U.T.I , au ni makosa ya wataalam wa upimaji ?

niishie hapa kwa leo
 
Uti ni janga aisee, unaweza ukapimwa vyote lkn utajikuta una uti .
 
Sijawahi sikia/kuona mtu anamaliza tatizo la U.T.I kwa kutumia vidonge elekezi, zaidi tu utasikia hii U.T.I imekuwa SUGU watakiwa kuchomwa sindano...Hata hiyo pia hubuma.

Tiba mbadala:
Chemsha maganda ya nanasi, chuja, kunywa.
Baada ya wiki kacheck U.T.I

Hili zoezi ukiwa walifanya angalau mara moja kwa mwezi U.T.I utaisikilizia kwa jirani.
 
Baba uti ipo kwenye std's hiyo ni mpya

Sasa hutaki mkuu? Kwani STDs nini? Si ni magonjwa yanaambukizwa kwa ngono? U.T.I si yaweza kuambukizwa ngono pia?

Chanzo chaweza kisiwe ngono, inakuwa S.T.D pale mmoja wenu akiwa nao, ujue mmoja wenu huenda akaambukizwa na yeye akichepuka anaambukiza mwingine hivyohivyo network inaendele hence , sexual transmission disease.
 
Moderator hii mada ni ya muhimu sana...ithaminishwe zaidi.
 
UTI ya bacteria infections ni chache sana tena sanaa..kuna baaz ya mitambo ya kupimia UTI mwisho wa kuona ni michubuko ktk njia ya mkojo sasa tatizo linaanzia je hiyo michubuko imesababishwa na bacteria au ni nini? Na madokta wengi wao wakishaona michubuko wanaandika UTI na wana assume ni infections wanatoa doz matokeo yake kila mwezi unarudi hospital. Nakumbuka nilienda mkoa fulani nikaanza kuumwa uo ugonjwa dah ilikua ndio mazoea kupigwa visindano vya UTI yaani mpaka hospital ikanizoea. Siku moja nikapata safari narudi dar nikasema nikapime mkojo pale regency nikapima asubuhi mpaka saa nne usiku ndio napata majibu ikanibidi nirudi kesho yake kumuona dokta. Dokta akaniambia ni kweli nimekua na michubuko kwenye njia ya mkojo lakini haisababishwi na bacteria, akaniambia mkojo wangu una chumvi nyingi sana mpaka kupeleke ile chumvi inatengeneza kama vimchanga hivi ndivyo vinavyosababisha hiyo michubuko. Wakaniambia ninaonekana sinywi maji mengi pia situmii vyakula na matunda yenye maji maji vya kutosha. Wakanipa dawa ya kuponya ile michubuko ila wakaniambia nisipobadirika ktk hilo nitakua naenda hospital daily, basi tangu uo mwaka nakumbuka ilikua 2013 mpaka leo siijui UTI
 
Vyoo vya kukaa zamani vilikua vyoo vya kulenga
 

Tatizo sikuhizi hata mwenye gono na kaseende nayeye anaambiwa/anasema ana U.T.I
 
Shida ni pale unapopewa dawa ambayo inatibu UTI na maralia inatibu pia.
unazifaamu zile dawa zina paracetamal ndani yake?
Paracetamol haijawahi kutibu Malaria. Hii ni pain killer. Inapunguza maumivu.
 
Kunyweni maji mengi jamani UTI mtaisikia kwa majirani..mie nna zaidi ya mwaka wa 6 sijaugua UTI
 

Namba mbili ndio sbb kubwa zingine blabla tu kunywa maji vizuri UTI utaisikia kwa watu tu
 
Mkuu embu jaribu kuibadilisha hii...
 
Kipimo gani ulipima mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…